Kagame awatuhumu SADC na Ramaphosa kuwaunga mkono Congo. Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama SADC ni Rais Samia!

S
SADC sio Tanzania, na jeshi la Tanzania haliwezi beba majukumu ya SADC
Jeshi la Tanzania linaweza kuchukua jukumu Hilo endapo Jeshi la DRC litaomba msaada, Kwa sasa vikosi vya SADC viko chini ya south Africa ambayo haina uzoefu wowote katika vita ndio mana tunaomba DRC kuharakisha mazungumzo na Tanzania ili JWTZ waingie kazini wao kama wao
 
Hii ndio solution
Lazima nguvu ya kijeshi itumike Kwanza ndio duplomasia ianze
Sababu M23 Kwa sasa ni invaders kutoka Rwanda
 
Kamgombeza kama mtoto mdogo Rais wa Afrika Kusini kuhusu majeshi yake yanavyoisaidia Congo.

Kawananga SADC ambayo mwenyekiti wa Kamati yake ya Siasa na Usalama ni Rais Samia kuhusu support wanayoitoa kwa Congo.
Kinachompa kiburi Kagame ni jeshi lake wakisaidiana na M23 wanavyopeleka moto mkali huko kwa ufanisi na kutwaa maeneo kiulaini na kuteka wanajeshi wa serikali na wa UN...


View: https://youtu.be/lBQEcK7UXQY?si=vBnu6QaizqKtIFay
 
Rais Paul Kagame awauliza marais wenzie swali gumu bila kupepesa macho, kuwa hali iliyopo Mashariki ya Kongo walikuwa hawalitegemei ?

Jinsi Rwanda ilijibu ombi la wafanyikazi wa UN Kongo ndani ya dakika 15​


View: https://m.youtube.com/watch?v=AIpyLOzTIGQ
Hakika intelejensia na mifumo ya serikali ya Rwanda ilishaliona suala hili kitambo na kuk8chukulia hatua kwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama na vya kiraia kujipanga kutoka Rubavu mpaka na Gima hafi Kigali...

Muwakilishi anasimulia A-Z walivyopata ushirikiano kutoka Rwanda kusaidia zaidi ya wafanyakazi 1,000 wa UN na familia zao kuweza kuvuka mpaka kutoka Congo kuingia Rwanda hadi kupewa makazi katika hoteli za hadhi 34 nchini Rwanda wakiendelea na mipango ya kuwasafirisha kwenda ...
 
Mwenyekiti wa kamati yausalama SADC ni nani? Kwa hiyo amepata CV mpya ya kuisambaratisha Congo chini ya utawala wake.
 
Mtanzania sahv issue kubwa ni kukata mauno,udaku, uchawa,kubishana mambo ya mpira tu

Ova
 
Wewe ndio unayetakiwa kuwa na adabu. Ukiwaita binadamu wenzako kenge basi ujue wewe, wazazi wako, watoto wako na ndugu zako wote nao ni KENGE!
basi sio kenge ni fisi maji, na wewe ndio fisimaji mwenyewe unayetaka kuleta stress
 
Hayo majukwaa yamebaki ni ya kwenda kulia "bata" tu, basi.
 
M23 asogeee nchi fulani alete amshaamsha

Ova
 
Hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu!
 

Mkuu Lord Denning , matamshi ya Kagame yamekuja kutokana na kauli ya rais Ramaphosa aliyoitoa siku chache nyuma wakati akitoa taarifa na kuomboleza vifo vya askari 13 wa South Africa waliouawa na M23, DRC. Ramaphosa alisema wameuawa katika shambulio lililofanywa na M23 na jeshi la Rwanda.
Na Kagame katumia kuteleza kwa Ramaphosa kidiplomasia kwa kuitaja Rwanda kuhusika na hilo shambulizi kama kivuli cha kuficha uhalifu wake halisi wa kuwafundisha,kuwapa silaha na kupigana moja kwa moja kijeshi na M23.
Kwa kutumia hicho kivuli akapindisha ukweli kwamba majeshi ya SADC yaliiyopo Congo yanasaidia jeshi la serikali,japo anajua ukweli kwamba hilo jeshi lipo pale kulinda amani tu kama lilivyokuwa jeshi la UN......Na ndo maana askari wa hilo jeshi wanauawa kwa kuviziwa wakiwa katika relaxed mode, na siyo katika combat action.
Ndo maana nasisitiza kama nilivyosema jana kwamba kulisaidia jeshi la Congo kimya kimya kwa mlango wa nyuma ni njia bora zaidi kwa vile inamnyima Kagame na washirika wake nafasi ya kupindisha maneno.
Uhuni wa Kagame wa uvamizi wa Goma ni strategy yake kuilazimisha DRC iingie katika meza ya mazungumzo kwa terms za Rwanda.
Imekuwa jambo bora DRC imetangaza kujitoa katika mazungumzo....na kwa vyovyote kwa ushauri wa wanaotoa backing nyuma ya pazia.
Ni suala la muda tu....when the screws are tightened hard enough on the battle ground...,that tall and lean statesman will surely feel the heat and ....will utter a different rhetoric.
Isitoshe, Kagame naye alipotea kidilomasia katika hotuba yake fupi ya malalamiko. Aliji implicate katika kile anachotumiwa kwa muda mrefu. Alisema anashangaa nchi zote zimefumbia macho raia wa Congo wenye asili ya kitusi wanavyoteswa kwa muda mrefu ndani ya DRC kiasi wengi wao kuwa wakimbizi ndani ya Rwanda. Akasema, .."hao watusi wakinyanyaswa na kushambuliwa na jeshi la Congo ,nchi zote zinakaa kimya... lakini M23 ambao wakiwatetea hao wanaonyanyaswa ,kila mtu anawashutumu.... hii haikubalik ...lazima jambo lifanyikei".
Kwa kauli yake hiyo inayoonesha yuko sympathetic na M23, amejikamatisha mwenyewe.
 
Kagame yuko right. Waasi wa Congo wana haki ya kusaidiwa kama waasi sehemu zingine wanavyosaidiwa.

Wacha wapigane lakini Tanzania huo ugomvi hautuhusu hivyo kama wewe binafsi unakereheka nao jiunge na jeshi ka congo upigane na hao waasi lakini Tanzania hiyo vita haituhusu.
 
USAHIHI wa Kagame uko sehemu gani?
Kwanza si lweli kwamba hao wakimbizi aliowasema wapo. Hakuna wakimbizi wa DRC waliopo Rwanda...hiyo imekuwa officially established.
Kagame kuvamia kwake Congo na kuteka maeneo na kufanya eneo zima lisiwe na amani na utulivu...,ndo anakuwa sahihi?
utulivu wa mashariki ya Congo na watu kufanya shughuli zao kiuchumi kuna uhusiano wa moja kwa moja na maslahi ya Tanzania. Pata picha moja tu rahisi..,..japo Congo kuna utajiri wa miti mingi kuliko Tanzania,lakini wakazi wa mashariki ya Congo ndo wanunuzi wakubwa wa mkaa Tanzania,...unafikiri hizo bidhaa nyingine amabzo kule hazizalishwi wanazinunua kwa kiasi gani huku kwetu?
Kwa kuwa kuzingatia jiografia ya eneo na ukaribu na miundo mbinu ya kuifikia Dar port..kwa vyovyote wakazi wa mashariki ya Congo wanaitegemea Tanzania kama export getaway. Utasemaje hatunufaiki na DRC?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…