Pre GE2025 Joseph Mbilinyi (Sugu) kajidhalilisha sana kuungana na Mbowe ili kumkabili Lissu

Pre GE2025 Joseph Mbilinyi (Sugu) kajidhalilisha sana kuungana na Mbowe ili kumkabili Lissu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2020
Posts
7,799
Reaction score
14,215
Habari zenu wanaJF wenzangu

Inashangaza sana mtu kama Sugu alieanza kuikanyaga ardhi ya Kaburu kabla ya vijana wengi wa Tanzania hawajawa na akili ya kufika huku, ameshindwa kusoma alama za nyakati ambazo bila chenga wala mizengwe zinaonesha fika kwamba awamu hii ni zamu ya Lisu iwe mvua au liwe jua.

Mimi nafikiri hata kama ni chawa wa mwenyekiti lkn kwa jinsi upepo unavyoelekea yeye angejifanya hana upande ili Lisu atapochaguliwa waweze kufanya kazi pamoja.

Sasa kwa namna yoyote ile ikiwa Lisu atachaguliwa kuongoza Chadema, nina imani Sugu atashindwa kufanya nae kazi vizuri mwenyekiti wake mpya, na kwa vile ashaonesha kumpinga wazi wazi mwenyekiti wake mtarajiwa basi ninahisi pengine huko mbele atafanya maamuzi ya kukimbilia CCM ili akachaguliwe kuwa naibu waziri wa michezo na utamaduni, huku Mwana FA ambae anashika nafasi hiyo kwa sasa, huenda atapandishwa cheo na kuwa waziri kamili.

Kuna kila dalili kuwa Mbowe akishindwa atawatelekeza wote waliompambania na kuendelea na biashara zake zinazompatia ugali, hivyo Sugu atakosa mtu wa kumshika mkono chamani na kuamua kutimka bila kufukuzwa.
 
Kama CDM wameamua kufanya uchaguzi wa mwenyekiti maana yake ni Demokrasia na Kila mtu ana haki yakuchagua ampendaye.

Swali: kwenye Katina ya CDM kuna mahala panakataza kumuunga mkono Mbowe au Lissu?, kwenye Katiba ya CDM kuna mahala pameandikwa ukishakuwa mwenyekiti huruhusiwi tena kugombea?
 
Habari zenu wanaJF wenzangu

Inashangaza sana mtu kama Sugu alieanza kuikanyaga ardhi ya Kaburu kabla ya vijana wengi wa Tanzania hawajawa na akili ya kufika huku, ameshindwa kusoma alama za nyakati ambazo bila chenga wala mizengwe zinaonesha fika kwamba awamu hii ni zamu ya Lisu iwe mvua au liwe jua.

Mimi nafikiri hata kama ni chawa wa mwenyekiti lkn kwa jinsi upepo unavyoelekea yeye angejifanya hana upande ili Lisu atapochaguliwa waweze kufanya kazi pamoja.

Sasa kwa namna yoyote ile ikiwa Lisu atachaguliwa kuongoza Chadema, nina imani Sugu atashindwa kufanya nae kazi vizuri mwenyekiti wake mpya, na kwa vile ashaonesha kumpinga wazi wazi mwenyekiti wake mtarajiwa basi ninahisi pengine huko mbele atafanya maamuzi ya kukimbilia CCM ili akachaguliwe kuwa naibu waziri wa michezo na utamaduni, huku Mwana FA ambae anashika nafasi hiyo kwa sasa, huenda atapandishwa cheo na kuwa waziri kamili.

Kuna kila dalili kuwa Mbowe akishindwa atawatelekeza wote waliompambania na kuendelea na biashara zake zinazompatia ugali, hivyo Sugu atakosa mtu wa kumshika mkono chamani na kuamua kutimka bila kufukuzwa.
Amelamba asali, njaa mbaya sana
 
Nakushauri sugu na wajumbe wengine jitokezeni kumliwaza mbowe aka tapeli kuwa mpo pamoja naye na system waone kuwa atashinda ila siku ya kupiga kura afanyiwe surprise kwa kupata kura 1 ya kwake.mimi sina wasiwai na wajumbe Lisu atapata zaidi ya kura 1,000.
 
Back
Top Bottom