Mwingine kapewa nchi miezi 24 tayari kauza Bandari,kauza NGORONGORO,Kauza KIA,Kauza Misitu........Nyerere bado ataendelea kuwa number moja mpaka kesho.Mwalimu Nyerere angeamua angeuza nchi, angeuza bandari, angeuza mbuga za wanyama, angeuza kila kitu.
Mpeni Mwalimu Nyerere maua yake.
Nan...Legacy ya Mwalimu haiwezi kufutwa kizembe maalim.Ni kiongozi ambaye Africa haijawahi pata mfano wake.Kwa uelewa wako ukipewa nafasi ya kumlinganisha na marais wote wa Tanzania,yupi anamzidi Mwalimu intergrity na
Nyerere hakuingizwa kwenye harakati kwa kuonewa huruma,he earned it kwa merits mzee!
Shida ni kwamba unaieleza as if Mwalimu alipewa favor kwa kuonewa huruma.Mwalimu alikuwa na elimu na akili na mbali na vyote he was charismatic as compared to other colleagues at that time.Kiufupi He deserved it.He was smarter than the sykes etal.The Mwapachus needed Mwalimu more than he needed them.
Kama ambavyo nimewahi kukueleza hapo awali na leo narudia,Wewe huna hati miliki ya ukweli kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.Silazimiki kuamini sources unazozitoa kwa sababu katika kusoma kwangu nimeufahamu ukweli
Nakushauri uangalie movie ya Black Hawk dawn.kuna Phrase inasema "history remembers only Kings and not warriors"na hii ndo Kanuni ya dunia.Umar alipigania sana uislam lakini anayeongelewa ni mtumeNan...
Umesema kweli "legacy" ya Mwalimu ni kubwa.
Kitabu cha Abdul Sykes kimepata umaarufu sababu yake ni Nyerere.
Kitabu kimeeleza yale ambayo Nyerere mwenyewe hakupata kuyasema wala mwanahistoria yeyote kuyaandika.
Hiki ndicho kilichowavutia watu wengi.
Lakini wako waliofadhaishwa na kitabu hiki kwa kuona kuwa Nyerere anagawana historia yake na watu ambao wao hawakupata kuwasikia hata siku moja.
Wako waliojiuliza mbona historia hii tunayosoma leo haikusomeshwa?
Iweje kadi za TANU tatu za mwanzo mbili ni za ndugu wawili khalis Abdulwahid na Ally Sykes?
Nini maana ya jambo hili?
Hili si suala la uadilifu au uzalendo wa Nyerere.
Maswali ninayoulizwa kote vyuoni ninapozungumza ni imekuwaje taifa likapoteza historia yake yote ya wazalendo wake waliopigania uhuru?
Prof. Haroub Othman hili lilimtatiza.
Angalia video hiyo namzungumza Prof. Haroub alivyotafuta maelezo kutoka kwa Mwalimu Nyerere:
View: https://youtu.be/lCyNc0C46Zo?si=X11DvnNUTCtbaOak
Nyerere was King Sykes etal were warriors.History remembers Kings only.Nakushauri uangalie movie ya Black Hawk dawn.kuna Phrase inasema "history remembers only Kings and not warriors"na hii ndo Kanuni ya dunia.Umar alipigania sana uislam lakini anayeongelewa ni mtume
Historia hukumbuka wafalme na si wanajeshi.Aliyeshinda vita ya Uganda ni Nyerere na si Msuguri wala SarakikyaNan...
Sifa zote ulizompa Mwalimu anastahili na mimi nimezieleza katika kitabu cha Abdul Sykes.
Lakini ukweli utabakia ukweli hauwezi kufutika.
African Association iliasisiwa na Kleist Sykes mwaka wa 1929.
Mwaka wa 1933 akaasisi Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) na vyama hivi viwili vilishirikiana katika kupambana na ukoloni wa Muingereza.
Ukiikataa historia hii tayari unaingia katika matatizo makubwa.
Walioikwepa historia hii leo ndiyo hawa wanahangaika na Mohamed Said.
Mohamed Said anawajibu na kuwaeleza historia ya kweli.
Sasa ikiwa huzikubali Nyaraka za Sykes utakubali nyaraka za nani?
Mwalimu Nyerere kama atakuwa na nyaraka za historia ya TANU basi zitakuwa kuanzia 1953.
Mimi sijaziona popote hata Maktaba ya CCM Dodoma hazipo.
Mimi nimeziona Nyaraka za Sykes zenye historia ya harakati kuanzia 1924.
Nan...Nakushauri uangalie movie ya Black Hawk dawn.kuna Phrase inasema "history remembers only Kings and not warriors"na hii ndo Kanuni ya dunia.Umar alipigania sana uislam lakini anayeongelewa ni mtume
Nan...Historia hukumbuka wafalme na si wanajeshi.Aliyeshinda vita ya Uganda ni Nyerere na si Msuguri wala Sarakikya
Nan...Nyerere was King Sykes etal were warriors.History remembers Kings only.
Nyerere aliiacha nchi ina kila kiwanda cha wakati huo.Katika viongozi waliokuwa na maono na walio litendea haki hili taifa ni JK.Nyerere.
Hata akiitwa mtakatifu haina ttzo,bila yeye tungekua tuna chinjana na kutengana kwa minajili ya dini,ukanda na kubila kama wewe mzee mudi unachotaka kulileta katika taifa hili.
Nyinyi ndio misukule yenyeweFikra na mawazo ya mtakatifu Nyerere ziendelee kudumu
Gamm...Nyinyi ndio misukule yenyewe
Umeandika kwa tafsida, sijaambulia kituMwalimu Kambarage Nyerere, kama mtu, alikuwa ni mchakato...
Historia haitengenezi watu, watu wanatengeneza historia.
Historia ni uso wa juujuu wa tafsiri za muktadha wa sura za watu/jamii, matendo na matukio/sura ya utukufu wake.
Watu wanaitengeneza 'historia' kwa mujibu wa ule muktadha wa 'maadili na miiko' ujayo na/kwa 'mila na desturi' -- mila na destiri zinazoshindanishwa kimapana ya nyakati na matukio na utashi--'Wakati-Jamii-Machaguo ya Kitaasisi-Matukio'....
'Mila na desturi' ni mambo yajayo na kadiri ya kiasi cha mwangaza/Elimu ama mapokeo ya jamii--lakini mwangaza ni jambo kuu kuliko 'mila na desturi' yeyote.
Kambarage Nyerere alikuwa ni 'Mtu wa Mwangaza'--watu wa mwangaza wananamna ya kutizamwa na kubayanishwa asili ya matendo yao, na basi nguzo za imani zinazokadirisha mapana ya 'dhamira, uono na vina vya tafsiri' kwa ajili ya kujichagulia kwao..
Hili linafanya sura sahihi ya kubayanisha muktadha wa wito, matendo na urithi/legasi ya mtu wa mwangaza kuwa na ufundi wake mahususi--si jambo la hoja, mijadala na midahalo.
Ufundi huu unaitwa Elimu 2.0: Uono na ufikirifu mifumo.
Mambo ya elimu 2.0 na Elimu 3.0 ndiyo yanaweza kubangulia undani wa wito, matendo na legasi ya Mwalimu Nyerere. In Shaa Allah, hili tunakuja kulifahamu ilivyobora wakati muafaka; na linatengeneza kitovu cha 'kuifumua historia mbovu' na 'vina visivyo sahihi vya tafsiri ya wito, matendo na legasi'--Hata ya Mwalimu Nyerere; kwa kuwa kuna upande wa ndani wa mambo ambavyo watu wa namna hii ama ile, silika hiii ama ile, imani hii ama ile hongozwa kukadirisha 'Jaala' ya 'Waja Wema'...
Kwa hivyo hata mambo ya kukadirisha muktadha na kadiri ya 'Utume' wa mtu fulani ni jambo la 'Usanii' tu; lina makusudi yake--yanaweza kuwa ni 'mema' ama 'si mema hasa'. Inategemeana na upeo wa mtu kiakili, kihisia na kiroho.
Watu wa mapana hasa--mapana hasa ya kiakili, hisia na kiroho--watu wa Elimu 3.0 ndiyo wenye 'Utashi wa kweli' na 'Hekima'.
Hawa wakidhihiri hekima hiyo kwa umma ndipo ndipo umma utazinduka na kuzifahamu mbichi na mbivu za ustaarabu na ustawi wao...
Watu wa hekima hawafanyi vikundi vya mipango na hadaa, bali hawa hasa ni walinzi na waongozeaji wa hatma za jamii, mataifa na tawala. Kuwa mmoja wao si suala la 'maombi na kukubaliwa' ili kuifanya 'Taasisi fulani'; watu hawa 'hujichagua/kujichagulia wenyewe' na 'kufanya yao'--husaidiana kwa sura ya wazi na sura isiyo ya wazi kuitengeneza njia ya 'dhamira zao njema'.
Historia ndiyo inaweza kupotosha isipoweza kubaini ama kuotea 'matendo ya ndani' ya 'washirika' katika kuongozea umma -- kuongozea umma katika utu bora na maendeleo...
Siku si nyingi karibia kila kitu kitafahamika kuhusu 'Uhuru wa Ndani' wa wanajamii na 'Ushirika katika Imani ya UTU wema'--jambo linalokwenda kuwa chachu kuu ya mageuzi na mapinduzi ya kijamii Tanzania, Afrika na Duniani...
'Utume wa Nyerere' ni fumbo la Imani kwa watu 'wasio na macho'--kusubiri wengine wawape tafsiri ya mambo...
'Utume wa Nyerere' ni fumbo la kuitika wito wa kudhamiria UTU bora, Amani na Mapenzi mema Duniani.
'Utume wa Nyerere' ni fumbo la kubidi kufumbuliwa kitendawili cha 'Mapinduzi'-- Mapinduzi ni 'Muda wa Ufunuo', na hali 'mapinduzi endelevu' ni 'ukuwakujia wa UTU bora', 'Amani' na 'Mapenzi mema duniani'...
Hmmm
Kama kawaida yako ukikaa kidogo lazima utengeneze thread ya kumdogosha Mwl Nyerere. Unapata nini kwa kufanya yote haya?Gamm...
Hapana haja ya kutumia lugha kali.
Tujitahidi kuisomesha historia ya TANU kwa utulivu na lugha ya kuwavutia wasomaji.
Jambo lolote ukilitia upole litapendeza.
Wao hadi sasa wameshaujua ukweli kuwa historia ya uhuru wa Tanganyika ilifanyiwa khiyana.
Hawa wanajua kwa yakini kabisa ya nafsi zao kuwa Mohamed Said ameisahihisha historia ya Tanganyika.
Niliombwa nifanye kipindi cha Nyerere Day.
Kipindi kilikuwa cha Kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Kambarage Nyerere ambacho kilirushwa na AZAM TV.
Mtangazaji Jaffar Mponda alitaka twende Mtaa wa Stanley na Sikukuu aone nyumba ya Abdul Sykes ambayo Mwalimu Nyerere alipelekwa kujulishwa kwake na Joseph Kasella Bantu mwaka 1952.
Nyerere akaja kuishi nyumba hii baada ya kuacha kazi ya ualimu mwaka wa 1955.
Iko picha nipo hapo lakini Dar-es-Salaam ile ya miaka ya 1950 si hii ya leo.
Nyumba ndogo hazipo tena.
Ni ghorofa ndefu kila upande wa mtaa pamoja na nyumba ya Abdul Sykes ni ghorofa.
Jaffar Mponda alitaka tuanze kipindi chetu hapo.
Tulipofika nilimuonyesha Jaffar Mponda kuwa ile nyumba ya Abdul Sykes ambayo Nyerere aliishi hapo baada ya kuacha kazi mwaka wa 1955 ni hilo jumba mbele yetu maofisi na juu ni nyumba za kupanga.
Mtaa wa Stanley ulibadilishwa jina na kuwa Aggrey Street kwa heshima ya Dr. Kwegyir Aggrey kutoka Ghana.
Dr. Aggrey alikuja Tanganyika mwaka wa 1924 na alikutana na Kleist Sykes, baba yake Abdul.
Alikuwa Dr. Aggrey ndiye aliyempa Kleist wazo la kuunda African Association.
African Association ndiyo iliyounda TANU 1954.
Mtaa huu umebadilishwa jina unaitwa Max Mbwana lakini kibao cha jina jipya hakijawekwa.
Kuna mtu anaeweza kuipinga historia hii?
Waangalie video hii ya TBC.
View: https://youtu.be/qgo7OpTu8eI?si=u3cSI9x9G1-o5lgH
Inside,Nimeishia kwenye heading na nimegundua harufu ya udini, dhihaka na chuki zako dhidi ya nyerere..
Katika chuki unataka kujiheshimisha na wafuasi ktk viambaza vya mtoro, idrisa, ujiji na buguruni kama sio mwembechai.
Cc Nguruvi3
Stux...Kama kawaida yako ukikaa kidogo lazima utengeneze thread ya kumdogosha Mwl Nyerere. Unapata nini kwa kufStuxanya yote haya?
Sihutaji kuyajua hayo Mkuu wangu.Nachojua historia huwakumbuka wafalme tuu.Bahati mbaya sana mashujaa kama babu zako hawawezi kuongelewa kwa gravity kama ya nyerere hilo lazima ukubali.Nyerere ana mchango mkubwa sana kwa ustawi wa taifa hili kuliko wazee wako.Nan...
Historia ya Kleist Sykes inaanza 1894.
Nyerere hakuwapo wala Abdul Sykes.
Hapo niliposimama katika video hii ndipo waliposimama Abdulwahid Kleist Sykes na Julius Kambarage Nyerere kugombea urais wa TAA mwaka wa 1953.
Ulikuwa unayajua haya?
View: https://youtu.be/HTN5khgI0-M?si=wjsRCQlh5uWElmdh