Julius Nyerere Mtume wa Afrika 1950s - Julius Nyerere Mtakatifu Mwenye Kheri 2000s

Julius Nyerere Mtume wa Afrika 1950s - Julius Nyerere Mtakatifu Mwenye Kheri 2000s

Uwongo tu ndiyo umeusimamia. Nyererer ni true African Nationalist anayeshindanishwa na akina Kwame Nkrumah na Mandela tu, wala huwezi ku UNDO legacy yake hata uandike kitabu kikubwa kama Quran au ukafanye mhadhara Mecca wakati wa Rid ya kuchinja.

Ungefurahi sana nchi ya Tanzania iwe ya kiislamu ili muishi peke yenu lakini bahati mbaya nchi yetu ni secular, madhehebu yote yapo. Utulivu tulio nao ni kwa kazi kubwa ya J K Nyerere unaye mnanga kutwa kucha

Utulivu kweli kwani kila uchaguzi huku wanauliwa watu na kutiwa vilema , mbali ya ule uvamizi alituvamia 1964 na kuteka nchi yetu , RIH Laanatullahi Nyerere
 
Hata kama ni uongo basi ni ule wenye faida, kupambana kuutafuta ukweli WA historia ya Tanzania ni ujinga ilihali aman ipo nchini, history ingekuwa tofauti Leo hii ingekuwa vita mwanzo mwisho, udini ungehusishwa kwenye ukombozi WA taifa letu, bas Tanzania ingekuwa ya dini flani, dini na amani havikai pamoja, sote tunafahamu kwenye udini ndiko chuki, zipo, history inatengenezwa, tutengeneze history yetu ambayo haitokuwa na mapungufu, kuendelea kujihusisha na yaliyopita ni kuutafuta chuki dhidi yetu.

Ikiwa kama Nyerere alifanya makosa kwenye utawala wake, basi Kwa wakati huu WA miaka 30 tangu ukomo WA utawala wake, tungesha fanya mabadiliko, lakini tunapoendelea kumlilia na kumwita majina mazuri mpaka Leo ni dhahiri hayupo aliyemzidi Kwa jitihada zake, kama ukishindwa kufahamu ukubwa WA mwalimu, fikilia madhara ya ukabila na udini katika baadhi ya nchi za Afrika na nje ya afrca huko Israel vs parestina,.

Pengine mifumo aliyotumia, ilifaa Kwa muda huo, ambayo Kwa sasa unaonekana ni ya kijinga, kwenye serikali ya wakati huo na wakati huu, wapo watu wote na wale ambao mnadai hawakuhusishwa kwenye harakati za kudai uhuru, ni wamefanya mabadiliko.


Sijui kama huu uchawa umetoka Kwa Nyerere
Na sijui kama kwenye matolea yajayo utauzungmzia vp
Utausifu kwakuwa umechipuka wakati huu?

Tutengeneze history yetu ambayo haitokuwa na mapungufu

Amani aliyoleta Nyerere ndiyo hii ya kuvamiwa huku kwetu na kuwekewa majeshi kila mtaa ?? huku tukiletewa majeshi mpaka ya Burundi katika jitihada zenu za kuweka vibaraka wenu


View: https://www.youtube.com/watch?v=gmxrblkDnbc&t=71s&pp=ygVEa2lsaWNob3dhcGF0YSB3YWxpb3dla3dhIGt3ZW55ZSB2aXp1aXppIHZ5YSBtYXRlc28gdWNoYWd1emkgemFuemliYXI%3D
 
Sihutaji kuyajua hayo Mkuu wangu.Nachojua historia huwakumbuka wafalme tuu.Bahati mbaya sana mashujaa kama babu zako hawawezi kuongelewa kwa gravity kama ya nyerere hilo lazima ukubali.Nyerere ana mchango mkubwa sana kwa ustawi wa taifa hili kuliko wazee wako.
Umemaliza✍️
 
Utulivu kweli kwani kila uchaguzi huku wanauliwa watu na kutiwa vilema , mbali ya ulöe uvamizi alituvamia 1964 na kuteka nchi yetu , RIH Laanatullahi Nyerere
Mmoja wa wafuasi wanataka wa mzee ms ndio kama ww na wengi kawateka
 
Mzee wa ajabu sana wewe. Hii heading yako inaelezea kila kitu kuhusu wewe. Kusoma sio lazima kuelimika. Na ukidhani umesimama, wahenga wanasema angalia usianguke.

Hao unaowapigania sababu ni dini yako, ndio wanaharibu Tanzania. sababu watanzania kama mimi hatuangalii mtu sababu ni dini gani, tunamsema sababu ameharibu.
Utakatifu wa mtu si kazi yako kuhukumu maana hata wewe utahukumiwa. Nina hakika Mungu unayemtumikia hana urafiki na wanafiki na waongo. Jipime na kujitafakari.
Kitu kimoja nina hakika. You are a failure. Umeshindwa hata usema au ufanye nini
Asante kwa kuandika nilichofikiri
 
Utulivu kweli kwani kila uchaguzi huku wanauliwa watu na kutiwa vilema , mbali ya ule uvamizi alituvamia 1964 na kuteka nchi yetu , RIH Laanatullahi Nyerere
Bila Nyerere mungekuwa mumechinjana na mumemalizana. Hakuna Zanzibar nje ya Muungano bali kuna Unguja na Pemba
 
Inside,
Tuanze na hili la udini.
Bila shaka unakusudia Uislam.

Hili wala usiwe na shaka.
Nimeandika kitabu sasa maarufu kitabu hiki kimechapwa mara nne.

Kitabu kinaitwa: ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,'' Minerva Press London, 1998.

Sababu ya kuandika kitabu hiki ni pale historia iliyoandikwa ya harakati za uhuru ilifuta mchango wa Waislam.

Nimeweka bold kwa makusudi na kukudhihirishia kuwa hilo ambalo wewe unaliita udini hakika ni Uislam na ndiyo nililokusudia.

Ingekuwa kauli na maandishi yangu ni chuki dhidi ya Nyerere TBC, AZAM, ITV na vyombo vingine vya habari visingekuwa vinakuja kwangu kwa ajili ya kufanya vipindi vinavyomuhusu Nyerere.

Angalia picha hiyo hapo chini nafanya kipindi cha Nyerere Day nimesimama Mtaa wa Stanley na Sikukuu mbele ya nyumba ya Abdul Sykes ambayo Nyerere alifikishwa na Kasella Bantu kuja kutambulishwa kwa Secretary na Act. President wa TAA Abdulwahid Sykes mwaka wa 1952.

Hapo nimezungukwa na watu wengi sana wamevutiwa kuona camera za TV na mimi nazungumza historia ya Nyerere na Abdul Sykes.

Watu wamenizunguka mimi na Jaffar Mponda Mtangazaji wa AZAM wanatusikiliza.

Wamepigwa na butwaa kusikia kuwa Nyerere na Mama Maria waliishi hapo.

Nyumba hiyo ninayoizungumza haipo hivi sasa badala yake kuna ghorofa.

Huwezi kuonyesha chuki dhidi ya Baba wa Taifa TV ikakurekodi na kurusha kipindi Watanzania na dunia wakione.

Kinachokuumiza wewe na mko wengi ni kwa nini historia ya Mwalimu Nyerere kote kazungukwa na Waislam?

Nataka nikufahamishe kitu.

Huko ulikotaja Ujiji, Buguruni na baadhi ya misikiti ya Dar es Salaam huko siko ninakoheshimika.

Mimi naheshimika kwenye Vyuo Vikuu vinavyosomesha African History, Marekani na Ulaya.

View attachment 3001350
View attachment 3001355
Northwestern University, Evanston Chicago


Hakuna cha Uislamu kwenye kugombea uhuru wa Tanganyika bali kuna wananchi wa Tanzania waliopigana kuondoa ukoloni.

Hii mambo ya kuuweka Uislamu mbele ni kukosa akili na kudharau juhudi za waasisi wa Taifa hili waliohakikisha Tanzania inakuwa nchi isiyo na dini.

Kwa kuwa unapenda Uislamu basi nenda Somalia. Wanaongea lugha moja na wote ni Waislamu, lakini wanauana kama wanyama.

Au mzee Mohamed Said hamia Sudan au Afghanistan. Sikutegemea kwa umri wako mkubwa ujikite kwa issues za kidini kiasi hicho. Ni kero
 
Asante kwa kuandika nilichofikiri
Hakuna kitu kibaya kama kuwa loser kwenye maisha, na ukadhani ni mmoja ya watu wenye elimu na akili sana. Unaweza kujikuta unatumbukia shimoni.
Kwa hili la kuleta hadithi zake za kutunga, ameshafeli. Ni mfa maji tu asiyeisha kutapatapa
 
Bila Nyerere mungekuwa mumechinjana na mumemalizana. Hakuna Zanzibar nje ya Muungano bali kuna Unguja na Pemba
Stux...
Unguja na Pemba imekuwapo toka dunia ilipoumbwa.

Tanzania imekuja mwaka wa 1964.

Mimi si Mzanzibari.
 
Hakuna kitu kibaya kama kuwa loser kwenye maisha, na ukadhani ni mmoja ya watu wenye elimu na akili sana. Unaweza kujikuta unatumbukia shimoni.
Kwa hili la kuleta hadithi zake za kutunga, ameshafeli. Ni mfa maji tu asiyeisha kutapatapa
Tanga...
Nimetunga hadithi...

Maasi ya Tanganyika Rifles (TR) mwaka wa 1964 ni hadithi iliyotungwa na Mohamed Said?:

Angalia kipindi cha TBC:


View: https://youtu.be/8VELwiHeHZM?si=Rn69xnK7lIyAOT4e
 
Hakuna cha Uislamu kwenye kugombea uhuru wa Tanganyika bali kuna wananchi wa Tanzania waliopigana kuondoa ukoloni.

Hii mambo ya kuuweka Uislamu mbele ni kukosa akili na kudharau juhudi za waasisi wa Taifa hili waliohakikisha Tanzania inakuwa nchi isiyo na dini.

Kwa kuwa unapenda Uislamu basi nenda Somalia. Wanaongea lugha moja na wote ni Waislamu, lakini wanauana kama wanyama.

Au mzee Mohamed Said hamia Sudan au Afghanistan. Sikutegemea kwa umri wako mkubwa ujikite kwa issues za kidini kiasi hicho. Ni kero
Stux...
Umeghadhibika.
Sikiliza kipindi nilichofanya na DW:


View: https://youtu.be/8a0UyyCVyy4?si=DBg3MBsBudS1nraY
 
Mtu mwenye admission letter na mwenye masters nani ana sifa za kuwa kiongozi by then?
Nan...
Nafasi ya President wa TAA 1953 wakati Abdul Sykes na Hamza Mwapachu wanajitayarisha kuunda TANU hofu ya Hamza Mwapachu ilikuwa wasiunde chama kudai uhuru kiongozi akiwa Muislam.

Alihofu wengine watasita kujiunga na TANU kwa kuona kuwa harakati za siasa ni za Waislam peke yao.

Nimeeleza hapa mara nyingi mkutano wa Abdul Sykes, Ali Mwinyi Tambwe nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio, Ukerewe.

Haikuwa elimu ya Nyerere peke yake iliyomfanya aingizwe kwenye uongozi.

Nafasi ile ilimtaka kiongozi ambae si Muislam ili ajenge umoja kwa kuwavutia wengine waliokuwa nje ya siasa.
 
Nan...
Nafasi ya President wa TAA 1953 wakati Abdul Sykes na Hamza Mwapachu wanajitayarisha kuunda TANU hofu ya Hamza Mwapachu ilikuwa wasiunde chama kudai uhuru kiongozi akiwa Muislam.

Alihofu wengine watasita kujiunga na TANU kwa kuona kuwa harakati za siasa ni za Waislam peke yao.

Nimeeleza hapa mara nyingi mkutano wa Abdul Sykes, Ali Mwinyi Tambwe nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio, Ukerewe.

Haikuwa elimu ya Nyerere peke yake iliyomfanya aingizwe kwenye uongozi.

Nafasi ile ilimtaka kiongozi ambae si Muislam ili ajenge umoja kwa kuwavutia wengine waliokuwa nje ya siasa.
Nyerere alikuwa charismatic na alikuwa na vigezo.Hakupewa favor!Hao wazee wako walimhitaji Mwalimu kuliko Mwalimu alivyowahitaji wao.Mtu charismatic aina ya Nyerere ndo pekee alisikilizwa na jamii yote ya watanzania regardless ya ethnicity na religious orientations
 
Nyerere alikuwa charismatic na alikuwa na vigezo.Hakupewa favor!Hao wazee wako walimhitaji Mwalimu kuliko Mwalimu alivyowahitaji wao.Mtu charismatic aina ya Nyerere ndo pekee alisikilizwa na jamii yote ya watanzania regardless ya ethnicity na religious orientations
Nan...
Waungwana kuna mambo mwiko kukumbusha.
 
Back
Top Bottom