Kabla ya maisha kuwapiga Watu wengi Knockout, wengi walifikiri wakifika miaka 30 wangekuwa na nyumba na Gari

Kabla ya maisha kuwapiga Watu wengi Knockout, wengi walifikiri wakifika miaka 30 wangekuwa na nyumba na Gari

Habari za Jumapili!

Maisha sio Pouwa! Nakubaliana na wale wanaosema Maisha ni majaliwa. Na jitihada hazizidi kudura.

Wapo waliosoma kwa bidii mila hiyo na waliona taa ya matumaini kulingana na matokeo ya darasani waliyokuwa wakiyapata. Waliamini kuwa maisha yao na hatma yao ipo mikononi mwao kumbe sivyo.

Ilifika hatua wakawa wanadharau wale ambao walikuwa wanaonekana hawana mipango na mikakati kutokana na kutoipenda shule.

Wengi walifikiri kuwa kabla ya miaka 30 tayari wangekuwa wamekomesha jeuri na kiburi cha Umaskini katika maisha yao.
Tayari kichwani walikuwa na picha za jumba kubwa la kifahari ambalo walijua ndio watakayoishi. Bongo zao zilishakuwa na miundombinu ya flyover ambapo gari yao ilikuwa ikipita juu yake huku ndani akiwa yeye na Pisikali moja matata ambayo ndio mkewe.

Kwa wasichana, wao nao walikuwa na maisha yao mazuri katika vichwa vyao. Wanaume Handsome, warefu na wenye vipato na Watanashati walikuwa katika fikra zao.

Sasa miaka imekimbia, hawaelewi nini kimetokea. Matumaini yameyoyoma, ngumi ya matumpa upper cut moja matata imepiga kidevu vijana chali.
Hata zile ramani za majengo na magari walizokuwa nazo miaka hiyo zimefutika.

Yule Mwanamke mrembo akilini waliyemfikiria wangekuja kumuoa wanawaona kwenye magazeti, filamu na kwenye riwaya. Hakuna faraja tena, tumaini limeota mbawa. Wamejiunga kwenye chama cha faraja ya mpito cha Kataa Ndoa.
Hawakumbiki tena ndoto ya kuwa na familia bora baada ya kuyapata maisha mazuri yanayotamanika.
Ni Tekniko Knockout.

Hawakujua kuwa maisha yanakupa yale ambayo hujayaomba na yale ambayo huyataki. Tena maisha hukupa yale ambayo hukudhania kwamba ungekuwa nayo. Kwa sababu maisha ni Nasibu, maisha ni bahati tuu.

Sasa mipango imevurugwa na kuvurugika. Kila kitu pangala pangala! Hata kupanga hawataki kupanga tena. Hata wakisema wapange wanaona wanapoteza muda wao. Sasa ni bora liende túu! Wapo tayari kwa lolote na huo ndio mfumo wa maisha unavyotaka.

Mtu ambaye alipanga kabla ya miaka 30 awe na jumba na gari leo hii hata kodi ya chumba cha laki moja hawezi kuhimili. Unaweza kuona pigo alilopigwa ni zito kwa kiwango kipi.

Kijana, unapopanga mipango yako. Muombe Mungu

Suleiman aliwahi kusema;

Mhubiri 9:11 NEN​

Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.


Acha Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hakika umenena Robert!
 
Life is not predictable.

Kikubwa fanya kazi kwa bidii na nidhamu ya pesa kuwa nayo.

Ukweli ni kwamba mtu anaekuja kukupa deal ni mtu mmoja tu na kupitia hapo unakuwa mtu mwingine tofauti kabisa kiuchumi
.
Hili nimejifunza kwa watu wangu wengi wa karibu walikuja kuinuliwa na watu

Hapa ndipo nilijifunza kwa udhiirisho kwamba mtu huinuliwa na mtu kupitia ukuu wa Mungu.


Hata mtu unae muona leo ana maisha mazuri ukifuatilia utakuta alikuwa kwnye harakati zake ghafla akatokea mtu akamshirikisha ndio ukawa mwanzo wa kutoka.

Kadhalika wahalifu nao hupiga tukio moja tu na kupitia hapo ndio mwanzo wa kutoka.

So pambana lift itakukuta njiani.
Ndio kikubwa uwe njiani tu usijifungie ndani maana mtu wa kukupa mchongo wa kutoka ni mmoja tu. Unakutana nae kwenye harakati zako tu.
 
Hapo napingana na wewe Kikwete alitegemea urais na kweli akawa rais
Hapa kwa kikwete kuna cha kujifunza katika angle nyingine.

Kikwete aliutaka urais 1995 (kumbuka hii ilikuwa ndoto yake hapa ameshafanya lobbing za kutosha mpaka 1995)

Lakini Mungu akamwambia NO
umri bado unahitaji kuimarika zaidi kwenye hekima busara na subira.

Kikwete hakukata tamaa akaendelea na UTHUBUTU NA UJASIRI hatimaye

Ndoto yake ikafanikishwa na Mungu 2005 akawa president.

Mungu hubariki wenye Subira, wanyenyekevu na uthubutu.

Hivyo tusiache ndoto zetu ikiwa Mungu ametutaka tufikie destinations zetu.

Bahati hutukuta katika harakati zetu.

Mimi huwa namwomba Mungu anifanikishe mambo flani flani

Naona-ga kama ananicheleweshea ila nikajifunza kwamba.

Wakatu mwingine kabla hujainuliwa unapaswa uwe umeeondoa kiburi, madharau na umejua matatizo ya watu pia uwe na subiria, uvumilivu, unyenyekevu na hekima ili ukiinuliwa umkubuke Mungu uwatendee watu haki.


Lakini hili linashangaza zinaweza kuwa ni fikra tu but ukiangalia humu duniani
Kuna watu wamefanikiwa licha ya uovu wao na tabia zao mbaya.

Lakini hilo linatokea ili lile neno lipate kutimia "Mungu huwanyeshea mvua wenye dhambi na wasio na dhambi"
 
Sasa kama msaada wake hautegemei unamuomba au haumuombi, Utasemaje vijana hawafanikiwi kwa sababu ya Mungu?
Mambo ya kumuomba we inakuuma nini
We siumesema hakuna Mungu sasa unachukizwa nini ukisikia mtu anasema anamuomba Mungu

Watu tumefanikiwa sababu ya Mungu na ushuhuda tunao aya kasirika
 
Kuna kundi kubwa la vijana linasali na kumsifu huyo Mungu lakini bado maisha yao ni pangu pakavu tia mchuzi..

Hakuna mpango wa Mungu kwenye mafanikio ya binadamu.

Sera mbovu, siasa uchwara, mazingira ya rushwa, ujinga, elimu mbovu, serikali za hovyo ndio chanzo cha umaskini na ukosefu wa fursa kwa vijana wengi hasa barani Afrika.





Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
[emoji817][emoji817]
 
Yesu Kwa miaka yake 33 duniani hakuwahi mmiliki nyumba Wala gari( punda) Kwa wakati Ule.

Nyumba na gari ni minor issue, muhimu ni tuutafute Ufalme wa Mungu na HAKIKA yake, hayo mengine tutazidishiwa.
Yesu alikuwa ni tajiri mkubwa tena mno...kufanya miujiza na kuwapa watu elimu ya kuendesha maisha haukuwa utajiri wa kawaida.

Yesu hakutaka kumiliki hivyo ulivyo orodhesha kwa kuwa ni Materials.

Hapa duniani alikuja kwa kusudi maalumu
 
Talk is cheap bruh, siku ukipitia chagamoto na mwenye nyumba anatishia kuifukuza familia yako ndio utelewa kwanini watu wana amani kwa kujenga nyumba zao za kuishi tu hata kama nyumba iko Chanika mwisho.
Mkuu mbona naelewa sana? Kweli unaniweka kwenye kundi la watu wasiojua changamoto za kulipa kodi? Nilichopinga mimi ni watu kuona kama ndiyo kielelezo cha mafanikio. Yaani nakubali kuwa ni mafanikio lakini siyo kama ndiyo umemaliza kila kitu. Je, utakubaliana na mimi kuwa mtu akiwa na utajiri mkubwa, unaweza kuishi kwenye nyumba za kupanga maisha yako yote na akahesabika ana mafanikio kuliko mtu mwenye nyumba na hana fedha? Kipi ni mafanikio sasa, nyumba au utajiri?
 
Habari za Jumapili!

Maisha sio Pouwa! Nakubaliana na wale wanaosema Maisha ni majaliwa. Na jitihada hazizidi kudura.

Wapo waliosoma kwa bidii mila hiyo na waliona taa ya matumaini kulingana na matokeo ya darasani waliyokuwa wakiyapata. Waliamini kuwa maisha yao na hatma yao ipo mikononi mwao kumbe sivyo.

Ilifika hatua wakawa wanadharau wale ambao walikuwa wanaonekana hawana mipango na mikakati kutokana na kutoipenda shule.

Wengi walifikiri kuwa kabla ya miaka 30 tayari wangekuwa wamekomesha jeuri na kiburi cha Umaskini katika maisha yao.
Tayari kichwani walikuwa na picha za jumba kubwa la kifahari ambalo walijua ndio watakayoishi. Bongo zao zilishakuwa na miundombinu ya flyover ambapo gari yao ilikuwa ikipita juu yake huku ndani akiwa yeye na Pisikali moja matata ambayo ndio mkewe.

Kwa wasichana, wao nao walikuwa na maisha yao mazuri katika vichwa vyao. Wanaume Handsome, warefu na wenye vipato na Watanashati walikuwa katika fikra zao.

Sasa miaka imekimbia, hawaelewi nini kimetokea. Matumaini yameyoyoma, ngumi ya matumpa upper cut moja matata imepiga kidevu vijana chali.
Hata zile ramani za majengo na magari walizokuwa nazo miaka hiyo zimefutika.

Yule Mwanamke mrembo akilini waliyemfikiria wangekuja kumuoa wanawaona kwenye magazeti, filamu na kwenye riwaya. Hakuna faraja tena, tumaini limeota mbawa. Wamejiunga kwenye chama cha faraja ya mpito cha Kataa Ndoa.
Hawakumbiki tena ndoto ya kuwa na familia bora baada ya kuyapata maisha mazuri yanayotamanika.
Ni Tekniko Knockout.

Hawakujua kuwa maisha yanakupa yale ambayo hujayaomba na yale ambayo huyataki. Tena maisha hukupa yale ambayo hukudhania kwamba ungekuwa nayo. Kwa sababu maisha ni Nasibu, maisha ni bahati tuu.

Sasa mipango imevurugwa na kuvurugika. Kila kitu pangala pangala! Hata kupanga hawataki kupanga tena. Hata wakisema wapange wanaona wanapoteza muda wao. Sasa ni bora liende túu! Wapo tayari kwa lolote na huo ndio mfumo wa maisha unavyotaka.

Mtu ambaye alipanga kabla ya miaka 30 awe na jumba na gari leo hii hata kodi ya chumba cha laki moja hawezi kuhimili. Unaweza kuona pigo alilopigwa ni zito kwa kiwango kipi.

Kijana, unapopanga mipango yako. Muombe Mungu

Suleiman aliwahi kusema;

Mhubiri 9:11 NEN​

Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.


Acha Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Ukweli mtupu [emoji48][emoji48]
kumbe bado tuna wanasalfasa katika nchi hii
 
Back
Top Bottom