Kama dunia inazunguka, kwanini miamba na milima haiporomoki? Na kwa nini bahari isimwage maji yake?

Kama dunia inazunguka, kwanini miamba na milima haiporomoki? Na kwa nini bahari isimwage maji yake?

Mkuu Anheuser,

Kiswahili ni sio lugha yangu, na mimi ninajitahidi sana kuchagua maneno ya kufahamika. Kwa hiyo ningefurahi ungeliweza kunisahihisha katika neno hilo, kwani niliuliza wengine hapa maana ya mass nao wakaniambia kuwa ni uzito, na kwa kuwa sikuweza kufanikiwa na neno sahihi sikuwa na budi ila kulitumia uzito wakati mimi mwenyewe sikukubaliana nalo.

NAterejea utanielimisha hapo. Nashukuru sana.

Je ulichoandika ni kile ulichoelewa? au ni tafsiri ya neno kwa neno aka direct tu kwa kiswahili kutoka sehemu?
 
Kuna vitu vinanitatiza sana sijui ni sababu ya kutaka kujua kila kitu Mimi sio mtaalam wa Geography japo wakati nipo sekondari tu kwa nadharia na kuna concept inasema dunia huwa inazunguka au inajizungusha kwenye mhimili wake. Ila maswali ninayojiuliza inazunguka vipi? Na kwanini isifike kipindi leo tujione tupo upande huu kesho upande mwingine? au mwaka huu tupo upande huu mwaka kesho tupo upande mwingine.

Na pia pia kama inazunguka nilitegemea kwa hali ya kawaida kama unavyozungusha kitu chochote chenye maji kisicho na mfuniko maji yale yatamwagika lakini maji ya bahari mbona hayamwagiki? au ndio hiyo gravity? Na pia effect ya miamba na milima hainokeni labda kupomoka zaidi ya ile wanayosema plate movement kwenye Physical Geography.

Swali la msingi kama inazunguka Je, kwanini kila siku tunajiona tupo sehemu ileile?016¡è7

Sio tu dunia ndiyo inayozunguka hata jua linazunguka. Jua na nyota na sayari vyote huzunguka,mzunguko hufanyika kwa nyota na vyote kuzunguka kutokea kizio cha galax. mfano, mzuri ni kama vile unavyoona vumbi la chamchela inavyozunguka tokea kiini cha katikati.Sasa tuchukulie vile vipande vya vumbi ndio nyota

Sasa inakuwaje hatuhisi mzunguko huo? Dunia ni kubwa mno na katika mzunguko huo dunia ina kwenda kwa kasi ya takriban kilometa 110,000 kwa saa julizunguka jua na Jua linatumia takriban miaka milion 250 kuzunguka kiini cha galax. Kasi ya jua kuzunguka kiini cha galax ni kilometa 220,000 kwa sekunde moja. Hii inajenga picha ya namna upana wa galax tuliomo (Milky Way) ulivyo.

Hivyo ukubwa wa dunia hauwezi kutufanya tuone na kuhisi huo mzunguko na pia upana wa eneo la galax yetu hautoifununu ya kuona kasi ya vile tuzungukavyo na dunia yetu.

Aidha,galax ya milky way ni moja kati ya mabilion ya galax.

NB: Mwacheni Mungu aitwe Mungu!
 
Wakuu ahsanteni sana nimewalewa sana sana salute i appriciate to maximum.
 
Sasa inakuwaje hatuhisi mzunguko huo? Dunia ni kubwa mno na katika mzunguko huo dunia ina kwenda kwa kasi ya takriban kilometa 110,000 kwa saa julizunguka jua na Jua linatumia takriban miaka milion 250 kuzunguka kiini cha galax. Kasi ya jua kuzunguka kiini cha galax ni kilometa 220,000 kwa sekunde moja. Hii inajenga picha ya namna upana wa galax tuliomo (Milky Way) ulivyo.

Mkuu 1954tanu, Nimefurahi kusoma maandishi yako, ila tu ningelipenda kusahihisha hayo yaliyo andikwa hapo kwa rangi nyekundu, naterejea kusudi lako ni kilometa 220 kwa sekunde.
 
Jaribu kufikiria Sumaku kubwa iliyoganda kwenye vichuma vidogo vidogo!!

Je hiyo sumaku ikizunguka hivyo vichuma navyo vitaanguka? Au vitajiachia kwenye sumaku?

Pia kuzunguka ingawa ni suala la kifizikia (Motion) but lina impact kwenye saikolojia pia (kizunguzungu), sasa mbona hatusikii kizunguzungu kama kweli muda wote tunazunguka? Jibu ni rahisi, kila kitu ni kinazunguka.

Yaani wakati tunazunguka hakuna ambacho hakizunguki kwamba ukikiangalia utaona kiko palepale. Wewe unazunguka na vyote unavyoviona navyo vinazunguka.
 
Wakuu Anheuser na alhajry na wengine wote

kwanza ningependa "tujadili" kidogo kuhusu tungamo na uzito(mass and weight)

Kwa watu tunaoishi duniani tu hizo ni nadharia tu lakini kwa wenzetu wanaoenda kwenye anga za mbali,mwezini na kwingineko hivi vitu kwao wanavishuhudia

Mass(tungamo) ni kiasi cha maada kilichopo ndani ya maada fulani,yaani mfano atom flani ina particles kiasi gan hiyo ni mass.Mass haibadiliki popote unapoenda ulimwenguni iwe kwenye anga au mwezini kwasababu hata ukienda huko "damu yako,ubongo na kila kitu atoms vitabaki ndani ya mwili wako tu haviwezi kutoka...

Tukija upande wa pili weight(uzito) ni kile kiasi ambacho unakua unavutwa na gravity..yaani ni kwa kiasi gani gravity inaact kwako...ndio maana hua uzito unabadilika unapotoka duniani na kwenda mwezini hipungua na unapoenda kwenye space weight inaweza kua sifuri kabisa yani huna uzito

Na hiyo ndiyo tofauti ya mass na weight

NB:inawezekana hayo maneno ya kiswahili(tungamo na uzito) nikawa nimekosea ikawa ni kinyume si mnaelewa elimu yetu wakuu ni ya "kingelesa" lakin nadhani nipo sawa.
Mkuu; kwanza nikuondoe wasiwasi kuhusu usahihi wa maana ya tungamo na uzito. Uko sahihi kabisa kuwa Tungamo ni Mass na Uzito ni Weight.
Rejea Kanuni ya pili ya mwendo ya Newton: KANI = Tungamo * Mchepuo wake (i.e Weight = Mass * Acceleration)
Baada ya kuwa nimekuondolea hofu hiyo, ningependa kuongezea maarifa kidogo kuhusu badiliko la uzito wa kitu kiwapo maeneo tofauti.
Ieleweke tu kuwa uzito wa kitu hubadilika kutegemea na kiasi cha nguvu ya uvutano wa dunia (gravitational force) cha mahali kitu kilipo, ama sehemu kwenye uso wa dunia au sehemu mbali na uso wa dunia (ndani au nje).
Kwenye uso wa dunia kiasi cha nguvu hii ki-tofauti katika maeneo ya Ikweta na katika maeneo ya ncha mbili za dunia yaani ncha ya kaskazini na ncha ya kusini (Northern and Southern poles). Hii iko vile kutokana na umbo halisi la dunia lilivyo.
Dunia ina umbo mfano wa boga (oblate structure) ambalo limebonyea katika sehemu mbili zinazokabiliana, ndizo kwenye ncha ya kaskazini na ncha ya kusini. Umbo hili hufanya uso wa dunia kwenye ncha hizi mbili kuwa na umbali mfupi zaidi kutoka kwenye kitovu cha dunia kuliko uso wa dunia kwenye Ikweta na hivyo kuwepo nguvu tofauti ya uvutano, hivyo tofauti ya uzito wa kitu kiwapo kwenye maeneo haya mawili.
Nawasilisha.
 
Sasa inakuwaje hatuhisi mzunguko huo? Dunia ni kubwa mno na katika mzunguko huo dunia ina kwenda kwa kasi ya takriban kilometa 110,000 kwa saa julizunguka jua na Jua linatumia takriban miaka milion 250 kuzunguka kiini cha galax. Kasi ya jua kuzunguka kiini cha galax ni kilometa 220,000 kwa sekunde moja. Hii inajenga picha ya namna upana wa galax tuliomo (Milky Way) ulivyo.

Mkuu 1954tanu, Nimefurahi kusoma maandishi yako, ila tu ningelipenda kusahihisha hayo yaliyo andikwa hapo kwa rangi nyekundu, naterejea kusudi lako ni kilometa 220 kwa sekunde.

Shukrani
 
Mkuu; kwanza nikuondoe wasiwasi kuhusu usahihi wa maana ya tungamo na uzito. Uko sahihi kabisa kuwa Tungamo ni Mass na Uzito ni Weight.
Rejea Kanuni ya pili ya mwendo ya Newton: KANI = Tungamo * Mchepuo wake (i.e Weight = Mass * Acceleration)
Baada ya kuwa nimekuondolea hofu hiyo, ningependa kuongezea maarifa kidogo kuhusu badiliko la uzito wa kitu kiwapo maeneo tofauti.
Ieleweke tu kuwa uzito wa kitu hubadilika kutegemea na kiasi cha nguvu ya uvutano wa dunia (gravitational force) cha mahali kitu kilipo, ama sehemu kwenye uso wa dunia au sehemu mbali na uso wa dunia (ndani au nje).
Kwenye uso wa dunia kiasi cha nguvu hii ki-tofauti katika maeneo ya Ikweta na katika maeneo ya ncha mbili za dunia yaani ncha ya kaskazini na ncha ya kusini (Northern and Southern poles). Hii iko vile kutokana na umbo halisi la dunia lilivyo.
Dunia ina umbo mfano wa boga (oblate structure) ambalo limebonyea katika sehemu mbili zinazokabiliana, ndizo kwenye ncha ya kaskazini na ncha ya kusini. Umbo hili hufanya uso wa dunia kwenye ncha hizi mbili kuwa na umbali mfupi zaidi kutoka kwenye kitovu cha dunia kuliko uso wa dunia kwenye Ikweta na hivyo kuwepo nguvu tofauti ya uvutano, hivyo tofauti ya uzito wa kitu kiwapo kwenye maeneo haya mawili.
Nawasilisha.

mkuu kijiko

Asante kwa kunikumbusha,mchango wako ni mzuri.Watu wengi hufikiria dunia ni duara kamili lakini sivyo,dunia ipo kama boga na kuna ushahidi wa kutosha juu ya hilo mkuu..

Nashukuru tena.
 
Last edited by a moderator:
Vp kuhusu ndege ikipaa huwa inakuwa wap dunian au wap? , km dunia inazunguka kwa nini ndege huwa azikose lengo wakat zinatua? Na je ni kweli tupo up side down?

swali lako la ndege kukosea halijajibiwa sijui hakuna marubani humu hata mi ningependa kujua please pilot
 
swali lako la ndege kukosea halijajibiwa sijui hakuna marubani humu hata mi ningependa kujua please pilot


Wakuu mdukuzi na MWAMFUPE

Mzunguko wa Ardhi hauathiri kabisa ndege ikiwa inapaa angani au imetua Ardhini, sababu kubwa na muhimu ni mvutano wa Ardhi (Earth Gravity) hufanya kuwa kila kitu kinazunguka pamoja na mzunguko wa Ardhi hata anga nayo inazunguka kwa speedi ya Ardhi.
 
Wakuu mdukuzina MWAMFUPE

Mzunguko wa Ardhi hauathiri kabisa ndege ikiwa inapaa angani au imetua Ardhini, sababu kubwa na muhimu ni mvutano wa Ardhi (Earth Gravity) hufanya kuwa kila kitu kinazunguka pamoja na mzunguko wa Ardhi hata anga nayo inazunguka kwa speedi ya Ardhi.

Hapana!! Ukisema "hauathiri kabisa" unakosea na labda hujui hilo, mzunguko wa Dunia unaleta Coriolis effect hivyo kuna athari inayotokana na tofauti ya vitu hivi viwili (Dunia na Ndege) kuwa viko kwenye position tofauti, ingawa athari hii ni ndogo sana kwa kuwa speed ya rotation ya Dunia si kubwa. Ndege haikai katika stationary state inapokuwa angani (ina engines zinazoisukuma) hivyo kama ingekaa katika hali ya kutulia sehemu moja tu kungekuwa na athari zaidi kutokana na gravity na pia coriolis effect kwa kiasi kidogo.

Vitu vyote vinavyoruka angani umbali mkubwa vinaathiriwa na Coriolis effect kwa kiasi fulani na Pilots wa yale madege makubwa wanajua kuhusu hili kwa ufasaha. Ndege haiwezi kuruka mstari ulionyooka kutoka bara moja hadi jingine bila Pilot kuweka sawa njia yake kwa sababu Dunia inazunguka. Ukisema haiathiri kabisa ina maana una ignore physics laws na sayari nyingine zenye rotation ya kasi zaidi ya Dunia huko Coriolis effect ni kubwa zaidi na inaathiri anga maradufu ya Dunia. Vimbuga vya huko hapa duniani hatujawahi kuona.

Wakati Corioris effect iko mahali pake na Earth gravity pia iko mahali pake, Ndege na Dunia vinaendelea kuathiriwa na Gravity pull ya Jua hivyo hata kama ndege itakuwa juu na ikae katika stationary state dhidi ya mzunguko wa Dunia bado ingeendelea kulizunguka jua pamoja na Dunia. Jua nalo liko katika mwendo kuzunguka kiini cha galaxi yetu MilkyWay kama nyota nyinginezo hivyo pia linaathiriwa na mvuto mkubwa wa super massive blackhole katika center ya galaxi.
 
Mheshimiwa Dreadnaught,

Nafurahi sana kuwepo na wakuu wakubwa wenye kufikiria kwa kutumia logic za akili kabisa, na kama tulivyo binadamu tunaweza kukosea na pia kufanikiwa. Ili muradi ni kubadilishana mawazo na busara ili kuelimishana.

Kuhusu swala lako la kuzaliana kwa viumbe kama binadamu na wanyama wengine na mimea kwa ujumla, Jee huzidisha uzito wa Ardhi? kwa hakika kuongezeka kwa viumbe hapa Ardhini haizidishi uzito wowote ule juu ya Ardhi, kwa sababu kama walivyo tujuulisha wakuu wakubwa hapo juu ya kuwa vyote hivi vimetokeana na vitu vilivyomo Ardhini hapa hapa na vinarejea tena ndani yake. Kwa hivyo hakuna kitu kipya cha kuzidisha uzito.

Lakini kama tulivyosoma pia hapo juu ya kuwa Ardhi inaongezeka uzito wa tani 40,000 kila mwaka kwa kupokea vumbi ya angani inayo vutwa na gravity ya Ardhi, pia tunaona kuwa Ardhi kila mwaka inapoteza tani 95,000 kwa muujibu wa kutoroka kwa hydrogen na tani 1600 ya helium pia katika center ya Ardhi hupetea tani 16,000 kwa sababu ya nuklia fusion, kwa hivyo ni jumla ya kadiri ya tani 50,000 ya uzito wa Ardhi yapunguka kila mwaka, nayo ni kadiri ya 0.000000000000001% ya uzito wa Ardhi yenye lengo la uzito wa tani 5,973,600,000,000,000,000,000.

Je! inatubidi tuwe na khofu kwa kupunguka kwa uzito wa Ardhi kila mwaka? hakika hapana khofu kabisa kwa kupoteza hydrojen katika hewa kila mwaka kwa kiasi hicho, kwani itahitajia miaka karibu ya trillioni kuisha kwake. Hapo ikiwa Ardhi ingali hai hata wakati huo!

Mkuu tafadhali naomba uandike kwa maneno huo uzito wa dunia ulioainisha hapo juu tafadhali...mim nimeshindwa..!
 
Sio tu dunia ndiyo inayozunguka hata jua linazunguka. Jua na nyota na sayari vyote huzunguka,mzunguko hufanyika kwa nyota na vyote kuzunguka kutokea kizio cha galax. mfano, mzuri ni kama vile unavyoona vumbi la chamchela inavyozunguka tokea kiini cha katikati.Sasa tuchukulie vile vipande vya vumbi ndio nyota

Sasa inakuwaje hatuhisi mzunguko huo? Dunia ni kubwa mno na katika mzunguko huo dunia ina kwenda kwa kasi ya takriban kilometa 110,000 kwa saa julizunguka jua na Jua linatumia takriban miaka milion 250 kuzunguka kiini cha galax. Kasi ya jua kuzunguka kiini cha galax ni kilometa 220,000 kwa sekunde moja. Hii inajenga picha ya namna upana wa galax tuliomo (Milky Way) ulivyo.

Hivyo ukubwa wa dunia hauwezi kutufanya tuone na kuhisi huo mzunguko na pia upana wa eneo la galax yetu hautoifununu ya kuona kasi ya vile tuzungukavyo na dunia yetu.

Aidha,galax ya milky way ni moja kati ya mabilion ya galax.

NB: Mwacheni Mungu aitwe Mungu!

Mkuu kumbe na jua pia huzunguka(galaxy)?? Kwa elimu yangu ya jiografia ya darasa la saba nilijua dunia na sayari zingine ndiyo huzunguka jua..!!
 
Kwa kua hapa ni suala la fikra zaidi na wengine Jiografia ilitupita pembeni, naomba kujuzwa yafuatayo:-

1- Hiyo gravity inavuta vitu kuelekea katikati ya dunia?
2 - Hiyo grafity force ipo kwenye sayari ya dunia tu au kila sayari ina gravity force yake?
3 - Jua nalo linavuta vitu kuelekea kwake, namaanisha sayari zote zinavutwa kuelekea katikati (jua liliko)?

Natanguiza shukrani
 
Kuna swali kauliza bwana mmoja halijajibiwa wakuu"" kama mtu ukiruka na chombo angani ukiwa hapa dar na ukakaa stationary kwa masaa kazaa huko angani atakaporudi ardhini anaweza kujikuta eneo tofauti na dar?"""
 
Back
Top Bottom