TANZIA Kaka wa Freeman Mbowe, Charles Mbowe afariki Dunia

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Taarifa zilizotufikia kutoka Chadema zinaeleza kwamba Freeman Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho amelazimika kukatisha kampeni za operesheni haki huko Zanzibar na kurejea Tanganyika baada ya kupokea taarifa za kifo cha Kaka yake aitwaye Charles Mbowe.

Pia soma > Mbowe awataka wananchi wasihudhurie msiba wa Kaka yake kuepuka maambukizi ya COVID-19



Kwa niaba yangu binafsi na familia yangu na kwa niaba ya wanaJF wote, nachukua nafasi hii kumpa pole kamanda Mbowe na ndugu zake kwa msiba huo.

INNALILLAH YA INNALILLAH RAJUUN.
 
Apumzike kwa amani Charles Mbowe.

Familia ya Mh. Mbowe ionyeshe mfano kwa kuweka sababu za kifo hadharani na kwa uwazi.

Mola awape nguvu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu.
 
...
Kwa niaba yangu binafsi na familia yangu na kwa niaba ya wanajf wote , nachukua nafasi hii kumpa pole kamanda Mbowe na ndugu zake kwa msiba huo .
...
Pole nyingi kwa Mh. Mbowe na familia. Marehemu apumzike kwa amani - AMINA.

Hapo red; isomeke "Mimi binafsi" na sio "Kwa niaba yangu binafsi"; huwezi kujiwakilisha!
 
... Pole nyingi kwa Mh. Mbowe na familia. Marehemu apumzike kwa amani - AMINA.
Hapo red; isomeke "Mimi binafsi" na sio "Kwa niaba yangu binafsi"; huwezi kujiwakilisha!
Asante kwa masahihisho ya Kiswahili, sikijui sana mkuu, najua cha kuombea maji tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…