John Obi Mikel: Familia za Kiafrika zinachangia kuwavuruga Wachezaji waliofanikiwa kifedha

John Obi Mikel: Familia za Kiafrika zinachangia kuwavuruga Wachezaji waliofanikiwa kifedha

Umesikiliza interview yake yote???
Jinsi familia yake ilivyompangia majukumu na wanavyo mfanya jamaa??
Utajiri wa huyo kijana ni Dola million 45, hii ni zaidi ya bilioni 100. kwetu sisi tuliozaliwa africa, hata ukitoa tu bilioni 10 out of 100 kusaidia ndugu zako, una hasara gani?

Unamkumbuka Chavez, yule wa Mancity, aliondoka kwenda uarabuni au china kama sikosei, kwa sababu tu ya pesa ndefu waliyomwahidi, akaipata, alienda kununua mtaa, akabadilisha nyumba zote zikawa za kisasa akagawia ndugu zake. hizo bilioni zote atakufa nazo?
 
Obi mwenyewe anaongea ivyo kwa sababu yeye katoboa vinginevyo na yeye angekua anapiga mizinga ndugu waliotoboa. Mifumo ya maisha yetu Afrika haipo vizuri katika kumwezesha mtu afikie potential yake kwaiyo kufanikiwa ni kama bahati nasibu tu. Ukifanikiwa wainue ndugu zako hao wazungu tunaotaka kujifananisha nao wao maisha yao yapo systematic kuanzia mtu anapozaliwa mpaka anafikia kujitegemea.
Unahoja mkuu
 
Kuna ndugu yangu alienda Germany akaoa hukohuko akaileta familia yake bongo alipoondoka ndiyo mpaka leo inawezekana sababu ndiyo hiyohiyo: uchawa kwenye mafanikio ya watu mpaka watu wanajitoa kwenye ukoo, hahah!
 
Utajiri wa huyo kijana ni Dola million 45, hii ni zaidi ya bilioni 100. kwetu sisi tuliozaliwa africa, hata ukitoa tu bilioni 10 out of 100 kusaidia ndugu zako, una hasara gani?

Unamkumbuka Chavez, yule wa Mancity, aliondoka kwenda uarabuni au china kama sikosei, kwa sababu tu ya pesa ndefu waliyomwahidi, akaipata, alienda kununua mtaa, akabadilisha nyumba zote zikawa za kisasa akagawia ndugu zake. hizo bilioni zote atakufa nazo?
"Mtegemea cha ngugu hufa masikini."

Kwanini upigie hesabu pesa ambazo haujazifanyia kazi? Mtu kuwa tajiri kwenye ukoo haimaanishi ndiyo wote mpeleke shida zenu kwake. Zipo familia nyingi tu unakuta kuna mtu ana uwezo mkubwa kifedha ila kila mtu na maisha yake, kusaidiana ni kwenye shida za kifamilia na siyo kupiga simu kila saa kuanza kusumbua watu na familia zao.
 
Afrika tumelaaniwa walah,sio wanasoka tu mtu yeyote akifanikiwa iwe kwenye kazi au biashara akionekana na unafuu wa maisha tu ndugu hata wale wenye undugu wa mbali wanaanza na wao kutaka haki ya kuwa sehemu ya mafanikio yako,mizinga haiishi nk
Huu ni utamaduni ambao tumeshauzoea. Kuondokana nao itachukuwa muda sana. Kwenye familia mmoja akifanikiwa wengine wote wanataka mgao.
 
Ndio maana Waafrika wakifika Ulaya, Marekani, Canada na nchi nyingine za wazungu wanapata shida sana kuishi,
Wenyewe wanasema hakuna maisha ya ujamaa na community!
Mfano mzuri ni Bill Gates ana utajiri unaokadiriwa kuwa ni $133 billion ila dada yake, Kristianne Gates ana $1 million.

Sasa Africa wanataka hizo $133b kila mwanafamilia apate mgao. Wenzetu wanaishi maisha ya kujitegemea sana kiasi kwamba watoto nao wanarithi mfumo huo wa maisha.
 
emmanuel adebayor aligombana mpka na mama yake mzazi na ndugu zake karibia wote.

ishu yake ilienda viral sana .
wengine ambao nimewahi wasikia
kuna
michael Essien
paul pogba nk
Samatta pia kwenye kipindi cha "Salama Na" alisema vizinga kutoka kwa ndugu ni vingi sana ikabidi amkatishe Salama hiyo mada akihofia itamletea matatizo na ndugu. 😁
 
Utajiri wa huyo kijana ni Dola million 45, hii ni zaidi ya bilioni 100. kwetu sisi tuliozaliwa africa, hata ukitoa tu bilioni 10 out of 100 kusaidia ndugu zako, una hasara gani?

Unamkumbuka Chavez, yule wa Mancity, aliondoka kwenda uarabuni au china kama sikosei, kwa sababu tu ya pesa ndefu waliyomwahidi, akaipata, alienda kununua mtaa, akabadilisha nyumba zote zikawa za kisasa akagawia ndugu zake. hizo bilioni zote atakufa nazo?
Mkuu umesikiliza interview yake. Ishu sio msaada ishu ni majukumu.
Kapewa yeye. Ukute dada yako kazaa na wanaume 4 tofauti na wapo na maisha yao. Ila majukumu ya kulea umepewa wewe , why? Jibu hio.
Na ukute unadada 2 hapo au 3.
Unajua majukumu??
 
Ndo maisha ya waafrika mtu una hangaika , unateseka saa nyingine unakutana na kifo uso kwa uso kuyatafuta mafanikio.
La kushangaza ukisha yapata hayo mafanikio ndugu wanarazimisha yawe ya ukoo mzima.

Hapa Africa usipo kuwa mnonko utoboi.
Mbaya zaidi ukiwa umefanikiwa peke yako katika familia ya watoto kadhaa ni balaa. Utakuta wengine wanakuomba fedha eti Baba yetu alikusomesha. Sasa la kujiuliza, kwani ulimkataza Baba yako asiwapeleke shule? Kwa kweli Waafrika tunatakiwa tubadilike.
 
Obi mwenyewe anaongea ivyo kwa sababu yeye katoboa vinginevyo na yeye angekua anapiga mizinga ndugu waliotoboa. Mifumo ya maisha yetu Afrika haipo vizuri katika kumwezesha mtu afikie potential yake kwaiyo kufanikiwa ni kama bahati nasibu tu. Ukifanikiwa wainue ndugu zako hao wazungu tunaotaka kujifananisha nao wao maisha yao yapo systematic kuanzia mtu anapozaliwa mpaka anafikia kujitegemea.
Hata huku tunaweza kuweka mifumo bora itakayotusaidia.

1. Elimu bora.

2. Dhana ya kuwa kila anayesoma lazima aajiriwe ibadilike vichwani mwa watu. Shule zianze kuandaa watu ktk fani zote: mitaala ya elimu iangaliwe upya.

3. Elimu ya fedha.

4. Watoto wafundishwe kujiamini (sna hakika kama hili ni somo). Ila kwa % kubwa Africa vijana wengi hawajiamini. Ndiyo tunaishia kuwa na taifa la watu wa kubahatisha. Mafanikio siyo bahati.

Ila vyote hivyo ni ngumu kutimia kama bado shule zetu za msingi zinaweza kutoa wahitimu wasiojua kusoma na kuandika.
 
Kiungo wa zamani wa Chelsea na Nigeria, John Obi Mikel amedai Waafrika wengi waliofanikiwa kiuchumi wanakumbana na presha kubwa kutoka kwa Familia wakitakiwa kutoa msaada wa fedha kwa lazima na wasipofanya hivyo wanaonekana wabaya na wengine wanapewa vitisho.

Anasema "Hatuzungumzi sana kuhusu hili lakini linawaharibu Wachezaji Kisaikolojia, ukipata fedha zinakuwa sio zako ni za ndugu, Binamu na wengineo, ni tamaduni isiyofaa, tuwaambie wachezaji wanaochipukia kuwa wanatakiwa kuwa imara na maamuzi ya fedha zao.”

Anadai alikuwa mhanga wa hali hiyo kuanzia alipoanza kufanikiwa kisoka, miaka mitano iliyopita aligeuka kuwa adui kwa ndugu baada ya kusitisha kutoa fedha.

---------------

John Obi Mikel on African players sending money to family back home

John Obi Mikel says African footballers are effectively subject to an extra tax as they often support extended family and hangers-on back home.

The former Chelsea and Nigeria midfielder has claimed some players are even "threatened by their own blood" if they do not offer financial assistance.

"When you come from Africa - and this is something I don't think we speak a lot about - when you make money, it is not your money," said Mikel, speaking on Rio Ferdinand's Vibe with FIVE.

"You have all these relatives, cousins, whatever.

"Your sisters, they go off and get married to some guy. He just wants to get married into John Obi Mikel's family because then [he thinks] 'my life is sorted'.

"You start looking after this guy and you send money to your sister and the money goes to him and he does whatever he does with it.

"This is the thing nobody knows about - your money is not your money.

"You get a salary and say 'I'll put this aside for this person, put that aside for that person, and put that aside for my mum and dad'. Before you know it, you are getting less than them.

"That is the culture. They expect you to do that. For them, you owe them.

"This story needs to be told. A lot of young African players that are coming up now need to be told this because they will go through similar situations.

"They will need to know how to deal with this."

Mikel says players have to be strong if they decide to stop assisting others financially, as there can be a backlash.

"Sometimes you have to say 'Enough is enough, I don't care'. For me that moment came about five years ago," the 36-year-old added.

"I said 'No more', because I have been doing this since I started playing football.

"You become the bad guy. They stop answering your phone calls. They are used to calling you - not to check up on you but to ask 'What are you giving me?'.

"You have to be strong enough. I was giving so much to the family.

"All you do is keep giving and they are so comfortable that they expect you to do that for the rest of your life."

Mikel says players could even be emotionally blackmailed.

"They give you this thing whereby 'If you don't do it [pay], we are going to go to the press'.

"You are thinking, 'You are family. After all I've done for you guys?'.

"In Africa not everybody comes out and speaks about this, because we think 'How are we going to talk about this?'.

"You get threatened by your own blood."

Source: BBC
100% truly.
 
Afrika tumelaaniwa walah,sio wanasoka tu mtu yeyote akifanikiwa iwe kwenye kazi au biashara akionekana na unafuu wa maisha tu ndugu hata wale wenye undugu wa mbali wanaanza na wao kutaka haki ya kuwa sehemu ya mafanikio yako,mizinga haiishi nk
Hatujalaaniwa, tumejilaani wenyewe. Hata hivyo jamii zinatofautiana sana hata hapa TZ. Kuna jamii ukioa huko umeoa ukoo mzima.
 
Inaonekana na wewe ni ombaomba kama anaowasema obi.
Chanzo cha umaskini wa Afrika ni utamaduni unaoutetea huwezi mtegemea mwenzako afanye kazi alafu wewe upewe tu ukimaliza unaomba tena huo ni utahira umaskini hauwezi kuisha
Unapumuliwa kisogoni? Wapi nimesema mtu awe omba omba. Afrika kutoboa ni kibahati sio kimfumo kwaiyo ukifanikiwa jitahidi kuwainua wengine nyumbani
 
Back
Top Bottom