Julius Nyerere Mtume wa Afrika 1950s - Julius Nyerere Mtakatifu Mwenye Kheri 2000s

Julius Nyerere Mtume wa Afrika 1950s - Julius Nyerere Mtakatifu Mwenye Kheri 2000s

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Mwalimu Julius Nyerere historia yake ni kubwa sana.

Walioandika maisha yake wameandika vitabu vitatu zaidi ya kurasa 1000.

Bahati mbaya sana kitabu hiki hakikuweka mengi ambayo yalihusu historia ya Mwalimu na Waislam wa Tanganyika.

Sijui kwa nini.

Kukosekana kwa hili kumeondoa utamu na ladha katika maisha na historia ya Baba wa Taifa kama alivyoishi na watu wa Dar-es-Salaam.

Historia ina kawaida ya kujirudia.

Wakati mwingine mapenzi ya watu kwa viongozi wao yanafika mbali sana.

Sikiliza kisa cha Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU 1954 - 1958:


View: https://youtu.be/cDXRaONNaCY?si=cT3yTTxutMuBv5Gb
 
Katika viongozi waliokuwa na maono na walio litendea haki hili taifa ni JK.Nyerere.

Hata akiitwa mtakatifu haina ttzo,bila yeye tungekua tuna chinjana na kutengana kwa minajili ya dini,ukanda na kubila kama wewe mzee mudi unachotaka kulileta katika taifa hili.
 
Nyerere alikuwa ni mnyama hana utume wowote, alitesa sana waliokuwa wakimpinga na alitutia umasikini wa kutupwa na kufanya wabongo kuwa wavivu wa kutupwa kutegemea kila kitu wafanyiwe na serikali bila kuchangia.
 
Mwalimu Kambarage Nyerere, kama mtu, alikuwa ni mchakato...

Historia haitengenezi watu, watu wanatengeneza historia.

Historia ni uso wa juujuu wa tafsiri za muktadha wa sura za watu/jamii, matendo na matukio/sura ya utukufu wake.

Watu wanaitengeneza 'historia' kwa mujibu wa ule muktadha wa 'maadili na miiko' ujayo na/kwa 'mila na desturi' -- mila na destiri zinazoshindanishwa kimapana ya nyakati na matukio na utashi--'Wakati-Jamii-Machaguo ya Kitaasisi-Matukio'....

'Mila na desturi' ni mambo yajayo na kadiri ya kiasi cha mwangaza/Elimu ama mapokeo ya jamii--lakini mwangaza ni jambo kuu kuliko 'mila na desturi' yeyote.

Kambarage Nyerere alikuwa ni 'Mtu wa Mwangaza'--watu wa mwangaza wananamna ya kutizamwa na kubayanishwa asili ya matendo yao, na basi nguzo za imani zinazokadirisha mapana ya 'dhamira, uono na vina vya tafsiri' kwa ajili ya kujichagulia kwao..

Hili linafanya sura sahihi ya kubayanisha muktadha wa wito, matendo na urithi/legasi ya mtu wa mwangaza kuwa na ufundi wake mahususi--si jambo la hoja, mijadala na midahalo.

Ufundi huu unaitwa Elimu 2.0: Uono na ufikirifu mifumo.

Mambo ya elimu 2.0 na Elimu 3.0 ndiyo yanaweza kubangulia undani wa wito, matendo na legasi ya Mwalimu Nyerere. In Shaa Allah, hili tunakuja kulifahamu ilivyobora wakati muafaka; na linatengeneza kitovu cha 'kuifumua historia mbovu' na 'vina visivyo sahihi vya tafsiri ya wito, matendo na legasi'--Hata ya Mwalimu Nyerere; kwa kuwa kuna upande wa ndani wa mambo ambavyo watu wa namna hii ama ile, silika hiii ama ile, imani hii ama ile hongozwa kukadirisha 'Jaala' ya 'Waja Wema'...

Kwa hivyo hata mambo ya kukadirisha muktadha na kadiri ya 'Utume' wa mtu fulani ni jambo la 'Usanii' tu; lina makusudi yake--yanaweza kuwa ni 'mema' ama 'si mema hasa'. Inategemeana na upeo wa mtu kiakili, kihisia na kiroho.

Watu wa mapana hasa--mapana hasa ya kiakili, hisia na kiroho--watu wa Elimu 3.0 ndiyo wenye 'Utashi wa kweli' na 'Hekima'.

Hawa wakidhihiri hekima hiyo kwa umma ndipo ndipo umma utazinduka na kuzifahamu mbichi na mbivu za ustaarabu na ustawi wao...

Watu wa hekima hawafanyi vikundi vya mipango na hadaa, bali hawa hasa ni walinzi na waongozeaji wa hatma za jamii, mataifa na tawala. Kuwa mmoja wao si suala la 'maombi na kukubaliwa' ili kuifanya 'Taasisi fulani'; watu hawa 'hujichagua/kujichagulia wenyewe' na 'kufanya yao'--husaidiana kwa sura ya wazi na sura isiyo ya wazi kuitengeneza njia ya 'dhamira zao njema'.

Historia ndiyo inaweza kupotosha isipoweza kubaini ama kuotea 'matendo ya ndani' ya 'washirika' katika kuongozea umma -- kuongozea umma katika utu bora na maendeleo...

Siku si nyingi karibia kila kitu kitafahamika kuhusu 'Uhuru wa Ndani' wa wanajamii na 'Ushirika katika Imani ya UTU wema'--jambo linalokwenda kuwa chachu kuu ya mageuzi na mapinduzi ya kijamii Tanzania, Afrika na Duniani...

'Utume wa Nyerere' ni fumbo la Imani kwa watu 'wasio na macho'--kusubiri wengine wawape tafsiri ya mambo...

'Utume wa Nyerere' ni fumbo la kuitika wito wa kudhamiria UTU bora, Amani na Mapenzi mema Duniani.

'Utume wa Nyerere' ni fumbo la kubidi kufumbuliwa kitendawili cha 'Mapinduzi'-- Mapinduzi ni 'Muda wa Ufunuo', na hali 'mapinduzi endelevu' ni 'ukuwakujia wa UTU bora', 'Amani' na 'Mapenzi mema duniani'...

Hmmm
 
Mwalimu Julius Nyerere historia yake ni kubwa sana.

Walioandika maisha yake wameandika vitabu vinne zaidi ya kurasa 1000.

Bahati mbaya sana kitabu hiki hakikuweka mengi ambayo yalihusu historia ya Mwalimu na Waislam wa Tanganyika.

Sijui kwa nini.

Kukosekana kwa hili kumeondoa utamu na ladha katika maisha na historia ya Baba wa Taifa kama alivyoishi na watu wa Dar-es-Salaam.

Historia ina kawaida ya kujirudia.

Wakati mwingine mapenzi ya watu kwa viongozi wao yanafika mbali sana.

Sikiliza kisa cha Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU 1954 - 1958:


View: https://youtu.be/cDXRaONNaCY?si=cT3yTTxutMuBv5Gb

Wakati mwingine, tukubali kung'atuka. Hii Viseo Mzee mwenzangu ina ujumbe gani kwetu wasikilizaji. Haieleweki
 
Nyerere alikuwa ni mnyama hana utume wowote, alitesa sana waliokuwa wakimpinga na alitutia umasikini wa kutupwa na kufanya wabongo kuwa wavivu wa kutupwa kutegemea kila kitu wafanyiwe na serikali bila kuchangia.
Miaka zaidi ya 20 amakufa,na miaka zidi ya 30 tangu alipoacha na na uraidi,mbona huo utajiri siuoni,ach kulia lia pambana mtoto wa kiume utaolewa bure.
 
Miaka zaidi ya 20 amakufa,na miaka zidi ya 30 tangu alipoacha na na uraidi,mbona huo utajiri siuoni,ach kulia lia pambana mtoto wa kiume utaolewa bure.
Mbuzi wewe
Mwanaume unaweka picha ya mwanaume mwenzako kwenye avatar, utakuwa una vinasaba vya upunga
Mtoto mdogo kwanza wewe nenda kamuulize baba yako alivyokuwa anavaa nguo za viraka na kupanga foleni kwenye duka la kaya
 
Wakati mwingine, tukubali kung'atuka. Hii Viseo Mzee mwenzangu ina ujumbe gani kwetu wasikilizaji. Haieleweki
Wakati mwingine, tukubali kung'atuka. Hii Viseo Mzee mwenzangu ina ujumbe gani kwetu wasikilizaji. Haieleweki
Narumuk,
Hiyo video imetanguliwa na maelezo naeleza ukubwa wa historia ya Nyerere na vipi waandishi wa historia yake walivyoipunguza kwa kukosa kueleza jinsi alivyoingiliana na watu wa Dar-es-Salaam.

Laiti wangefanya hivyo wangeijua historia kama hii ya Sheikh Suleiman Takadir alipomnyanyua Nyerere na kumtia kwenye daraja la Utume kwa Bara la Afrika.

Utume anatoa Mwenyezi Mungu.

Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU kwa hili amelipiku Kanisa kwa mbali sana kwa kutoa cheo cha "Mwenye Kheri" cheo wanachotoa binadamu.

Kwenye video naeleza nguvu ya chama cha TANU kupitia Tawi la Mtaa wa Mvita.

Kwenye video naeleza jinsi TANU ilivyokuwa na mbinu ya kumzingira Mwingereza.

Serikali imempiga marufuku Nyerere asifanye mkutano.

TANU inapiga taarab na kuwaalika watu waende kusikiliza na katika mkusanyiko ule Nyerere anasalimiana na wananchi.

Kwa kitendo hiki Nyerere bado anaonekana na wananchi wakiwa nyuma yake.

Njama za Gavana Edward Twining zinaambulia patupu.

Ikiwa bado hujaelewa nifahamishe.
 
Pamoja na madhaifu yake mengi, ila mwalimu Nyerere alikua genius sana kuweza kudhibiti ukanda na udini haikua kazi ndogo
Mpaji...
Katika kitabu cha Abdul Sykes: "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,"(1998) sehemu ya tatu ya kitabu anuani yake ni hii: "Conspiracy Against Islam."

Nini kilitokea baada ya uhuru 1961 kupelekea EAMWS kuvunjwa bila ridhaa ta Waislam wakati inajenga Chuo Kikuu na serikali kuunda BAKWATA.

Ukitaka kujua tatizo la dini ni lazima usome hii sehemu ya tatu ya kitabu.

Naweza kukupa rejea nyingine lakini muhimu uanze hapo.

Muhimu pia usikilize audio hapo chini.

Haya mambo yanataka utafiti si ya kusema bila ushahidi wenye ithibati:


View: https://youtu.be/toPDVAgEJu0?si=NsSl26z900MXQWQ2
 
Ili nijue tatizo la udini ni mpaka nisome kwenye kitabu chako?

Katika hali ya kawaida siwezi fanya observation?
Mpaji...
Hapana si lazima usome kitabu changu.

Unaweza ukasoma kitabu cha Bergen (1981), Sivalon (1992) na Njozi (2002).

Kitabu cha Njozi kilipigwa marufuku na serikali.

Hivyo viwili vimeondolewa kimya kimya.

Havitakuwi visomwe.

Observation ni sehemu ya vipengele vinavyotumika katika utafiti lakini kusoma tafiti ni muhimu sana.
 
Mwalimu Julius Nyerere historia yake ni kubwa sana.

Walioandika maisha yake wameandika vitabu vitatu zaidi ya kurasa 1000.

Bahati mbaya sana kitabu hiki hakikuweka mengi ambayo yalihusu historia ya Mwalimu na Waislam wa Tanganyika.

Sijui kwa nini.

Kukosekana kwa hili kumeondoa utamu na ladha katika maisha na historia ya Baba wa Taifa kama alivyoishi na watu wa Dar-es-Salaam.

Historia ina kawaida ya kujirudia.

Wakati mwingine mapenzi ya watu kwa viongozi wao yanafika mbali sana.

Sikiliza kisa cha Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU 1954 - 1958:


View: https://youtu.be/cDXRaONNaCY?si=cT3yTTxutMuBv5Gb

Mtakatifu Nyerere ndiye binadamu wa kwanza duniani kuyaunganisha zaidi ya makabila 120 kuwa kitu kimoja.
Mtakatifu Nyerere kila alilolifanya hata kama lilikuwa kosa lilikuwa na nia njema kwa maslahi ya taifa la Tanzania.
Hakuna mbaguzi wa kidini atampenda mtakatifu Nyerere kwa sababu mtakatifu Nyerere angependa kuibadili hii nchi iwe ya dini yake kusingekuwa na wa kumzuia.
Mtakatifu Nyerere alikuwa mzalendo kwelikweli na aliipenda nchi hii upeo.
Mtakatifu Nyerere ndiye nembo ya uadilifu ya bara la Afrika,hakujilimbikizia mali wala kuuza raslimali za taifa letu.
Alichukia wezi,mafisadi, wadini na wajinga wore wenye nia ya kuligawa taifa.
Fikra na mawazo ya mtakatifu Nyerere ziendelee kudumu
 
Narumuk,
Hiyo video imetanguliwa na maelezo naeleza ukubwa wa historia ya Nyerere na vipi waandishi wa historia yake walivyoipunguza kwa kukosa kueleza jinsi alivyoingiliana na watu wa Dar-es-Salaam.

Laiti wangefanya hivyo wangeijua historia kama hii ya Sheikh Suleiman Takadir alipomnyanyua Nyerere na kumtia kwenye daraja la Utume kwa Bara la Afrika.

Utume anatoa Mwenyezi Mungu.

Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU kwa hili amelipiku Kanisa kwa mbali sana kwa kutoa cheo cha "Mwenye Kheri" cheo wanachotoa binadamu.

Kwenye video naeleza nguvu ya chama cha TANU kupitia Tawi la Mtaa wa Mvita.

Kwenye video naeleza jinsi TANU ilivyokuwa na mbinu ya kumzingira Mwingereza.

Serikali imempiga marufuku Nyerere asifanye mkutano.

TANU inapiga taarab na kuwaalika watu waende kusikiliza na katika mkusanyiko ule Nyerere anasalimiana na wananchi.

Kwa kitendo hiki Nyerere bado anaonekana na wananchi wakiwa nyuma yake.

Njama za Gavana Edward Twining zinaambulia patupu.

Ikiwa bado hujaelewa nifahamishe.
Kudhibiti ukanda na udini haikuwa kazi ndogo.Ungekuwa wewe usingeweza Mkuu wangu.Mwalimu apewe maua yake.Bila Mwalimu kusingekuwa na wakristu mijini.Mwalimu alifanikiwa kufanya intergration ya hali ya juu kabisa.Hufurahii haya mkuu wangu?
 
Mtakatifu Nyerere ndiye binadamu wa kwanza duniani kuyaunganisha zaidi ya makabila 120 kuwa kitu kimoja.
Mtakatifu Nyerere kila alilolifanya hata kama lilikuwa kosa lilikuwa na nia njema kwa maslahi ya taifa la Tanzania.
Hakuna mbaguzi wa kidini atampenda mtakatifu Nyerere kwa sababu mtakatifu Nyerere angependa kuibadili hii nchi iwe ya dini yake kusingekuwa na wa kumzuia.
Mtakatifu Nyerere alikuwa mzalendo kwelikweli na aliipenda nchi hii upeo.
Mtakatifu Nyerere ndiye nembo ya uadilifu ya bara la Afrika,hakujilimbikizia mali wala kuuza raslimali za taifa letu.
Alichukia wezi,mafisadi, wadini na wajinga wore wenye nia ya kuligawa taifa.
Fikra na mawazo ya mtakatifu Nyerere ziendelee kudumu
Nan...
Huwa kuna mambo mengine napata shida kuyaeleza kwani najisikia vibaya.

Haya ni yale ambayo wengi mmeyaamini kutokana na mliyojifunza katika historia iliyokuwa si ya kweli.

Hapajakuwa na tatizo baina ya makabila.

Hayo mengine uliyoeleza inahitaji usome hizo rejea nilizoweka: Bergen, Sivalon na Njozi.

Utakutana na mambo ambayo hukuwa unayajua.
 
Kudhibiti ukanda na udini haikuwa kazi ndogo.Ungekuwa wewe usingeweza Mkuu wangu.Mwalimu apewe maua yake.Bila Mwalimu kusingekuwa na wakristu mijini.Mwalimu alifanikiwa kufanya intergration ya hali ya juu kabisa.Hufurahii haya mkuu wangu?
Nan...
Hapajakuwa na tatizo la dini baina ya Waafrika wenyewe.

Laiti lingekuwapo isingewezekana Nyerere kutiwa katika uongozi wa TAA 1953 na TANU ikaundwa 1954 Nyerere akiwa kiongozi mkuu.

Historia hii ya kikao cha Nansio nyumbani kwa Hamza Mwapachu kuweka mipango ya kumuingiza Nyerere katika uongozi wa TAA nimeieleza mara nyingi sana.

Kitabu cha Abdul Sykes kimeeleza hili kwa kirefu.

Kwa bahati mbaya historia hii haikuwa inafahamika.

Unaeleza fikra zako kutokana na historia uliyosomeshwa ambayo haikuwa sawa.

Angalia video hiyo kipindi cha TBC1 naeleza vipi Nyerere alivyochaguliwa kuongoza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Unaweza kusoma historia yote ya Mwalimu Nyerere hapa:

mohamedsaidsalum.blogspot.com.



View: https://youtu.be/oLkefadOoJ0?si=EoMPlmY2QdWclftV
 
Nan...
Huwa kuna mambo mengine napata shida kuyaeleza kwani najisikia vibaya.

Haya ni yale ambayo wengi mmeyaamini kutokana na mliyojifunza katika historia iliyokuwa si ya kweli.

Hapajakuwa na tatizo baina ya makabila.

Hayo mengine uliyoeleza inahitaji usome hizo rejea nilizoweka: Bergen, Sivalon na Njozi.

Utakutana na mambo ambayo hukuwa unayajua.
Legacy ya Mwalimu haiwezi kufutwa kizembe maalim.Ni kiongozi ambaye Africa haijawahi pata mfano wake.Kwa uelewa wako ukipewa nafasi ya kumlinganisha na marais wote wa Tanzania,yupi anamzidi Mwalimu intergrity na uzalendo?
 
Nan...
Huwa kuna mambo mengine napata shida kuyaeleza kwani najisikia vibaya.

Haya ni yale ambayo wengi mmeyaamini kutokana na mliyojifunza katika historia iliyokuwa si ya kweli.

Hapajakuwa na tatizo baina ya makabila.

Hayo mengine uliyoeleza inahitaji usome hizo rejea nilizoweka: Bergen, Sivalon na Njozi.

Utakutana na mambo ambayo hukuwa unayajua.
Legacy ya Mwalimu haiwezi kufutwa kizembe maalim.Ni kiongozi ambaye Africa haijawahi pata mfano wake.Kwa uelewa wako ukipewa nafasi ya kumlinganisha na marais wote wa Tanzania,yupi anamzidi Mwalimu intergrity na
Nan...
Hapajakuwa na tatizo la dini baina ya Waafrika wenyewe.

Laiti lingekuwapo isingewezekana Nyerere kutiwa katika uongozi wa TAA 1953 na TANU ikaundwa 1954 Nyerere akiwa kiongozi mkuu.

Historia hii ya kikao cha Nansio nyumbani kwa Hamza Mwapachu kuweka mipango ya kumuingiza Nyerere katika uongozi wa TAA nimeieleza mara nyingi sana.

Kitabu cha Abdul Sykes kimeeleza hili kwa kirefu.

Kwa bahati mbaya historia hii haikuwa inafahamika.

Unaeleza fikra zako kutokana na historia uliyosomeshwa ambayo haikuwa sawa.

Angalia video hiyo kipindi cha TBC1 naeleza vipi Nyerere alivyochaguliwa kuongoza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Unaweza kusoma historia yote ya Mwalimu Nyerere hapa:

mohamedsaidsalum.blogspot.com.



View: https://youtu.be/oLkefadOoJ0?si=EoMPlmY2QdWclftV

Nyerere hakuingizwa kwenye harakati kwa kuonewa huruma,he earned it kwa merits mzee!
Shida ni kwamba unaieleza as if Mwalimu alipewa favor kwa kuonewa huruma.Mwalimu alikuwa na elimu na akili na mbali na vyote he was charismatic as compared to other colleagues at that time.Kiufupi He deserved it.He was smarter than the sykes etal.The Mwapachus needed Mwalimu more than he needed them.
Kama ambavyo nimewahi kukueleza hapo awali na leo narudia,Wewe huna hati miliki ya ukweli kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.Silazimiki kuamini sources unazozitoa kwa sababu katika kusoma kwangu nimeufahamu ukweli
 
Legacy ya Mwalimu haiwezi kufutwa kizembe maalim.Ni kiongozi ambaye Africa haijawahi pata mfano wake.Kwa uelewa wako ukipewa nafasi ya kumlinganisha na marais wote wa Tanzania,yupi anamzidi Mwalimu intergrity na uzalendo?
Legacy ya Mwalimu haiwezi kufutwa kizembe maalim.Ni kiongozi ambaye Africa haijawahi pata mfano wake.Kwa uelewa wako ukipewa nafasi ya kumlinganisha na marais wote wa Tanzania,yupi anamzidi Mwalimu intergrity na uzalendo?
Nan...
Umesema kweli "legacy" ya Mwalimu ni kubwa.

Kitabu cha Abdul Sykes kimepata umaarufu sababu yake ni Nyerere.

Kitabu kimeeleza yale ambayo Nyerere mwenyewe hakupata kuyasema wala mwanahistoria yeyote kuyaandika.

Hiki ndicho kilichowavutia watu wengi.
Lakini wako waliofadhaishwa na kitabu hiki kwa kuona kuwa Nyerere anagawana historia yake na watu ambao wao hawakupata kuwasikia hata siku moja.

Wako waliojiuliza mbona historia hii tunayosoma leo haikusomeshwa?

Iweje kadi za TANU tatu za mwanzo mbili ni za ndugu wawili khalis Abdulwahid na Ally Sykes?

Nini maana ya jambo hili?

Hili si suala la uadilifu au uzalendo wa Nyerere.

Maswali ninayoulizwa kote vyuoni ninapozungumza ni imekuwaje taifa likapoteza historia yake yote ya wazalendo wake waliopigania uhuru?

Prof. Haroub Othman hili lilimtatiza.

Angalia video hiyo namzungumza Prof. Haroub alivyotafuta maelezo kutoka kwa Mwalimu Nyerere:


View: https://youtu.be/lCyNc0C46Zo?si=X11DvnNUTCtbaOak
 
Back
Top Bottom