Kama chanzo cha uhai kinaweza kubadilika basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti hadi sasa. Je, ni upi msingi wa uhai?

Kama chanzo cha uhai kinaweza kubadilika basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti hadi sasa. Je, ni upi msingi wa uhai?

ulimwengu wa roho ni mpana sana na una mambo mengi sana
na haya yote yanayoendelea hapa duniani yote yanatoka huko
Sasa Inategemea na wewe unaleta nini huku
Na hiv vitabu vya kiimani vinatusaidia na vinatupa msingi wa kujua yaliyoko huko
Tuendelee kutafakari
Uko sahihi mkuu
 
Hoja kwamba muda si kitu halisi kwa sababu ya nadharia ya Uhusiano wa Einstein na hiyo Relativity theory yake pamoja na fizikia ya Quantum kwa maana ya Quantum Mechanics, ni sahihi kwa muktadha wa kisayansi, kwamba ni kweli mwanga unasafiri bila kufuata mtiririko wa muda kwa mtazamo wake, na ni kweli pia kuwa sababu na matokeo yaani cause and effect hayafuati utaratibu wa kawaida katika kiwango cha quantum.

Lakini nikuulize mkuu, je, hii hoja yako inamaanisha kwamba muda haupo kabisa kwa hali zote?

Kwasababu tukiangalia katika uhalisia wa kila siku, muda ni jambo lenye athari kwa wanadamu, na ndio maana ulivyokua miaka 20 iliyopita sivyo ulivyo leo, na hii inamaanisha kutokea kuzaliwa, hadi kuzeeka na hadi kufa ni kwamba muda umetumika, kwasababu wewe na Mimi wote ni mashahidi ya kwamba mabadiliko haya yote yana mwelekeo fulani kwa maana ya kwamba haubaki kama ulivyo (ndio maana mtoto huanza kuzalia, anajifunza kukaa chini, anatambaa, kisha kusimama na kutembea, hivi vyote hutokea baada ya muda fulani).

Kwahiyo ingawa nadharia za kisayansi zinaonyesha kuwa muda ni wa mlinganisho kwa maana ya relative, lakini hii haiwezi kuwa sababu ya kutufanya tuukane kabisa katika maisha yetu ya kawaida, hivyo basi, kwakua chanzo ni kitu kinachotegemea sana muda na uhusiano huo wa kisababishi basi si sahihi kusema eti chanzo ni kitu ambacho hakipo kabisa.

Na hapa wacha niseme hivi, ya kwamba chanzo kinaweza kuwa hakipo katika uhalisia wa juu kabisa kwa maana ya ultimate reality, lakini ni kitu ambacho kipo katika uhalisia wetu wa kawaida kwa maana ya practical reality na sidhani kama unapingana na hii hoja.

Ila kama hiyo haitoshi, basi chukulia mfano huu, tunaposema "mimi ni chanzo cha furaha yako," hatumaanishi kwamba hakuna hali nyingine inayoweza kuleta furaha ila tunamaanisha kuwa katika mazingira fulani, uhusiano wa kisababishi upo, na ndio maana chanzo kina maana katika muktadha huo lakini chanzo hiki kinaweza kubadilika baadae (naongelea juu ya muda kaka).

Na kama wewe bado utaendelea kupinga chanzo kwa misingi ya nadharia ya uhusiano au Quantum Mechanics, basi pia unapaswa kukana dhana ya maisha ya kila siku, pamoja na effect zake (na sidhani kama unaweza kufanya hivyo).

Kwa hiyo, badala ya kukana kabisa uwepo wa chanzo, ni bora tukubali kwamba ni dhana inayotegemea muktadha, iwe ni katika maisha ya kila siku, falsafa, au imani za kidini, kwahiyo rudi katika mada na tuendelee kujadili chanzo cha uhai ni nini katika muktadha ambao andiko limelenga.

Tusijibane kwenye kaeneo fulani kadogo na kujinyima uwanda mpana wa Kutafakari juu ya mambo fulani fulani, embu tujipe uhuru wa Kutafakari kwanza halafu tuone tunaweza kufikia wapi.
Sijasema muda haupo, nimesema muda si kitu cha msingi, si kitu fundamental, ni derivative, ni kitu kinachotokana na kitu kingine.

Muda ni kama kivuli ambacho hakiwezi kimuwepo bila ya kuwepo mwanga na kitu cha kuukinga huo mwanga.

Na kitu kisipokuwa fundamental, kikiwa derivative tu, inakuwa si lazima kiwepo.

Kama wewe ni lazima uzaliwe na mama yako ili uwepo, mama yako asipokuwepo hivyo na wewe huwezi kuwepo.

Ndiyo maana unaweza kuwa na mwanga ukakosa kitu cha kuukinga huo mwanga usiwe na kivuli.

Unapoongelea chanzo, kwa maana halisi, unaongelea kitu absolute, kitu fundamental.

Sasa utakuwaje na chanzo absolute na fundamental, ambacho kinategemea muda, kinategemea cause and effect, ambayo inakuwepo kutokana na muda, wakati muda wenyewe si absolute ni relative?

Unawezaje kushona nguo ya bluu wakati kitambaa chako cha kushonea nguo ni chekundu na hakibadiliki rangi?
 
Kwa nini unadhani kila kitu lazima kiwe na msingi?

Kwa nini unadhani uhai una msingi?

Kwa nini hudhani kwamba uhai unaweza kuwepo bila msingi?

Kama uhai lazima uwe na msingi, Je msingi wa "msingi wa uhai" ni nini?
Sidhani kama lazima Kila kitu kiwe na msingi ila nadhani ya kwamba Kila chenye chanzo lazima kiwe na msingi.

Ndio maana hoja ya andiko imejengwa juu ya neno "Mungu ni chanzo cha uhai", na ndio nikaanzia hapo kuelezea.

Na kutokana na hilo na kwakuzingatia muktadha huo pia inamaana kama chanzo cha uhai ni Mungu basi uhai utakua uko na msingi wake ambao Mimi na wewe bado hatujaujua.

Na msingi ni mwanzo wa chanzo.

Lete maneno mkuu...
 
Hebu fikiria mambo ambayo watu wanayafanyanya hapa duniani
haya mambo ya Sayansi ,katika nyanja mbalimbali
Mambo makubwa ya kushangaza
na kila mvumbuzi anashangazwa na uvumbuzi wa mwingine
kwa hiyo kumbe watu wanavumbua vitu villivyo fichika,wapi kwenye fiikra

na fikra hazionekani kwa macho haya ya damu na nyama
kwa hiyo lazima kuna chanzo ambako watu wanatoa haya mambo

huko kwenye nguvu ya asili,ulimwengu wa roho(fikra) au ufahamu unaoishi
 
Kama msingi ndio huunda vyanzo mbalimbali, Je msingi unaanza tu from nowhere?
Hili swali unaweza kujijibu labda kwa kuanza Kutafakari na kujiuliza maswali ya hapa na pale kwa mfano msingi wa nyumba unayokaa msingi wake ni nini?😅😅😅.

Ajali ambayo ilitokea na kuua watu ni msingi na hutengeza vyanzo mbalimbali vya habari, je, msingi wa ajali hiyo ni nini?😅😅😅

Wacha kwanza tutrace back kutoka kwenye chanzo hadi kwenye msingi halafu tukifika hapo kwenye msingi tutarudi tena ubaoni tuone kama msingi unaweza kuwa na msingi
 
Sidhani kama lazima Kila kitu kiwe na msingi ila nadhani ya kwamba Kila chenye chanzo lazima kiwe na msingi.
Kama si lazima kila kitu kiwe na msingi, Basi uhai na wenyewe hauna msingi.
Ndio maana hoja ya andiko imejengwa juu ya neno "Mungu ni chanzo cha uhai", na ndio nikaanzia hapo kuelezea.
Kwanza Mungu hayupo.

Na kama Mungu hayupo, Basi uhai chanzo chake sio Mungu.
Na kutokana na hilo na kwakuzingatia muktadha huo pia inamaana kama chanzo cha uhai ni Mungu basi uhai utakua uko na msingi wake ambao Mimi na wewe bado hatujaujua.
Chanzo cha uhai sio Mungu.

Chanzo cha uhai ni viumbe hai.

Pasipo viumbe hai hakuna uhai.
Na msingi ni mwanzo wa chanzo.
Kama msingi ni mwanzo wa chanzo, Je huo msingi ulitokea tu wenyewe?
Lete maneno mkuu...
 
Hujajibu direct, Nimeuliza nishati ni intelligent being maana ina uwezo wa ku transfer taarifa na kuzihifadhi kwa code kiasi ambacho haziwezi kuwa modified easily,.yaani What naturalistic process explains the origin of this information, given that information is not a property of matter or energy but requires an intelligent source?......unaongea simple lakini uhalisia ni complex zaidi,.. ngoja nisiende deep maana hutokua na majibu ya maswali husika.
Intelligent how ? Ninavyoongelea Nishati ninamaanisha ni kama wewe unavyojaza mafuta kwenye gari lako mafuta ndio baada ya ile spark kubadilisha form na kuwa gasi ni Nguvu kubwa sana inatokea ili iweze kuendesha Piston..., sasa tukija kwenye information ukienda at a deeper level wala sio ngumu ni kama unatoa photocopy ukichukua nakala moja unazalisha nyingine kama ulikuwa unakula mihogo kwa bahati mbaya ukachafua lile karatasi basi huenda kuanzia muda huo kukawa na nakala zenye alama ya dole gumba lako....
Ila si unajua kwamba Dunia nzima tunaweza kukubaliana kwamba jambo fulani ni fact lakini kumbe kiuhalisia wote tupo wrong?
Kukubaliana wote huenda ikawa ngumu na hata tukikubaliana haimaanishi the underlying truth inabadilika (Argumentum Ad Populum) ; Na hapo ndio Sayansi comes into it's own hata wewe mmoja leo ukija na ukatwambia kwamba tulikuwa tumekosea sababu ya A, B, C basi wote tutakuunga mkono; Tufauti na Imani itabadilisha premise nzima na kukwambia kwamba you were right all along ni basi tu ulishindwa kuelewa maelezo yako mwenyewe...
Yaani kimsingi ni kwamba baada ya kudadisi tunafikia hitimisho at a certain point in time na kuona kwamba tumefikia ukweli even though hicho tunachoita ukweli sio ukweli halisia!
It a journey and we seeker of knowledge hatufiki bali tunaendelea na mpaka sasa tuna known knowns, known unknowns na unknown unknowns... And the journey continues until the day we stop breathing ambapo watakuja wengine watakaoona further sababu ya kusimama kwenye Shoulders za Giants of the Past....
 
Hili swali unaweza kujijibu labda kwa kuanza Kutafakari na kujiuliza maswali ya hapa na pale kwa mfano msingi wa nyumba unayokaa msingi wake ni nini?😅😅😅.
Msingi wake ni ardhi ambapo nyumba imejengwa juu yake.

Bila ardhi huwezi kujenga nyumba.
Ajali ambayo ilitokea na kuua watu ni msingi na hutengeza vyanzo mbalimbali vya habari, je, msingi wa ajali hiyo ni nini?😅😅😅
Kwanza hakuna msingi wa ajali.

Kuna vyanzo mbalimbali vinavyoweza kusababisha ajali.

Hakuna msingi wa ajali.

Ndio maana nilikuuliza mwanzoni, Je unadhani kila kitu lazima kiwe na msingi?

Ukajibu "Sidhani".

Hivyo uhai hauna msingi.

Pia ajali haina msingi.
Wacha kwanza tutrace back kutoka kwenye chanzo hadi kwenye msingi halafu tukifika hapo kwenye msingi tutarudi tena ubaoni tuone kama msingi unaweza kuwa na msingi
Hakuna msingi wa kila kitu.

Kuna vyanzo mbalimbali vya kitu.

Una elewa hilo?
 
Bila shaka mko salama waungwana...

Kikawaida neno msingi na chanzo ni maneno mawili ambayo ukiangalia kwa jicho la kawaida ni kama yanafanana hivi lakini ni maneno yaliyo na utofauti mkubwa.

Kwa maana chanzo huwa kinatengeneza muendelezo usio na ukomo lakini msingi huwa unatengeneza muendelezo mgumu ambao huwa haueleweki pasipo kurudi tena kwenye msingi kwa maana nyingine ni kwamba msingi ndio unaounda vyanzo mbalimbali.

Ndio maana mkusanyiko wa vyanzo vingi vya habari fulani unaweza kuleta mkanganyiko wa mambo hasa inapotokea vyanzo vyote vinaongelea habari moja ila vinatofautiana katika taarifa zao, hii hufanya mtu ashindwe kuelewa aamini chanzo kipi kati ya hivyo, na ili kuondoa huu mkanganyiko basi mtu hupaswa arudi kwenye msingi wa habari yenyewe na baada ya kufanya hivyo basi ni rahisi kujua kati ya vyanzo hivyo ni kipi na kipi kimeandika habari kwa kuzingatia msingi wake.

Kwahiyo kuna nyakati neno chanzo hutumika zaidi kwenye mambo ambayo msingi wake haujulikani au uhakika wa moja kwa moja juu ya msingi wake haupo lakini msingi ndio ambao unabeba chanzo.

Lakini pia chanzo wakati fulani huwa kinakua na mbadala wake wakati msingi huwa hauna mbadala (ndio maana habari unaweza kuipata jamiiforum, milard ayo na media zingine ila msingi wa habari hiyo hauwezi kubadilika).

Kwamfano wewe ni chanzo cha watoto wako kuzaliwa na wao ni chanzo cha wajukuu zako kuzaliwa lakini pia wajukuu zako ni chanzo cha vitukuu kuzaliwa na hii itaendelea namna hii bila ukomo na wewe hujawa msingi kwasababu nyuma yako alikuwepo baba yako ambae alikua chanzo cha wewe kuzaliwa ila pia Kabla ya baba yako alikuwepo babu yako ambae yeye alikua chanzo cha baba yako kuzaliwa na hii itarudi nyuma katika umbali usio julikana na ndio maana tumetumia neno chanzo.

Lakini pia mtu ni roho, na kama hii ndio basi hizo roho ambazo wewe umezileta hapa duniani haimaanishi kwamba wewe ndio mtu pekee ambae unao uwezo wa kuleta roho hizo isipokua wewe uliwin tu kwenye ile probability ila usingezileta wewe basi angekuwepo mtu mwingine ambae angeweza kuzileta, na vivyo hivyo wewe kwa baba yako na baba yako kwa babu yako na kadhalika.

Kwahiyo neno chanzo linapotumika katika eneo lolote ujue tayari kuna hali isiyo na ukomo imetengenezwa kwa kwenda mbele au kwa kurudi nyuma kwa maana ule msingi kamili wa jambo hilo haujulikani au kuna namna mbadala ya jambo hilo kwenye kutokea kwake au kufanyika kwake ukiachana na namna hiyo ambayo imetumika.

Okay, wacha twende mbali kidogo, watu husema Mungu ni chanzo cha uhai, hii tayari ni sentensi ambayo haina ukomo, kwa kurudi nyuma au kwenda mbele, lakini pia kwa kusema hivi unamaanisha asingekua yeye basi chanzo cha uhai kingeweza kupatikana kwa namna nyingine.

Angalia hii, wewe ni chanzo cha mkeo kuolewa au tuseme ni chanzo cha ndoa yenu ila sio msingi wa hiyo ndoa kwa maana hata kama wewe usingemuoa basi angeweza kuolewa na mtu mwingine, na huyo mtu mwingine nae angekua tu chanzo ila wala sio msingi kwa maana huyo mtu mwingine asingemuoa basi angeolewa na mtu mwingine tena, kwahiyo hii unaona inakua ni infinity loop.

Kwahiyo kama Mungu ni chanzo cha uhai basi msingi wa uhai bado haujulikani na ukomo wa uhai huo huo haujulikani pia (naomba usome ukiwa katika utulivu wa akili ili unielewe vizuri hapa).

Hii inamaanisha nini? Hii inamaanisha kwamba ni eidha Mungu ni neno moja linalotumika kuwakilisha jamii ya viumbe fulani kama vile neno binadamu linavyotumika kutuwakilisha Mimi na wewe au ukiachana na Mungu basi kuna viumbe vingine venye uwezo wa kutoa uhai (wacha tusonge taratibu huku tukiongeza tafakuri juu ya tafakuri hapa).

Kama Mungu ni kiwakilishi cha jamii ya viumbe fulani kama lilivyo neno binadamu basi neno la tumfanye mtu kwa mfano wetu halitakua na maana yoyote iliyojificha zaidi ya lilivyo na limekuwepo pale kama uthibitisho wa kwamba Mungu ni neno la jumla linalowakilisha jamii fulani kama ilivyo kwa neno binadamu.

Na kwa uthibitisho zaidi wa jambo hili ni pale Mungu anaposema aabudiwe yeye na wala sio miungu mingine, hii inamaana anajua ya kwamba katika jamii ya kimungu hayupo peke yake.

Ni sawa na wewe utengeneze robot lako ikiwa wewe ndio mkuu wa mradi licha ya kwamba ndani yake kutakua na ma-engineer wengine ambao ni binadamu na ghafla ukaanza kuona yule robot anaanza kuwatii watu wengine kuliko wewe mkuu wa kitengo lazima urudi umwambie unaefaa kunyenyekewa ni wewe na wala sio binadamu wengine.

Kama hiyo haitoshi lakini pia kuna maeneo kadhaa Mungu alijitokeza kwa kujitambulisha ya kwamba yeye ni Mungu wa vita mara Mungu wa maarifa na kadhalika, hii sio bahati mbaya na wala huna haja ya kuilazimisha ikae kwa namna tofauti na hiyo kwa maana hivyo ndivyo ilivyo na hii inaweza kuthibitisha kwamba Mungu ni sawa na kusema binadamu (yote ni maneno yanayowakilisha jamii ya viumbe fulani).

Na kwa hoja hiyo sasa, ndio maana ukisema Mungu ni chanzo cha uhai inamaana si Mungu wote ambao walishiriki kwenye mradi wa kumpa uhai binadamu ila ni jopo tu la Mungu kadhaa ndio ambao walifanya hii project na ndio maana neno chanzo limetumika kwa maana ya kwamba kama hao waliokaa wasingekaa basi Mungu wengine wangeweza kukaa na kumpa uhai binadamu kama wangeamua kufanya hivyo.

Lakini kama tukiendelea kubaki na msimamo wetu wa kwamba Mungu ni mmoja na wala sio jamii ya viumbe fulani basi hapa tunaweza kuibua hoja mpya ya kwamba kumbe ukiachana na Mungu katika puzzle hii pia kunao uwezekano wa kuwepo jamii fulani ya viumbe wenye uwezo wa kutengeneza watu au kumpa mtu uhai, na kama kweli chanzo cha uhai kinaweza kubadilika kinamna hii basi uhai wenyewe hauna msingi thabiti.

Na hii ndio sababu ya neno chanzo kutumika badala ya neno msingi.

Najua kuna mtu hapa anaweza asielewe ila kama unataka uelewe zaidi unaweza Kutafakari kwa kina juu ya neno chanzo na msingi kisha ukishapata point urudi usome tena hili andiko.

Kwa mfano huwa tunasema chanzo cha mapato wala sio msingi wa mapato kwa maana kuna njia nyingi ambazo mtu anaweza akazitumia ili zimuingizie mapato.

Chanzo cha furaha yangu ni wewe, kwa maana usipokua wewe basi anaweza akawa mtu mwingine ambae anaweza akanipa hii furaha unayo nipa kwakua duniani binadamu haupo peke yako.

Chanzo cha Mimi kupata kazi ni wewe, hii inamaanisha hata usingekua wewe ningepata kazi kwa maana nisingekutana na wewe basi ningekutana na mtu mwingine ambae angekuwa chanzo kama ambavyo wewe umekua(kwa maana wewe si mtu wa kwanza na wa mwisho kuwa na connection au roho ya upendo wa namna hii).

Tengeneza msingi wa maisha yako, kwasababu wewe pekee ndio mwenye uwezo wa kutengeneza maisha yako na wala hakuna mbadala wa wewe.

Kwahiyo ukisoma kwa umakini na Kutafakari hapa, utagundua ya kwamba ndani ya chanzo kuna msingi, na msingi mmoja unaweza ukatengeneza vyanzo mbalimbali (usichanganyikiwe sasa na wewe, ili uelewe hapo rudi mwanzo mwa andiko nilikwambia msingi ndio hutengeza complex things na ili uweze kuondoa ucomplex ni lazima uanze kuyagawa mambo hayo kwenye namna fulani rahisi ili uufikie msingi wake).

Ndio maana mtu akifariki huwa wale watu wanaomfahamu wanapopata taarifa huwa wanauliza chanzo cha kifo chake ni nini, kwa maana wanajua kifo kinaweza kusababishwa na mambo mengi ya msingi ambayo ndio huweza kuunda chanzo.

Kwahiyo kama haujui msingi wa jambo fulani huwezi kusolve puzzle yake, na hapa duniani mambo mengi yapo kwenye puzzle na puzzle ni muunganiko wa mambo mbalimbali ya msingi na ili uweze kusolve puzzle nyingi za kilimwengu lazima uuelewe vizuri msingi wake ni nini.

So, kama Mungu ndio chanzo cha uhai basi hii tayari inakua ni complex puzzle kwa maana iko na vyanzo vingi hadi kufikia ule msingi wake na ili tuweze kuisolve lazima tuujue msingi wake ni upi.

Je, msingi wa uhai ni nini?

NITARUDI.
Mungu ni mwanzo na mwisho sio Chanzo Halisi.

Kuna tofauti kubwa kati ya mwanzo na Chanzo au kwa kingereza genesis na Source.Unaposema Mungu unamaanisha mwanzo na mwisho au alfa na omega.

But unaposema Chanzo unamaanisha umilele (eternity) hana mwanzo wala mwisho.
 
Sijasema muda haupo, nimesema muda si kitu cha msingi, si kitu fundamental, ni derivative, ni kitu kinachotokana na kitu kingine.

Muda ni kama kivuli ambacho hakiwezi kimuwepo bila ya kuwepo mwanga na kitu cha kuukinga huo mwanga.

Na kitu kisipokuwa fundamental, kikiwa derivative tu, inakuwa si lazima kiwepo.

Kama wewe ni lazima uzaliwe na mama yako ili uwepo, mama yako asipokuwepo hivyo na wewe huwezi kuwepo.

Ndiyo maana unaweza kuwa na mwanga ukakosa kitu cha kuukinga huo mwanga usiwe na kivuli.

Unapoongelea chanzo, kwa maana halisi, unaongelea kitu absolute, kitu fundamental.

Sasa utakuwaje na chanzo absolute na fundamental, ambacho kinategemea muda, kinategemea cause and effect, ambayo inakuwepo kutokana na muda, wakati muda wenyewe si absolute ni relative?

Unawezaje kushona nguo ya bluu wakati kitambaa chako cha kushonea nguo ni chekundu na hakibadiliki rangi?
Ni kweli ya kwamba muda kulingana na fizikia, si kitu fundamental bali ni derivative kwa maana unatokana na mwingiliano wa mwanga, nafasi, na blah blah nyingine, lakini mkuu hii haiwezi kupingana na hoja ya kwamba si kila kitu kinachotokana na kitu kingine basi lazima kiwe cha kipuuzi au hakina umuhimu kabisa.

Kwa mfano hapo umesema kivuli hakiwezi kuwepo bila mwanga na kitu cha kuukinga mwanga, lakini je, hiyo inamaanisha kivuli hakina maana?

Kwasababu hatuwezi kupima mwanga bila kuwepo kivuli kwenye baadhi ya hali na ili uweze kuthibitisha hili basi unaweza kurejea ile dhana ya event horizon kwenye black holes.

Kwahiyo inawezekana ni kweli muda si fundamental, lakini kama unaleta uhalisia wa vitu vinavyotokea, sasa kwanini tusiuweke kuwa sehemu ya dhana ya chanzo?.

Kwa maana nadhani Dunia iko na dhana nyingi zisizo fundamental na zinaathiri ulimwengu kwa namna ambayo inafanya ziwe (ingawa naweza kukosa mifano yake kwa sasa ila kama tukishirikiana Mimi na wewe tunaweza kukubalina juu ya hili).

Kwahiyo basi katika hoja yako ya kusema chanzo kwa maana halisi ni kitu absolute na fundamental, kwa maana ya kwamba huwezi kuwa na chanzo kinachotegemea muda kwa sababu muda si absolute.

Nami naomba nikuulize swali hapo hapo, Je, kila chanzo lazima kiwe absolute?(Na kama ndivyo basi naomba unieleweshe kwa kina hapa).

Kwasababu ukiangalia sana hoja yako mkuu, imebezi kwenye absolute truth kuliko relative, na kama huko ndiko ulikojikita basi hapa duniani yapaswa kila kitu kingine kinachotegemea chanzo cha kitu fulani kiwe derivative ya kitu hiko, lakini sasa katika mfumo wa maisha ya kawaida na hata kwenye sayansi nadhani, kikawaida huwa tunaweza kuwa na vyanzo vya mlinganisho kwa maana ya relative sources, ambavyo huwa vina maana ndani ya muktadha fulani (hii nayo unaizungumziaje mkuu).

Lakini pia niseme tu, ya kwamba nimeupenda mfano wako wa kushona nguo ya bluu kwa kutumia kitambaa chekundu, lakini vipi kama tunaweza kupaka kitambaa hicho rangi ya bluu? 😅😅

Mimi sio mtaalam sana wa mambo ya quantum (ila kuanzia sasa nitajikita zaidi huko kwa maana inawezekana baadhi ya puzzle zinasolvika kirahisi huko), ila naelewa jambo moja ya kwamba katika ulimwengu wa quantum, kuna mifano mingi inayoelezea kitu kuweza kuwa na hali mbili tofauti kwa wakati mmoja.

Kwa hiyo, kutokana na hilo basi swali lako liko na dhana ya ukweli wa moja kwa moja, iilhali ukweli mara nyingi huwa ni wa mlinganisho kulingana na muktadha.
 
Chanzo cha uhai ni viumbe hai.
Nadhani hapa umeleta kitu kingine tena, na hii ni puzzle pia, na kama usemavyo ni kweli ya kwamba chanzo cha uhai ni viumbe hai basi bado msingi wa uhai haujulikani.
 
Mungu ni mwanzo na mwisho sio Chanzo Halisi.

Kuna tofauti kubwa kati ya mwanzo na Chanzo au kwa kingereza genesis na Source.Unaposema Mungu unamaanisha mwanzo na mwisho au alfa na omega.

But unaposema Chanzo unamaanisha umilele (eternity) hana mwanzo wala mwisho.
Najua kuna utofauti kati ya chanzo na mwanzo lakini pia unaposema ninaposema chanzo inamaanisha kutokua na mwanzo wala mwisho hii inamaanisha ni infinity loop na ndio kitu ambacho kimefanya nilete hili andiko kwa maana nyingine si kwamba msingi wake haupo ila ni loop yenye mlolongo mrefu hadi kufikia msingi wake.
 
Ni kweli ya kwamba muda kulingana na fizikia, si kitu fundamental bali ni derivative kwa maana unatokana na mwingiliano wa mwanga, nafasi, na blah blah nyingine, lakini mkuu hii haiwezi kupingana na hoja ya kwamba si kila kitu kinachotokana na kitu kingine basi lazima kiwe cha kipuuzi au hakina umuhimu kabisa.

Kwa mfano hapo umesema kivuli hakiwezi kuwepo bila mwanga na kitu cha kuukinga mwanga, lakini je, hiyo inamaanisha kivuli hakina maana?

Kwasababu hatuwezi kupima mwanga bila kuwepo kivuli kwenye baadhi ya hali na ili uweze kuthibitisha hili basi unaweza kurejea ile dhana ya event horizon kwenye black holes.

Kwahiyo inawezekana ni kweli muda si fundamental, lakini kama unaleta uhalisia wa vitu vinavyotokea, sasa kwanini tusiuweke kuwa sehemu ya dhana ya chanzo?.

Kwa maana nadhani Dunia iko na dhana nyingi zisizo fundamental na zinaathiri ulimwengu kwa namna ambayo inafanya ziwe (ingawa naweza kukosa mifano yake kwa sasa ila kama tukishirikiana Mimi na wewe tunaweza kukubalina juu ya hili).

Kwahiyo basi katika hoja yako ya kusema chanzo kwa maana halisi ni kitu absolute na fundamental, kwa maana ya kwamba huwezi kuwa na chanzo kinachotegemea muda kwa sababu muda si absolute.

Nami naomba nikuulize swali hapo hapo, Je, kila chanzo lazima kiwe absolute?(Na kama ndivyo basi naomba unieleweshe kwa kina hapa).

Kwasababu ukiangalia sana hoja yako mkuu, imebezi kwenye absolute truth kuliko relative, na kama huko ndiko ulikojikita basi hapa duniani yapaswa kila kitu kingine kinachotegemea chanzo cha kitu fulani kiwe derivative ya kitu hiko, lakini sasa katika mfumo wa maisha ya kawaida na hata kwenye sayansi nadhani, kikawaida huwa tunaweza kuwa na vyanzo vya mlinganisho kwa maana ya relative sources, ambavyo huwa vina maana ndani ya muktadha fulani (hii nayo unaizungumziaje mkuu).

Lakini pia niseme tu, ya kwamba nimeupenda mfano wako wa kushona nguo ya bluu kwa kutumia kitambaa chekundu, lakini vipi kama tunaweza kupaka kitambaa hicho rangi ya bluu? 😅😅

Mimi sio mtaalam sana wa mambo ya quantum (ila kuanzia sasa nitajikita zaidi huko kwa maana inawezekana baadhi ya puzzle zinasolvika kirahisi huko), ila naelewa jambo moja ya kwamba katika ulimwengu wa quantum, kuna mifano mingi inayoelezea kitu kuweza kuwa na hali mbili tofauti kwa wakati mmoja.

Kwa hiyo, kutokana na hilo basi swali lako liko na dhana ya ukweli wa moja kwa moja, iilhali ukweli mara nyingi huwa ni wa mlinganisho kulingana na muktadha.
Again, sijasema muda hauna maana, nimesema muda si fundamental, si kitu cha msingi.

Na unapoongelea chanzo, kitu ambacho ni fundamental, hutakiwi kuongelea kitu kinachotegemea kitu derivative, unatakiwa kuongelea kitu fundamental, si kitu derivative.
 
Nadhani hapa umeleta kitu kingine tena, na hii ni puzzle pia, na kama usemavyo ni kweli ya kwamba chanzo cha uhai ni viumbe hai basi bado msingi wa uhai haujulikani.
Si lazima kila kitu kilichopo kiwe na msingi wake.

Kama uhai lazima uwe na msingi wake, Hata huo msingi wa uhai, lazima uwe na msingi wake mwingine.

Msingi huo wa uhai, Hauwezi kuwepo tu bila msingi wowote.
 
Again, sijasema muda hauna maana, nimesema muda si fundamental, si kitu cha msingi.

Na unapoongelea chanzo, kitu ambacho ni fundamental, hutakiwi kuongelea kitu kinachotegemea kitu derivative, unatakiwa kuongelea kitu fundamental, si kitu derivative.
Namimi nimekubaliana na wewe lakini pia nimekupa sababu za kwamba kutokua kitu cha msingi haimaanishi hakipaswi kutumika katika muktadha huo.
 
Si lazima kila kitu kilichopo kiwe na msingi wake.

Kama uhai lazima uwe na msingi wake, Hata huo msingi wa uhai, lazima uwe na msingi wake mwingine.

Msingi huo wa uhai, Hauwezi kuwepo tu bila msingi wowote.
Ndio maana nikakwambia kwanza tuanzie hapo turudi nyuma hadi kufikia msingi halafu tutaanzia hapo kujadili tena kama msingi ni lazima uwe na msingi.

Kwahiyo hoja yako ya msingi kuweza kuwa na msingi hakuwezi kuondoa hoja ya chanzo kuwa na msingi, kwahiyo kabla hatujarudi hapo kwenye msingi kuwa na msingi kwanza tujadili msingi wa uhai ni nini.
 
Namimi nimekubaliana na wewe lakini pia nimekupa sababu za kwamba kutokua kitu cha msingi haimaanishi hakipaswi kutumika katika muktadha huo.
"Muktadha huo" ni muktadha gani?

Hutakiwi kuongelea kitu cha msingi kama chanzo kwa kutumia kitu derivative.

Habari ya chanzo si habari fundamental, inaweza kuwa na maana katika muktadha fulani tu.

Kwa hivyo, unapoongelea chanzo, ni lazima uweke muktadha.
 
Ndio maana nikakwambia kwanza tuanzie hapo turudi nyuma hadi kufikia msingi halafu tutaanzia hapo kujadili tena kama msingi ni lazima uwe na msingi.

Kwahiyo hoja yako ya msingi kuweza kuwa na msingi hakuwezi kuondoa hoja ya chanzo kuwa na msingi, kwahiyo kabla hatujarudi hapo kwenye msingi kuwa na msingi kwanza tujadili msingi wa uhai ni nini.
Kwa nini ujadili msingi wa uhai ni nini, wakati hujui msingi wa msingi wa uhai ni nini?

Kwa sababu kuna vitu vipo lakini havina msingi.

Hata uhai na wenyewe hauna msingi.

Kuwa na chanzo si lazima kuwe na msingi.

Chanzo kinaweza kuwepo bila msingi.
 
Back
Top Bottom