Kaka yangu ananichukia

Kaka yangu ananichukia

Achana nae....mie ni dada yangu alikuwa hanikubali kabisaa ikawa inaniuma sana nilijaribu kuomba msamaha kwa kosa ambalo silijui ila yeye akawa hataki kabisa...mpaka tumekuwa watu wazima tuna watoto na kazi simtafutagi....simpigii simu....tukikutana nyumban ni salamu kila mtu anafanya mambo yake...sitak shobo...wala namba yake sina....tuko mkoa mmoja wala sijui anapokaa...tunakutana nyumban kwa matukio maalum ya kifamilia namsalimia kawaida kama hamna tatizo....nadeal na wanaonipa furaha basi inatosha
Dada ako atakua mchawi
 
Za leo ndugu zangu, natumai mko poa kabisa.

Kuna jambo limekuwa linanitatiza kwenye maisha yangu nalo ni chuki aliyonayo kaka yangu juu yangu.

Hili jambo nimekosa wa kumshirikisha ikabidi nililete hapa jukwaani kuna watu wanaweza kunisaidia.

Huyu kaka yangu kaanza zamani kunichukia toka tupo wadogo mpaka alipomaliza chuo na kupata kazi hajawahi kunisaidia kitu chochote .

Mwanzo nilidhani labda ana mambo mengi hivyo kipato hakitoshi ila nikaona mbona anasaidia watu wengine lakini mimi nikimuomba chochote ansema hana kitu. Mpaka naanza masomo yangu ya chuo namaliza bro hakuwahi kunisaidia chochote na nilikuwa nasoma chuo Dar es salaam, hata sehemu nilipokuwa napanga hakuwahi kuja.

Ila kwa watu wengine ambao hawana undugu nae safi tu anwatembelea na kuwasaidia wanapokwama.

Huyu bro ameoa ila alikuwa ananiponda Sana kwa shemeji yangu hata ndugu zake na shemeji. Hii hali imekuwa inaninyima amani japo chuo nilishamaliza na ndio napambana na maisha yawe mtaani ila huyu ndugu yangu anaonekana kunichukia sana.

Kuna kipindi alinipita njiani kama hanijui na mimi ikabidi nimkaushie. Nyumbani tupo watoto sita ila huyu ni kaka yetu mkubwa najiuliza kwa nini ana chuki sana namna hiyo.
Unalazimisha undugu kiruuuuh..... Me ndugu wa hvo nawapenda sana nawatesa kimaendeleo sio kimaneno
 
Mkuu ni heri uyo anayekuchukia live live kuliko yule anaekuchukia kimoyoni alafu usoni anakuchekea, ila uyo kaka yako yawezekana ni mchawi so kuna kitu labda alitaka kufanya kwako lkn anajikuta anashindwa kikubwa kaa nae mbali tu
 
Za leo ndugu zangu, natumai mko poa kabisa.

Kuna jambo limekuwa linanitatiza kwenye maisha yangu nalo ni chuki aliyonayo kaka yangu juu yangu.

Hili jambo nimekosa wa kumshirikisha ikabidi nililete hapa jukwaani kuna watu wanaweza kunisaidia.

Huyu kaka yangu kaanza zamani kunichukia toka tupo wadogo mpaka alipomaliza chuo na kupata kazi hajawahi kunisaidia kitu chochote .

Mwanzo nilidhani labda ana mambo mengi hivyo kipato hakitoshi ila nikaona mbona anasaidia watu wengine lakini mimi nikimuomba chochote ansema hana kitu. Mpaka naanza masomo yangu ya chuo namaliza bro hakuwahi kunisaidia chochote na nilikuwa nasoma chuo Dar es salaam, hata sehemu nilipokuwa napanga hakuwahi kuja.

Ila kwa watu wengine ambao hawana undugu nae safi tu anwatembelea na kuwasaidia wanapokwama.

Huyu bro ameoa ila alikuwa ananiponda Sana kwa shemeji yangu hata ndugu zake na shemeji. Hii hali imekuwa inaninyima amani japo chuo nilishamaliza na ndio napambana na maisha yawe mtaani ila huyu ndugu yangu anaonekana kunichukia sana.

Kuna kipindi alinipita njiani kama hanijui na mimi ikabidi nimkaushie. Nyumbani tupo watoto sita ila huyu ni kaka yetu mkubwa najiuliza kwa nini ana chuki sana namna hiyo.


Rahisi sana. Kazana na maisha yako. Tafuta sana hela ufanikiwe... Imetokea tu nyota zenu haziivi so usilazimishe, fanya mishe zako nyingine tu...
 
hakuna tatizo hapo wew tu ndo unahisi kuna tatizo hustle kivyako fanya maisha yako ndugu acha akusaidie akijisikia ila kama hakusaidii komaa tu mkuu.. mimi kulazimisha mzoea na ndugu ni jambo nisilowezaa undugu wa kumtafuta yeye tu wew anahisi unajikomba piga kimyaa..
 
Ni ndugu yako Lkn kuna siku hata moja umewahi kumuuliza shida ni nini maana, kiume ni kuangaliana usoni na kuuliza shida bila kuogopa kama ni Mwanaume kweli atanyoosha maelezo mtayamaliza lakini kama Hatonyoosha maelezo nakushauri achana naye tena usiendelee kumtatilia wala kutaka misaada kutoka kwake. Huenda akikuona unamfatilia sana na hayuko tayari kuyamaliza Ukaongeza tatizo baada ya kupunguza
 
Achana nae....mie ni dada yangu alikuwa hanikubali kabisaa ikawa inaniuma sana nilijaribu kuomba msamaha kwa kosa ambalo silijui ila yeye akawa hataki kabisa...mpaka tumekuwa watu wazima tuna watoto na kazi simtafutagi....simpigii simu....tukikutana nyumban ni salamu kila mtu anafanya mambo yake...sitak shobo...wala namba yake sina....tuko mkoa mmoja wala sijui anapokaa...tunakutana nyumban kwa matukio maalum ya kifamilia namsalimia kawaida kama hamna tatizo....nadeal na wanaonipa furaha basi inatosha

Kwenye ukoo hawajosekanagi aisee mtu hujui umemkosea nin ila anakuchukia vibaya
 
  • Thanks
Reactions: THT
Achana nae, nina huyo ndugu tena wa tumbo moja nae ana pigo hizo hizo nimetemana nae mwaka wa nne huu na tukikutana kila mtu na lake. Mtu kama hakutaki usilazimishe endelea na maisha yako.
 
Achana nae....mie ni dada yangu alikuwa hanikubali kabisaa ikawa inaniuma sana nilijaribu kuomba msamaha kwa kosa ambalo silijui ila yeye akawa hataki kabisa...mpaka tumekuwa watu wazima tuna watoto na kazi simtafutagi....simpigii simu....tukikutana nyumban ni salamu kila mtu anafanya mambo yake...sitak shobo...wala namba yake sina....tuko mkoa mmoja wala sijui anapokaa...tunakutana nyumban kwa matukio maalum ya kifamilia namsalimia kawaida kama hamna tatizo....nadeal na wanaonipa furaha basi inatosha
Ila Kama huna nmb zake bas mkeo anazo na pengine wanawasiliana Sana

Mm shemeji angu Sina nmb zake na Wala Hana zangu amemuoa dada angu sijui wanako ishi uko arusha
 
  • Thanks
Reactions: THT
Kwa sauti kubwa nasema,"ACHANA NAE" asilimia 90 ya wadau wamesema hivyo.
Angalia maisha yako ufanyaje yawe Bora. That's it
 
Kuna watu huwa tunatunza kumbukumbu hata za zaman,yawezakuwa zaman mkiwa wadogo uliwah mfanyia kitu kilichomkaa mpaka leo
Kweli kabisa, au kujibizana nae, kubisha kila akikutuma kitu, vitu hivi tulifanya kwa wakubwa zetu wakati wa utoto, japo si vizuri, wengine wanaweka kinyongo.
 
Mkuu mi sijaona tatizo lolote hapo acha kujiumiza akili kwasababu et kaka yako akusaidii kila mtu duniani anamaisha yake wewe kakayako kukusaidia au kutokusaidia hilo ni swala la hiari yake na kwenye haya maisha ishi kivyako.
Mimi ni wa mwisho kwetu tupo wa3 na wa2 ni kaka zangu wote mzee wao ni wanamaisha ya hatari bata South Africa bata Dubai kwao ni kawaida Sana kwenda kula bata mimi ndo nilimaliza chuo nina mwaka wa 3 saivi nipo napambana na maisha yangu sina time na mtu yoyote na hawajawah kuskia SIM zao zinaita namba yangu kwa shida yoyote mbaka kuna time wakajua kuwa nina weza kuishi bila wao na ndo wakaanzaga kunitafutaga wakinisalimia na kuniuliza kama nina shida yoyote nawajibu sina shida yoyote niko powa tu mambo yanaenda.
Sasa wewe unaanza kulalamika kuwa kakayako akusaidii heheheh utateseka Sana usipo badilika mkuu wewe kaza pambana mwenyew muonyeshe kuwa unauwezo wakushi bila yeye na ukaenjoy life Mungu ndo kila kitu kwenye haya maisha badilika kiongoz am telling you
 
Achna nae huyo, mchukulie kama sio ndugu yako... We unaona kabisa mtu anakuchukia bado unaendelea kujikomba komba mpaka kufungua thread? Jitambue kumbavu ww
Ukiwa kwenye situation hiyo huwezi kuignore, kwasababu ya maswali mengi, mtu a najiuliza kwani kuna nini ama amefanya nini hata ndugu yake hataki mazoea nae kabisa kabisa
 
huenda kuna jambo lilitokea huko nyuma mwenzako kabaki nalo mpaka sasa!

kaa naye chini, weka tofauti, umri na uwezo pembeni mtete!

ila jitayarishe kwa lolote! huenda kashuhudia kitu ama kaambiwa jambo na likawa la ukweli!

malizeni tofauti zenu! najua ni rahisi kusema kuliko kuyatenda, jaribu tu!
 
Ndo wapo hivyo ndugu zetu.Mimi ni miaka 6 sasa brother hatuwasiliani wala kuonana.Hata namba za simu sina za yule jamaa.Kila mtu afe kivyake ndo nimeamua hivyo
 
Back
Top Bottom