Jinsi ya kufungua kanisa 'la Mchongo' la kilokole na upige pesa Kwa Muda mrefu

Jinsi ya kufungua kanisa 'la Mchongo' la kilokole na upige pesa Kwa Muda mrefu

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
1:Anzia kijijini. Kule utapata wafuasi wengi wasio na uwezo wa kuhoji kipindi uwezo wako wa kushawishi Bado mdogo.

2: TUMIA Muda mwingi kusoma vitabu vya uchawi ili ujue watu wanalogwaje, vitabu vya migogoro ya ndoa, magomvi ya familia na ukoo. Ujue watu wakienda Kwa waganga Huwa wanafanywaje. Hii itakupa usikivu maana wote wanaoamini wamerogwa au watarogwa.

3: Soma vitabu vya ndoto na tafsiri zake. Vya kiislam,kijadi na walokole waliofanikiwa duniani.

4; Jifunze demonology. Uyajue makini na kazi zake kutoka katika vitabu vya wanaoyapenda. Kariri majina yake na hakikisha unayatajataja.

5: Soma biblia ukichagua vifungu vya kutia moyo watu. Jiaminishe kabisa kuwa nikweli.

6:Jipe Jina la utata la kukupa kiki. Kama utapenda ushirikina kidogo Jina Hilo ndio litakuwa code ya kuvutia nguvu za Giza kupumbazia watu. Ila bila ushirikina litatia utisho na urasmi flani mioyoni mwa vichwa vyako.

7: Be private. Jifichefiche watu wasikujue. Kaa mbali na watu kabisa. Muda mwingi uwe umejifungia ndani ukireheso tricks na kanuni za kuwafanya watu wakuamini. Ni rahisi kusema ulienda mbinguni na Kuna maelekezo umepewa na Yesu utaaminika maana watu hawjui Huwa uko wpi. Hat ukisema sijawahi kuugua au umefunga bila kula siku arobaini hakuna mwenye ushahidi wa kukupinga. Wakati mwingine hata mkeo/mmeo au watoto wasikujuejue.

Unaweza ukaanzia hapa.
 
Jifunze kuongea kwa sauti kali na lafudhi ya nyanda za juu kusini,mtu muite mutu,mfano tamka mufano,kila ukihubiri ukiona wanaanza kusinzia tunga stori ya uongo ipakeoake mafuta,watu wanapenda mifano ya stori sana kanisani ,anza hivi siku moja nikiwa london,mutu mumoja akanishika bega,nikashangaa huu muji wa wazungu nani ananijuwa.
 
Sio rahisi hivyo..ingekua rahisi kila mtu angefanya.

Get a job.

#MaendeleoHayanaChama
Ni kweli sio rahisi, ndio maana katika waganga wote wanaopiga hela ndefu ni wachache wanaofanikiwa hasa waliobobea kwenye udanganyifu usioweza kugundua kirahisi.

Watumishi wa kweli wapo ila huduma zimevamiwa! Hadi siku yakukute ndio utaelewa. Mimi kuna familia naifahamu hayo makanisa yamewavuruga hadi yamemfanya sasa anasali na familia yake nyumbani kwake! Hataki kwenda kanisa lolote.
 
Back
Top Bottom