Kagera: Mwalimu ampiga mpaka kuua mwanafunzi wa kidato cha tatu aliyevunja mlango wa nyumba yake ili kuiba simu

Kagera: Mwalimu ampiga mpaka kuua mwanafunzi wa kidato cha tatu aliyevunja mlango wa nyumba yake ili kuiba simu

Hiyo ni kuua bila kukusudia akipata wakili mzuri kesi nyepesi hiyo
Anafungwa tena anafungwa mchana kweupe.
*Mtuhumiwa nadhani ni under age if 18 alikua ana uwezo wa kumdhibiti,na katika maelezo kijana alikua anajaribu kukimbia inamaana huwezi ukasema ni act if defence ilhali mtu hakuwa anakushambulia.
Hiyo ni murder case mzee sio homicide/manslaughter.
 
Mwalimu wa Shule ya Msingi...
Mwanafunzi ni kidato cha tatu...
Huenda Mwalimu alikuwa anajua anapigana na Mwizi, na hakumtambua Mwizi kama ni mwanafunzi wake.
 
Stress za mafukara. Hata waajiriwa wa serikal haswa waalim ni mafukara tu, unawezaje piga mtoto hadi umuue
 
Huyo kakusudia kuua kumpigia ngumi usoni kisha akaenda kutafuta nondo na kumpigia nayo ni mwilini ni first degree murder
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera linamshikilia Mwalimu wa Shule ya Msingi Igurwa, Adrian Tinchwa (36) kwa tuhuma za kumuua, Phares Buberwa mwanafunzi wa kidato cha tatu Shule ya Sekondari Igurwa.

Taarifa iliyotolewa jana Jumanne Septemba 24, 2024 na Kamanda wa Polisi mkoani humo, Blasius Chatanda imesema mwalimu huyo ambaye ni mkazi wa Kata ya Kanoni wilayani Karagwe, inadaiwa alimshambulia marehemu kwa kumpiga ngumi kwenye paji la uso na kutumia nondo kumpiga nayo miguuni na mikononi baada ya kumtuhumu kuiba simu yake.

Soma pia: Mwalimu adaiwa kumpiga ngumi mwanafunzi na kumng'oa jino, eti Kisha kapata alama 29 za Hisabati

"Tukio hili lilitokea Septemba 18, 2024 saa 8:00 mchana katika kijiji cha Kanoni Wilaya ya Karagwe, ambapo mtuhumiwa awali mnamo tarehe hiyo saa 3 asubuhi, imedaiwa alifika nyumbani kwake na kukuta kufuli la mlango wa nyumba yake likiwa limevunjwa na alipotaka kuingia ndani alikutana na Phares Buberwa mlangoni akiwa anatoka ndani huku akijaribu kukimbia," amesema.

"Na ndipo mtuhumiwa alimkamata na kuanza kumshambulia hadi kusababisha kupata majeraha makubwa mwilini mwake na baadaye mtuhumiwa alimpeleka hadi nyumbani kwa wazazi wake na kumkabidhi kisha wazazi wake walimpeleka katika Kituo cha Afya cha Rwambaizi kwa ajili ya kupatiwa matibabu ambapo alifariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu," amesema Kamanda Chatanda.

Source: Mwananchi
Kwahiyo alimpiga mwizi?
 
Back
Top Bottom