Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, Naomba Usiruhusu Udhalilishaji Huu Ndani ya Mahakama Zetu!.

Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, Naomba Usiruhusu Udhalilishaji Huu Ndani ya Mahakama Zetu!.

Pascal Mayalla,
Naona hapo ni kama kuonesha ushindi kuwa mtuhumiwa tayari amepatikana na ''hatia'' na suala la kusubiri hukumu ya Mahakama kumtia hatiani ni suala la ''uhakika'' bila shaka kwa asilimia 100%.

Picha nyingi za watuhumiwa Hazina tofauti na picha za wawindaji na ''kipusa'' wakipata picha ya ushindi wa kazi yao porini

01trophyhunting.adapt.1190.1.jpg

Photo: trophy hunting of elephants courtesy of Nationalgeographic.com http://news.nationalgeographic.com/...ng-elephants-tusks-poaching-zimbabwe-Namibia/
 
kiukweli polisi wetu wamekua wanafanya show off bila kuzingatia sheria za nchi....kuna muda hua nafikiria polisi wangepitia kusoma sheria za nchi angalau mwaka mmoja kabla hawajaanza kazi.....maana hua nahis hawajui
 
Hata mimi naliona sana hili kufanywa kwa baadhi wa watu.
Lakini naamini kitu kimoja..ukikataa pale kuinama sidhani kama watakupiga mbele ya mahakama.
Ni kukataa tu pale kuna public na media
Hakuna sheria hio ya kudhalilisha watuhumiwa.
Hata wale watuhumiwa wa bashite nao walifanywa kama hivi
 
Bora Paskali umelisisitiza hilo, kama mwahabari, na kulikemea. Inadhihirisha ni kwa jinsi gani tunavyotumia vibaya uhuru wa mawazo kutoa na kupata habari, hasa wakati huu wa utitiri wa social media.

Zaidi ya hilo Kuna watu wanataka waadhibiwe pasipo kuhukumiwa maana wamekwisha kuwahukumu kabisa. Hata baadhi wa wanasiasa na tena wanasheria wanataka, ambao wanawahisi wameshiriki, nao wakamatwe. . Hakika hii ni Nchi ya watu wa kujua kila kitu.

Mungu Ibariki Tanzania, kwenye utawala huu tusikia na kuona mengi, kwa kuwa tu Rais amethubutu kuchukua hatua ambazo ni kiongozi mwenye utashi wa kisiasa anaweza kufanya hivyo. Kwa sababu hiyo wapo wa kumuunga mkono na wapo wa kumkejeli, na wapo viongozi wa kujikomba mwishowe wakafanya kinyume na ustaarabu na sheria.
 
Mbona huo ni utaratibu wa kawaida pale mahakamani. Mtuhumiwa akitoka ndani ya Mahakama wakati anasubiri karandinga anatakiwa kuchuchumaa ili asikimbie. Huu utaratibu umekuwepo kwa muda tu. Nashangaa leo kuna watu mnajitoa fahamu! Au kwa kuwa ni Singasinga na Ruge!? Inapelekea kuamini kwamba Bwana Pascal Mayalla umeshachukua bahasha kutoka huko kunako "Dude".

Umesahau ya kwamba Yona na Mramba nao walichutama wakati wanasubiri karandinga!?

Hawasubiri karandinga bali huwekwa vile kwa ajili ya picha. Wakisha maliza waandishi ndio wanaondoka
 
Nakubaliana na mtoa Mada. Jana nilimuona yule Mzee Rugemalira na Mwenzake Singh wakichuchuma kwa taabu sana. Singh alikosa nafasi ya kuchuchuma ilibidi Rugemalira asogee kidogo ili apate nafasi.Tusirudie vitendo kama hivi tena. Sisi wote ni binadamu. Leo kwako kesho kwa mwingine.
 
Paskali hajaandika vilema wale kula kipigo posta!
Niliandika Wapenda sifa hapa JF au Waoga Wakafuta hoja! JF saa nyingine wanavuruga sana! I am really Frustrated! Jina langu lipo, na Nasemaga Nikisema kitu hapa JF nipo Tayari kushitakiwa, lakini wapo mamods wanahofu kwa niaba yangu!
 
Dah! Nilifikiri ni mimi tu nimeliona, kutokana na muhemuko wa hili Jambo nikaona ngoja nikae kimya, ni kweli hao jamaa wanatuhumiwa kwa kuhujumu uchumi lakini sikuona sababu yoyote ile ya kuwadharirisha, sasa walipiga magoti ili iweje??
Inawezekana macho yako yanachagua cha kuona ila vingine huoni. Kwa kiasi gani kuna kundi inchi hii linadhalilishwa zaidi ya hao kama sio watanzania. Na haya ni madhara ya kuchua maafisa usalama wenye Zero form four.
 
Nakubaliana na mtoa Mada. Jana nilimuona yule Mzee Rugemalira na Mwenzake Singh wakichuchuma kwa taabu sana. Singh alikosa nafasi ya kuchuchuma ilibidi Rugemalira asogee kidogo ili apate nafasi.Tusirudie vitendo kama hivi tena. Sisi wote ni binadamu. Leo kwako kesho kwa mwingine.
Wanafiki katika ubora wenu. Wamechutama tu mnalialia na kuleta UZANDIKI hapa, Je wakipigwa mikwaju 12 wakati wanaingia na 12 wakati wa kutoka si ndio mtajitapakaza inyee mwili mzima.
 
Back
Top Bottom