Kabla hujaoa Usukumani, zingatia haya ili ndoa yako idumu

Kabla hujaoa Usukumani, zingatia haya ili ndoa yako idumu

Sema katika jamii ya wasukuma uke wenza ni nje nje na jambo la kawaida sana pamoja na Kwamba ni wakristo.
Sijui ni Kwanini ??
Tuseme kanda ya ziwa kote huko bara iko hivyo.
Nimekuja kujua hilo Mwaka Jana Sijui Mwaka juzi tu.
Mimi nilijua sababu ni wakristo ni mke mmoja kumbe thubutuuu yake !

Ukimuuliza msukuma yeyote randomly “ kwenu mmezaliwa wangapi ?
Atakuuliza kwanza ;
“ kwa mama tu au kwa baba “ ??
Maana yake kwa baba huwa ni zaidi ya mama mmoja.

Kwa hiyo wale wanawake mnaotegemea kuingia kwenye uhusiano na wanaume wa kisukuma kuweni na hiyo provision 👌👌👌
Na wanaume wa bara wakurya, wahaya n.k
Na uzoefu unaonesha mke ukiolewa ukijitia choyo na jeuri mma mkwe anamtafutia mwanae mwanamke mwingine wa kumpa furaha na utulivu,
Shoga yangu ukijakujua na watoto walishazaliwa siku nyingi.
Kaza roho.
Hii ni kweli nilishangaa huko Magu mzee na heshima zake tena msabato ana wake wawili live
 
Nikiona mada za watu wanasema wasukuma ni washamba huwa nacheka sana maana kwa uzoefu wangu wa kuzunguuka vijijini na mijini kwenye maeneo mengi ya nchi nimegundua washamba wapo wengi sana bila kujali kabila ila wasukuma wanaonekana washamba kutokana na kuwa ni wapambanaji na risk taker kwa maana ya kwamba ni kawaida kwa msukuma kutoka kijijini kwake na kwenda mkoa wowote kwa gharama zake bila woga wala kuomba msaada kwa yoyote. Sasa unategemea mtu atoke kijijini alafu ukutane nae wewe wa mjini atakuwa na mtazamo kama mtu wa mjini. Makabila mengine yanajificha kwenye kigezo cha ujanja ila ukweli ni kwamba asilimia kubwa huwa wanabaki maeneo waliyozaliwa kwa muda mrefu na hata akitoka anatoka kwa hofu na mtu wa kumokea mjini anakuwepo huku muda mwingi yupo kimya anasikilizia asigundulike wa kuja. Ila msukuma akipanda kwenye gari wakiwa wawili watatu wanajiachia na story tu wengine wanabaki kuwashangaa
Uko sahihi,resources kama ardhi ni changamoto kwa hiyo wanaume wengi hujiongeza kutafuta ardhi popote pale.

Tofauti na wanawake wa kisukuma ukitaka kumuoa ukimwambia tukaishi mkoa wa mbali yuko radhi avunje hiyo ndoa ila sio kwenda ugenini
 
Obheja mimi wa Dar sasa nishampenda msukuma sasa[emoji23][emoji23]
kuwa na heshima tu,na uanze jeramba la kusonga ugali mgumu na kutikisa maziwa kwenye kibuyu!karibu nyumbani shemeji
 
kuwa na heshima tu,na uanze jeramba la kusonga ugali mgumu na kutikisa maziwa kwenye kibuyu!karibu nyumbani shemeji

Woyi sio wakijijini ni wa mjini ni zile familia wote wasomi… sizani kama bado wapo primitive kiasi cha kutaka iwe lazima mimi kujua kupika hivyo
 
Kuna jirani yangu mmoja hapa Dom ni askari polisi (huwa natoka na mkewe kisirisiri) huyu mwamba mkewe ni msukuma kuna kipindi alipata kutembelewa na timu ya watu 9 Yaani baba Mkwe na mama Mkwe,

wadogo wa mkewe na Kaka mkubwa wa mkewe akiwa na mke na watoto Yaani jamaa ailkosa nafasi ya kuwalaza wageni ikabidi aje kuomba nafasi nyumba moja ya mama mmoja mstaafu hapa jirani Yaani wageni walijaa nyumbani eti wamekuja kusalimia mke wa jamaa baada ya kujifungua halafu walikaa zaidi ya mwezi jamaa alinyooka maana budget ya siku ilipanda mara dufu!
Wewe mwamba unajiamini unatoa code
Ngoja wakudake upakwe wese[emoji3][emoji1787]
 
Woyi sio wakijijini ni wa mjini ni zile familia wote wasomi… sizani kama bado wapo primitive kiasi cha kutaka iwe lazima mimi kujua kupika hivyo
kuna siku mtaenda kutembelea ndugu,au utakuwa mpenz mtazamaji?anyway people change,lakin ni vyema kudokoa vitu fulan ili usiwe mgen sana!
 
Si unamuoa msukuma mwenzako afande?
Hivi hiyo chale kwanza inakuaje yani?
chale nimekua naziona sijui ilikuwaje, ila wanasema ni imani yao kuwa wanalindwa zidi ya uchawi. tangu nikue nikajitambua sioni tena faida yake
 
Mbona umefungua saana code,umejiweka wazi na umemuweka wazi mke wa Askari kujulikana

Jirani yako
Askari polisi
Mkewe unaetembea nae ni msukuma

Alishatembelewa na familia nzima
Askari akiiona hii,ameshapata mchoro
Kweli kabisa ameweka code peupe
 
Back
Top Bottom