Kafulila: Anayetaka kuwekeza TANESCO na aje,Tanzania inajengeka kwa Kasi mno mwaka 2050 tutahitaji zaidi ya Megawatt 60K wakati leo tuna Megawatt 4K

Kafulila: Anayetaka kuwekeza TANESCO na aje,Tanzania inajengeka kwa Kasi mno mwaka 2050 tutahitaji zaidi ya Megawatt 60K wakati leo tuna Megawatt 4K

Tuna Megawatt 4K ?!!!!! Yaani huyu mtu ambaye hata basics anakosea ndio tunampa udalali wa kuuza moyo wa nchi (NISHATI)?!!!!

Ni kwamba Bwawa lingekamilika tunge double capacity na kama wangekuwa na akili na busara badala ya kuendelea kuwa madalali wa LPG inayotoka ughaibuni hizo hizo double capacity zingesaidia watu kupikia umeme kuliko kuchukua Kodi zao ili kununua gesi kutoka Nje...


Na kwa kufanya hivyo watu wangebakia na pesa za kutumia kwa shughuli nyingine

Na kama ni issue ya kuwekeza wangeweza kumtumia Mtanzania mwenyewe kila mtu mwenye makazi ili achangie uzalishaji na hivyo kuweza kupikia kwa kutumia gharama ya 0
Hujui unachoandika naona
 
===
Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Ubia nchini PPPC Bwana David Kafulila akihojiwa katika Kipindi Cha One on One Cha Wasafi TV amesema Tanzania katika miaka 25 ijayo inatarajia kujenga Uchumi mkubwa karibu mara mbili ya Uchumi wote wa Africa ya Kusini ya Leo.

Kafulila anaendelea kwa kusema kama Africa ya Kusini ya leo Wana Umeme unaofikia Megawatt 60,000 huku sisi tukitarajia kujenga Uchumi marambili ya Uchumi huo wa Africa Kusini leo maana yake lazima tuwe na Umeme unaozidi umeme wa Africa ya Kusini ya leo ambao ni zaidi ya Megawatt 60,000.

Swali tunaloweza kujiuliza kwa pamoja, ni Je, bila kushirikisha mitaji na Ujuzi toka sekta binafsi PPP Tanzania kwa kutumia Kodi na Mikopo pekee tunaweza kufikia kumiliki umeme wa Megawatt zaidi ya 60 ifikapo mwaka 2050 Jibu ni "HAPANA" lazima PPP ichukue nafasi kwenye hili kwa manufaa ya kizazi hiki na manufaa ya kizazi kijacho.







View attachment 3202423



====


Tanzania nchi ya ajabu sana. Kuna wawekeaji wamekuja kuanzia Songas na wengine. Wakija wanaombwa rushwa na hao hao wanasiasa halafu wanalalamika mikataba mibaya baada ya kupata 10%. Tukivunja mikataba ni madeni.

Kafukila atueleze serikali imelipa kiasi gani kwenye kesi za uwekezaji Tanesco kwa miaka 15 iliyopita?
 
Hujui unachoandika naona
Na hicho ndio unifanya kuwa bora kila kukicha sababu nafahamu kwamba sijui hivyo kujifunza kupembua na kutafuta ukweli wa kila jambo na sio kama wewe kulishwa kila unacholishwa na kukikubali kama kilivyo...
  • Hawa madalali unawaoamini kila wanachokwambia na kuwapa leeway kwamba watafutie mwarobaini shida zetu ndio walitaka kutuingia chaka na ADANI katika umeme na huyu akiwa dalali namba moja (one has to think labda alikuwa naive au amekula mlungula) na sababu hatuna uhakika ngoja tuangalie yenye uhakika
  • Je hawa watu wangempenda mwananchi wangempelekea mitungi ya gesi ambayo mwisho wa siku gharama ni Tshs mia tatu na ushee wakati ageweza kutumia umeme kwa gharama ya Tshs 100 /=?
Punguza kuwa cheerleader na kupembua hoja na unachoambiwa hata kama unalipwa sidhani kama malipo hayo yanazidi gharama ambayo utatumia maisha yako yote kwa kupikia iwapo tutaendelea na LPG badala ya Umeme at an affordable Cost....
 
Tanzania nchi ya ajabu sana. Kuna wawekeaji wamekuja kuanzia Songas na wengine. Wakija wanaombwa rushwa na hao hao wanasiasa halafu wanalalamika mikataba mibaya baada ya kupata 10%. Tukivunja mikataba ni madeni.

Kafukila atueleze serikali imelipa kiasi gani kwenye kesi za uwekezaji Tanesco kwa miaka 15 iliyopita?
Wewe hayo maswali peleka TANESCO
 
Kwa nini awekeze Tanesco? Hawezi kuwa na shirika lake likawa linauza umeme kwa Tanesco? Huyu jamaa anyone Tanesco inapona kutoka mikataba ya hovyo, kila siku anawaza kuirudisha Tanesco ilkotoka. Hovyo kabisa.

Muwekezaji, Atafute chanzo cha umeme kisha aiuzie Tanesco, alipwe kwa anachouza, sio capacity charges
 
Kafulila ana ndoto hizo,ni kweli umeme tulionao kibindoni,kwa miaka 5 ijayo hautatosha kabisa ukuzaji viwanda vikubwa.

Lakini Mungu aja tutupa kwa kutumia rasilimali zetu tuna uwezo wa kufua hata Mega Watt 200,000 na zaidi kwa vyanzo hivi.:-
1.Kufua umeme kwa kujenga mitambo midogo midogo ya nuclear kutokana na utitili wa madini ya uranium yanayopatikana maeneo mbali mbali nchini kwetu.
Serikali ya Uganda inayoongozwa na Museveni imeishatenga eneo mahususi la kujenga mitambo ya kufua umeme wa nuclear.
Mradi huu PPP hatumuhitaji kwa maslahi mapana ya taifa letu.
Bila kumungunya maneno bingwa wa kujenga mitambo salama na bila masharti magumu ni France.

2.Solar power,Wind turbine Power,Geothermal power,Battery Power n.k serikali na taasisi binafsi wanaweza kuzalisha nishati ya kututosheleza sisi na hata majirani zetu kuwaunganisha kwenye grid ya taifa.
Lakini bado tuna machungu ya makampuni binafsi za Richmond, IPTL,Songas.
Ni bora kwanza kuunda sheria,au kanuni zenye kumlinda mtumiaji asinyonywe kama huku nyuma.

Mwisho Kafulila tumia muda huu kuishawishi serikali kujenga uwezo wa wananchi waweze kusimamia na kumiliki miradi mikubwa mikubwa.
Kwa akili ya CCM ya kugawa t-shirt na chumvi Kwa wapiga Kura itawezekana?
 
Ninamaana sekta binafsi.
Kwani umekatazwa ? Hata jana au Juzi au miaka kadhaa iliyopita haukukatazwa kuzalisha (Ndio kina Mobisol walivyokuwa wanafanya kwa kuuza Solar) Au Makamba alivyoingia Mikataba na wale mimi ninaowaita Matapeli ili wazalishe Solar na kuuzia Tanesco kwa bei mbaya, hakuna tofauti na kina Dowans, Symbion na watu kama hao... Ndio maana nilishasema na nitaendelea kusema yoyote anayeweza kuzalisha na azalishe ila Tanesco wanunue na kusambaza na wanunue iwapo tu cost itakuwa ni ndogo kuliko Tanesco anavyoweza kufanya mwenyewe...

 
Dalali tumbili kazini.
image-insert-your-face-monkey-baby-animal-34515.jpg
 


Shida zaidi ni hao media wenyewe nchi ina energy plan, ambayo ni ya hovyo kwenye finance tu.

Yaani wana mipango ya projects za kuanza utekelezaji miaka mitano baadae na estimated costs, udhani kama wana inflation adjustments.

Worst katika hiyo mipango yao hakuna sehemu inayozungumzia industry structure to attain that goal.

Anachoongea Kafulila na strategic panning ya serikali ni vitu tofauti,

Mambo kama haya ni possible kwenye ‘banana republic’ kama Tanzania.
 
===
Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Ubia nchini PPPC Bwana David Kafulila akihojiwa katika Kipindi Cha One on One Cha Wasafi TV amesema Tanzania katika miaka 25 ijayo inatarajia kujenga Uchumi mkubwa karibu mara mbili ya Uchumi wote wa Africa ya Kusini ya Leo.

Kafulila anaendelea kwa kusema kama Africa ya Kusini ya leo Wana Umeme unaofikia Megawatt 60,000 huku sisi tukitarajia kujenga Uchumi marambili ya Uchumi huo wa Africa Kusini leo maana yake lazima tuwe na Umeme unaozidi umeme wa Africa ya Kusini ya leo ambao ni zaidi ya Megawatt 60,000.

Swali tunaloweza kujiuliza kwa pamoja, ni Je, bila kushirikisha mitaji na Ujuzi toka sekta binafsi PPP Tanzania kwa kutumia Kodi na Mikopo pekee tunaweza kufikia kumiliki umeme wa Megawatt zaidi ya 60 ifikapo mwaka 2050 Jibu ni "HAPANA" lazima PPP ichukue nafasi kwenye hili kwa manufaa ya kizazi hiki na manufaa ya kizazi kijacho.







View attachment 3202423



====
Tanzania haiwezi kufikia umeme huo unaotajwa, huo ni 20 times threshold ya SA, uliopo sasa haupo stable unakatikatika kila wakati. Kwanini hamsemi ukweli. Kwa culture hii ya kutekana mtapata wawekezaji wa ovyo labda watoke China, Vietnam na Turkey waliozoea mambo ya kutoheshimu haki za binadamu, na hao wawili wa mwanzo watawafanyisha kazi kama punda. Hawawajali ninyi waafrica.
 
Back
Top Bottom