Julius K. Nyerere: Ikulu ni pahali patakatifu, sio pango la wanyang'anyi

Julius K. Nyerere: Ikulu ni pahali patakatifu, sio pango la wanyang'anyi

Tatizo kuna kizazi ambacho kilikua kinaogopa kuhoji,na unaposhindwa kumkosoa mtu kisha akaja kujiona alifanya makosa anakuona wewe ulieshindwa kumkosoa ni mpumbavu..kizazi hichi hakina uoga kinahoji hakimsujudu mtu isipokua Mungu tu.
Siamini katika misemo ya zamani...naamini katika kizazi hichi kilichojaa wajasiri wengi,wenye vipaji na akili na moyo wa kujituma..lakini tatizo kuna mfumo kandamizi uliowekwa na chama twawala..naamini katika kumpa kura yangu yule anayesisitiza elimu,elimu,elimu..elimu bora na fursa kwa vijana.yule atakayeingiza katiba iliyopendekezwa na wananchi inayoziba mianya ya rushwa na kuunda "fair playground" kwa wote,yule aliye na uwezo wa kusimamia maamuzi mwenyewe bila kuyumbishwa na chama...anayekubalika na vijana wengi,wazee wengi,kina mama na hata watoto,Rais wa nchi inatakiwa uwe na muonekano wa tumaini kwa wananchi wako,na watanzania wanaona tumaini kwa Edward Ngoyai Lowassa.hivyo nikiwa hukuhuku ndani ya ccm nitampa kura yangu EL.
Kwa kijana mwenzangu kuepuka miaka kadhaa ijayo kuja kuulizwa na watoto pia na wajukuu zako..."baba/babu..kwanini mlikua mnakichagua chama kimoja miaka 54 pamoja na kua kilikua kinaendelea kuwaletea umaskini na sio maendeleo"
FANYA MABADILIKO SASA KWA KIZAZI CHAKO NA KIZAZI KIJACHO.
 
Katika moja ya hotuba zake mwalimu aliwakumbusha wanaccm na watanzania kwa ujumla kuwa Ikulu ni mahali patakatifu. Na akasisitiza sana kuwa mtu awe tayari kumwambia mkewe, ndugu jamaa na marafiki kuwa ikulu ni mahali patakatifu na akuchaguliwa ili kupafanya pango la wanyang'anyi.

Ninachojiuliza mimi ni lini tutapata mtu aliye na ujasiri wa namna hii, kumuuenzi mwalimu kwa vitendo? Mh. Magufuli kajitahidi kuanza vizuri, je ataendelea hivi au naye ni nguvu ya soda tu?

Kama watanzania bila kujali itikadi zetu tuungane kwa pamoja kudai katiba mpya itakayojenga taasisi imara ya urais ili kauli ya baba wa taifa ienziwe kwa vitendo.
 
Nina hakika hawezi kuendelea na mbio hizo ama kasi aliyoanza nayo maana tayari wakubwa waishagundua dhamira take na sasa ile kasi hakuna tena!
 
Nina hakika hawezi kuendelea na mbio hizo ama kasi aliyoanza nayo maana tayari wakubwa waishagundua dhamira take na sasa ile kasi hakuna tena!
Tatizo
Nina hakika hawezi kuendelea na mbio hizo ama kasi aliyoanza nayo maana tayari wakubwa waishagundua dhamira take na sasa ile kasi hakuna tena!
kumuumbua baba yako hadharani inataka ujasiri
 
Nina hakika hawezi kuendelea na mbio hizo ama kasi aliyoanza nayo maana tayari wakubwa waishagundua dhamira take na sasa ile kasi hakuna tena!
Tatizo
Nina hakika hawezi kuendelea na mbio hizo ama kasi aliyoanza nayo maana tayari wakubwa waishagundua dhamira take na sasa ile kasi hakuna tena!
kumuumbua baba yako hadharani inataka ujasiri
 
NIKITAFAKARI HUWA MACHOZI YANANITOKA:
Tulianza na Mwalimu Nyerere aliyepiga` kwata miaka 24 [1961 – 1985] pale Magogoni – Ikulu; kwanza kama Waziri Mkuu [1961], kisha kama Rais hadi mwisho. Yeye aliyaona maisha ya Ikulu kuwa mzigo; akasema, mtu mwenye hekima na busara atatamani daima kuutua mzigo huo kipindi kinapowadia ili kuwaachia wengine nao wajaribu kuubeba. Alitaka kuutua mwaka 1978 kama isingekuwa kuzuka kwa vita vya Kagera; akaona haikuwa busara kuiacha nchi ghafla katika vuguvugu la vita na baada ya hapo.

Mwalimu alijua, alilinda, alitetea na kuzingatia heshima ya Ikulu ikaheshimiwa. Kuitwa Ikulu enzi zile ilikuwa ni ama kuwajibishwa/kukanywa, kufukuzwa kazi kwa utendaji kazi usioridhisha, au kupongezwa kwa kazi nzuri na kutunukiwa cheo. Zilikuwa enzi za wajibu na kuwajibika. Waovu na wenye kulemewa na mizigo ya “dhambi” hawakukatisha; waliondolewa sawia wasije wakachafua Taifa.

Uteuzi wa viongozi haukuwa kwa njia ya urafiki, upendeleo wala kubahatisha. Vyombo vya dola, hasa Usalama wa Taifa, vilifanya kazi kwa weledi na uadilifu mkubwa kuhakikisha kwamba, wale walioteuliwa kushika madaraka walikuwa watu safi, wasio na makandokando. Tukasifika kwa uzalendo, uadilifu na uwajibikaji wa hali ya juu. Na huu ndio msingi wa amani na utulivu tunayojivunia leo; lakini amani hiyo inayoyoma haraka kutokana na “ufisadi” na mafisadi kuachwa kutamba kiasi cha kutaka kuteka mhimili wa uongozi wa nchi.

Chini ya Mwalimu, Ikulu ilikuwa “kisima cha uzima na uhai wa Taifa” kwa sababu yeye mwenyewe alijitoa mhanga kutumikia kwa wema na si kwa maslahi binafsi. Wakati wengine wachache enzi hizo na hata leo, walifikiri Ikulu ni mahali pa kutumbua vinono, starehe na kujizolea mali ; Mwalimu alipaona ni mzigo na tundu la sindano kuweza kupita kufika hapo.

Alisema, “Ikulu ni mahali patakatifu; si pango la wevi na wanyang’anyi”; akatahadharisha kwamba, “mtu yeyote anayelilia kuingia Ikulu kwa udi na uvumba ni wa kuogopwa kama ukoma”, kwa maana atakuwa na lake jambo, na si kwa maslahi ya nchi.Kwa Rais DR.JPM naliona hili na matumaini mapya ya utaifa wetu utarudi soon,ilimradi tu akaze buti kwani watz tumempa dhamana hiyo.Nikitazama picha napata majibu haraka na baadhi ya maswali yangu ambayo mwl,Nyerere aliyafanyia kazi enzi hizo,na wewe tazama vizuri picha hizo unapata ujumbe gani???????????????????.
upload_2016-5-22_8-16-14.png


NCHI YANGU TANZANIA:KATIKA HILI LAZIMA TUITETEE NCHI NA WATU WAKE NA SI BIASHARA YA WACHACHE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!RAIS WETU TWENDE TU MUNGU NI ASILI YA MEMA YOTE MABAYA NI YA SHETANI.
 
Umenena vema mkuu. Napata picha unafahmu Tanzania imetoka wapi, imepitia wapi, imefika wapi na inaelekea wapi. Historia hii wengi wa kizazi cha leo hawaifahamu kiasi cha kutaka kufanya maamuzi ya hatari sana kwa mustakabali wa taifa letu. Uzi huu ni moja kati ya nyuzi bora kabisa ambao nimekutanao humu jf. Kongole, mtoa uzi.
 
Mkuu hapo umenena, maneno yako umeyapangilia vilivyo na ndivyo ilivyo. Mwelekeo unaonekana kabisa kwamba heshima ya Ikulu inakaribia kurudi. Wacheza bao hawana nafasi tena pale.
 
Arudishe Azimio la Arusha atakuwa kamwezi Hayati Baba wa Taifa Mwl.Nyerere
 
Mleta mada ubarikiwe sana kwa hilo, umenifanya niwaze kidogo, maana historia uliyotoa kuhusu mwl nyerere mwaka 1978, sikuifamu. Hadhi ya ikulu sasa inarejea tena.
 
Mh.JPM Ndiye Kiongozi anayestahili kukaa na Kuishi IKULU YA MAGOGONI hatukufanya MAKOSA Kumchagua .Mh.JPM rudisha Hadhi ya Taifa Letu na Kurudisha Maadili na Nidhamu ya UTUMISHI WA UMMA.Usichoke wala usurudi Nyuma.Wakati wa Kampeni Ulituambia na Kutuaminisha Uyatendao.Ni ukweli Unayaishi Maneno yako.Ninukuu moja ya kauli zako,"Ulisema Nikikuteua kuwa Waziri Ufanye Kazi Kwelikweli au Iiiiiiiiiiiiii.Ukatuacha ktk Fumbo .SASA TUMEELEWA ULIAMINISHA NINI.Mungu akutangulie BIG UP Mzee Magu.
 
Ikulu ni zaidi ya majengo meupe, yale majengo yaliyojengwa na wazungu hayana maana ikiwa moyo wa yule anayeyatumia kama ofisi yake haujashikamana na wananchi wengi haswa wale masikini.
Ikulu huwa na heshima wakati mwenye mamlaka anapoamua kukiheshimu cheo chake. Mwalimu Nyerere wakati akiwa anajenga hoja aliwahi kutumia mfano wa kwenye biblia akisema huwezi kuwatumika mabwana wawili, yaani Mungu na mali.
Kuna suala la mtu kuweza kukwepa kishawishi cha mali ili utakatifu wa IKulu uweze kuwepo. Huo ni mtihani mgumu sana kwa wanasiasa wengi wa bara letu.
JPM pia anao mtihani huu, maadam ameamua kupambana na wale wenye mali ambao siku zote wanataka kubakia wao tu kama wenye mali hizo, basi wala asilegeze kamba. Vita ndio kwanza imeanza, ili Ikulu iweze kubaki na utakatifu wake.
 
NIKITAFAKARI HUWA MACHOZI YANANITOKA:
Tulianza na Mwalimu Nyerere aliyepiga` kwata miaka 24 [1961 – 1985] pale Magogoni – Ikulu; kwanza kama Waziri Mkuu [1961], kisha kama Rais hadi mwisho. Yeye aliyaona maisha ya Ikulu kuwa mzigo; akasema, mtu mwenye hekima na busara atatamani daima kuutua mzigo huo kipindi kinapowadia ili kuwaachia wengine nao wajaribu kuubeba. Alitaka kuutua mwaka 1978 kama isingekuwa kuzuka kwa vita vya Kagera; akaona haikuwa busara kuiacha nchi ghafla katika vuguvugu la vita na baada ya hapo.

Mwalimu alijua, alilinda, alitetea na kuzingatia heshima ya Ikulu ikaheshimiwa. Kuitwa Ikulu enzi zile ilikuwa ni ama kuwajibishwa/kukanywa, kufukuzwa kazi kwa utendaji kazi usioridhisha, au kupongezwa kwa kazi nzuri na kutunukiwa cheo. Zilikuwa enzi za wajibu na kuwajibika. Waovu na wenye kulemewa na mizigo ya “dhambi” hawakukatisha; waliondolewa sawia wasije wakachafua Taifa.

Uteuzi wa viongozi haukuwa kwa njia ya urafiki, upendeleo wala kubahatisha. Vyombo vya dola, hasa Usalama wa Taifa, vilifanya kazi kwa weledi na uadilifu mkubwa kuhakikisha kwamba, wale walioteuliwa kushika madaraka walikuwa watu safi, wasio na makandokando. Tukasifika kwa uzalendo, uadilifu na uwajibikaji wa hali ya juu. Na huu ndio msingi wa amani na utulivu tunayojivunia leo; lakini amani hiyo inayoyoma haraka kutokana na “ufisadi” na mafisadi kuachwa kutamba kiasi cha kutaka kuteka mhimili wa uongozi wa nchi.

Chini ya Mwalimu, Ikulu ilikuwa “kisima cha uzima na uhai wa Taifa” kwa sababu yeye mwenyewe alijitoa mhanga kutumikia kwa wema na si kwa maslahi binafsi. Wakati wengine wachache enzi hizo na hata leo, walifikiri Ikulu ni mahali pa kutumbua vinono, starehe na kujizolea mali ; Mwalimu alipaona ni mzigo na tundu la sindano kuweza kupita kufika hapo.

Alisema, “Ikulu ni mahali patakatifu; si pango la wevi na wanyang’anyi”; akatahadharisha kwamba, “mtu yeyote anayelilia kuingia Ikulu kwa udi na uvumba ni wa kuogopwa kama ukoma”, kwa maana atakuwa na lake jambo, na si kwa maslahi ya nchi.Kwa Rais DR.JPM naliona hili na matumaini mapya ya utaifa wetu utarudi soon,ilimradi tu akaze buti kwani watz tumempa dhamana hiyo.Nikitazama picha napata majibu haraka na baadhi ya maswali yangu ambayo mwl,Nyerere aliyafanyia kazi enzi hizo,na wewe tazama vizuri picha hizo unapata ujumbe gani???????????????????.
View attachment 349742

NCHI YANGU TANZANIA:KATIKA HILI LAZIMA TUITETEE NCHI NA WATU WAKE NA SI BIASHARA YA WACHACHE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!RAIS WETU TWENDE TU MUNGU NI ASILI YA MEMA YOTE MABAYA NI YA SHETANI.
Umenena mkuu
 
Umenena vema mkuu. Napata picha unafahmu Tanzania imetoka wapi, imepitia wapi, imefika wapi na inaelekea wapi. Historia hii wengi wa kizazi cha leo hawaifahamu kiasi cha kutaka kufanya maamuzi ya hatari sana kwa mustakabali wa taifa letu. Uzi huu ni moja kati ya nyuzi bora kabisa ambao nimekutanao humu jf. Kongole, mtoa uzi.
Kjn uko vzr kwe kiswahil,,, vijana wachache wanaowez kutumia neno "KONGOLE "Congura....
 
Ikulu ni zaidi ya majengo meupe, yale majengo yaliyojengwa na wazungu hayana maana ikiwa moyo wa yule anayeyatumia kama ofisi yake haujashikamana na wananchi wengi haswa wale masikini.
Ikulu huwa na heshima wakati mwenye mamlaka anapoamua kukiheshimu cheo chake. Mwalimu Nyerere wakati akiwa anajenga hoja aliwahi kutumia mfano wa kwenye biblia akisema huwezi kuwatumika mabwana wawili, yaani Mungu na mali.
Kuna suala la mtu kuweza kukwepa kishawishi cha mali ili utakatifu wa IKulu uweze kuwepo. Huo ni mtihani mgumu sana kwa wanasiasa wengi wa bara letu.
JPM pia anao mtihani huu, maadam ameamua kupambana na wale wenye mali ambao siku zote wanataka kubakia wao tu kama wenye mali hizo, basi wala asilegeze kamba. Vita ndio kwanza imeanza, ili Ikulu iweze kubaki na utakatifu wake.
Mkuu dhaaa,kwa kweli ni sisi wa kizazi hiki hatusomi maana ni mengi aliyoyasema na kuandika mwl.Nyerere ambayo yalipaswa yatuongoze.Tukiwa na watu aina hii naamini tutalisaidia sana taifa na watu wake.
 
Mkuu dhaaa,kwa kweli ni sisi wa kizazi hiki hatusomi maana ni mengi aliyoyasema na kuandika mwl.Nyerere ambayo yalipaswa yatuongoze.Tukiwa na watu aina hii naamini tutalisaidia sana taifa na watu wake.
Ni bora uwe uchi kimwili kuliko kiakili - Julius Nyerere akiongea na UWT pale Karimjee Hall miaka ya 80.
 
Back
Top Bottom