Jinsi "wasaliti " wanavyoula CCM, huku wafia chama wakitoswa

Jinsi "wasaliti " wanavyoula CCM, huku wafia chama wakitoswa

Mtaelewa tu nyie wenyewe mnapiga piga kelele ili mbowe awape hata vyeo vya mgambo maana kwenu kila mtu kamanda
 
Sizonje ni mwanasiasa mshamba, hakuwahi kujua ngoma anayong'ang'ania kuicheza sasa kumbe ilishachezwa sana na wenzie hapo zamani na ikasahaulika.

Zilipendwa.
Mkuu rudi tu ukampigie magoti Sizonje atakukumbuka japo kwa ukuu wa wilaya.

We ulifikiri utakula milele pale kwenye ile nafasi yako?
 
bila juhudi za hao unaowakebehi kama wafia chama wahamiaji wasingeshawishika kujiunga na chama.

kwa vyovyote vile wahamiaji ni matunda ya jasho la wafia chama.

Kusema kuwa ccm inagawa vyeo ni kuitusi.

CCM inaangalia kwanza maslahi ya watanzania hivyo hata teuzi za Nafasi yoyote hufanywa kwa misingi hiyo.
Wanaotoka upinzani kwenda ccm wananjaa ila wanaotoka ccm kwenda upinzani wameshiba kwa mujibu wa msemaji wa ccm -polepole
 
Ni vizuri sana mana anawaandaa wafia vyama kisaikolojia ili waikubali katiba ya Warioba.

Naona kama Magufuli ana nafasi ya kuwa rais bora kabisa barani Afrika kwani naona jinsi anavyoweka mazingira mazuri ya kuileta ile katiba ya wananchi.

Wale majamaa ya kijani hayaikubali ile katiba kwa sababu ya kuwaza vyeo tu.
Sasa kimekija chuma na sasa anatema checheeeeeee!!

Hapa Kazi tu.

Tumuunge mkono Rais!
Anafanya vizuri sana kwenye teuzi zake.

Ili chakula kiwe safi ni lazima na sahani iwe safi.

Ni vema akawaweka pembeni baadhi ya watu walioshiriki sana kwenye madhaifu yaliyokuwepo hasa yale ya makusudi.

Tena ikiwezekana awachunguze sana mali zao kuanzia hao mabalozi, maDC, mawaziri ,Makatibu wakuu, MaRC, Wakurugenzi ili abaini kuwa wengi walikua wanahomora mafeze ya umma kwa manufaa yao ,wakae pembeni hata kama watahamia wote upinzani. Lakini tujenge Tanzania mpya na mawazo mapya. Uzalendo uwe wa kweli.
Nachukia mtu anayejiita mzalendo huku akijua wazi kuwa alifanya ubadhirifu wa mali za umma halafu bado anabaki kwenye serikali. Mkuu wa Taifa hili waweke pembeni wale waliokua wanshiriki huo uharibifu ili twende sawa na dhamira yako ya kweli.
Tusiwafunge gerezani lakini tusiwaache tena kwenye madaraka wale waliohujumu nchi .Wakae pembeni tupime uvumilivu wao. Nao waone machungu ya mabadiliko.
Hakuna kulinda cheo cha mtu.

Wapinzani wote wana sifa ya kupata nafasi kwani walipigania sana haki na uzalendo wa nchi hii wakati CCM bila aibu wakikua wanawazomea mchana kweupe.
Dr. Slaa akiwa mmoja wapo aliyepigania sana taifa letu.
Anastahili kupewa ubalozi.

Waache CCM URITHI wavimbe wapasuke. Mabadiliko ya kweli mbele kwa mbele.

Hawezi kuileta katiba ya Warioba, kwa jinsi anavyonuka ufisadi na rushwa. Atafungwa.
 
bila juhudi za hao unaowakebehi kama wafia chama wahamiaji wasingeshawishika kujiunga na chama.

kwa vyovyote vile wahamiaji ni matunda ya jasho la wafia chama.

Kusema kuwa ccm inagawa vyeo ni kuitusi.

CCM inaangalia kwanza maslahi ya watanzania hivyo hata teuzi za Nafasi yoyote hufanywa kwa misingi hiyo.
Ndiyo maana teuzi za wakuu cha mokoa zinazingatia kujua kusoma na kuandika kwa maslahi ya wa-Tanzania?
 
Mkuu nimeipenda sana hii thread, ccm ipo ktk wakati mbaya kuliko wakati mwingine wowote. Amkeni akina nape njooni 'kipande hii' hakuna stress ni full starehe.
 
Kwa hiyo nyie CDM mnapojiunga na chama sio kuwa mnataka kuiendeleza Tanzania bali mnataka mkapewe kula?

Wana CCM halisi walimchagua Magufuli ili aiongoze Tanzania na kutuletea maendeleo. Sasa kama ameziona talanta ndani ya Kitila, Mgwira na Slaa ziungane na zile za viongozi maelfu wa CCM kutekeleza azma yake ubaya upo wapi?

Nyie hamna jema. Mkiwekwa pembeni mnasema Magufuli hataki ushauri wa wapinzani. Akiwachukua mumsaidie kufanya kazi zake manambeza eti mbona unawaacha wana CCM.

Kweli sikio la kufa halisikii dawa.
Kwa kufanya hayo unadhani anafanikiwa au anachemka?. Waliotangulia kufanya hayo walishindwa kufanikiwa yy ataweza?.
 
stroke kama mfia chama namba moja humu jf, unafaidikaje? usifiche. Wafaidika hawashindi mitandaoni wanakuwa na shughuli nyingi. Utakufa kwa stroke soon.
sifaidiki na chochote mkuu, natumia tu haki yangu ya kikatiba ya kutoa maoni.
 
Hili liwe angalizo kwa vijana wa CCM wanaokesha mitandaoni kutetea wanachokiita chama chao, lakini kumbe chama kina wenyewe.

Sasa ni dhahiri kwamba watu ambao kwa miaka mingi wameiponda CCM hadharani na gizani ndio wanaoteuliwa kushika vyeo ndani ya serikali, huku wanaojiita wafia chama wakipuuzwa na kuonekana vilaza.

Juliana Shonza, Kitilla Mkumbo, Augustino Mrema , Anna Mughwira, Mtella Mwampamba, Humphrey Polepole ni baadhi ya majina machache tu ya walioiponda ccm kwa miaka mingi, lakini wakaonekana lulu baada ya kusaliti walikotoka.

Ndugu yangu unayejifanya CCM ni yako kiasi cha kutetea hata maovu, huu ni wakati wa kujitafakari nafasi yako ndani ya CCM , The time is now.

Majuto ni mjukuu.
Hawakuwa wanaponda chama mkuu,hiyo inaitwa constructive criticism.Sasa wewe kama unaunga mkono kila jambo si hypocrite,kihiyo na mchumia tumbo tu,upewe cheo cha nini,fungukeni.A competent person anajiamini on what he says and does.
 
Hili liwe angalizo kwa vijana wa CCM wanaokesha mitandaoni kutetea wanachokiita chama chao, lakini kumbe chama kina wenyewe.

Sasa ni dhahiri kwamba watu ambao kwa miaka mingi wameiponda CCM hadharani na gizani ndio wanaoteuliwa kushika vyeo ndani ya serikali, huku wanaojiita wafia chama wakipuuzwa na kuonekana vilaza.

Juliana Shonza, Kitilla Mkumbo, Augustino Mrema , Anna Mughwira, Mtella Mwampamba, Humphrey Polepole ni baadhi ya majina machache tu ya walioiponda ccm kwa miaka mingi, lakini wakaonekana lulu baada ya kusaliti walikotoka.

Ndugu yangu unayejifanya CCM ni yako kiasi cha kutetea hata maovu, huu ni wakati wa kujitafakari nafasi yako ndani ya CCM , The time is now.

Majuto ni mjukuu.
Unanifanya nikumbuke story ya mwana-mpotevu katika bible! Yule mzee alimfanyia sherehe kubwa yule mtoto aliyedai urithi wakati babake akiwa hai na akapewa (haikuwa kawaida). Akatapanya mali na marafiki zake pamoja na malaya hadi pesa ikaisha. Kisha akakumbuka nyumbani palipojaa neema na utajiri. Akaamua kurudi kwa baba yake. Baba akamtunuku vingi hadi mtoto mkubwa akaona wivu kuwa, mie pamoja na kubaki nyumbani, kushinda shambani, .... hujanichinjia hata ndama aliyedhoofu!.......
Msione wivu waliopotea wakirudi nyumbani na "kupewa mavazi mazuri/mapya/safi na kuchinjiwa ndama aliyenona".
 
Kiongozi umenikela kuatach uzi wangu mahali ambako mimi sikuhitaji. Wewe unanipeleka mahali kwa lazima bila hiyari. Sijawahi kukumbwa na hili toka niwe member humu ukweli sijalifurahia. Umekaa umetulia pekee yako ukaona uunganishe uzi Wangu na huu. Basi poa.
 
Tumsikilize,tumsome na isiishie hapo TUMUELEWE PIA.

mwenyewe anapenda kusisitiza MAJIZI hayana chama yapo CCM,CUF,UDP NA HATA CDM nk tushirikiane tujenge nchi.

Hizi teuzi toka UPINZANI ni za kujivunia saana inapaswa upinzani utembee kifua mbele.

Kwani umeandaa wananchi tayari kupokea majukumu yoyote ya kiserikali jiaminini.
Shangilieni mko wasafi mkuu haoni kwenye kundi lake.

Anawaona nyinyi pigeni makofi TAFADHALI.
 
Mgeni anapewa mnofu wenyeji wanaendelea kula vipapatio, makanyagio, utumbo na vichwa

Ningependa kusikia ya moyoni kutoka kwa wasotea chama waliokipigania chama kabla, wakati na baada ya uchaguzi ambao bado hawajateuliwa katika ngazi yoyote ile huku wapinzani ambao muda wao wote wamekuwa wakikiponda chama wanateuliwa na kupewa minofu mitamumitamu..

Hata kama wewe sio msotea chama ila umepata nafasi ya kuwasikiliza mkiwa either private au public nini mtazamo wao na wanajisikiaje

Ni kasumba ya mwanadamu ambaye analipigania jambo fulani baada ya kufanikiwa hupenda kuwa sehemu ya wanufaika hata kama amesahaulika... Anaweza akacheka na kuunga mkono maamuzi hadharani lakini ukimtazama sana kwa umakini unaweza kuona hisia zake, matendo yake, sura yake haviendani na kile anachokikubali hadharani..

Narudia tena ningependa kusikia ya moyoni kutoka kwenu either umemshuhudia au wewe mwenyewe ukiwa kama msotea chama uliyefungiwa milango nini maoni yakoView attachment 636840 View attachment 636839

Hata Dr. Slaa ilimuuma sana lowasa alivyopewa nafasi ya kugombea bure bure wakati waliosotea chama wapo.
 
Mgeni anapewa mnofu wenyeji wanaendelea kula vipapatio, makanyagio, utumbo na vichwa

Ningependa kusikia ya moyoni kutoka kwa wasotea chama waliokipigania chama kabla, wakati na baada ya uchaguzi ambao bado hawajateuliwa katika ngazi yoyote ile huku wapinzani ambao muda wao wote wamekuwa wakikiponda chama wanateuliwa na kupewa minofu mitamumitamu..

Hata kama wewe sio msotea chama ila umepata nafasi ya kuwasikiliza mkiwa either private au public nini mtazamo wao na wanajisikiaje

Ni kasumba ya mwanadamu ambaye analipigania jambo fulani baada ya kufanikiwa hupenda kuwa sehemu ya wanufaika hata kama amesahaulika... Anaweza akacheka na kuunga mkono maamuzi hadharani lakini ukimtazama sana kwa umakini unaweza kuona hisia zake, matendo yake, sura yake haviendani na kile anachokikubali hadharani..

Narudia tena ningependa kusikia ya moyoni kutoka kwenu either umemshuhudia au wewe mwenyewe ukiwa kama msotea chama uliyefungiwa milango nini maoni yakoView attachment 636840 View attachment 636839
Hata Dr. Slaa ilimuuma sana lowasa alivyopewa nafasi ya kugombea bure bure wakati waliosotea chama wapo.
 
Back
Top Bottom