Kama Biblia ni kitabu cha kutungwa, nani alikitunga na chanzo na kusudio lake ni nini?

Kama Biblia ni kitabu cha kutungwa, nani alikitunga na chanzo na kusudio lake ni nini?

vitabu vya mungu na mitume waliopewa vitabu hivyo ni

Zaburi kwa daudi
Torati kwa mussa
Injili kwa issa
Qur an muhammad

Mnaposema biblia nacho ni kitabu cha muumba
inabidi pia mseme mtume aliepewa kitabu hicho ni mtume gani.
Wakikupa jibu,sijui,ngoja tuone.
 
Unapodai kuwa Tanzania haimo kwenye Biblia, je hiyo Tanzania ina historia ya miaka 700 iliyopita? Ilikuwaje?
Tanzania na Biblia ni vitu viwili tofauti.

Unaunganisha vitu viwili tofauti visivyo na uhusiano wowote kutaka kuunda hitimisho potofu.

Unafanya Logical non sequitur.

Biblia ni hekaya kama zilivyo hekaya za Abunuwasi, Esopo, kalume kenge na Alfu lela ulela.
 
Ungejiuliza kwanza kwa nini Allah huwa anasema "enyi watu wa KITABU " nadhani usingeendelea kusumbua watu humu
.
Siyo kinachoitwa biblia. Biblia yenyewe haijijui kama inaitwa biblia.
 
.
Siyo kinachoitwa biblia. Biblia yenyewe haijijui kama inaitwa biblia.
Kitu gani kinajijua kama kinaitwa Jina husika?

Yaani mlima Kilimanjaro unajijua kama unaitwa Kilimanjaro? Yaani kitabu kinajuaje kama kinaitwa Jina Fulani?
 
MIMI NIMESOMA BUBILIA MWANZO HADI UFUNUO.
IMEANDIKWA KWA UWEZO MKUBWA MNO.

HAKUNA BINADAMU WA KAWAIDA MWENYE UWEZO KUANDIKA KIASI KILE.
 
MIMI NIMESOMA BUBILIA MWANZO HADI UFUNUO.
IMEANDIKWA KWA UWEZO MKUBWA MNO.

HAKUNA BINADAMU WA KAWAIDA MWENYE UWEZO KUANDIKA KIASI KILE.
Ipo hoja kuwa imetungwa na wetu wenye uwezo wa juu sana wa kiakili wa zama hizo.
 
Biblia ni maandiko ya utamaduni na maisha ya watu hasahasa jamii ya waisraeli wa kale na nchi nyingi za mashariki ya kati.

Ndio maana kwenye Biblia hakuna Maisha ya waafrika watanzania, waafrika wakenya, waafrika waganda, waafrika wanyarwanda n.k

Maeneo mengi yaliyo tajwa kwenye Biblia ni maeneo ya Bara la Asia huko mashariki ya kati, Na baadhi ya maeneo machache ya Afrika yanayo pakana na nchi hizi, Na sehemu mbalimbali walizo tembelea wahusika wa kwenye Biblia,

kama palestina, Uturuki,Roma, na nchi nyinginezo

Waafrika pia walikuwa na vitabu vyao vya dini zao za kale na utamaduni wao

Lakini kupitia ujio wa wakoloni, Tamaduni nyingi na maandiko ya waafrika yalipotezwa.

Na waafrika waka anza kuaminishwa na kufundishwa dini(imani) na utamaduni wa wakoloni
(wazungu na waarabu) kupitia vitabu vyao hivyo (Biblia & Quran).
Naomba kuuliza kidogo, umesema biblia kwa wakristu na msaafu kwa waislamu, kwa waafrika kitabu chao kilipotea kama unavyodai kiliitwaje? Na hakuna hata masalia yaliyobakia hata kurasa mbili tatu zimepatikana scheme tukafanya kama refer ya hicho ulichokiandika kuhusu dining yetu ya kiafrika. Ahsante.
 
Naomba kuuliza kidogo, umesema biblia kwa wakristu na msaafu kwa waislamu, kwa waafrika kitabu chao kilipotea kama unavyodai kiliitwaje? Na hakuna hata masalia yaliyobakia hata kurasa mbili tatu zimepatikana scheme tukafanya kama refer ya hicho ulichokiandika kuhusu dining yetu ya kiafrika. Ahsante.
Waafrika kuna jamii nyingi.

Na kila jamii ina namna yake walivyokuwa wanamwabudu Mungu.

Kwa mfano Wamasai Mungu wao wanamwita Ngai na wana namna yao wanavyo muelezea Mungu wao.

Biblia na Quran ni maandiko ya kuletwa na wakoloni.

Yesu ni Mungu wa wazungu.

Na huyo Allah ni Mungu wa waarabu.

Waafrika tumeletewa tu hayo mavitabu yao.
 
Biblia ni maandiko ya utamaduni na maisha ya watu hasahasa jamii ya waisraeli wa kale na nchi nyingi za mashariki ya kati.

Ndio maana kwenye Biblia hakuna Maisha ya waafrika watanzania, waafrika wakenya, waafrika waganda, waafrika wanyarwanda n.k

Maeneo mengi yaliyo tajwa kwenye Biblia ni maeneo ya Bara la Asia huko mashariki ya kati, Na baadhi ya maeneo machache ya Afrika yanayo pakana na nchi hizi, Na sehemu mbalimbali walizo tembelea wahusika wa kwenye Biblia,

kama palestina, Uturuki,Roma, na nchi nyinginezo

Waafrika pia walikuwa na vitabu vyao vya dini zao za kale na utamaduni wao

Lakini kupitia ujio wa wakoloni, Tamaduni nyingi na maandiko ya waafrika yalipotezwa.

Na waafrika waka anza kuaminishwa na kufundishwa dini(imani) na utamaduni wa wakoloni
(wazungu na waarabu) kupitia vitabu vyao hivyo (Biblia & Quran).
 
Naomba kuuliza kidogo, umesema biblia kwa wakristu na msaafu kwa waislamu, kwa waafrika kitabu chao kilipotea kama unavyodai kiliitwaje? Na hakuna hata masalia yaliyobakia hata kurasa mbili tatu zimepatikana scheme tukafanya kama refer ya hicho ulichokiandika kuhusu dining yetu ya kiafrika. Ahsante.
 
biblia ni neno la mungu kabisa Mungu hajadiliwi utaona cha moto
Huyo Mungu aje hapa na huo moto wake tuonyeshane nani mbabe zaidi.

Huyo Mungu kama yupo ajitokeze hadharani mwenyewe kama ana huo uwezo.
 
Kuna dhana kwamba Biblia imejaa hadithi za kutungwa. Wasemaji wa utungaji huo wa hadithi za Biblia ni wale wapinzani wa yaliyomo hasa dhana na nadharia kwamba kuna MUNGU.

Lakini utungaji wa Biblia ulianza lini?

Hadithi za Biblia zilitungwa na kina nani na jee majina yao yanajulikana?

Watunzi Wa hadithi za kwenye Biblia walikuwa wangapi?

Hao watunzi walikuwa kutoka taifa Moja ama walitoka mataifa tofauti tofauti?

Walikubaliana wapi na vipi kuwa watunge hadithi hizo za Biblia na lengo lao lilikuwa lipi?

Jee walitumia vigezo gani kuchagua wahusika wa hizo hadithi zao na majina ya wahusika hao?

Ilichukua miaka mingapi hadithi hizo za Biblia kutungwa?

Baada ya utunzi wa hadithi hizo nani aliyetoa majina ya vitabu vinavyobeba hadithi hizo za kutungwa?

Baada ya wao kumaliza kutunga hizo hadithi Kuna watu wakati Wa zama zao waliowahi kutunga kitabu kingine kukanusha hizo hadithi zilizotungwa na hao watunzi wa hadithi za kwenye Biblia?
Ukijua uwezo wa akina James Hardley Chase ktk utumgaji basi huna cha kuuliza juu ya uwezo wa aliyetunga kitabu cha hadithi cha biblia ambapo main character ni yesu
 
vitabu vya mungu na mitume waliopewa vitabu hivyo ni

Zaburi kwa daudi
Torati kwa mussa
Injili kwa issa
Qur an muhammad

Mnaposema biblia nacho ni kitabu cha muumba
inabidi pia mseme mtume aliepewa kitabu hicho ni mtume gani.
Ujinga wenu ni mzigo kwenu
 
MIMI NIMESOMA BUBILIA MWANZO HADI UFUNUO.
IMEANDIKWA KWA UWEZO MKUBWA MNO.

HAKUNA BINADAMU WA KAWAIDA MWENYE UWEZO KUANDIKA KIASI KILE.
Ipo hoja kuwa imetungwa na wetu wenye uwezo wa juu sana wa kiakili wa zama hizo.
Uwezo upi wakuu?

Ukianza tu kusoma Bibilia unakutana na Hekaya za Nyoka kuongea na inamalizia na hekaya za dragon mwenye vichwa saba
 
Uwezo upi wakuu?

Ukianza tu kusoma Bibilia unakutana na Hekaya za Nyoka kuongea na inamalizia na hekaya za dragon mwenye vichwa saba
Ni kweli Biblia inaanza na habari za nyoka kuongea na siyo habari za uumbaji?

Wewe kuongea ni kupi? Unajua siku hizi Kuna kompyuta zinazoweza kutenda jambo kwa mtu kuziangalia tu?

Maana yangu njia za kuongea zipo nyingi tu si lazima iwe kwa kutamka maneno.
 
Hakuna kitabu Cha mungu kinachoitwa biblia vitabu vinavo julikana ni 4 na vilishushwa Kwa kila zama
1.Zaburi
2.Torati
3.Injili
4.Quran
Endeleeni kufata wazungu na warabu mkija kujua ukweli wa dunia inavoeenda mmechelewa
Huyu jamaa ni either muongo au hajui alichokiandika.
Sitaki nikuchoshe na Doctrine of scriptures ila nitakupa kipande kidogo kusaidia uelewa wako.

Kwa Nini Biblia Inaweza Kuaminika?
1. Uhalisia wa Kihistoria – Matukio, maeneo, na watu waliotajwa katika Biblia yamethibitishwa na uchunguzi wa akiolojia na kumbukumbu za kihistoria. Mfano ni kuwepo kwa Mfalme Daudi, Uhamisho wa Babeli, na jamii ya Wahiti.

2. Ushahidi wa Hati za Kale – Biblia ina nakala nyingi zaidi za kale kuliko kitabu kingine chochote cha kihistoria. Agano Jipya lina zaidi ya manuskripti 5,800 za Kigiriki, zingine zikiwa zimeandikwa miongo michache tu baada ya matukio, kuhakikisha uhifadhi wake sahihi.

3. Utimilifu wa Unabii – Manabii wa Agano la Kale walitabiri matukio mengi yaliyotimia katika Agano Jipya, hasa kuhusu Yesu Kristo (mfano: Isaya 53, Zaburi 22, Mika 5:2). Hii inaashiria maarifa ya kimungu kabla ya wakati.

4. Uthabiti kwa Muda Mrefu – Licha ya kuandikwa na waandishi zaidi ya 40 katika kipindi cha miaka 1,500, kutoka sehemu na tamaduni tofauti, Biblia ina ujumbe mmoja thabiti kuhusu Mungu, wanadamu, dhambi, na wokovu.

5. Maarifa ya Kisayansi na Maadili – Ingawa si kitabu cha sayansi, Biblia ina ukweli unaolingana na ugunduzi wa kisasa (mfano: umbo la mviringo la dunia katika Isaya 40:22). Pia, mafundisho yake ya maadili yameathiri sheria na maadili duniani kwa karne nyingi.

6. Maisha Kubadilika – Mamilioni ya watu katika historia wanashuhudia kuwa maisha yao yamebadilika kupitia ujumbe wa Biblia, jambo linaloonyesha nguvu na ukweli wake.

Ushahidi wa Kihistoria wa Biblia
1. Ustaarabu wa Wahiti – Wakosoaji kama wewe waliwahi kutilia shaka kutajwa kwa Wahiti katika Biblia (Mwanzo 15:20, 2 Wafalme 7:6), wakidai hawakuwahi kuwepo. Hata hivyo, mwishoni mwa karne ya 19 na mwanzoni mwa karne ya 20, wanakiolojia waligundua mabaki ya Wahiti na maandiko yao nchini Uturuki, yakithibitisha uwepo wao kihistoria.

2. Maandishi ya Tel Dan (Nyumba ya Daudi) – Mwaka 1993, wanakiolojia waligundua maandiko ya kale kaskazini mwa Israeli yanayotaja "Nyumba ya Daudi" na "Mfalme wa Israeli". Ugunduzi huu unathibitisha kuwa Daudi alikuwa mtu wa kihistoria, kinyume na madai ya awali kwamba alikuwa tu hadithi ya Biblia.

3. Magombo ya Bahari ya Chumvi (1947–1956) – Magombo haya, yaliyopatikana Qumran, ni miongoni mwa nakala za zamani zaidi za vitabu vya Agano la Kale, zinazorudi nyuma zaidi ya miaka 2,000. Magombo haya yanaonyesha kuwa maandiko ya Biblia yamehifadhiwa kwa usahihi wa hali ya juu kwa muda mrefu.

4. Birika la Bethzatha na Siloamu (Yohana 5:1-9, Yohana 9:1-7) – Wengine walitilia shaka uwepo wa mabirika haya yaliyotajwa katika Injili ya Yohana. Hata hivyo, baadaye mabirika yote mawili yamegunduliwa Yerusalemu, kuthibitisha kuwa maandiko ya Yohana yalihusu maeneo halisi.

5. Maandishi ya Pontio Pilato – Juzi juzi tu hapa Mwaka 1961, maandiko ya kale kwenye jiwe yaligunduliwa huko Caesarea Maritima, yakitaja jina la Pontio Pilato, gavana wa Kirumi aliyemhukumu Yesu kifo. Ugunduzi huu unathibitisha uwepo wake kihistoria, kama inavyosimuliwa katika Injili.

Ushahidi wa Unabii wa Biblia
1. Anguko la Tiro (Ezekieli 26:3-14)
Takriban mwaka 590 KK, Ezekieli alitabiri kuwa mji wa Tiro ungeangamizwa, magofu yake yangesukumwa baharini, na wavuvi wangetandaza nyavu zao hapo.
Utimilifu: Mwaka 332 KK, Aleksanda Mkuu aliteka Tiro. Aliamuru magofu yake yasukumwe baharini kujenga njia ya ardhini, na leo wavuvi hutandaza nyavu zao juu ya mabaki hayo.

2. Uharibifu wa Babeli (Isaya 13:19-22, Yeremia 51:26, 43)
Biblia ilitabiri kuwa Babeli ingeharibiwa na isingejengwa tena.
Utimilifu: Ingawa Babeli ilikuwa ufalme mkubwa, ilianguka na haijajengwa tena. Hata Saddam Hussein alipojaribu kuijenga upya, alishindwa.

3. Ujenzi wa Yerusalemu na Kuja kwa Masihi (Danieli 9:24-26)
Danieli alitabiri muda halisi wa kuja kwa Masihi baada ya Yerusalemu kujengwa upya.
Utimilifu: Yesu alikuja ndani ya kipindi kilichotabiriwa (takriban miaka 483 baada ya agizo la kujenga Yerusalemu, lililotolewa mwaka 457 KK).

4. Kuzaliwa kwa Yesu Bethlehemu (Mika 5:2)
Mika, akiandika karibu mwaka 700 KK, alitabiri kuwa Masihi angezaliwa Bethlehemu.
Utimilifu: Yesu alizaliwa Bethlehemu (Mathayo 2:1-6), ingawa familia yake ilitoka Nazareti.

5. Kusulubiwa kwa Yesu Kulitabiriwa (Zaburi 22, Isaya 53)
Zaburi 22 inaeleza kwa kina mateso ya msalabani: "Wamenitoboa mikono na miguu yangu" (Zaburi 22:16), ingawa wakati huo kusulubiwa hakukuwa kumevumbuliwa bado.
Isaya 53 inazungumzia "mtumishi wa mateso" ambaye angekufa kwa ajili ya dhambi za watu wengine, azikwe, na baadaye afufuke.
Utimilifu: Yesu alisulubiwa na kufufuka, kutimiza unabii huu kwa usahihi.
 
Back
Top Bottom