Jinsi Ziwa Natron linavyoweza kuifanya Tanzania kuwa moja ya mataifa tajiri duniani

Mkuu rasmi nakutoa kwenye list ya wale mbu watatu(mbu+mbu+mbu) wa mzee rage.
 
Halafu eti WAZUNGU wanatudanganya kuwa tumelaaniwa.

SASA nani anakulaani halafu akupe kila kitu??
 
Miaka kadhaa iliyopita kampuni yaTata Chemicals ya India ilianza mchakato wa kujenga kiwanda cha kutengeneza Soda Ash (Sodium Carbonate) lakini kukawa na upinzani kutoka watu wa Mazingira kwa madai kuwa kiwanda hicho kingeathiri mazalia ya ndege aina ya flamingo ambao ni kivutio cha utalii,inavyoelekea watetezi wa mazingira walishinda ndiyo maana hiyo project ilikufa natural death.
 
Katiba yetu ya sasa ukiwa na rais lege lege na mvivu wa kufikiria akifanyiki kitu,kila kitu kitaenda mlama,maana rais amerundikiwa majukumu mengi.
 
 
Ni mawazo finyu kwa kweli. Lake Natron ni eneo pekee Afrika Mashariki ambamo ndege aina ya "lesser flamingos" wanazaliana. Hawa wanaweza kuwa sehemu ya vivutio vya utalii kwa mamia ya miaka ijayo wakati hiyo soda ash itaweza kuvunwa sana sana kwa miaka 150 tu. Aidha, tunajua kuwa watakaoajiriwa katika kiwanda hawatakuwa wenyeji wa hilo eneo na faida itakayopatikana haitatumika kwa manufaa.
Ni watu myopic ndio peke yao wanaweza kuupigia debe mradi huu.
Inanikumbusha suala la vyura wa Kihansi. Hatukutaka kusikia lolote tulipoambiwa umuhimu wa wale vyura. Wamarekani wakawachukua baadhi na kuwatunza Marekani. Sasa tunajifanya kuwataka maana wametoweka kabisa kwetu. Hivyo hivyo tusimlaumu mtu hao lesser flamingos wakihamia Kenya au kwingine.

Amandla....
 

Vingine tuwaachiage viumbe wengine. Dunia si yetu peke yetu. Hapo tuwaachie flamingo na watoto wao. Kwanza humo hakuna madini ya betri.

Pamoja na kwamba najali sana umuhimu wa kutunza viumbe hai na asili, nadhani hii project inaweza kufanyika bila kuathiri uwepo wao.

Kwanza sidhani kama hao flamingo wasipokunywa maji ya Ziwa Natron, wakapewa vyanzo vingine vya maji na chakula watakufa na kupotea.

Baada ya post yangu nimeona gazeti la The Citizen la wiki hii limesema serikali inaenda kuuendeleza huu mradi. Nilitaka kuocopy ile article ila nimeshindwa. Unaweza kuisoma kwa kwenda kwenye link hii.

Tanzania revives controversial Lake Natron soda ash project
 
Ni mchanganyiko wa madini na joto la ziwa hilo ndio inawawezesha kuzaliana pale. Yale maji sio ya kunywa tu. Hali ya ziwa ikibadilika wataondoka na kutafuta sehemu nyingine yenye mazingira kama hayo. Mazingira ya Lake Natron ni unique ndio maana yanawafaa. Ingekuwa mazingira ya maziwa mengine yanawafaa pasingekuwa mahali pekee Afrika Mashariki ambapo wanazaliana. Uvunaji na ujenzi wa kiwanda na nyumba za makazi vitaharibu kabisa mazingira. Na tukisha yaharibu hatutaweza kuyarudisha tena.

Amandla....
 
Usiseme sana mpaka Zanzibar wakasikia. Hawachelewi kuwahamisha wenyeji wa hapo kwa nguvu kisha kwa kisingizio wanachafua mazingira Kisha, wakalamba mzigo wote na kuwaacha Watanganyika wakiwa hoi.
 
Ccm Bora wampe mwarabu kwa kisingizio Cha uwekezaje ili tubaki maskini ngozi nyeupe watajirike sisi tuendelee kuimba iyenaiyena .
 
Ila Cha kushangaza utasikia wanasayansi wetu wanataka kutengeneza Ndege na treni ya mwendokasi

Badala ya kutengeneza vitu vyenye tija Kwa Taifa kama hizo Betri

Hi nchi tumelogwa na aliyetuloga ameshakufa
Eti vitu rahisi kabisa kama teknolojia ya kutengeneza betri tunashindwa kweli?
 
Hili wazo ni kama lile la kujenga lifti ya kupanda mlima Kilimanjaro ili wapande watalii wengi na sisi tupate madola kibao. Nasikia upuuzi huu nao unafanyiwa kazi. Tunataka kuongeza mahoteli Ngorongoro. Tunataka kujenga reli kukatiza Serengeti! Mungu atusamehe kwa kweli.

Amandla...
 
Siyo kwa Tanzania ambayo ina wapumbavu wengii

Mbumbavu ni mtu aliyebobea kwenye jambo fulani lakini anaahirisha kufikiri kwa nafsi a.k.a kujizima data, (chawa),

Tanzania watu wanaopewa dhamana huwa niwale ambao hawawezi kuthubutu

Tanzania is where people are busy with their status quo, thereby not concerned with national service delivery
 
Tumeshindwa kutajirika kwa Gesi, Dhahabu na Tanzanite tuje tutajirike kwa baking soda, acha basiii 😅

Hii nchi hii. 🚮
🤣🤣🤣🤣........shida Iko wapi hapo kwenye baking oowder? Si mama ntilie na migahawa zitapika maandazi mengi kwa gharama nafuu kuwezesha walaji kununua maandazi kwa bei nafuu? Pato la mama ntilie itaongezeka maradufu. Siyo utajiri huo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…