Joti hana mpinzani kwenye tasnia ya uchekeshaji

Joti hana mpinzani kwenye tasnia ya uchekeshaji

joti wa sasa uchekeshaji wake umejaa ngono sana sasa hivi,mpaka unakela
Yap hyo ni moja ya error Kwa Sisi wapenda maadili , may be anaangalia soko, trends ya matukio na mengine ambayo as hatuyajui, hata kwenye masuala mengine anajitahd Sana Nafkr crew yake pia ipo poa
 
Wadau Leo nakuja kivingine , huyu jamaa nilikuwa bado sijampata vyema , Joti ni legendary anayeishi upande wa commedy , mwamba anaweza Igiza angle yyte unayotaka wewe ,..... Hata script za proffesinal jamaa anacheza vizur Sana, kuanzia utoto , mwanamke, babu , mpaka mlala Hoi au mchungaji...jamaa pote anapita Tu fresh .....

Ana uwezo mkubwa Sana hakuna WA kumfikia hapa bongo , na itachukua mda kumpata mwamba kama huyu tena ,nimeamua nimpe sifa zake akiwa bado hai ..... Joti asifananishwe na mchekeshaji yyte ni kumkosea heshima Sana

Nimalizie Kwa kusema kama Una stress, huna amani, unahtaji kuburudika na hata kufurah basi angalia clip za joti nafkr zpo YouTube .....angalizo tu huyu jamaa usipokuwa makini utamaliza hela kununua bando Kwa ajili yake....

View attachment 1760950
Sidhani kama anataa amfikie brother k. Na senga.
 
Joti ni legend lakini ubunifu unafika mwisho. Mbinu anazotumia haziendani na ulimwengu wa vichekesho wa sasa.
Kwangu mimi joti na mpoki nawaweka kundi moja pale juu. Wote ni wakali, joti anafanya character tofautitofauti wakati mpoki anafanya mpaka stand up. Hawa wawili ndio naweza kusema wako pale juu. Kwa urahisi sana naweza kumwongeza Deo gratias aliyekuwa Cheka tu na sasa yuko watu baki kwa sababu kwenye stand up comedy kwa sasa hakuna anayemfikia.
Kiukweli wachekeshaji wetu wanahitaji kujiupdate na kujiendeleza sambamba na kubuni mbinu mpya za kuchekesha na kujijengea profile ili waweze kutoboa hata masoko ya kimataifa. Vinginevyo ndio tutakaa hapa tunajadili wababe wa comedy tunamtaja mkojani na dullyvanny!
 
Mzee Majuto jina lilimbeba alikuwa anafurahisha lakini sio comedian mzuri Mungu amrehemu ni kama watu wakisema Kanumba Mungu amrehemu, mimi sikuona kikubwa kwake uhalisia ulikuwa hakuna unaona kabisa huyu ana act lakini kuna watu walikuwa na wanampenda hayo ni maoni yao na naheshimu ila bado hatujapata watu waka act katika kuvaa uhusika bado, Joti yuko vizuri short video zake script zake mara nyingi wako vizuri.
Kufurahisha ndio komedi yenyewe hiyo.
 
Kufurahisha ndio komedi yenyewe hiyo.
Anafurahisha ule muonekano wake kuna watu wanafurahisha muonekano wao tu lakini sio kazi zao mimi sijawahi kucheka sana katika kazi zake sasa inategemea kila mtu na chaguo lake mimi nimeongelea kama mimi wako waliokuwa wanafurahishwa ila mimi hapana.
 
Kuna moja hyo inaitwa gari ya Baba , ha haaa kakumbana na demu wa R-chuga aisee hyo lazima utabasamu tuu, Joti ni professional bhana
 
Anafurahisha ule muonekano wake kuna watu wanafurahisha muonekano wao tu lakini sio kazi zao mimi sijawahi kucheka sana katika kazi zake sasa inategemea kila mtu na chaguo lake mimi nimeongelea kama mimi wako waliokuwa wanafurahishwa ila mimi hapana.
Okay ila Joti ni mtundu tu na vituko sio mchekeshaji wa daraja hilo analopewa.

Mfuatilie Victaza au Sumaku wa Mizengwe utajua Joti hajui.
 
Hao wote uliowataja ni one sided na wabakuchekesha kwenye comment only , Ila huyu jamaa Joti aisee kile ni kipaji bhana , kuanzia muonekano, anavyoongea, na hata mazingira full kucheka
Joti jinsi anavyofit kwenye kila idara inaonyesha ni kiasi gani ana kipaji halazimishi kuchekesha.
He is the best comedian so far
 
Back
Top Bottom