Jinsi ya kupika maharage kwa njia rahisi bila kutumia gharama kubwa

Jinsi ya kupika maharage kwa njia rahisi bila kutumia gharama kubwa

Habari za mapumziko ya mwisho wa wiki,

Leo nimeona bora niwashirikishe jambo moja hasa wale wanaoishi single a.k.a bachelor.

Mara nyingi nimeona watu wa kada hii husumbuka sana katika maandalizi ya chakula na kupelakea kuwa na mahusiano mazuri na wauza chips au Mama lishe ili angalau kuitendea haki miili yao, na mara nyingine wanabuni mboga rahisi kama mayai, dagaa wa kukaanga na mtindi ili kukamilisha zoezi. Lakini napenda kuwajulisha sasa unaweza kupika maharage kwa dk 10 na ukafurahia maisha, fuata maelekezo haya;

1. Andaa maharage yako tayari kwa kupikwa,

2. Washa jiko lako kisha tenga maharage yako, subiri mpaka yachemke kabisa (boiling point)

3. Mimina maharage na maji yake kwenye Thermos (chupa ya chai) hakikisa chupa yako haipozi, na pia hakikisha maji yanajaa mpaka juu.

4. Funika chupa yako vizuri kisha ondoka nenda kazini.

5. Ukirudi toka kazini njoo na nyanya,vitunguu,karoti nk tayari kuunga maharage yako tayari kwa kuliwa.

Nawatakia Siku njema, nasubiri mrejesho.

Stay blessed
Nitajaribu hii..!
 
Kujipikilisha sio tatizo, vyombo ndo ishu. Ukifika kwa mabachelor wengi utakuta kuna ndoo imejaa vyombo vikiwa na uvundo wa ugali.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Asante kwa uzi nzuri nimeama home Nina miez 4 inakaribia sijawah kula wala kupika maharange kwa huu uzi nitaende kununua maharange ili nipike.

Naomba unifafanulie namba 2 hii " 2. Washa jiko lako kisha tenga maharage yako,
subiri mpaka yachemke kabisa (boiling point)"

Ni unachesha hayo maharange yakichemka unayamiminia na Maji yake kwenye chumba
 
Hii kitu nimeitumia sana nilifundishwa na mama yangu!
 
Asante kwa uzi nzuri nimeama home Nina miez 4 inakaribia sijawah kula wala kupika maharange kwa huu uzi nitaende kununua maharange ili nipike.

Naomba unifafanulie namba 2 hii " 2. Washa jiko lako kisha tenga maharage yako,
subiri mpaka yachemke kabisa (boiling point)"

Ni unachesha hayo maharange yakichemka unayamiminia na Maji yake kwenye chumba
Mimi nilikua nachemsha maji naweka kwenye chupa naweka maharage asubuhi nakuta yamelainika ila chupa isiwe inapoza.
 
ninaishi na ndugu zangu tupo karibu 8 na watoto hayo maharage gani yataingia kwenye tharmos na ikatutosha
 
Leo nimejaribu kupika maharage masaa 8 hayajaiva!nikaamua tuu niende nikanunue nyanya nikala ugali na kachumbari
 
Back
Top Bottom