Kafulila: Serikali inakopa T-bills kwa 5% wakati Msumbiji 17%, Kenya 16%, Malawi 16%, Zambia 10%, Namibia 9%, Uganda 9%, SA 8%. Uelekeo wetu ni sahihi

Ni wapi katika sentensi zangu nisema Thailand haina madeni? jibu hoja, kwa nini tunafurahia sana kukopa? yaani akinya tembo lazima na wewe unye, si ndio? Hii mikopo ina tofauti gani na kausha damu? tuna utaratibu gani wa kujikwamua kutoka katika madeni au kila siku ni kula vya watu. Kukopa harusi, kulipa matanga sio ndio maana yake au? siku hazigandi, ipo siku utasikia tumewekwa kwenye, "highly indebted countries" na kufika hapo sijui utasemaje....
 
Ni wapi katika sentensi zangu nisema Thailand haina madeni? jibu hoja, kwa nini tunafurahia sana kukopa? yaani akinya tembo lazima na wewe unye, si ndio?
Nimejibu hii ishu Yako mara nyingi na hii itakuwa mara ya mwisho
-Kukopa ni lazima Kwa sababu ni economic tool
-Iko.wazi Nchi maskini Zina Changamoto ya Mitaji(as per vicious circle of poverty) na the only way utapata mtaji ni kukopa na kuvutia wawekezaji Ili uweze ku exploit resources na kubadili kuwa weath

Mwisho kukopa na kukopesha is a must,hakuna Nchi iliwahi endelea bila kukopa na msilete dhana zenu duni za mikopo ya mtaani kwenye muktadha wa Nchi,hakunaga kitu kama hicho.
 
Ingia kwenye website ya BOT Kuna Mnada wa T-Bills na T-Bonds utapata
Kwani mikopo wanakopa Govement Bonds ( Treasury bonds na Bills) au ni zile za nje ya nchi. Nisaidie mambo ya nchi bila kupewa muongozo unaweza kujikuta unashangilia hewa.
 
Kwanini kwa hizo nchi nyingine ametumia data zenye viwango vya riba vya mwaka huu, wakati Tanzania ametumia vieango vya riba vya mwaka 2021? Tatizo nini? Kwanini Tanzania haitaki ku update takwimu zake?
 
Kwani mikopo wanakopa Govement Bonds ( Treasury bonds na Bills) au ni zile za nje ya nchi. Nisaidie mambo ya nchi bila kupewa muongozo unaweza kujikuta unashangilia hewa.
Kwa muktadha wa hoja ni mikopo ya ndani ya Nchi(bonds na bills) japo hata hizo inaweza kushikiliwa na Nchi za Nje au private sector ya Nje but Sina hakika kama sheria zimebadilishwa Kwa Sasa ila Kwa USA,China ndio anaongoza kushikiliwa hizo T bills za Marekani.
 
Hakuna mantiki yoyote ya kulinganisha riba wanazopewa wengine na riba anayopewa Tanzania au Tanganyika. Haijawahi kutokea kwenye elimu ya fedha popote. Hata hizo data za Kafulila hazina ushahidi wowote!
Kwa maneno rahisi unaweza tu kulinganisha na uwezo wako wa kuzalisha ziada kutokana na mikopo ili uwe na uwezo wa kurudisha huo mkopo. Kama uwezo wako wa kuzalisha ziada ni 6% ukikopa kwa 9% kama Uganda maana yake uwezo wako wa kulipa kutokana na ziada ni mdogo kwa hiyo lazima ukimbilie kwenye riba ndogo.
 
Safi sana. Lakini hii Kafulila hawezi kuielewa!
 
Nilikiwa sijui. Sasa hizi takwimu za Mh tunazihakikia wapi ili tuungane kushangilia mafanikio ya mama kwa uelewa
 
Kumbe Kuna nchi zinazotamani kukopa kwa riba kubwa?
 
Sio Sifa ila hata familia yako kama unataka kuwa tajiri kuwazidi wengine lazima ukope, Bakresa pia analoan kibao kwenye mabenki
Utajiri wa Bakhresa ulichangiwa kwa kiasi kikubwa kwa kupewa mali za Tanganyika bure na Rais Mwinyi wakati wa utawala wake. Mali hizo hizo ambazo shirika la umma la serikali lililoshindwa biashara ya kuuza mikate (ujinga au rushwa) alizopewa bure ndizo anatumia kama dhamana kuchukua mikopo.
 
Hili Mimi sikufahamu na sijui kama ni kweli lakini mwisho unakiri alikopa ndio maana Leo ni tajiri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…