Kaimu IGP Masengeli ahukumiwa kifungo cha miezi 6 jela kwa kudharau Mahakama

Uhuru wa mihimili. Ngoja tuone kama walitengeneza katiba au walitengeneza ujinga. Yaani IGP afungwe miezi sita? Executive kabisa mwenye askari wenye bunduki?

Askari wakikubali boss wao akamatwe watakuwa wamekosea sana.

Inatakiwa huyo Jaji akamatwe kwa kuutukana mhimili. Akae mahabusu za polisi ili ajue mipaka yake
 
Very nice.
Katiba ya Kenya inanikosha roho Sana Mimi. No one is above the law!
 
Kaimu Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Kenya, Gilbert Masengeli amehukumiwa kifungo cha miezi sita gerezani baada ya kudharau wito wa mahakama mara saba mfululizo.

Masengeli alitakiwa kuieleza Mahakama kuhusu madai ya kutekwa nyara ndugu wawili na mwanaharakati mmoja kwa kipindi cha wiki mbili, ambao walichukuliwa kinguvu na watu waliovalia suti, wanaodaiwa kuwa maofisa wa Polisi kutoka Nairobi, huku wakishindwa kutoa sababu za kuwakamata.
 
Katiba ya Kenya ni nzuri. No one is above the law
 
Katiba ya Kenya ni nzuri. No one is above the law
 
Kwel uchawi upo nchi jirn hvo nchi nyingne sasa hadi afisa mkuu n chawa kuna nn sasa kwa mteuliwa wa presida
 
Nchini kenya Kaimu IGP kahukumiwa miezi 6 jela kwa kosa la kutoheshimu wito wa mahakama.

Sasa je kwa upande wa kwetu tanzania kitu kama hiki kinaweza kufanyika na je wataalamu wa sheria mtusaidie kwa nchi yetu kuna vifungu vinaweza wabana wakuu wa vikosi kama hawa kama ilivyo kwa nchi ya Kenya?

Tupe dondoo...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…