Kabla ya vita USD 1 ilikuwa sawa na Rubles 77, sasa hivi ni sawa na Rubles 55. Tunajifunza nini kutokana na hali hii kama Taifa huru?

Kabla ya vita USD 1 ilikuwa sawa na Rubles 77, sasa hivi ni sawa na Rubles 55. Tunajifunza nini kutokana na hali hii kama Taifa huru?

Dr Akili

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
5,119
Reaction score
4,569
Tarehe 1 January 2022 dola moja ya Marikani (USD) ilikuwa sawa na Rubles 77 za Russia. Baada ya vita kati ya Russia na Ukraine mwezi Februari 2022, Russia iliwekewa vikwazo (sanctions) lukuki za kiuchumi na dunia inayoongozwa na Amerika na nchi za Ulaya. Lakini leo nchi hizi zilizoweka vikwazo zinalia kwa njaa na mfumuko mkubwa wa bei ambao haujawahi kutokea tangu dunia hii iumbwe. Nchi hizi sasa zinabadili USD 1 kwa Rubles 55 ili kupata chakula na nishati kutoka Russia. Mara nyingi zinalazimika kupata vitu hivi kupitia kwa nchi janja za China na India.

Hii ndiyo maana ya nchi kumiliki rasilimali asili zake. Nchi zetu nyingi zimeshindwa kufanya hivyo. Utakuta nchi kama Nigeria yenye rasilimali kubwa ya mafuta ya petroleum, mafuta yake yote huenda ughaibuni na yenyewe kulazimika kuagiza mafuta yake kutoka Uarabuni kama sisi. Gesi ya LNG inayovunwa Mozambique yote huenda ughaibuni na wao kuambulia kiduchu. Yote haya yanatokea kwa sababu nchi hizi siyo wamiliki wa rasilimali hizi kufuatana na mikataba waliyowekeana na hizo nchi tajiri za ughaibuni.

Sisi mambo yakoje? Jee huo mkataba wa mradi mkubwa wa LNG unasemaje? Jee tumejipangaje kulisha dunia kwani tuna ardhi tele na mito tele ya umwagiliaji? Ardhi yenye rutuba na malighafi tele ya kutengeneza mbolea.
 
Ni aibu na fedhea kwa nchi zetu za kiafrica. Tuna rasilimali za kutosha ila tunategemea vitu ving kutoka kwa watu wanao beba rasilimali zetu.

Sisi africa tumekali u dini tu. Kucha kutwa ni kuangaika na dini zilizoletwa na wao wenyewe.

Tanzania tuna chuma ya kutosha huko liganga ila mpka leo hatujaanza kuvuna na chuma imegundulika toka karne ya 17. Sasa inawezekanaje sisi mpka leo tushindwe kuchimba chuma kama walivyochimba karne ya 17
 
America wamebugi sana kwenye hii vita, wangekuwa na akili wala wasingetaka kui-prolong iendelee kupiganwa kwa muda mrefu kwa kuendelea kuwapa silaha Ukraine.

Walitegemea kuidhoofisha Russia, lakini mambo yamekuwa kinyume, ruble inazidi kupanda thamani na uchumi wa Russia kuimarika, mfumko wa bei kwenye nchi magharibi ni wa kutisha, yaani kila kitu kimeparaganyika kwa sasa. Kwa jinsi wamarekani walivyo wabinafsi watataka hali iendelee hivyo tu kwa sababu ya interests zao.
 
Tarehe 1 January 2022 dola moja ya merikani (USD) ilikuwa sawa na Rubles 77 za Russia. Baada ya vita kati ya Russia na Ukraine mwezi Februari 2022, Russia iliwekewa vikwazo (sanctions) lukuki za kiuchumi na dunia inayoongozwa na Amerika na nchi za Ulaya...
Msumbiji/Mozambique mradi wa LNG ndio upo kwenye utekelezaji bado hawajaanza kunufaika nao
 
Ni aibu na fedhea kwa nchi zetu za kiafrica.. Tuna rasilimali za kutosha ila tunategemea vitu ving kutoka kwa watu wanao beba rasilimali zwtu....
Chuma kilichopo Liganga kinatosha matumizi ya dunia nzima kwa zaidi ya miaka 100. Kiasi cha gesi iliyopo kwenye ardhi na bahari yetu inaizidi ile iliyoko Russia na Ukraine combined.

Lakini tunajiona wanyonge kwenye dunia hii na kuendelea kuwa ombaomba wa dunia kama walivyo ndugu zetu na watani zetu Wagogo kwa akina Ndugae!

Tuna maelfu kwa maelfu wa tembo wenye nzuri zenye thamani kubwa sana duniani ambazo tungaliweza kuwa tunazivuna bila kuwaua tembo (bali tunawapandikizia za bandia). Thamani ya pembe za tembo 100 kwa mwezi ingalituwezesha kuteremsha bei ya mafuta ya petroli hadi kufikia Sh buku moja au hata jero kwa lita!!!
 
Tarehe 1 January 2022 dola moja ya merikani (USD) ilikuwa sawa na Rubles 77 za Russia. Baada ya vita kati ya Russia na Ukraine mwezi Februari 2022...
Dr Akili una akili, sisi kujipanga ni ngumu maana wanaotutawala hawana akili kama ulizonazo wewe. Wenye akili wamenyimwa mamlaka ya ubunifu na wasio na akili, ubunifu kwa sababu wanaendekeza njaa.

Sisi tunazo kila aina ya raslimali na baadhi take ni adimu lakini AKILI za kiuongozi ni zero.
 
America wamebugi sana kwenye hii vita, wangekuwa na akili wala wasingetaka kui-prolong iendelee kupiganwa kwa muda mrefu kwa kuendelea kuwapa silaha Ukraine. Walitegemea kuidhoofisha Russia, lakini mambo yamekuwa kinyume, ruble inazidi kupanda thamani na uchumi wa Russia kuimarika, mfumko wa bei kwenye nchi magharibi ni wa kutisha, yani kila kitu kimeparaganyika kwa sasa. Kwa jinsi wamarekani walivyo wabinafsi watataka hali iendelee hivyo tu kwa sababu ya interests zao.
EU ni mitoto mijinga mijinga, imeshikiwa akili na US
 
Kalaga baho! Hata maziwa Victoria na Tanganyika yana gesi. TPDC hawana uwezo wa kufanya utafiti. Tunawategemea hao wazungu watufanyie utafiti, na wakiigundua inakuwa mali yao.

Hiyo sasa ni speculation. Proven natural gas reserves zetu ni nothing ukilinganisha na za Russia na Ukraine.

 
Back
Top Bottom