UNAONA UKIVURUGA MADA ,BASI WATU HAWATAUJUA UKWELI?
WANAFUNZI WA YESU
Na majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya; Wa kwanza Simon aliyeitwa Petro, na Andrea nduguye; Yakobo wa Zebadayo, na Yohana nduguye; Filipo, na Bartholomayo; Tomaso, na Mathayo mtoza ushuru; Yakobo wa Alfayo; na Thadayo; Simon Mkananayo, na Yuda Iskariote, naye ndiye mwenye kumsaliti. (Marko 10:2-4).
Kila mti hutambulika kwa matunda yake (Luka 6:44).
Basi tuone mti uliopandwa na Bwana Yesu Kristo, matunda yake ni ya ladha gani?
Madaraja yaliyofundishwa na Bwana Yesu tuone wanafunzi wake walikuwa wa aina gani?
Yesu alipoleta imani, basi tuone kiwango cha imani ya waaminio wake.
Sina kawaida ya kuwafundisha watu kwa maneno yangu bali nawafundisha kulingana na maandiko yao matakatifu.
Sasa tuone hali na imani ya wanafunzi wa Bwana Yesu.
1. Yesu alisema, hata sasa ninyi nanyi mngali hamna akili? (Mathayo15:16).
2. Alimwambia Petro kwamba; “Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka? (Mathayo 14:31).
3. Petro alikanusha kuwa mfuasi wa Yesu mara tatu bali alimlaani. (Mathayo 26:69-75).
4. Yuda Iskariote alimuuza Yesu kwa shilingi 30 tu. (Mathayo 26:15).
5. Wakati Yesu alikuwa hatarini, wanafunzi waliendelea kulala). Mathayo 26:40-45; Marko 14:36:041).
6. Yuda alijinyonga. (Mathayo 27:5).
7. Imani ya wanafunzi: “Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu” (Mathayo 17:20).
8. Ndipo wanafunzi wote wakamwacha wakakimbia. (Mathayo 26:50).
9. Wengi wataniambia siku ile; Bwana, Bwana hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri. Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu. (Mathayo 7:22-23).
Hapa juu mmesoma hali na imani ya wanafunzi wa Bwana Yesu sawa na Biblia.
Lakini sisi Waislamu hatuamini kwamba Nabii yeyote anaweza kushindwa kiasi hiki kwamba asiweze kupata matunda ya juhudi yake na athari nzuri isitokee kwa mahubiri na mafundisho yake.
Hata katika Qur'an Tukufu wanafunzi wa Bwana Yesu wametajwa kuwa mfano mzuri juu ya ulimi wa Bwana Yesu menyewe.
Qur'an: “Enyi mlioamini! Muwe wasaidizi wangu kwa Mwenyezi Mungu kama alivyosema Isa bin Mariam kuwaambia wanafunzi (wake):
Ni nani wasaidizi wangu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu? Wanafunzi wakasema: Sisi ni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu.” (Qur'an 61:15).