Kabla ya Samia kuwa Rais nilidhani ni lazima Rais wa nchi atoe hotuba ndeefu

Unaongea kwa kireeefu kama unacho cha kuongea.
 
Mkuu mbona ni kama una hasira na mama binafsi sioni kama kuna ubaya maana nilistushwa na ufupi wa hotuba za aliyekuwa mgombea urais chadema 2015 pia ccm walizoea kumcheka na kumdihaki kwamba hana cha kusema kumbe walikuwa hawajui kama mimi. Kupitia mama ndo nimejua kwamba kumbe ni jambo la kawaida
 
Ina maana wewe ulikkuwepo tangu uongozi wa Awamu ya Kwanza??
 
kwani nimesema msukuma mwenzetu ni standard? Labda Nyerere
Samia kaboresha maslai ya wafanyakazi, ameruhusu Uhuru wa wajinga na wapumbavu kumtukana na kumkosoa, Magufuli mlikuwa hamthubutu kumkosoa,

Samia serikali yake imekuwa ya uwazi na ukweli, magufuli wenu mpk leo hatujajua makusanyo ya hela za vitambulisho vya umachinga zilipatikana sh. Ngapi na zilienda wapi,

Awamu ya Sita hatusikii Tena habari za kutekana,Wala kupeana makesi ya hovyo,

Nyie chuki yenu kwa huyo mama Ni juu ya imani yake tu, maana hakuna lingine, hii Nchi Kuna mijitu Ina chuki za udini na mfumo dume na ukabila
 
Eti kupeana makesi ya hovyo,wewe upo nchi gani? Huoni watu wanavyo pata aibu mahakama ya uhujumu uchumi huko. Kwenye kesi ya Ugaidi
 
Siyo lazima...

Hata unaweza simama ukasalimia ukaenda zako...
 
Umesema yote[emoji122][emoji122]
 
Kwa hiyo haya yanahusiana nini na urefu au ufupi wa hotuba!?
 
Ina maana wewe ulikkuwepo tangu uongozi wa Awamu ya Kwanza??
Ndio nilikuwepo ingawa sikuwa mtu mzima sana but nilikuwa nasikiliza hotuba mbona ni kama swali lako linaashiria unajua umri wangu au limelenga nini!?
 
Inavyoonekana mambo yanafanyika kwa utashi wa Rais aliyepo.

Itakuwa hakuna muongozo maalum kwa mujibu wa Katiba.
Mbona kila kitu mnasingizia Katiba Mpya? Katiba mpya haiwezi kukupa kila kitu. Kwani Kenya hapa wenye Katiba mpya ya mwaka 2010 wamemaliza matatizo yao? Au linhanisha Trump aliyekuwa anatawala kupitia Twitter na Joe Biden ambaye anarumia Twitter kwa mambo machache

Watanzania ni wagumu kwa kudikiri
 
Cha maana ni quality sio quantity au urefu wa hotuba. Unaweza kuhutubia dakika 15 ukasema la maana linalopaswa kusemwa kuliko anayeongea saa 1 na nusu lakini ni pumba na kujisifu na matusi.
Watanzania tumezoea mipasho na umbeya ndio sababu magazeti ya udaku na redio zisizokuwa serious zina wateja wengi.
 


Kwa hiyo wakenya kubadilisha Katiba yao mara kwa mara wewe unaona ni tatizo?

Kwa hiyo ndio iwe sababu ya kuacha kudai swala la Katiba?

Unafahamu nini kuhusu “continuous improvements theory “?

Sasa nikufahamishe uweze kujua;

Ni kawaida kabisa kufanya regular review ya kikatiba mpaka pale itakapoonekana inakidhi mahitaji ya wengi.

The World is not static, it is dynamic.

Technologys keep on changing in every second always.

Hivyo swala la continuous improvements kwa jamii ya werevu ni inevitably.

Asomaye na afahamu.
 
Huyu hata swala la kuuwawa kwa askari 4 na yule Msomali sikuwahi kumsikia akiliongelea kabisa.

Au Mimi ndiye linipita bila kusikia?!
Yule muuwaji wa Askari wetu alikuwa Mtanzania na sio msomali. Usomali ni watu wa taifa la Somalia, ukitaka kujua kabila lake, alikuwa MAJERTAIN
 
Ndio nilikuwepo ingawa sikuwa mtu mzima sana but nilikuwa nasikiliza hotuba mbona ni kama swali lako linaashiria unajua umri wangu au limelenga nini!?
Nilitaka nifahamu tu...kwani sisi wengine upo wakati tulikuwa tunasafiri naye kikazi..
Sisi ni kizazi Cha mwalimu...kwa hiyo tuna bahati ya kuona awamu zote tano...nasema awamu tano makusudi kwani hakuna kitu Kama awamu ya sita...huo ni upotoshaji tu katika kujaribu kufuta legacy ya Magufuli...2025 ndipo tutakuwa na awamu ya sita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…