Joseph Butiku: Vyombo vya Ulinzi na Usalama visijifanye havijui mambo yanayoendelea nchini

Joseph Butiku: Vyombo vya Ulinzi na Usalama visijifanye havijui mambo yanayoendelea nchini

Mzee Butiku ana busara sana na anawafahamu waandishi wetu wa habari na tabia zao hivyo amezungumza kwa level yao.

Hawezi kufunguka sana maana kitachoandikwa kesho chaweza kuwa ni kitu kingine.

Ila Mzee Butiku na mzee Warioba, Jenerali Ulimwengu na Issa Shivji na watu makini sana na wana hazina ya maarifa.

Kawapa homework wamtafute waziri Masauni wamhoji na hii ndo opportunity kwa Mr Odemba kuitumia.
Lakini tunataka wauaji na waliowatumwa wakamatwe na kuwekwa nguvuni.

Kuuwa kwa kumtoboa mtu macho asiye na hatia macho ni unyama mkubwa kuzidi wa Idi Amin
 
Kweli vilikuwepo vikundi vya vijana wa chama cha NAZI cha Hitler na mamluki wa kigeni ndani ya GESTAPO SS waliofadhiliwa na kuratibiwa na machawa wa Hitler ambao waliogopwa na Polisi pia kuogopwa na jeshi rasmi.

Hili kundi la TASK FORCE la paramilitary la watu wasiojulikana Tanzania litakuwa limeundwa kwa mtindo huo huo wa GESTAPO na SS
Mungu atulinde
 
Huyu mtu Maliyamungu wa Tanzania na wenzie, inatakiwa apatikane, hata kwa kutolewa 'sadaka' si kwa kuuawa bali wafikishwe mahakamani na kuhukumiwa baada ya vyombo rasmi vya ulinzi na usalama kupewa meno kuwakamata ili amiri jeshi mkuu asalimike na fedheha hii kwa taifa, ijulikane kama je viliundwa na mtangulizi kiasi rais aliyepo anaagwaya kuvikabili.

Lakini umma wa ndani tayari kupitia kelele za wananchi zinampa mamlaka rais awashughulikie kwa mujubu wa sheria Maliyamungu na wavuta bangi wenzie wote waliopo katika Task Force.

Sidhani kama ni wavuta bangi. Ni watu na akili zao ambao wamedhamiria kutishia umma wasijihusishe na siasa za upinzani.
Kuna kosa gani kuwa na mawazo tofauti, kama mtu havunji sheria na taratibu? Haya mambo ya kulazimisha kila mtu awe anaunga mkono juhudi, yalifanya USSR isambaratike. Maana nguvu zote walikuwa nazo watu wachache na walizitumia vibaya.
Putin mpaka leo anateseka na ndoto na ujinga ule. Anataka USSR irudi ilhali ilishaenda na ujinga wake. Jamii yetu isijiingize kwenye mtego kama ule. Tujenge nchi yenye kuheshimiana na kuheshimu sherai na taratibu.
Na hakuna mtu aliye juu ya sheria. Hata ukiwa unafanya kazi gani, bado hakuna aliyekupa mamlaka juu ya sheria. Tusijisahaulishe au kujizima data, tukaiharibu nchi yetu kwa ujinga wetyu wenyewe
 
Nchi nyingi zinazoelekea kwenye machafuko dalili zake huwa ni extrajudicial killings na kupotezwa kwa raia na mambo kama hayo.
Bangladesh ni mfano mmojawapo na mwishoe waziri mkuu Hasina akasepa.

Katika utawala wa Hasina, watu watatu tu kati ya 150 ndo walopatikana baada ya kutekwa na kupelekwa kusojulikana.

Leo hii kasepa watu hao watatu wamepatikana na wameungana na familia zao huku wale 147 ambao wamepotezwa mazima wakiwa ni historia.

Bangladesh wao wana magereza ya siri (secret prisons) zinoangaliwa na wanajeshi wa Military Intelligence na watu zaidi ya 700 walipotelea huko.

Na hawa wahindi weusi wana roho mbaya kupita kiasi na siku walipoingia barabarani Hasina hakuwa na chance akasepa na chopa kwenda India hadi leo yuko huko.
 
20240910_122533.jpg
 

TAARIFA YA TAASISI YA MWALIMU NYERERE KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU TABIA MBAYA ZINAZOHATARISHA USALAMA WA MAISHA YA WATANZANIA NA MALI ZAO

Ndugu wanahabari nimewaiteni hapa, kuwaombeni kwanza; muisaidie Taasisi ya Mwalimu Nyerere kuwataarifu Watanzania wote na kuwaomba sisi sote tushirikiane kuunga mkono kwa dhati Rais wetu Mhe. Dr. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada anazofanya za kukomesha tabia mbaya zilizozuka katika Taifa letu za kulawiti, kuteka, kunyanyasa na kuua Watanzania wenzetu.

Tunaye Rais mmoja tu sio wawili wala watatu tuliye mkabidhi Katiba ya nchi yetu ili aitumie kuongoza Taifa letu na kulinda na kuhakikisha usalama wa Watanzania wote na wageni halali wanaoingia katika Taifa letu, na pia kulinda mali zetu. Huu ni wajibu wa Kikatiba wa Rais wetu anautekeleza kwaniaba yetu tumuunge mkono bila maswali.

Pili: kupendekeza kwa Watanzania wote, wananchi na viongozi, kukubali kwamba Taifa letu si la wauaji wala la wahuni, ni Taifa la watu wanaoishi kwa kuzingatia Katiba ya nchi yetu na sheria zinazotokana na Katiba hiyo sisi sote tunao wajibu wa kufuata na kutii Katiba yetu na sheria zote zinazotokana Katiba hiyo, na ambazo hazikiuki Katiba. Hakuna nafasi wala ruhusa kwa raia yoyote wa nchi hii kuishi nje ya utaratibu huu. Huu ndio msingi wa amani, umoja, na maendeleo yanayo shirikisha wananchi wote kwa faida yao. Kwa maana hii, sisi Watanzania ni wastaarabu.

Tusiseme hatuwajui wahalifu hao, tunawajua. Wanaishi miongoni mwetu na katika kaya zetu, wako ndani ya vyombo vyetu vya dola, wako makanisani na katika misikiti. Tunawajua, lazima serikali yetu iwajue. Kwahiyo Taasisi ya Mwalimu Nyerere inaomba tumsaidie Rais kupata taarifa sahihi kuhusu wabaya wetu hao ili achukue hatua stahili. Anavyo vyombo vya dola vyenye majukumu mahsusi ya kumpa taarifa za uhakika. Nchi yetu imeviwezesha kuwa na uwezo wa kutosha wa utaalamu na

Au kwa lugha nyingine , tutawashngaa TISS, Polisi na hata Jeshi letu(kwa kiasi) wasipowaleta hadharani hawa wauaji.
Na kama hawatapatikana basi je, Kiongozi yeyote wa kitaifa akitekwa itakuwepo picha ipi?
 

TAARIFA YA TAASISI YA MWALIMU NYERERE KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU TABIA MBAYA ZINAZOHATARISHA USALAMA WA MAISHA YA WATANZANIA NA MALI ZAO

Ndugu wanahabari nimewaiteni hapa, kuwaombeni kwanza; muisaidie Taasisi ya Mwalimu Nyerere kuwataarifu Watanzania wote na kuwaomba sisi sote tushirikiane kuunga mkono kwa dhati Rais wetu Mhe. Dr. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada anazofanya za kukomesha tabia mbaya zilizozuka katika Taifa letu za kulawiti, kuteka, kunyanyasa na kuua Watanzania wenzetu.

Tunaye Rais mmoja tu sio wawili wala watatu tuliye mkabidhi Katiba ya nchi yetu ili aitumie kuongoza Taifa letu na kulinda na kuhakikisha usalama wa Watanzania wote na wageni halali wanaoingia katika Taifa letu, na pia kulinda mali zetu. Huu ni wajibu wa Kikatiba wa Rais wetu anautekeleza kwaniaba yetu tumuunge mkono bila maswali.

Pili: kupendekeza kwa Watanzania wote, wananchi na viongozi, kukubali kwamba Taifa letu si la wauaji wala la wahuni, ni Taifa la watu wanaoishi kwa kuzingatia Katiba ya nchi yetu na sheria zinazotokana na Katiba hiyo sisi sote tunao wajibu wa kufuata na kutii Katiba yetu na sheria zote zinazotokana Katiba hiyo, na ambazo hazikiuki Katiba. Hakuna nafasi wala ruhusa kwa raia yoyote wa nchi hii kuishi nje ya utaratibu huu. Huu ndio msingi wa amani, umoja, na maendeleo yanayo shirikisha wananchi wote kwa faida yao. Kwa maana hii, sisi Watanzania ni wastaarabu.

Tusiseme hatuwajui wahalifu hao, tunawajua. Wanaishi miongoni mwetu na katika kaya zetu, wako ndani ya vyombo vyetu vya dola, wako makanisani na katika misikiti. Tunawajua, lazima serikali yetu iwajue. Kwahiyo Taasisi ya Mwalimu Nyerere inaomba tumsaidie Rais kupata taarifa sahihi kuhusu wabaya wetu hao ili achukue hatua stahili. Anavyo vyombo vya dola vyenye majukumu mahsusi ya kumpa taarifa za uhakika. Nchi yetu imeviwezesha kuwa na uwezo wa kutosha wa utaalamu na

Tukiahirisha kufikiri kizalendo tunawaita wasiojulikana, yaani unawajua lakini unajizima data na kusema huwajui, kwakuwaita wasiojulikana
 
Mbona taarifa nyingi

Vyombo vya ulinzi vipewe nafasi vifanye uchunguzi vilete taarifa

Wameshasema wanachunguza sasa jamii itulie isubiri taarifa

Matamko yanatosha sasa
Acha upuuzi wako ! Walikuwa wapi kufanya uchunguzi mpaka Rais awaagize!
Matamko ni muhimu na yanapaswa kuendelea kutolewa kwa nguvu na ukali zaidi ili vyombo hivyo vijue watu wamechoka na uzembe wao wa kuliaibisha Taifa hili !
 
Back
Top Bottom