Julius Nyerere: Tunao wanasiasa wana tabia za kimalaya malaya, heshima yao inauzwa na ina bei (mercenary)

Julius Nyerere: Tunao wanasiasa wana tabia za kimalaya malaya, heshima yao inauzwa na ina bei (mercenary)

Jk
jk%2B2.jpg
 
Wakuu,

Nlikuwa nasikiliza hotuba ya baba wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyoitoa Julai 22 mwaka 1967 Baada ya kuwapokea Vijana waliotembea kwa Miguu kutoka Moshi.

Alikuwa anaongelea kuhusu wanasiasa kununulika, Yaani hawa wananunulia na kusaliti vyama vyao au jamii iliyowachagua kwa vipande vya pesa akawaita ni Mwanasiasa Malaya ambao wao wanajali hela tu kama mercenary.

Nikaona inaendana na Wakati huu tulionao wa wanasiasa kuhama vyama ambapo inadaiwa baadhi yao wananunuliwa na wengine wanahama kwa utashi wao.

Hapa chini namnukuu alichokionge kuhusu wanasiasa wanaoambatana na mtu kisa tu wamepewa hela.

Anaanza kwa kusema, "Unakuta mtu anafuatana nalo hadi unajiuliza, huyu anafuatana nalo kwanini? Manake si heshima huyu kuandamana na yule, lakini unagundua anaandamahela. Hii ni tabia ya Kimalaya malaya. Na tunao wanasiasa wenye tabia ya Kimalaya malaya namna hii, wananunulika, heshima yao inauzwa, ina bei. Anakuuliza anaona... unasema fanya kitendo kadhaa ambacho ni kitendo cha aibu, lakini anakuuliza ngapi bwana?, Ukitoa bei ukimlipa basi, anakubali. Mwanasiasa ana tabia ya kimalaya malaya.

Mtu mwenye tabia ya kimalaya malaya ananunulika anafikiri kila mtu ananunulika. Kwahiyo anatoka anaenda kwa watu wengine, anadhani watu wengine wanaweza kufanya mambo ya aibu aibu ambayo hayana heshima..halafu anajuta, anajuta.

Kuna majeshi duniani humu yanaitwa Majeshi ya mercenary, yalikuwa hapo Congo, wengine ni vijana wadogo mnajua mercenary. mercenary ni mtu anafanya kazi kwa malipo, kwa pesa tu. Sababu yake kufanya kitendo kile ni pesa tu. Ukimuuliza kwanini unafanya hivi? anakujibu nalipwa.

Na hajali nani anayemlipa. INawezekana nchi mbili adui zinapigana hii na hii, anaweza kwenda kwa hii akasema mtanialipa? Kama hamuwezi kumlipa atawapigania hawa wengine kuua hawa. Yeye hana upande, anajua pesa tu. Maaskari hawa wanaitwa mercenary... anajua pesa tu, ni Malaya Malaya tu. Yupo tayari kuua au kuchukua hatari ya kuuawa sababu ya pesa tu. Askari wa kawaida yupo tayari kuua au kufa kwa sababu ya heshima ya nchi yake.

Lakini huyu yupo tayari kufa au kuuawa kwa sababu ya pesa tu. mercenary ana tabia ya Kimalaya Malaya tu.

Na tunao Wanasiasa mercenary, ni mercenary. Mtu yoyote anaweza kuwalipa tu, mtu yoyote, anakwambia mapesa haya hapa, utanifanyia kazi

Na tunayo mijitu humu, inafanya kazi si za wananchi hapa ni za watu wengine..hawa ni mercenary.. malaya Malaya tu. Halafu wapumbavu hawa, wanafikiri tunaunda jeshi la mercenary, wendawazimu hawa.

Sasa wamekiona cha mtema kuni. Na tumewatangazia, tumesema waende wapumbavu hawa kama hatujawatia ndani wote hawa. Tumepata aibu mara moja wanafikiri tunaweza kupata aibu mara mbili tena.

Jeshi letu ni jeshi la Wananchi wa Tanzania..sijui hawaelewi!!? Ni jeshi la Wananchi wa Tanzania Sio jeshi la Vibaraka Malaya Malaya eeh?.

Kwahiyo Vijana msijali, Msiwe na wasiwasi hata kidogo. Tunawajua, tutawasaka mmoja mmoja, mmoja mmoja.. Malaya watupu hawa, tutawasaka mmoja mmoja, na kila tutakapo wasaka tutawatangazieni kwamba Malaya mmoja tumeshamshika." Mwisho wa kumnukuu.

Je, unamtizamo gani juu ya haya aliyoyasema kutokana na hizi zama tulizo nazo. Je, wanaohama Wanaunga juhudi za rais au ni mercenary?


Mwenye kamusi ya TUKI anisaidie tafsiri ya neno "MALAYA"
 
Hivi ccm wanajisikiaje wakisikia hotuba ya mwalimu juu ya Malaya wa kisiasa au askari wa kulipwa mercenaries
Naomba wanaccm mje mtuambie ile hotuba mnaitafsirije?

Naomba mwenye namba ya waitara na wasaliti wote walionunulika watumiwe hotuba ile ya mwalimu kupitia wasap
Kabla hujaipata number ya Waitara, kwanza si ungewatumia akina Lowasa, Sumaye na Nyalandu, alafuatilia hao wengine. Tuache siasa za kinafiki na kishirikina.
 
Naona hapa kwetu kuna mambo kama hayo wanaendelea wasikie Maneno ya Mwalimu kwamba " wana tabia za kimalaya malaya wana bei,wananunulika, watajuta baadae!".
 
Tunao wanasiasa leo hii, malaya malaya. Tunawajua. Wananunulika wanahama chama kwa pesa. Malaya malaya hawa.

Wapo, naweza kuwaweka hapa chini, wapumbavu hawa, wendawazimu. Malaya watupu hawa.
Inasikitisha Malaya Malaya anapotoka kanda maalumu!!!! Ni Malaya tu!
 
Wakuu,

Nlikuwa nasikiliza hotuba ya baba wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyoitoa Julai 22 mwaka 1967 Baada ya kuwapokea Vijana waliotembea kwa Miguu kutoka Moshi.

Alikuwa anaongelea kuhusu wanasiasa kununulika, Yaani hawa wananunulia na kusaliti vyama vyao au jamii iliyowachagua kwa vipande vya pesa akawaita ni Mwanasiasa Malaya ambao wao wanajali hela tu kama mercenary.

Nikaona inaendana na Wakati huu tulionao wa wanasiasa kuhama vyama ambapo inadaiwa baadhi yao wananunuliwa na wengine wanahama kwa utashi wao.

Hapa chini namnukuu alichokionge kuhusu wanasiasa wanaoambatana na mtu kisa tu wamepewa hela.

Anaanza kwa kusema, "Unakuta mtu anafuatana nalo hadi unajiuliza, huyu anafuatana nalo kwanini? Manake si heshima huyu kuandamana na yule, lakini unagundua anaandamahela. Hii ni tabia ya Kimalaya malaya. Na tunao wanasiasa wenye tabia ya Kimalaya malaya namna hii, wananunulika, heshima yao inauzwa, ina bei. Anakuuliza anaona... unasema fanya kitendo kadhaa ambacho ni kitendo cha aibu, lakini anakuuliza ngapi bwana?, Ukitoa bei ukimlipa basi, anakubali. Mwanasiasa ana tabia ya kimalaya malaya.

Mtu mwenye tabia ya kimalaya malaya ananunulika anafikiri kila mtu ananunulika. Kwahiyo anatoka anaenda kwa watu wengine, anadhani watu wengine wanaweza kufanya mambo ya aibu aibu ambayo hayana heshima..halafu anajuta, anajuta.

Kuna majeshi duniani humu yanaitwa Majeshi ya mercenary, yalikuwa hapo Congo, wengine ni vijana wadogo mnajua mercenary. mercenary ni mtu anafanya kazi kwa malipo, kwa pesa tu. Sababu yake kufanya kitendo kile ni pesa tu. Ukimuuliza kwanini unafanya hivi? anakujibu nalipwa.

Na hajali nani anayemlipa. INawezekana nchi mbili adui zinapigana hii na hii, anaweza kwenda kwa hii akasema mtanialipa? Kama hamuwezi kumlipa atawapigania hawa wengine kuua hawa. Yeye hana upande, anajua pesa tu. Maaskari hawa wanaitwa mercenary... anajua pesa tu, ni Malaya Malaya tu. Yupo tayari kuua au kuchukua hatari ya kuuawa sababu ya pesa tu. Askari wa kawaida yupo tayari kuua au kufa kwa sababu ya heshima ya nchi yake.

Lakini huyu yupo tayari kufa au kuuawa kwa sababu ya pesa tu. mercenary ana tabia ya Kimalaya Malaya tu.

Na tunao Wanasiasa mercenary, ni mercenary. Mtu yoyote anaweza kuwalipa tu, mtu yoyote, anakwambia mapesa haya hapa, utanifanyia kazi

Na tunayo mijitu humu, inafanya kazi si za wananchi hapa ni za watu wengine..hawa ni mercenary.. malaya Malaya tu. Halafu wapumbavu hawa, wanafikiri tunaunda jeshi la mercenary, wendawazimu hawa.

Sasa wamekiona cha mtema kuni. Na tumewatangazia, tumesema waende wapumbavu hawa kama hatujawatia ndani wote hawa. Tumepata aibu mara moja wanafikiri tunaweza kupata aibu mara mbili tena.

Jeshi letu ni jeshi la Wananchi wa Tanzania..sijui hawaelewi!!? Ni jeshi la Wananchi wa Tanzania Sio jeshi la Vibaraka Malaya Malaya eeh?.

Kwahiyo Vijana msijali, Msiwe na wasiwasi hata kidogo. Tunawajua, tutawasaka mmoja mmoja, mmoja mmoja.. Malaya watupu hawa, tutawasaka mmoja mmoja, na kila tutakapo wasaka tutawatangazieni kwamba Malaya mmoja tumeshamshika." Mwisho wa kumnukuu.

Je, unamtizamo gani juu ya haya aliyoyasema kutokana na hizi zama tulizo nazo. Je, wanaohama Wanaunga juhudi za rais au ni mercenary?


wakihama ccm kwenda upinzani wanaitwa wamejitambua na wazalendo wakihamia ccm wanaitwa malaya so malaya ni hawa

lyatonga mrema
jems mbatia
zito kabwe
kitila mkumbo
juliana shonza
edward lowasa
Frederick, sumaye
na n.k
nchi hii imejaa malaya wengi kama ni hivyo kibaya ni uchama chama
 
Toeni povu ila nyerere anawaumbua mchana kweupeeeee malaya
 
Hivi ccm wanajisikiaje wakisikia hotuba ya mwalimu juu ya Malaya wa kisiasa au askari wa kulipwa mercenaries
Naomba wanaccm mje mtuambie ile hotuba mnaitafsirije?

Naomba mwenye namba ya waitara na wasaliti wote walionunulika watumiwe hotuba ile ya mwalimu kupitia wasap
nikupe namba ya lowasa
 
Na kipindi hiki kuna MALAYA wengi sana Mwalimu NYERERE!
 
Baba wa Taifa anaongea kama Lusinde Kibajaji wa Ludewa, misengenyo, matusi na uchochezi.

Anawachochea wana usalama wake wawatie ndani viongozi malaya, wakati kisheria hakuna kosa la kiongozi malaya, Baba wa Taifa hajui maana ya utawala wa sheria.

Halafu anadanganya kwamba wapo, anawajua, atawakamata na akiwakamata atawaambia wananchi, he never did that.
 
Leo hii tunafanya ziara na maburungutu ya noti; wala sio makaratasi ya cheki! Roho ikifurahi maburungutu nje, kwa nini malaya wasijitokeze kujiuza.

Kwa hiyo hali ya kimalaya malaya inaruhusiwa sana wakati huu; ni biashara inayolipa.

Kama wewe ni kiongozi na unajua umepewa nyumba, gari na unalipwa mshahara unalazimishwa na kuhimizwa kuwa malaya kwa kufanya yampendezayo aliyekupa ulaji huo na anakufanya uamini hela ni yake na anaitoa kwa hisani yake.

Chama chote kinakuwa kama gulio la malaya, hakuna anayeguna! Kwa nini malaya wasivune!
 
Back
Top Bottom