Joseph Mrindoko wa wachokonozi azichana vibaya shule za English Medium

Joseph Mrindoko wa wachokonozi azichana vibaya shule za English Medium

Tatizo English medium hakuna walimu kule, walimu n hawa wakuokoteza kapata zero unashangaa kawa mwalimu
 
Sio dharau ndio ukweli halisi mwandalie mtoto elimu nzuri hata hizo English medium zinafaa sana tena ni cheap izo st kayumba ndio zinazotoa vijana wavuta bangi wakabaji walevi wa pombe za nimeyaona haya mana ata Mimi nilisoma kayumba miaka hiyo
Elimu nzuri ni kuingea kiingereza?
 
Jamaa katupiga kamba,yaani chuo chenye graduates ambao hawajui hata kuandika kiswahili kwa ufasaha na ambao wakimaliza kusoma ubunifu wao ni kusubiria kazi za halmashauri ndio kiwe chuo kikubwa Africa,hahahaha
Udsm haipo hata kwenye top 10 ya vyuo bora africa, unataka kusema nini?
 
Kiingereza ndo kiswahili Cha Dunia, it's the exposure of the world, kayumba kiingereza hakipo, Kuna vilugha vya kienyeji, maisha ni exposure, Duniani kwa haraka haraka exposure unaipata uwe unajua kiingereza
 
Huyo jamaa ni mpuuz kachelewa kufika mjin hiyo erimu ya serikari imetoka wap kama sio kwa wazungu
 
Kwa hiyo wapekeke shule za serikali ambazo ni choka mbaya?Ni Bora upeleke English medium kuliko hizo za kata.Ukitaka kujua hizo shule za serikali ni takataka angalia watoto wa viongozi kama wanasoma hizo shule.
 
Ni wazazi limbukeni tu ndio wanaopeleka watoto wao huko wakiamini watapata elimu bora.

Cha ajabu watoto wanafundishwa kiingereza kibaya na walimu wa kuokoteza wao wenyewe hawajui lugha hiyo kwa ufasaha wanakaririsha watoto kiingereza kibovu.
Ni kweli zipo english medium ambazo walimu hawajui kiingereza. Na zipo.ambazo walimu wanajua. So inategemea na shule
 
Kwa mfumo wa elimu yetu ni bora (kama una uwezo),mpeleke mwanao English medium.

Komaa hivyo hadi pale Serikali ikiamua kutumia kiswahili kama lugha ya kufundishia kwa shule za sekondari.

Wapo baadhi ya wanafunzi wanafeli masomo yao ya Sekondari kutokana na kutokuwa na msingi wa lugha ya Kiingereza.

Ikumbukwe pia kuna watu wanakosa michongo kwa changamoto ya kutojua hicho Kiingereza.

N:B Kusomesha mwanao English Medium siyo upotevu wa pesa ila fanya hivyo kama una uwezo huo.
 
Amezichana vibaya shule za English Mediums na kuwaita " mbumbumbu "Watanzania wanao jistress kusomesha watoto wao kwenye shule hizo.

Ameongea point nyingi sana nenda kamsikilize mwenyewe You Tube.

Moja kati ya nukuu yake anasema " Waafrika tunataka kuwa kama wazungu. Wazungu hawataki kuwa kama sisi.

Tumekuwa mbumbumbu kiasi cha kulipa pesa ili watoto wetu watengenezwe wawe kama wazungu.

Cha ajabu hao tunao taka wawatengeneze watoto wetu wawe kama wazungu sio wazungu wala hawajui chochote kuhusu wazungu na uzungu
Hehe blaza matunguli yanagoma watoto wakiwa wanajua ki english nini maana umekomaa na hii kidumu na mfagio muda mrefu
 
Bongo hii wanafiki sana mtu anajifanya kupenda shule wakati wanae yupo huko huko si tunawaona pia kwenye misiba wakipngea kingereza kama wanaongea ma wageni na sio watanzania.

Wabongo wanafiki sana sio wa kuwasikilizq fanya ww utakavyoona na nafsi yako
 
English medium zilikufanyia nini?
Yaani!! Huyu Jamaa nishida...
Wakati Halmashauri ziko zinahangaika kuendelea kuzibadili shule zake from Swahili to English...huyu anaxidisha chuki.
 
Ila tuache utani.
Wale vijana wa WACHOKONOZI ni vijana wazalendo na wenye IQ kubwa
IQ kubwa ni kiasi gani labda na ndogo ni ipi. Jamaa wameamua kusema vitu ambavyo wengi huwa tunaishia kuvifikiria tu na hata Kama kusema sio kwenye media.
Wameacha kuzungumzia mitano Tena kwa mrengo wa IQ kubwa?
 
Kumbuka Kenya na Uganda wametupita kielimu jwa sababu ya lugha ya malkia. Angalau na sisi tujikomboe, hii lugha ni ya kimataifa huwezi kuikwepa. Wewe anzisha viwanda vingi vyenye tija, andika kila kitu kwa kiswahili, ili ueneze kiswahili duniani. Hata terminology za kisayansi uandike kwa kiswahili. Utaweza? Whether you like or not you ought to lean English. Naomba tu waalimu wa hizi shule wapikwe vizuri.
Wametupita nini, toa mifano 2 au 3
 
Yaani!! Huyu Jamaa nishida...
Wakati Halmashauri ziko zinahangaika kuendelea kuzibadili shule zake from Swahili to English...huyu anaxidisha chuki.
Ana matatizo sana huyu jamaa
 
Kumbuka Kenya na Uganda wametupita kielimu jwa sababu ya lugha ya malkia. Angalau na sisi tujikomboe, hii lugha ni ya kimataifa huwezi kuikwepa. Wewe anzisha viwanda vingi vyenye tija, andika kila kitu kwa kiswahili, ili ueneze kiswahili duniani. Hata terminology za kisayansi uandike kwa kiswahili. Utaweza? Whether you like or not you ought to lean English. Naomba tu waalimu wa hizi shule wapikwe vizuri.
Kenya hawajatupita kwa lugha ya wazungu tu, hata hulks yao ni kama wazungu. Hapa Bongo watoto wanaosomeshwa huko nje kimataifa, international na English medium wanabaki na hulka za Kiswahili na kichawa tu.
 
Back
Top Bottom