Kagame anajisifia kufunga makanisa na misikiti: Ajiandae kukutana na mkono wa Mungu!

Ila kwa namna nyingine yupo sahihi, watumishi wakasome

Yasijirudie ya kimbari
 
Yatakiwa Tz pia hiyo sheria ije...
Misikiti inajengwa hovyo, inaamua kupiga kelele

Makanisa yanajengwa hovyo, yanasababisha usumbufu usio na lazima
 
nchi yenyewe in 26000sqkm kama mkoa wa Tanga iwe na makanisa zaidi ya 6000 na misikiti zaidi ya 100. Ni lazima ufute mengine maaana itakuwa kila baada ya nyumba tatu kuna kanisa au msikiti. Wala si jambo la kujisifu, ye yote anaweza akafanya hilo
 
mimi sio mfuasi wa dini yoyote,ila naheshimu imani za watu.

katika hili najua wagalatia hawana shida, hutawaona wakilalamikia uamuzi wa paul kagame.

shida ni wale ndg zao wa upande wa pili, hawa itakuwa inawauma sana na wanatamani watume magaidi pale kigali wapalipuwe.
 
Huwezi kutumia mfano wa wachungaji waovu ili kuhalalisha kukataa huduma za wachungaji wote hata wale ambao ni wa kweliu. kinachotakiwa ni kuwachukulia hatua muafaka wale ambao ni fake na kuwatia moyo wale ambao ni wa kweli!
Ndio ameshawachukulia hatua barabara.
 
Unamtisha Kagame!!??
 
Ninachofurahia Ni Kagame kuwanyoosha matapeli barabara,Sasa Nyie wanakondoo suala la kulalamika sidhani Kama Ni inshu.
 
Acheni utumwa wa fikra nyie watu weusi, mzungu na mwarabu kawaletea dini kama utumwa mpya wa kifikra, Kagame ameona mbali sana huu upuuzi wenu wa dini msitishe nao, mbona wazungu wamechinja kondoo kwa malkia je, ni nini kama sio mila zao!? Heshimu mila zako, achana na dini zilizoletwa na wakoloni
 
Acha kutetea wapuuzi na ujinga wa hao jamaa,tena Sheria ilitakiwa ziwe Kali zaidi ya hizo za Kagame.
 
Heshimu mila zako, achana na dini zilizoletwa na wakoloni
Mbona kuingilia uhuru wa mwenzako? Wewe si uheshimu mizimu inatosha?

Halafu mbona nguo zilizoletwa na wakoloni unavaa bila tatizo? Hapo tukikukagua umejaa vitu vilivyoletwa na wakoloni.

Rudi kwanza kwenye nyumba za nyasi huko ndio nitaamini kweli unaamini ulichoandika
 
Sasa hapo amepinga dini au amewapinga wapigaji?
 
Natamani kuwe na kiongozi atakayepiga ban kama huyo Kagame. Baadhi ya makanisa yamekuwa kero. Hata huyo mungu tunayemwabudu ni mungu wa utaratibu. Hakuna haja ya maspika ya adhana, kila mtu ajue mda wake wa kwenda kuabudu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…