JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi

JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi

Unajua kuna maamuzi huwa tunafanya bila kuona mbele, nadhani hii inasababishwa na mihemiko na misukumo kutoka kwenye mob.

Hawa madogo walikuwa wamebakiza mkia tu ili kumaliza n'gombe mzima ila wamejiharibia sana.

Kwanini wanaandamana na wakati mikataba yao ilikuwa haijavunjwa?

Napendekeza wasisamehewe maana ni sumu mbaya sana kuwaweka katika kambi zetu. Kuna siku wataandamana tena na kitakachotokea ni kupindua nchi.

Kwao hawajui kwamba JKT haiajiri?

Uvumilivu unalipa sana....ukiona ujapata ujue Mungu hajaruhusu upate.

Always huwa kuna plan B.

Karibuni mtaani tupambane wadogo zangu.
Nisamehewe kwa hii komenti.
 
Lakini pia tuelewe kuwa, ikiundwa tume na ikapewa hadidu za rejea makini za kufuata kufukunyua uozo huu, hata mkuu wa majeshi mwenyewe anahusika moja kwa moja kwenye kadhia hiyo.

Ipo hivii?

Amiri jeshi ambaye ndiyo rais anapotoa tamko, kwa mfano wa kutoa ajira kwa hao vijana kama motisha kwa kazi maridhawa za kujitolea walizofanya, basi hilo agizo hugeuka na kuwa ni amri ya utekelezaji wa moja kwa moja na inakuwa ni haki kwa walengwa.

Sasa tangu Marehemu Maguli atoe tamko hilo umepita muda mrefu bila ya utekelezaji, je ni nani aliyekwamisha mchakato huo?

Je hao vijana walielezwa kilichochelewesha ajira zao ama kama wao wavyosema 'kuandikishwa'?

Tena nimekuja kushangaa kusikia bado walikuwa hawajapewa haki yao hiyo ya ahadi kama ilivyotamkwa na Amiri jeshi!

Ninadhani hii kadhia inajirudia rudia.

Kama sikosei, kama si mwaka jana basi itakuwa ni mwaka juzi, kuna wengine waliahidiwa hivyo hivyo, nadhani waliojenga ukuta ama kazi zinazofanana na hizo, lakini walirejeshwa makwao na tukasikia kwenye vyombo vya habari mkuu wa majeshi akiwatangazia vijana hao warejee makambi ya Jwtz na kuandikishwa jeshi ili kutekeleza agizo la rais.

Sasa tujiulize, ni nani huyo kati kati anayekuwa ni kisiki cha utetekezaji wa amri za rais na amiri jeshi mkuu?

Tume makini ikiundwa, lazima mnyororo wa uozo utajulikana na kuwekwa wazi.

Wenye makosa ya kiuwajibikaji huenda wakawa ni wengi sana kuliko hao vijana zaidi ya 800 waliowatoa kafara na viongozi kubaki wamekalia viti vyao bila ya kuwajibishwa.
Kweli mkuu, nimekuelewa.Ila Kibongobongo hawataunda hiyo tume kwa kisingizio eti masuala ya Jeshi ni nyeti na siri.
 
Wadau wana JF nawasalimu kwa jina la muungano ..nawashangaa vijana kukimbilia JKT hadi kula mafunzo na makazi kibao ili hali wanajua hakuna ajira. Sasa wamegoma wameasi wamerudi mtaani wanaanza kuomba tuwasaidie.


Kama una mdogo wako mkanye JKT hakuna ajira ni bora akaenda veta ufundi stadi atafanikiwa, miaka 3 veta unakuwa fundi haswa
 
Shida kubwa wengine wanaongea bila kuangalia uhalisia wa mambo na hawajui kinachoendelea kisa uongo uongo adi jeshini. Makosa ya namna ya kuajiri vijana toka jkt ilianza baada ya uongozi wa awamu ya tano kuingia.
Vijana wanapmaliza mafunzo ya miezi sita ya awali walikua wanatawanyishwa kwenye makambi mbalimbali yaliyopo chini ya jwtz kwa ajili ya uzalishaji mali na ulinzi kama sehemu ya malezi.

Wakiwa kwenye makambi ya malezi ndipo jeshi..magereza..usalama..bot..takukuru n.k wanakwenda kufanya recruitment wa vijana hawa kulingana na sifa wanazohitaji pindi wakiwa na uhitaji na kwa kwenda kwenye makambi yote ya malezi.

Shida ikaanzia kipindi cha magufuli; yeye alitoa amri wa kuajiriwa waliojenga Ukuta Marerani lakini waliokua wanalima mpunga Chita..wanaolinda mipaka huko Kigoma na Uganda na Rwanda hakuona kama wanasifa ya kuajiriwa..waliokua wanalima mahindi huko Mgambo Tanga hakuona kama wanastahili kuajiriwa sijui alifikiri wote waje Mererani kujenga ukuta bila kuwepo mgawanyo wa ki majukumu.
CDF na mkuu wa jkt wakajikalia kimya bila kuona kuna upendeleo kwenye ajira.

Watu wenye uwezo wakawapanyika vijana wao humo humo na ikawa rushwa ndani ya jeshi.
Ujenzi ulipoanza tena Chamwino stori ikawa ile ile waajiriwe wanaojenga ukuta..hao CDF na mkuu wa jkt wakawa kimya tu; vijana waliopo makambi ya mbali wakawa na vilio mbona wanaajiriwa wa Dodoma tu? then wenye michongo wakafanya wanavyojua vijana wao wakaja nao Dodoma kwenye ujenzi.

Uchaguzi ulipowadia pia wanachukuliwa vijana kwenda kuaribu uchaguzi kwa upendeleo huohuo kua wataajiriwa.

Sasa leo wanawaona kama wanaketa uasi. Swali ni je kwanini hawakushauri Magufuli kipindi hicho kuhusu ajira? wamwambie kua wao wanataratibu zao za kuwapatia vijana wa jkt ajira?
Mambo ni mengi ngoja niishie hapa.
Ni kweli kabisa, mwendazake aliharibu mifumo na taratibu katika taasisi mbalimbali

Kila kitu alikifanya Kama sehemu ya kujipatia sifa na kufanya political propaganda

Na alifanya hivyo kwasababu alijua kabisa hakuna wa kumshauri vingine
 
Ni kweli kabisa, mwendazake aliharibu mifumo na taratibu katika taasisi mbalimbali

Kila kitu alikifanya Kama sehemu ya kujipatia sifa na kufanya political propaganda

Na alifanya hivyo kwasababu alijua kabisa hakuna wa kumshauri vingine
sasa mzee mwendazake anaingiaje hapo wakati alishatoa maelekezo kwa CDF? vijana waajiriwe
 
Back
Top Bottom