Joh Makini, sitokusamehe kwa kutuharibia mziki wetu Nako 2 Nako Soldiers

Joh Makini, sitokusamehe kwa kutuharibia mziki wetu Nako 2 Nako Soldiers

Alfu mbona hip hop saiz ni laini hadi watoto wakike wanapenda miaka hiyo ya nyuma kukuta gal anapenda hip hop ni wachache sana tofauti na saiz kwasababu watu hawaimbi ngumu na ukiimba ngumu hutoboi na ndio maana kuna Trap imeongezeka saiz inawavutia gals kupenda hip hop. Joh makini hana kosa ni muziki umebadilika tu.
[emoji122] [emoji122]
 
Hawa jamaa mashairi yao huwa sielewi wanaimba nini zaidi ya kuchanganya changanya maneno tu.
 
Nako to nako kaskazini. Hii brand eyes akiamua kuiinua hata na vijana wapya haitochukua muda kusimama. Atafute vichwa wa kuirudisha asili ya arusha ya hip hop. Sema uhuni usiwepo
 
Salamu zikufikie,

Unajiita Mwamba, ni kwa ujanja wa nje uliofanikisha kumzima mpinzani baada ya kuangushwa vibaya ulingoni.

Wadau na walio timamu watakumbuka hili, Joh Makini na timu yake River Camp Soldiers. Si ajabu usikumbuke ngoma yoyote kali kutoka kwenye kundi hili, kama ipo tusaidiane.

River Camp Soldiers ikiongozwa na Joh Makini, na mdogo wake Nikki, Bonta na wengine kama wapo (wasiojulikana), haikuwa na maajabu kama kundi.

Sana sana ilitumika kumbeba Joh kwa kiasi kikubwa, huku akiibatiza majina mbalimbali kwa vipindi tofauti (Mfano Good Music Family ‘GMF’ hadi Ngumu Nyeusi ‘WEUSI’) lakini yote haikufua dafu.

Wakati huo akichezea ‘vitasa’ vikali kutoka kundi hasimu Nako 2 Nako Soldiers, likiongozwa na Lord Eyez, G Nako, Bou Nako na Ibra da Hustler.

Kama kundi walikuwa wakitamba kwa kila ngoma waliyoachia, walitamba na hakika walikosa upinzani, labda kwa mbaaali Kikosi Cha Mizinga ya Kalapina.

Kwa uchache tu nikukumbushe ngoma kali kama Ndo Zetu, Mchizi Wangu, Hawatuwezi, Bang! Hapo sijasahau Mchizi Wangu Remix, ni kwa vile nimeahidi kutaja mawe kwa uchache.

Joh Makini aliona kabisa mazishi haya hapa, ikabidi atumie ujanja na akili kubwa ili kujipatia ushindi wa mezani, nje ya uwanja.

If you can’t beat them, join them. Ndiyo turufu aliyotumia Joh Makini.

Akavizia kipindi Lord Eyez yupo ‘high’ kwa mihadarati, akamsajili kiungo wake mchezeshaji G Nako. Na kwa fitina nyingi kuhakikisha timu zinaungana ili awe kiongozi.

Hebu fikiria, Nako 2 Nako imesambaratika kipindi ambacho imepata ‘lebo’ Bongo Records kwa Godfather Majani, hii inawezekenaje!

Na hapo tayari wamesharekodi album nzima, wimbo pekee uliosikika kutoka album hiyo ni HAWATUWEZI, fikiria ngoma kali kiasi gani zimefia studio kwa Majani!

Sasa we jamaa Joh Makini, Mwamba, umeua ushindani kisha ufurahie tu kuwa kiongozi wa kundi lisilo na maana!

Hizi nyimbo zenu uchwara Wapoloo sijui Gere sijui Arosto kabisa unaona ni hadhi ya Lord Eyez au unamkomesha kijanja!

Nako 2 Nako tunawadai ngoma kali, lawama zote ni kwako Mwamba, binafsi sitokusamehe!

Bring back our NAKO SOLDIERS!
Joh makini haez wafikia waturutumbi,watengwa, na katuulia nako to nako yetu. Yani kwa kifupi kina stoper, Davi, jcb,chindo, spacdawg. Na hapo kwenye hiyo weusi ndo anamlalia Isaa( Lord eyes), Isaa sijui kwann haskii anakomeshwa tu pale. Ye ni mkuubwaa kuliko huyo mwamba
 
Kwanini nimtetee? na ili iweje?

Mziki wa Chuga huujui vizuri historia yake. Ibra alijitoa N2N mapema tu wakiwa kwenye harakati za kuzindua album ya Hawahemi street huslers vol 2. Baada ya kujitoa ndio utata ukaanzia hapo. Mnako Lord akakolea kwa Ray C na kwa stress akafundishwa kula kiariri na Ray C (Japo wengi wanasemaga Lord ndio kamfunza Ray C unga) Baada ya hapo ndio Joh akaingilia kati kumchukua G na mwishowe kuunda weusi.
Kweli kabisa. Na Isaa alikanywa Sana kuhusu kiuno bila mfupa hakuskia
 
Alfu mbona hip hop saiz ni laini hadi watoto wakike wanapenda miaka hiyo ya nyuma kukuta gal anapenda hip hop ni wachache sana tofauti na saiz kwasababu watu hawaimbi ngumu na ukiimba ngumu hutoboi na ndio maana kuna Trap imeongezeka saiz inawavutia gals kupenda hip hop. Joh makini hana kosa ni muziki umebadilika tu.

1. Kwahiyo siku hizi girls kwenye hiphop wameongezeka.?

2. Kwahiyo hao wasioimba ngumu ‘wangapi’ wametoboa.?
 
Back
Top Bottom