John Mnyika: Watu wenye silaha wamemchukua Mwanachama wa CHADEMA, Mdude Nyagali (Mdude CHADEMA)

John Mnyika: Watu wenye silaha wamemchukua Mwanachama wa CHADEMA, Mdude Nyagali (Mdude CHADEMA)

Kila siku wanapotea na hawarudi na wala hakuna mtu anayejali. Hatari sana
 
Walikuwa wametulia ..!!

Watasema eti CDM ndio wamemteka
 
Mbunge wa Kibamba kupitia CHADEMA, John Mnyika kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Twitter amesema kuwa Chadema Mdude amechukuliwa na Watu wenye silaha

Aidha, yeye mwenyewe amesema CHADEMA inafuatiloa suala hilo na taarifa zaidi itatolewa muda si mrefu
______

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

TAARIFA ZA AWALI KUHUSU TUKIO LA MDUDE NYAGALI (MDUDE CHADEMA)

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), katika hali ya dharura, kinafuatilia kwa karibu, taarifa za Mdude Nyagali (Mdude Chadema) kuvamiwa kisha kuchukuliwa na watu ambao hawajatambulika, akiwa ofisini kwake, eneo la Vwawa, Mbozi, mkoani Songwe, katika tukio lenye dalili za utekaji.

Kwa mujibu wa baadhi ya mashuhuda, majira ya jioni ya leo (saa 12 kuelekea saa 1) yalifika magari mawili katika eneo la ofisini kwa Mdude, Vwawa mjini, kisha wakatelemka takriban watu wanne, ambao walimkamata kijana mmoja aliyekuwa nje ya ofisi hiyo wakampeleka kwenye mojawapo ya magari waliyokuja nayo huku wengine wakiingia ndani ya ofisi, alikokuwa Mdude.

Imedaiwa kuwa baada ya muda mfupi kulisikika purukushani, watu hao wakijaribu kumkamata Mdude huku wakimpiga na yeye akipiga kelele za kupinga kitendo hicho na kuomba msaada.

Taarifa za awali ambazo Chama kimezipata kutoka kwa mashuhuda hao zimedai kuwa baada ya kusikika kwa purukushani na kelele hizo, baadhi ya wananchi walijitokeza kutaka kujua kinachoendelea na kutoa msaada, ghafla watu hao waliokuwa wakimpiga Mdude wakatoa silaha aina ya bastola na kuwatishia wananchi hao, kitendo kilichowaogofya wananchi na kukimbia kwa hofu. Imedaiwa kuwa watu hao walimuingiza Mdude kwenye 'buti' ya mojawapo ya gari hizo, wakamuachia yule kijana mwingine kisha wakaondoka na Mdude kuelekea kusikojulikana.

Tayari CHADEMA kupitia kwa Viongozi wa Chama katika eneo husika na Mbunge wa Mbozi Mashariki, Pascal Haonga, kimevitaarifu vyombo vya dola mkoani Mbeya, kwanza kutoa taarifa ya tukio hilo lenye mazingira ya utekaji pia kutaka kujua kama kuna askari waliopewa kazi ya kwenda kumkamata Mdude.

Hadi sasa haijulikani Mdude yuko wapi! Tupaze sauti zetu sote kulaani tukio hili na kutaka Mdude arudishwe au aachiliwe akiwa salama.

Katika hatua ya sasa, CHADEMA kwa nguvu zote kinalaani vikali tukio hilo. Tunavitaka vyombo vya dola, hususan Jeshi la Polisi lenye wajibu wa kulinda raia na mali zao, kufuatilia taarifa za tukio hilo kama zilivyoripotiwa kwa polisi katika eneo husika na kuhakikisha Mdude anapatikana na wahalifu waliotenda tukio hilo wanajulikana, kukamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.

Tutaendelea kuwapatia taarifa zaidi kadri itakavyohitajika.

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

View attachment 1088177
CHADEMA HAMUWAJUI WALIOMTEKA MDUDE KWELI? HAMUWAJUI TISS WANAOTEKA WOTE WANAOMKOSOA JPM?!!
ACHENI KUSEMA WATU WASIOJULIKANA SEMENI MOJA KWA MOJA NI TISS INATAKA KUNYAMAZISHA WATU.
KUMBUKENI MTU AKISHAKULA NYAMA YA MTU HAACHI, HUYO MTU ATAUA CHADEMA AKIWAMALIZA ANAHAMIA KWA CCM WENZIE, TIME WILL TELL!.
 
SHETANI HANA URAFIKI, ENDELEA KUMSUJUDIA IPO SIKU UTAJUA RANGI YAKE HALISI. MUULIZE NAPE, KINANA NA JANUARY WATAKWAMBIA!
Nissan ya Mbowe baada ya kumshughulikia Lisu kwa jina bandia imerudi kivingine tena?
 
Wasiojulikana kile kitengo maarufu cha Dikteta pale Ikulu ili kuwanyamazisha wanaomkosoa kwa kuwateka, kuwatesa na hata kuwaua kimeibuka tena kwa kasi ya kutisha.
Mwenzao kafa juzi Muhimbili pale.....we ngoja tu
 
"Ukishaonja nyama ya mtu huachi," aliwahi kusema Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (RIP). Kwa sasa idadi ya walioonja nyama ya Watanzania wenzao yaonekana inaongezeka kwa kasi ya kutisha awamu hii..je kwa kasi hii tutabaki salama?
Tutabakije salama wakati mtu mwenyewe hataki kuachia Uenyekiti!
 
Hii ya awamu ya tano kiboko, Boss anaamuru MTU anayemfanyia fujo kwenye mkutano wake awekwe ndani, huku vijana wanaojulikana wanamteka kada kupelekwa ndani. Ila CHADEMA waki-survive awamu hii hakuna system itakayo wapoteza tena mpaka mwisho wa dahari.
 
Nissan ya Mbowe baada ya kumshughulikia Lisu kwa jina bandia imerudi kivingine tena?
Vita ya uenyekiti wa chama itamaliza wengi.

Itaweza tembea Bila plate no kweli, ngoja tusubirie ccctv za ofisini kwake zitatuonyesha tukio lote
 
Hii ya awamu ya tano kiboko, Boss anaamuru MTU anayemfanyia fujo kwenye mkutano wake awekwe ndani, huku vijana wanaojulikana wanamteka kada kupelekwa ndani. Ila CHADEMA waki-survive awamu hii hakuna system itakayo wapoteza tena mpaka mwisho wa dahari.

True,upinzani still wameshindwa kuumaliza kwa mujibu wa ilani yao.Mikutano watu wanajaa kufata Pesa
 
Atakuwa kadhulumu watu huyo, acha wamshikishe adabu
Sawa mkuu, ila naomba utafakari methali ya kiswahili isemayo: "tumbili akisha miti, huja mwilini!" na "alieko juu, mngoje chini". Mambo hugeuka mkuu, kuna leo na kesho pia, mimi na wewe ya kesho hatuyajui!
 
Back
Top Bottom