John Mnyika, Sio rahisi CHADEMA kuendelea kuwa chama kikuu cha upinzani na kinachochochea maendeleo bila kuzingatia haya

John Mnyika, Sio rahisi CHADEMA kuendelea kuwa chama kikuu cha upinzani na kinachochochea maendeleo bila kuzingatia haya

Issue mleta mada anampigia mbuzi gitaa.Hayo aliyoshauri chadema wameshauriwa Sana wakaziba pamba masikioni.Sasa watakumbuka shuka wakati kumekucha?
Mkuu Yehodaya, hili la Chadema kukumbuka shuka kumekucha hata mimi nililisema hapa
QUOTE="YEHODAYA, post: 35565584, member: 315573"]
Hiki chama kilijitaji sura mpya kukirudisha enzi za dk slaa kinaenda kuwafia akina Mbowe mikononi mwao na halima mdee wake
[/QUOTE]Duh...!. Hapa umechapia!.
Kwenye kusoma maandishi ya mwandiko wa mkono, kupitia kitu kinachoitwa graphology, unaweza kubaini gender ya mwandishi na emotions zake wakati anaandika, lakini unapotumia keyboard kuandikia ni ngumu ku detects. Lakini kupitia hiyo last sentence yako, nine detects yafuatayo
  1. Naijua Gender yako!.
  2. Anamzimikia sana M!.
  3. Kuna uwezekano M. ali...na kuku dump, hivyo you are hurt!.
  4. Hivyo baadhi ya comments ni za mtu bitter anayelia wivu!.
  5. Kufuatia kumpenda sana M, unajikuta una mhate yoyote aliye karibu na M.
  6. Hivyo unamhate H kwasababu yuko close to M.
  7. Ikitokea chance ya kumflict pain kwa M, you inflic!.
  8. Ushauri kwa watu close to M. mwambieni amtafute huyu member Y to set the scores wamalizane yaishe vinginevyo...!.
NB. Sometimes graphology get it wrong, mfano kwa muda mrefu nikimsoma humu member anayeitwa Wakudadavuwa, graphology zilielekeza Wakudadavuwa ni female, hadi alipojitambulisha rasmi kuwa yeye ni male na ni mkubwa kwangu from then nikajua kumbe graphology sometimes get it wrong, toka pale nikawa namuadress as Kaka mkubwa Wakudadavuwa, na nikajikuta sikuwa peke yangu, Luna wengi walidhani Wakudadavuwa ni she, kumbe ni he, hivyo hii gender yako niliyoibaini kupitia graphology might be sio!.
P
 
Huu ni waraka wazi kwa John Mnyika Kama katibu mkuu mpya wa CHADEMA, Katika mazingira yaliyopo kunakitu Chadema kimekosa na kinaitaji marekebisho kadhaa ili kwa uwazi kionekane ni chama Cha kuwasemea watu na sio kukosoa tu na hivyo kuonekana ni chama adui kwa jicho la usalama na ustawi wa nchi

Kuna vitu vitatu muhimu CHADEMA inapaswa kuchukua hatua ili kuwa chama chenye nguvu zaidi.

1. Kiache kuwa chama Cha kupiga majungu au kutoa ukosoaji au propaganda Bali kiwe NI chama kinachoweza kutoa na kuzitangaza Sera zake mbadala bila kukashifu au kutukana mtu.

Wanao wajenga Sera wazuri, pia watumie wataalamu kuona namna Bora ya kusimama na kueneza Sera zao vizuri. Sera zao zikiwa wazi, nzuri na zinazoeleweka kunakuwa hakuna haja ya kuwa na akina kigogo au kimambi hakika chama kitajitangaza chenyewe.

2. Kiwe na majibu ya kero za watu sio kulalamika bila kuweka suluhisho wazi. Lazma waoneshe watu vipi wanaweza kuongoza, Mfano kwenye swala la kikokotoo ni busara za Bulaya na Mnyika kutoa hoja bila kutukana Wala kukashifu ziliwasaidia wastafu kwani Raisi aliwasikia na kuchukua hatua.

Unapokuwa chama pinzani lazma ufurahie matatizo ya watu yakitatuliwa kupitia Kazi yako ya siasa na sio kufuraia watu kuumia ukijipa moyo eti ni mtaji wa kisiasa. Pamoja na matatizo mengi kufanyiwa Kazi lkn upinzani umekua Sana nchi za Magharibi sababu vyama vinajitangaza kwa Sera Safi. Sikufuraia kabisa jinsi mdee alivyozifunga hoja za umuhimu ya watoto wa kike kuendelea na masomo kwenye furushi la kashfa, zarau na kejeri kisa tu anaamini havunji Sheria

3. Kije na majibu ya kero zote za watu, Nchi zinazoendelea ata Kama kiongozi akiwa mzuri vipi kero hazikosekani na NI nyingi mno. Cha kushangaza CCM kimekuwa aware na kero na kujua maisha ya watu kuliko ata upinzani. Bei ndogo ya mazao, mifumo mibovu ya ununuzi mazao,Bei Kali za viwatilifu,pembejeo na mbegu.

Haiwewezekani Bei ya kg moja ya mbegu ya mahindi iwe ZAIDI ya Bei ya debe mbili au kg 40 za mahindi. Mnakuja na wazo gani hapo. Inakuwaje land Locked country Kama Uganda kuwa na Bei nzuri ya bidhaa za viwandani kutoka nje, Bei juu ya mazao Kama kahawa Hadi watanzania tuna karibu kupeleka kwao kimagendo. Nje na utafiti NI kwanini iko ivyo na mtabadili vipi Mambo....

4. Msije na Sera kwenye misaafu watanzania hawawezi kusoma misaafu. Andaeni vijarida vyenye maelezo machache na picha. Fanyeni Kama wamisionari walivyoandaa vijitabu v na vijarida vya hadithi za biblia ili watu ziwafikie kila Kona. Mfano mnaweza kuandaa vijarida vidogo Kama Ishirini tofauti vyenye vipande vya Sera kwenye kundi Fulani la watu.

Mfano watumishi wa umaa, wafanyakazi sekta binafsi, Wakulima wa mazao tofauti Kama pamba, tumbaku, kahawa, Michele, mahindi, korosho, choroko,alizeti. Mfano Chadema na Wakulima wa pamba, Mnaonesha kero zao,mfano kuanza kukopwa, urasimu wa ushirika, viwatilifu kuwa Bei juu na mbegu Bora. mlichopanga kuwafanyia kuondoa kero mfano Bei ya pamba kutajwa kabla ya kuanza kulima, kugawa viwatilifu na mbegu bure kwa kufidia kwenye tozo, kuruhusu wanunuzi huru bila kulazmisha ushirika, (Nasisitiza utafiti NI kitu Cha msingi hapa) na kuzitatua na kuzigawa sehemu wanakolima pamba.
Vijarida hivyo viwe huru kupigwa kopi na kugawiwa watu husika. Napenda upinzani unaoanika Sera sio mivutano kila siku.

5. Cha mwisho na muhimu kuliko vyote jaribu kuepuka hasira na visasi kwenye kampeni na kuhakikisha wagombea wenu ata moja hakatwi. Ukiongozwa na hasira Huwezi kufanya lolote.

Naamini kinachoweza kuwabeba sad NI Sera Safi na namna Bora ya kuzifikisha kwa walaji kwa kuzingatia Hali halisi
Kumbuka hata mikutano ya ndani tu ya CHADEMA ambayo ingejadili hayo maoni yako inavamiwa. Hayo yatafanyika wapi?
Ruhusu uwanja wa siasa uwe huru kwa vyama vyote naamini hizo hoja zako sio sababu na hazina mashiko kabisa.
 
Shida ya Chadema nyingine kuu NI kuwa na watu waropokaji, wenye hasira, walizimishajj na sio wajenga hoja. Nje labda ya hasira zidi ya watawala Chadema imewezaje kuanika Sera na mitazamo inayoamini kwenye jamii yenye uelekeo wa kutatua kero zao ZAIDI ya kusema tunataka ikulu. Nje kwa hoja Kama wasomi sio hasira
Kwahiyo ccm kuna wajenga hoja WAzuri?

Kwa nini hukemei wanayofanyiwa ni vyombo vyenu vya dola.

Ccm haina uwezo wakushundana bila usaidizi WA vyombo vya dola.
 
Mkuu William Mushumbusi, bandiko lako hili, neno!. Kwanza naunga mkono hoja, na kukupongeza kuishauri Chadema kwa nia njema kabisa at this critical moment kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa rais na wabunge mwezi October mwaka huu ambapo ni miezi miezi 4 tuu imebaki kufikia uchaguzi.

Japo umependekeza mambo mengi makubwa na mazuri, lakini kwa muda uliobaki, it's already too little too late kwa Chadema kujiokoa na kuendelea kuwa chama kikuu cha upinzani kwa huku Tanzania bara, kwasababu ya kiburi tuu na jeuri yake kwa kutia pamba masikioni na kutosikiliza ushauri wa yeyote, hivyo kwa muda huu, kwa vile tayari imeisha ona dalili za kwenda kuwa wiped, katika kutapatapa kujiokoa labda this time wanaweza kusikia ushauri wako huu.

Hizi ni shauri mbalimbali kwa Chadema toka 2010 kwa ajili ya uchaguzi wa 2015, na 2015 kwa ajili ya uchaguzi wa 2020, na kila kwenye ushauri, niliweka faida za kufuata ushauri huo kwa kuonyesha matokeo chanya tarajiwa na pia kuweka angalizo la the consequences za kupuuza ushauri huo.

If you have time

Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition?!.

CHADEMA msipuuzie ushauri hata kama ni kutoka kwa shetani!, S'times the devils does good deeds!.

CHADEMA ni sikio la kufa? Iambiwe vipi ili isikie? Masha ana hoja za msingi, zisikilizwe, zizingatiwe, zisipuuzwe!

CHADEMA Hamkujipanga, hamjajipanga, hamjipangi na hamtajipanga!-2015 ni CCM tena!

Wito CHADEMA: Kuweni na Shukrani, Punguzeni Kulalamika, Shukuruni kwa Yote. Ile Kesi Mbaya! Shukuruni Mahakama, Mashinji, CCM, Magufuli na Watanzania.

Upinzani Tanzania una matatizo? Vyama havina Succession Plan hivyo vina Usultani! CHADEMA kuna Usultani? Usultani huu Utakiinua au Utakiangamiza?

Uchaguzi wa 2020, Kukumbuka shuka kumekucha, is it too little too late kwa CHADEMA or better late than never?

Wish you all the best ushauri wako kufuatwa.
P.
Mimi ningeiona ccm imara inapotumia hoja madhubuti bila vyombo vya dola. Msikilize Bashir u alishaeleza jinsi ccm inavyobakiadarakani.
 
Pamoja na mambo ya kununuliwa kwa baadhi, chadema ijitathimini kujua walikosea wapi na kufanya marekebisho. Tatizo ushabiki unasababisha watu kutokuona pale penye mapungufu.
 
Chadema imekuja kufa kwa aibu sana
Ikifa wewe matanga unaumia nini? Nadi sera zenu then wekeni tume huru muone kama fisiemu hatujawazika mapema sana. Ccm ndiyo chama kilichokufa ila kimebaki kutumia dola kubaki madarakani(katibu wenu wenu ni shahidi)
 
Shida ya Chadema nyingine kuu NI kuwa na watu waropokaji, wenye hasira, walizimishajj na sio wajenga hoja. Nje labda ya hasira zidi ya watawala Chadema imewezaje kuanika Sera na mitazamo inayoamini kwenye jamii yenye uelekeo wa kutatua kero zao ZAIDI ya kusema tunataka ikulu. Nje kwa hoja Kama wasomi sio hasira
Mbona wewe hujaja na hoja za chama chako? Kila siku mnawaza chadema tu,
 
Shida ya Chadema nyingine kuu NI kuwa na watu waropokaji, wenye hasira, walizimishajj na sio wajenga hoja. Nje labda ya hasira zidi ya watawala Chadema imewezaje kuanika Sera na mitazamo inayoamini kwenye jamii yenye uelekeo wa kutatua kero zao ZAIDI ya kusema tunataka ikulu. Nje kwa hoja Kama wasomi sio hasira
Mtu uliyetimamu unawezaje kuhangaika kiasi hiki na chama kilichokufa? Lazima kiwe Kinakunyima usingizisi bure
 
Usiende mbali na kuzungumza jumla jumla. Tupime mmoja mmoja kuanzia juu kuja chini kufikia wewe na mwanachadema mwingine.
Linganisha wenyeviti wa CCM na Chadema katika kutoa hoja, kuropoka na hasira jee unapata jibu gani? Nani una mpa credits? Bila shaka Freeman anashinda kwa knockout.
Mnyika waweza mlinganisha na Bashiru kwa kutoa hoja za kumsaidia mwananchi? Hapana maana huyu mmoja ana kiburi cha madaraka na dharau hivyo Mnyika yuko juu.
Ukija chini uliko wewe ndio taabu tupu sipati wa kukulinganisha naye maana ujuacho in kusifu tuu
Well said mkuu
 
Ebu shauri na upande was pili wasitumie polisi na mahakama kuwakwamisha kina Mnyika kufanya kazi na kutekeleza ushauri wako
Wakina Mandela walifanya siasa kwenye utawala wa kikatili na wakibaguzi na waliweza kuleta mabadiliko. Dira kuu ya chama ikiwa NI kuyasemea matatizo na kero za watu, kusahau misukosuko ya kisiasa na kutokuwa na hasira. Ata polisi watakuwa upande wenu kwani mkifanya Kazi kiuchunguzi mtajua kero zao na mtakuwa sauti yao.

Mandela alisema kiongozi lazma ajifunze kutochukia. Mnachuki kubwa na utawala na ccm na hapo ndipo mlipozidiwa Akili. Mmeshindwa kuwasemea watu mnajipigania wenyewe tu. Hivyo ukweli ZAIDI ya 90 hawaelewi mitazamo yenu halisi Ila wapo kwenu kwa chuki binafsi dhidi ya Hali ya maisha. Lazma muadress changamoto za watanzania na namna ya kuzitatua swala la sijui tumepigwa risasi , tumefungwa viwe vibwagizo ttu vilivyosheheneshwa na hoja Nzito.
 
Ushauri wa kipimbi wapelekee wenzio wa lumumba...hatuhitaji ushauri wa kibwege
 
Back
Top Bottom