Jionee mwenyewe jinsi teknolojia inayotumika Israel kuzuia makombora ilivyoboreshwa, akili iliyotumika kubuni huu mtambo si ya kawaida

Israel wanapewa dollars billion 3 ($ 3 billion) na US kila mwaka ili kugharamia huo mfumo wa Iron dome.

Kiufupi huo mfumo upo Israel ila unafadhiliwa na kugharamiwa na US.
Ni kweli nae Marekani anawapa support kimtindo, kumbuka pato la taifa la Israel kwa mwaka huu pekee ni dola bilioni 500 sawa na shilingi trilioni elf 1,400,
 
Mkumbushe matajiri wakubwa pale US ni waisrael so US lazima apeleke misaada sio kwa kujificha bali kwa kulinda maslahi ya kibiashara zaidi
 
Mkuu nikujuze tu ya kwamba pato la taifa kwa mwaka huu tu ni dola bilioni 500 sawa na shilingi zetu trilioni elf moja na mia nne, hapo kumbuka wana vita, itoshe kusema kiuchumi wamejitahidi
 
Mkuu nikujuze tu ya kwamba pato la taifa kwa mwaka huu tu ni dola bilioni 500 sawa na shilingi zetu trilioni elf moja na mia nne, hapo kumbuka wana vita, itoshe kusema kiuchumi wamejitahidi
Ila watu wana uchumi kudadeki hiyo bado sio nchi tajiri level za kina US China nk
 
Rocket za Hamas sio kipimo sahihi cha iron dome. Japo ndio mfumo wao wa IDS ila bado haijakutana na changamoto za ukweli. Siku nchi kama Tutkey, Iran na wahuni wa Hizbollah wakinukishe ndio watajua anga lao lipo salama kwa kiwango gani.
 
Waisrael ndio wanashikilia mifumo ya fedha, suala la pesa sio tatizo kwao ila hawasemi hadharani, missle moja ya iron dome kuwa dola elf 50 kwao ni kama kununua mawe ya manati.

Mambo ya fedha hayawaumizi vichwa.
Sasa kwanini wa naomba misaada marekani na Ulaya.
 
Hiyo ndio David Sling? Mtagin Faizafox aje atizame Burudani
 
Sasa kama Israel inajiweza hicho kielehele cha Marekani kupeleka meli ,silaha , na wanajeshi nchini Israel kinatoka wapi?

Kama ni historia hata Iran haina historia ya kushindwa vita tena dhidi ya maadui wenye nguvu kuwazidi hao maadui wa Israel kwa karne kadhaa mpaka sasa.

Mbona Lebanon hai kugawanywa nusu kwa nusu mwaka 2006 badala yake Israel ndo aliye razimika kutema ardhi aliye iteka kutoka kwa jeshi la Lebanon?

Mbona kwenye vita ya Sinai Israel hakuongeza eneo ndani ya misri badala yake akaitema Sinai baada ya Marekani kumshawishi Sadart azuie wanajeshi wa misri wasisonge mbele kwa ahadi za mabilioni ya dora kila mwaka kutoka Marekani?

Mpaka sasa Israel imesha dondosha mabomu 7,000 kwenye kieneo kidogo kama gaza lakini mpaka sasa bado hamas wanarusha maroketi ndani ya Israel sasa hiyo miundo mbinu ya hamas wanayo sema wanaipiga iko wapi?

Dunia kwa sasa imebadilika sana achana na mambo ya nyuma ya sijui historia kwa sababu hata Ujerumani kabla ya kushindwa vita ya dunia alikuwa amesha shinda vita huko nyuma.

Mfano Tz tuilishinda Uganda na mpaka tukaiteka kampala,ina maana Nyerere angeamua kuichukua wenda mpaka sasa Uganda ingekuwa sehemu ya Tz, lakini hilo halimaanishi ya kuwa leo tunaweza kwenda vitani na Uganda tukaiteka mpaka Kampala kama mwaka 1979.

Usalama wa Israel unadhaminiwa na Marekani na Unafiki wa waarabu full stop hizo zingine ni story za abunwasi.
 
Sasa kwanini wa naomba misaada marekani na Ulaya.
Ni mambo ya siasa za kimataifa, hata Uingereza ikiingia vitani inaweza kuomb isaidiwe hata chakula, si kwamba hawana chakula bali ni kusapotiana kwenye majanga (anaekusaidia kwenye shida ndie wa kumsaidia akipata shida)
 
Mkuu nikujuze tu ya kwamba pato la taifa kwa mwaka huu tu ni dola bilioni 500 sawa na shilingi zetu trilioni elf moja na mia nne, hapo kumbuka wana vita, itoshe kusema kiuchumi wamejitahidi
Sasa mkuu unalinganishaje banana republic na taifa lenye kutumia akili kila kitu.
Mimi nililinganisha Qatar, Saudi na Israel.

Nyongeza ya hapo, uchumi wao ungekuwa mzuri sana endapo wasingekuwa na majirani visirani. Waarabu huwa hawanunui bidhaa za Israel zenye substitutes hivyo inaipunguzia international market. Imagine Rwanda, Burundi, Kenya, Mozambique, Malawi, DRC hazinunui bidhaa za Tanzania.
 
Lini Israel imeshindwa Vita vya chini ?

T14 Armata
Ilisha shindwa vita nyingi tu na ndio maana walipingwa na kufurushwa mashariki ya kati na warumi wakaenda kutanga tanga duniani.

Mwaka 1972 alishindwa Vita dhidi ya Misri na ndio maana aliitema Sinai na Marekani kurazimika kuilipa mabilion ya dora Misri kila mwaka kwa sharti la kutoishambulia Israel.

Mwaka 2006 ali shindwa vita na Hizbulah na ndio maana alirazimika kuitema ardhi ya Lebanon aliyo kuwa ameiteka kutoka kwa jeshi la Lebanon.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…