Leo nimeangalia kipindi cha Bunge na kushangazwa na hoja ya Kishoa kuhusu uhalali ama uharamu wa ubunge wao!
Mbunge Kishoa alikuwa akitetea hoja ya Chadema kuzuiliwa kufanya mikutano yao.
Katika kutetea hoja, kajikwaa ulimi na kusema: 'kabla sijafukuzwa Chadema'..... hapo ndipo tatizo lilipoanzia na ndipo nilipoona tatizo.
Naibu spika Tulia akamwambia kuwa atengue kauli yake hiyo ya kufukuzwa, kwa sababu kanuni zilizopo haziruhusu mbunge kutokuwa ama kutotokea kwenye chama chochote cha siasa, mbunge Kishoa akatengua kauli na kuthibitisha kuwa hajafukuzwa uanachama.
Maswali yafuatayo yakajitokeza kichwani mwangu haraja haraka: je ni kweli hawajafukuzwa uanachama officially?
Kama walifukuzwa, je chama hakijapeleka nakala ya barua ya hatua hiyo kwa spika?
Je kama walifukuzwa uanachama, kwa nini wanaendelea kukitetea chama kilichokwisha wafukuza?
Je kama madai ya naibu spika yakawa na ukweli kuwa hawajapata barua ya kufuzwa uanachama wabunge hao, kwanini Chadema wasiandike tena barua rejea ya ku confirm hatua yao hiyo na kwenda kuikabidhi kiofisi?
Ninaomba kufahamishwa juu ya 'kakaenda kakarudi' na mustakabali wa seke seke hili la hawa wabunge 'Covid-19'.