Kabla ya Bagamoyo, Palikuwepo na mpango wa Bandari ya Mwambani, Tanga

Kabla ya Bagamoyo, Palikuwepo na mpango wa Bandari ya Mwambani, Tanga

Watanzania sijui tuna roho za namna gani tofauti na nchi nyingi duniani. Angalia waarabu walivyofanya kijana mmoja tu tena mmachinga aliuawa Tunisia, nchi zote za kiarabu kuanzia Algeria hadi Syria zilisisimka na kuanzisha vita dhidi ya watawala wanyanyasaji. Hapa kwetu kitendo cha Tundu Lissu kupigwa risasi kilitosha kuamsha vuguvugu la kudai haki lakini haikuwa hivyo. Halikadhalika uchaguzi mkuu uliopita usingewaacha baadhi ya viongozi wetu wa sasa salama.

Binafsi huwa sielewi ni malezi yetu au ni wingi wa makabila madogo madogo tuliyonayo yanayotufanya kukosa umoja na ushirikiano! Watanzania wengi hushangilia sana kusikia mwenzao mmoja kafukuzwa kazi hata bila sababu ya msingi na kufuata sheria. Tumejaa ubinafsi na kila mmoja anajijali binafsi na familia yake. Cho chote kinachomsibu jirani hakimuhusu na pengine hufurahia. Akionyesha kusikitika ni kwa unafiki tu.

Sasa ili kijinasua hapa tulipo kelele hazitasaidia sana. Kwanza kabisa hizo kelele hazitakuwepo zaidi ya kutoka kwa wapinzani wachache kama Mbowe na Lissu. Lakini pili kwa sababu ya propaganda za serikali dhidi ya hao wachache. Serikali itatumia dola kukandamiza kila aina ya kelele kama ilivyo sasa.

Tunachotakiwa kufanya ni kuyaomba mataifa makubwa kiuchumi na mashirika ya kimataifa kutusaidia. Tuliopo nchini tuendelee kukusanya ushahidi usioshaka namna ambavyo uhuru na haki zinavyogandamizwa. Waliopo nje ya nchi waendeleze harakati za kuelimisha kupitia vyombo vya habari na forums mbalimbali.
Yule kijana wa Tunisia aliuawa kweli? Kumbukumbu yangu inanikatalia kuwa ilikuwa hivyo, ila alichofanyiwa ni kweli ndicho kilichokuwa chachu ya yaliyotokea.

Chachu yetu bado mkuu. Kila kitu na wakati wake

Hata hivyo ninakubaliana kwa mengi uliyoandika kutuhusu tabia zetu waTanzania, lakini nina imani kwamba ni 'cheche' moja tu inayohitajika kuuwasha moto.

Hata mimi, kama wewe, nilitarajia kwamba hii cheche ingetokea wakati wa Magufuli kutokana na mengi yaliyotokea yaliyostahiri kuianzisha hiyo cheche, lakini haikuwa hivyo.
Mimi ninazo nadharia tofauti na zako kwa nini hiyo cheche haikutokea, lakini haina maana kwamba haitaweza kutokea kamwe wakati mwingine wowote hali ikiendelea kuwa mbaya.

Mimi bado nasisitiza mabadiliko yatokane na sisi wenyewe bila ya kuwategemea kwa kiasi kikubwa hao wa mataifa ya nje. Hawa kwa vyovyote hawawezi kutuletea mabadiliko yoyote ya maana, hata kama tukiamua kujiuza kwao kwa bei yoyote ile.Hivi uliwasikia jamaa wa Umoja wa Ulaya walivyoeleza msimamo wao juu yetu hivi karibuni?

Huko nje hakuna mategemeo yoyote mkuu, tutasubiri sana na hakuna lolote linaloweza kutokea bila ya juhudi zetu sisi wenyewe.

Ninachokubaliana nawe moja kwa moja, na mara nyingi nimekuwa nikiwasihi CHADEMA wakifanye kwa makini kubwa, ni kuweka kumbukumbu nzuri zenye ushahidi wote juu ya matukio yote yanatofanyika nchini. Kumbukumbu hizi ni muhimu sana kama ushahidi wakati zikihitajika huko mbele ya safari katika juhudi za kujikomboa kwa wakandamizaji, iwe CCM au kiongozi wao.

Ndiyo, kwa waTanzania waliopo nje, wao pia wana mchango maalum katika kuendeleza mapambano huko waliko.

Mwisho: Kazi kubwa waliyonayo vyama vya upinzani (CHADEMA) kwa sasa hivi, ni kutokata tamaa, bali waongeze juhudi kufanya kazi na wananchi kwa karibu zaidi ili wapate kuaminiwa nao kwamba wao ni tofauti na CCM. Kwamba, maslahi ya nchi hii hayashikiliwi na chama kimoja cha siasa.
Wananchi wanatakiwa wasikie na waamini hivyo. Ni kazi ngumu, lakini hakuna njia za mkato au mbadala wa kuifanya kazi hiyo kwa ufanisi.

Wakimudu kuifanya vyema,utaona cheche zinaibuka kila sehemu ya nchi toka kwa wananchi wenyewe.
 
Tuwe kama Kenya walioandamana kudai imf wasitoe mikopo wakati mwingine tunavyokaa kimya inakuwa kama tumeridhika
Hao Kenya wanajitahidi kweli kuanika uozo mwingi uliopo kwenye serikali yao, lakini jitihadi zao zinaishia hapo, hazizai matunda chanya.

Wewe angalia hali yao na hiyo SGR yao. Wamepiga kelele weee, hadi CAG wao kawaambia mchina asipolipwa Mombasa iliyowekwa rehani itanyakuliwa..., lakini wapi, hakuna lolote lililobadilika.

Sawa ni kweli wanao wigo wa kupiga kelele, lakini inapofika katika kuleta mabadiliko, ukabila unachukua nafasi yake, rushwa inakaza, n.k., n.k.. Kwa hiyo pamoja na kuwa na wigo huo, hawana tofauti kubwa na sisi tunaonyamazia kila jambo linapofanywa na viongozi wetu.

Hofu kubwa ninayoiona ikiinyemelea Tanzania kwa sasa hivi, ni hawa walafi wanaoibuka kwa kasi kubwa sana sasa hivi hapa kwetu.

Ni kama walikwenda kozi maalum huko Kenya, na kufuzu kuleta mambo mabaya ya viongozi wa huko. Hawa akina Kabwe wetu, akina Ndugai, Muhongo na wengine wamekwishaona wenzao wa Kenya wanavyojiingiza kwenye hujuma za taifa lao kwa manufaa yao wenyewe. Wanaanzisha vikampuni pembeni, wanapata vi'tender' hapa na pale au umiliki wa asilimia kadhaa kwenye hawa wawekezaji wa nje, ili taifa lisinufaike kikamilifu na miradi inayoanzishwa.

Na kwa vile tabia zetu waTanzania ni tofauti na hao wenzetu wakenya, ni nadra sana hata kusikia malalamiko popote. Magazeti hayaandiki chochote!

Tusipokuwa waangalifu, hali hapa itakuja kuwa mbaya zaidi ya Kenya kuhusu haya mamiradi na upigwaji wa taifa letu.

Sasa sijui kama Mama Samia atakuwa na stamina yoyote ya kuyakabili haya, au basi tena, na yeye ataamua kuwa mchezaji mashuhuri kwenye timu hiyo?

Tuvute subira tuone, vioja ama neema kwa taifa letu.
 
Yule kijana wa Tunisia aliuawa kweli? Kumbukumbu yangu inanikatalia kuwa ilikuwa hivyo, ila alichofanyiwa ni kweli ndicho kilichokuwa chachu ya yaliyotokea.

Chachu yetu bado mkuu. Kila kitu na wakati wake

Hata hivyo ninakubaliana kwa mengi uliyoandika kutuhusu tabia zetu waTanzania, lakini nina imani kwamba ni 'cheche' moja tu inayohitajika kuuwasha moto.

Hata mimi, kama wewe, nilitarajia kwamba hii cheche ingetokea wakati wa Magufuli kutokana na mengi yaliyotokea yaliyostahiri kuianzisha hiyo cheche, lakini haikuwa hivyo.
Mimi ninazo nadharia tofauti na zako kwa nini hiyo cheche haikutokea, lakini haina maana kwamba haitaweza kutokea kamwe wakati mwingine wowote hali ikiendelea kuwa mbaya.

Mimi bado nasisitiza mabadiliko yatokane na sisi wenyewe bila ya kuwategemea kwa kiasi kikubwa hao wa mataifa ya nje. Hawa kwa vyovyote hawawezi kutuletea mabadiliko yoyote ya maana, hata kama tukiamua kujiuza kwao kwa bei yoyote ile.Hivi uliwasikia jamaa wa Umoja wa Ulaya walivyoeleza msimamo wao juu yetu hivi karibuni?

Huko nje hakuna mategemeo yoyote mkuu, tutasubiri sana na hakuna lolote linaloweza kutokea bila ya juhudi zetu sisi wenyewe.

Ninachokubaliana nawe moja kwa moja, na mara nyingi nimekuwa nikiwasihi CHADEMA wakifanye kwa makini kubwa, ni kuweka kumbukumbu nzuri zenye ushahidi wote juu ya matukio yote yanatofanyika nchini. Kumbukumbu hizi ni muhimu sana kama ushahidi wakati zikihitajika huko mbele ya safari katika juhudi za kujikomboa kwa wakandamizaji, iwe CCM au kiongozi wao.

Ndiyo, kwa waTanzania waliopo nje, wao pia wana mchango maalum katika kuendeleza mapambano huko waliko.

Mwisho: Kazi kubwa waliyonayo vyama vya upinzani (CHADEMA) kwa sasa hivi, ni kutokata tamaa, bali waongeze juhudi kufanya kazi na wananchi kwa karibu zaidi ili wapate kuaminiwa nao kwamba wao ni tofauti na CCM. Kwamba, maslahi ya nchi hii hayashikiliwi na chama kimoja cha siasa.
Wananchi wanatakiwa wasikie na waamini hivyo. Ni kazi ngumu, lakini hakuna njia za mkato au mbadala wa kuifanya kazi hiyo kwa ufanisi.

Wakimudu kuifanya vyema,utaona cheche zinaibuka kila sehemu ya nchi toka kwa wananchi wenyewe.
Yule kijana wa Tunisia alijichoma moto kwa petroli baada ya kushindwa kuvumilia manyanyaso ya serikali.

Ni kweli tuendelee kuvipa moyo vyama vya upinzani vinavyotupigia kelele. Wasiwasi wangu ni kuwa hata kama wananchi wataamua kupitia sanduku la kura, CCM watatumia dola kuendeleza utawala wao.

Sasa ni namna gani tutavifanya vyombo vya dola viondokane na kushabikia siasa? Hivi sasa CCM inafanya kila hila watoa vyeo vya kisiasa kwa wanajeshi wetu, na kwa utamu wa kufanya kazi za kiraia unavyowakolea wanasahau wajibu wao.

Mimi nadhani ni muhimu takaanza kuipigia kelele serikali kutowapa kazi za kiraia wanajeshi wetu. Aidha na sisi tuanze kulipigia kelele na ikiwezekana kulizomea jeshi kukubali vyeo vya kiraia. Wanajeshi wakiondokana na kazi za kiraia wanaweza kuwa msaada katika kubadilisha msimamo wao wa kuisaidia serikali kubaki madarakani. Kazi watakayobaki nayo ni kutetea haki za wananchi kama viapo vyao vinavyowataka.
 
Yule kijana wa Tunisia alijichoma moto kwa petroli baada ya kushindwa kuvumilia manyanyaso ya serikali.

Ni kweli tuendelee kuvipa moyo vyama vya upinzani vinavyotupigia kelele. Wasiwasi wangu ni kuwa hata kama wananchi wataamua kupitia sanduku la kura, CCM watatumia dola kuendeleza utawala wao.

Sasa ni namna gani tutavifanya vyombo vya dola viondokane na kushabikia siasa? Hivi sasa CCM inafanya kila hila watoa vyeo vya kisiasa kwa wanajeshi wetu, na kwa utamu wa kufanya kazi za kiraia unavyowakolea wanasahau wajibu wao.

Mimi nadhani ni muhimu takaanza kuipigia kelele serikali kutowapa kazi za kiraia wanajeshi wetu. Aidha na sisi tuanze kulipigia kelele na ikiwezekana kulizomea jeshi kukubali vyeo vya kiraia. Wanajeshi wakiondokana na kazi za kiraia wanaweza kuwa msaada katika kubadilisha msimamo wao wa kuisaidia serikali kubaki madarakani. Kazi watakayobaki nayo ni kutetea haki za wananchi kama viapo vyao vinavyowataka.
Asante kwa kumbukumbu hiyo ya huyo kijana wa Tunisia.

Sasa mkuu wangu 'Ileje' nataka nikukumbushe ni kiasi gani tulichokuwa tumepiga hatua hapa hapa kwetu kabla ya ujio wa Magufuli, aliyeturudisha nyuma kabisa, kabisa na kutuvuruga.

Pamoja na wizi wao wa kura CCM walishaanza kulegea vizuri sana kabla ya Magufuli.

Unakumbuka ni wabunge wangapi wa upinzani waliokuwa kwenye Bunge la mwisho la Kikwete?

Unakumbuka wengi wa hawa wabunge waliingiaje kwenye bunge lile? Wananchi walishaanza kuona uzuri wa kura zao, na baadhi yao walianza kuunga mkono juhudi za kuzuia uharibifu wa kura zao. CCM walishaanza kukubali hali hiyo.

Akaingia Magufuli. Kaharibu kila kitu kwa vitisho na kuumiza watu.
Wakurugenzi waliokwisha tishwa na nguvu za wananchi wakati wanapovuruga kura, wakatishiwa kufutwa kazi, na wakahakikishiwa usalama wao dhidi ya wananchi wenye hasira.

Hapa ndipo kila kitu kilipotuvurugikia, tukarudi nyuma kabisa, kabisa, zaidi ya tulivyowahi kuwa, hata wakati wa enzi za chama kimoja.

Hapo ndipo tulipo sasa hivi.

Swali ni je, kuondoka kwa Magufuli kutatuanzishia safari yetunyingine ya kuelekea tulikokuwa tunaelekea kabla ya ujio wake?

Jambo nililo nalo uhakika ni hili: hata iweje, hakuna tena kiongozi mwingine, ndani ya CCM au nje ya chama hicho atakayetufikisha huko alikokuwa ametupeleka Magufuli.

CCM wanaweza kuendelea na janja zao za hapa na pale, kama kuwatumia askari n.k., kuwafanyia kazi. Lakini hawa askari nao ni miongoni mwetu, ni waTanzania kama sisi. Kwani wakati wa Kikwete hawa askari hawakuwepo.
Lakini kiasi cha ukatili kilichoonyeshwa na Magufuli kulizidi na kutia hofu kila sehemu, sio uraiani pekee, bali hata huko huko kwenye vyombo vyetu vya ulinzi.
Hakuna atakayetupeleka huko tena.
 
Mwambani ni wa serikali, bagamoyo ni uwekezaji (concession ya miaka 33) lakini pia tunakuwa na sheres tu. Ila tanga ni ya serikali. Ndio mjue tofauti
Sasa kama ni hivyo, kwa nini hawa wanaoifanyia kazi serikali watelekeze mradi wao wa Mwambani ni kulegea kama mlenda kwenye mradi ambao hauwahusu.

Wewe hapo huoni kwamba kuna kasoro tayari, na kukustua akili ufikiri?
 
Asante kwa kumbukumbu hiyo ya huyo kijana wa Tunisia.

Sasa mkuu wangu 'Ileje' nataka nikukumbushe ni kiasi gani tulichokuwa tumepiga hatua hapa hapa kwetu kabla ya ujio wa Magufuli, aliyeturudisha nyuma kabisa, kabisa na kutuvuruga.

Pamoja na wizi wao wa kura CCM walishaanza kulegea vizuri sana kabla ya Magufuli.

Unakumbuka ni wabunge wangapi wa upinzani waliokuwa kwenye Bunge la mwisho la Kikwete?

Unakumbuka wengi wa hawa wabunge waliingiaje kwenye bunge lile? Wananchi walishaanza kuona uzuri wa kura zao, na baadhi yao walianza kuunga mkono juhudi za kuzuia uharibifu wa kura zao. CCM walishaanza kukubali hali hiyo.

Akaingia Magufuli. Kaharibu kila kitu kwa vitisho na kuumiza watu.
Wakurugenzi waliokwisha tishwa na nguvu za wananchi wakati wanapovuruga kura, wakatishiwa kufutwa kazi, na wakahakikishiwa usalama wao dhidi ya wananchi wenye hasira.

Hapa ndipo kila kitu kilipotuvurugikia, tukarudi nyuma kabisa, kabisa, zaidi ya tulivyowahi kuwa, hata wakati wa enzi za chama kimoja.

Hapo ndipo tulipo sasa hivi.

Swali ni je, kuondoka kwa Magufuli kutatuanzishia safari yetunyingine ya kuelekea tulikokuwa tunaelekea kabla ya ujio wake?

Jambo nililo nalo uhakika ni hili: hata iweje, hakuna tena kiongozi mwingine, ndani ya CCM au nje ya chama hicho atakayetufikisha huko alikokuwa ametupeleka Magufuli.

CCM wanaweza kuendelea na janja zao za hapa na pale, kama kuwatumia askari n.k., kuwafanyia kazi. Lakini hawa askari nao ni miongoni mwetu, ni waTanzania kama sisi. Kwani wakati wa Kikwete hawa askari hawakuwepo.
Lakini kiasi cha ukatili kilichoonyeshwa na Magufuli kulizidi na kutia hofu kila sehemu, sio uraiani pekee, bali hata huko huko kwenye vyombo vyetu vya ulinzi.
Hakuna atakayetupeleka huko tena.
Tofauti ya Magufuli na viongozi waliomtangulia kama Kikwete ni kuwa waliomtangulia waliheshimu katiba na sheria na pia walikuwa na utu. Magufuli hakuheshimu katiba wala sheria na alitawala nchi kama anavyoendesha familia yake. Alijivua ubinadamu akajifanya mungu hivyo hakutaka kuhojiwa katika maamuzi yake.

Kwa vile Magufuli alifanya yote yasiyokibalika bila kukemewa na chama chake wala kuzomewa na wananchi, sasa kuna watu watapenda kuiga na hasa ndani ya CCM. Kwa sababu wameona inawezekana kufanya maovu bila kichukuliwa hatua. Hivyo si rahisi kurudi enzi zile za akina Kikwete bila kuchukua hatua, hii ni pamoja na kuwa na katiba mpya itakayotenganishi kwa uwazi dola, bunge na mahakama na pia itakayo muwajibisha ye yote atakayekiuka sheria. CCM wameonja nyama za watu hawawezi kuacha kuendelea kula, hivyo lazima tuendeleze harakati za kuwapinga kwa hoja na kuwazomea na kuwaaibisha pale wanapovuka mipaka ya sheria na haki.

Viongozi wa vyombo vya dola hasa polisi na JWTZ waambiwe kwa uwazi maovu yao na wazomewe pia mpaka akili ziwakae sawa. Kama hawa makamanda watajitenga na CCM basi ukombozi utakuja mapema.
 
Bagamoyo imekuwa Bagamoyo, kisa, Kikwete alivunja ahadi ya ujenzi wa bandari Mwambani, Tanga.

Sasa makelele yanasikika kila sehemu kuhusu Bagamoyo, na hakuna anayekumbuka Mwambani ilikuwaje?

Eleza, Mwambani haikuwa na vigezo ilivyonavyo Bagamoyo?

Ile bandari itapitisha bidhaa za Uganda, Rwanda, hadi DRC, kama inavyoweza kufanya Bagamoyo, tena kwa umbali wa karibu zaidi.

Tuiache Dar ihudumu bila mwingiliano. Jenga Mwambani, achana na Bagamoyo.
Ni kweli umenikumbumbusha ile feasibility study ya Mwambani ambayo ilikuwa inaendana na ujenzi wa reli Tanga hadi Mwanza Musoma. Wazo hilo lilianza kufloat miaka ya themanini wakati Museveni alipoingia madarakani akaomba Bandari ya Tanga kuwa maalumu kwa ku-handle cargo ya Uganda. Kikwete alirudia wazo la bandari hiyo tena mwaka 2012 hivi lakini lilikuwapo miaka 15 kabla; wazo la reli naona limekuwa linasuasa tu. Badala ya ujenzi wa reli kuna wakati Kikwete alitaka kujenga highway kutoka Arusha kwenda Musoma akapigwa vita na watu wa mazingira, na kuamua kuliacha wazo hilo lijifie. Ingekuwa ni Magufuli nadhani ujenzi ungefanyika tu.
 
Ni kweli umenikumbumbusha ile feasibility study ya Mwambani ambayo ilikuwa inaendana na ujenzi wa reli Tanga hadi Mwanza
Sasa wazee wetu ndio mtukumbushe, vijana bila mapokeo ni sawa na mtoto aliyezaliwa na kukua bila wazazi wala walezi! Hawa wanasiasa wanapenda kutugeuza wapendavyo kama wanavyokula samaki!
 
Tofauti ya Magufuli na viongozi waliomtangulia kama Kikwete ni kuwa waliomtangulia waliheshimu katiba na sheria na pia walikuwa na utu. Magufuli hakuheshimu katiba wala sheria na alitawala nchi kama anavyoendesha familia yake. Alijivua ubinadamu akajifanya mungu hivyo hakutaka kuhojiwa katika maamuzi yake.

Kwa vile Magufuli alifanya yote yasiyokibalika bila kukemewa na chama chake wala kuzomewa na wananchi, sasa kuna watu watapenda kuiga na hasa ndani ya CCM. Kwa sababu wameona inawezekana kufanya maovu bila kichukuliwa hatua. Hivyo si rahisi kurudi enzi zile za akina Kikwete bila kuchukua hatua, hii ni pamoja na kuwa na katiba mpya itakayotenganishi kwa uwazi dola, bunge na mahakama na pia itakayo muwajibisha ye yote atakayekiuka sheria. CCM wameonja nyama za watu hawawezi kuacha kuendelea kula, hivyo lazima tuendeleze harakati za kuwapinga kwa hoja na kuwazomea na kuwaaibisha pale wanapovuka mipaka ya sheria na haki.

Viongozi wa vyombo vya dola hasa polisi na JWTZ waambiwe kwa uwazi maovu yao na wazomewe pia mpaka akili ziwakae sawa. Kama hawa makamanda watajitenga na CCM basi ukombozi utakuja mapema.
Ila alikupa haki ya kumtukana. Jaribiu Rwanda.
 
Tofauti ya Magufuli na viongozi waliomtangulia kama Kikwete ni kuwa waliomtangulia waliheshimu katiba na sheria na pia walikuwa na utu. Magufuli hakuheshimu katiba wala sheria na alitawala nchi kama anavyoendesha familia yake. Alijivua ubinadamu akajifanya mungu hivyo hakutaka kuhojiwa katika maamuzi yake.

Kwa vile Magufuli alifanya yote yasiyokibalika bila kukemewa na chama chake wala kuzomewa na wananchi, sasa kuna watu watapenda kuiga na hasa ndani ya CCM. Kwa sababu wameona inawezekana kufanya maovu bila kichukuliwa hatua. Hivyo si rahisi kurudi enzi zile za akina Kikwete bila kuchukua hatua, hii ni pamoja na kuwa na katiba mpya itakayotenganishi kwa uwazi dola, bunge na mahakama na pia itakayo muwajibisha ye yote atakayekiuka sheria. CCM wameonja nyama za watu hawawezi kuacha kuendelea kula, hivyo lazima tuendeleze harakati za kuwapinga kwa hoja na kuwazomea na kuwaaibisha pale wanapovuka mipaka ya sheria na haki.

Viongozi wa vyombo vya dola hasa polisi na JWTZ waambiwe kwa uwazi maovu yao na wazomewe pia mpaka akili ziwakae sawa. Kama hawa makamanda watajitenga na CCM basi ukombozi utakuja mapema.
Hapana, bado nakataa.

Magufuli alikuwa haigizi. Hayo aliyokuwa akiyafanya ndiyo ilikuwa ni tabia yake hasa. Kwa hiyo hakuona ugumu wowote wa kuyafanya aliyoyafanya.

Kwa sasa hivi hakuna anayeweza kuigiza tabia zile na akawa kama alivyokuwa Magufuli; hili nalikataa katakata.

Kama Kikwete na viongozi wengine waliotangulia waliweza kuheshimu katiba, ni kwa sababu hawakuwa na tabia kama za Magufuli, wasingeweza kabisa kufanya ya Magufuli.

Magufuli hakuzomewa na chama chake wala na wananchi, kwa sababu CCM aliichukua na kuifanya kuwa yake. Hukumbuki alivyowadhibiti akina Kinana, Makamba wote wawili, na akina Nape? Baada ya hapo ni nani tena ndani ya CCM aliyeweza kunyanyua kidole?

Hukuona jinsi alivyowapitisha wabunge wote wa CCM waliomo sasa hivi Bungeni, kwa matakwa yake mwenyewe?

Hukuona alivyowatisha wananchi, hadi wasiseme lolote juu ya kura zao kwenye chaguzi zote walizotakiwa kwenda kupiga kura, tokea serikali za mitaa hadi 'Uchafuzi Mkuu'?

Ni kiongozi gani aliyetangulia angeweza kufanya haya yote, bila hata chembe ya aibu?

Kutafuta Katiba mpya, waTanzania wangeanzia wapi chini ya utawala wa Magufuli?

Ni kushukuru tu, kwamba Mungu aliamua kuiachia Tanzania. Sasa ni juu yetu wenyewe. Kama ni kwa ujinga wetu tutaendelea kubaki kama majuha bila ya kujali nchi yetu inatawaliwa vipi, hilo litakuwa ni kosa letu wenyewe wananchi kwa ujumla wetu.
 
Ni kweli umenikumbumbusha ile feasibility study ya Mwambani ambayo ilikuwa inaendana na ujenzi wa reli Tanga hadi Mwanza
Itapendeza kama kwenye 'archives' zako kuna kumbukumbu za aina hiyo.
 
Itapendeza kama kwenye 'archives' zako kuna kumbukumbu za aina hiyo.
Ni kweli umenikumbumbusha ile feasibility study ya Mwambani ambayo ilikuwa inaendana na ujenzi wa reli Tanga hadi Mwanza Musoma. Wazo hilo lilianza kufloat miaka ya themanini wakati Museveni alipoingia madarakani akaomba Bandari ya Tanga kuwa maalumu kwa ku-handle cargo ya Uganda. Kikwete alirudia wazo la bandari hiyo tena mwaka 2012 hivi lakini lilikuwapo miaka 15 kabla; wazo la reli naona limekuwa linasuasa tu. Badala ya ujenzi wa reli kuna wakati Kikwete alitaka kujenga highway kutoka Arusha kwenda Musoma akapigwa vita na watu wa mazingira, na kuamua kuliacha wazo hilo lijifie. Ingekuwa ni Magufuli nadhani ujenzi ungefanyika tu.
 
Ni kweli umenikumbumbusha ile feasibility study ya Mwambani ambayo ilikuwa inaendana na ujenzi wa reli Tanga hadi Mwanza Musoma. Wazo hilo lilianza kufloat miaka ya themanini wakati Museveni alipoingia madarakani akaomba Bandari ya Tanga kuwa maalumu kwa ku-handle cargo ya Uganda. Kikwete alirudia wazo la bandari hiyo tena mwaka 2012 hivi lakini lilikuwapo miaka 15 kabla; wazo la reli naona limekuwa linasuasa tu. Badala ya ujenzi wa reli kuna wakati Kikwete alitaka kujenga highway kutoka Arusha kwenda Musoma akapigwa vita na watu wa mazingira, na kuamua kuliacha wazo hilo lijifie. Ingekuwa ni Magufuli nadhani ujenzi ungefanyika tu.
Kuna zaidi.
Naona hata makampuni ya uwekezaji kama 'Brookwood Capital' walishaonyesha kuutaka mradi huo tokea 2012, lakini haionyeshi waliishia wapi.

Mara vu, 2017 (FOCAC) Forum on China-Africa Corporation na wao wakaipenda hiyo bandari; lakini haijulikani iligeuka vipi toka (Mwaporc) - Mwambani Port and Railway Project na kufika Bagamoyo!

Yapo mengi ya kujifunza hapa kuhusu maamuzi ya viongozi wetu.

Mambo ya nchi yanageuzwa tu kama miradi ya ujenzi wa mabanda yao ya kuku.
 
Hizi kelele za Bagamoyo zina jambo zito nyuma yake! Wananchi tunatilia shaka nguvu nyuma ya huu mradi!

..bagamoyo port inakwenda kuwa mradi wa kimkakati wa serikali ya rais samia hassan.

..wana-ccm muwe tayari kuunga mkono, na kuusifia mradi huo kama mnavyosifia sgr, stieglers gorge, chato airport,...miradi ya kimkakati ya Jpm.
 
..bagamoyo port inakwenda kuwa mradi wa kimkakati wa serikali ya rais samia hassan.

..wana-ccm muwe tayari kuunga mkono, na kuusifia mradi huo kama mnavyosifia sgr, stieglers gorge, chato airport,...miradi ya kimkakati ya Jpm.
Sidhani kuwa kutakuwa na mtu anayeweza kutoa kititakudhani tofauti na wazo lako hili, hiyo hela itakuwa ni halali yako kivyepesi kabisa.

Sasa basi, maadam hiyo tayari ni 'fait accompli'; tuombe mama alionee taifa letu huruma... mradi uweze kuwanufaisha wananchi maskini wa taifa hili angalao hata kwa kunusa kwa mbali kidogo.

Asikubali kutuuza kijumla jumla kwa mikataba itakayokuwa jiwe la shingoni kwetu na vizazi vyetu.

Na Dar je, ataiacha ife kifo cha mende?
 
Sidhani kuwa kutakuwa na mtu anayeweza kutoa kititakudhani tofauti na wazo lako hili, hiyo hela itakuwa ni halali yako kivyepesi kabisa.

Sasa basi, maadam hiyo tayari ni 'fait accompli'; tuombe mama alionee taifa letu huruma... mradi uweze kuwanufaisha wananchi maskini wa taifa hili angalao hata kwa kunusa kwa mbali kidogo.

Asikubali kutuuza kijumla jumla kwa mikataba itakayokuwa jiwe la shingoni kwetu na vizazi vyetu.

Na Dar je, ataiacha ife kifo cha mende?

..fedha tulizotapanya kujenga dodoma, na kununua midege toka kwa mabeberu, zingetumika vizuri kama zingeelekezwa kujenga bandari mpya ya Bagamoyo. Tusingelazimika kukubali masharti mabaya ya kinyonyaji toka kwa Wachina.

Cc Nguruvi3
 
Kwani mmekatazwa kujenga mwambani Tanga, haya nendeni mkajenge kwani shida iko wapi?

Mnaizungumzia bandari ya bagamoyo as if lengo ni bandari tu, wakati plan ya pale ni kuweka EPZ, ikiwemo mamia ya viwanda.

Lengo la bandari ya Bagamoyo kuwa karibu na Jiji kubwa linalochangia pato la Taifa kwa more than 70% hamuijui? —Bagamoyo ni extension ya jiji la Dar, na mji wa dar unakua kuelekea uelekeo huo!

Hata Magufuli ukimsikiliza kwenye video hii hapa chini anausifu mradi wa bandari ya bagamoyo na anamsifu Kikwete kwa kuuanzisha. Sasa Msgufuli kwa bahati mbaya alikuwa kigeugeu ni mtu wa ndimi mbili, baadae aligeuka!


 
Back
Top Bottom