Jirani anaweza kukufanya uchukie nyumba yako

Jirani anaweza kukufanya uchukie nyumba yako

Ha ha ha haaaa hivi na tulio kwenye nyumba za kupanga nao tuna majirani? Any way mimi mpangaji mwenzangu alikuwa kero kwangu kama ndio jiran basi ndiye huyo huyo.
Picha linaanza ana miaka 31 na ana watoto watano. Kinachotokea huduma muhim kwa familia hatoi chai ikipikwa sukari inawekwa kiasi kwamba chai ikiwa inaingia tumboni ndio unajua kuwa ilikuwa na sukari.
Uji ukikorogwa ni marufuk kuweka sukari anatia chumvi.
Samaki akinunua bichwa lote lake pekee yake watoto watajua wenyewe na kwa kuwa ni msabato anapitia humo humo kuwanyima familia baadhi ya huduma.
Shughuli kwa majirani watot wake wte wanajua ratiba ya majirani kula ha ha haaa ukitenga tu timu ya watoto wanne hao hapo kasoro mkubwa tu ndio anajitambia maana mkubwa yupo drs la pili.
Kumbuka watoto ni malaika maana huwezi wanyima chakula ila kero na lawama zinarudi kwa mzazi hasa wa kiume ni Nyau saana yule mwamba
Mungu atakubariki kwa ku share rizki na malaika hao.
 
Kuna sehemu moja mtaa wa pili jamaa mmoja anafuga nguruwe harufu iliyopo pale hata ukiwa nyumba ya 5 kutoka kwake harufu inafika sasa sijui yule jirani wa karibu anaishije harufu mbaya kinoma mimi mpita njia tu sikuhizi nimebadili njia
Ila nyama yake unakula husikii hiyo harufu mshehe??
 
Dar Es Salaam inapoteza sifa ya mji unaofaa kuishi binadamu. Huu uholela sijui population ikifikia 10M itakuwaje . Tatizo la Dar wamejaa washamba, . Wanafanya mambo ya kishamba yanayofaa yafanyike huko vijijini kwa kisingizio cha kutafuta pesa. Huwezi kuyaona haya kama tangu uzaliwe hujawahi kuishi nchi zilizoendelea
 
Hivi;hizo picha huwa mmeziandaa kabisa au mkisoma tu uzi mnawahi kutafuta tukio mfanano?🤣🤣🤣🙏
😅
FB_IMG_1699990708879.jpg
 
Kama kichwa cha habari kinavyoeleza z, unaweza kumpata jirani anafuga, inawezekana ikawa kuku, ng’ombe, bata nk.

Mifugo inatoa harufu inayoambatana na inzi, harufu inaweza kukukatisha hamu ya kula na unashindwa kupunga upepo nje ya nyumba yako kwa kero ya inzi pamoja na harufu.

Unapolalamika jirani hakuelewi kwakua ng’ombe wanampatia maziwa na yeye ndiye muuzaji wa maziwa mtaa..

Ukizingatia viwanja vyetu vya uswahilini hivi vya 20x20. Unawaza ningejua nitakutana na haya nisingenunua kiwanja hapa.

Kuku kwanza jogoo anakuamsha ile saa ya usingizi mzito na wala huna safari, kama unashighuli za kufanya unaweza kusema hii ndiyo alarm yako asubuhi.

Kuna jirani alikua anapika mama ntilie, mchana moshi wote unaingia sebuleni kwangu. Nilipomambia masikitiko yangu alianza kuniimbia nyimbo za vijembe. Ilibidi nipeleke malalamiko yangu kwa kiongozi wa mtaa. Baada ya kupata ujumbe kutoka serikali ya mtaa, amehamisha sehemu ya kupikia lakini sikuhizi hatusalimiani. Nimepata adui mpya.
Ndio hasara ya kuishi uswahilini
 
Kama kichwa cha habari kinavyoeleza z, unaweza kumpata jirani anafuga, inawezekana ikawa kuku, ng’ombe, bata nk.

Mifugo inatoa harufu inayoambatana na inzi, harufu inaweza kukukatisha hamu ya kula na unashindwa kupunga upepo nje ya nyumba yako kwa kero ya inzi pamoja na harufu.

Unapolalamika jirani hakuelewi kwakua ng’ombe wanampatia maziwa na yeye ndiye muuzaji wa maziwa mtaa..

Ukizingatia viwanja vyetu vya uswahilini hivi vya 20x20. Unawaza ningejua nitakutana na haya nisingenunua kiwanja hapa.

Kuku kwanza jogoo anakuamsha ile saa ya usingizi mzito na wala huna safari, kama unashighuli za kufanya unaweza kusema hii ndiyo alarm yako asubuhi.

Kuna jirani alikua anapika mama ntilie, mchana moshi wote unaingia sebuleni kwangu. Nilipomambia masikitiko yangu alianza kuniimbia nyimbo za vijembe. Ilibidi nipeleke malalamiko yangu kwa kiongozi wa mtaa. Baada ya kupata ujumbe kutoka serikali ya mtaa, amehamisha sehemu ya kupikia lakini sikuhizi hatusalimiani. Nimepata adui mpya.
Mkuu nadhani kutoelezana ukweli na kukumbatia unafiki yaweza kuwa ndiyo utamaduni halisi wa Mtz.

Unonaje teka teka inayoendelea, chanzo chake si ni kuambizana tu ukweli.

Kwa hiyo kumbe mtu kumweleza ukweli ili aweze kurekebisha, yeye kichwani mwake anafasiri tofauti, yaweza kuwa ni elimu ama chuki.

Na kununa huko yaweza kuwa kapata sababu, donge lilikuwepo rohoni mwake siku nyingi kutokana na life style yako, huwezi jua.

Umefanya vizuri kuhangaika naye mapema, vinginevyo ungeishi maisha ya kero kwa faida zisizokuhusu.

Kila mtu aishi maisha yake bhana asikutishe na ndita zake.
 
Kesi kama hizo ni kupelekwa kwa mwenyekiti wa serikali za mtaa kutoa lalamiko....Kuna sehemu ilikuwa "KOTA" walitengewa sehemu ya kufuga na si kwenye makazi yao.
 
Back
Top Bottom