IMEVUJAAA!!!!
Ujerumani na Marekani zapanga kuhujumu Tanzania
Taarifa kutoka ndani ya Balozi za nchi hizi mbili zimethibitisha kuwa kuna mipango inasukwa ya kuihujumu Tanzania. Mipango hiyo inaandaliwa na Marekani na Ujerumani kupitia Balozi zao nchini.
Taarifa zilizopo ni kwamba Dkt. DONALD J. WRIGHT (US Ambassador) na Bi. REGINA HESS (Germany Ambassador) walianza kutekeleza mipango hiyo baada kujionyesha wazi kwa kumsindikiza Airport aliyeshindwa Uchaguzi Mkuu Tanzania TUNDU ANTIPHAS LISSU
Maagizo yaliyotolewa kwa Mabalozi wa Nchi hizi mbili ni kwamba wahakikishe wanawasaidia Wagombea wote wa Upinzani ambao walishindwa Uchaguzi hususani wa CHADEMA ili waende kuishi Ujerumani pamoja na Familia zao.
Lengo ni kuwapa Mafunzo Maalum ya namna ya kuvuruga nchi ambayo yatahusishwa na Political Violence Vurugu za Kisiasa yatakayotolewa na Majasusi wa Marekani na Ujerumani.
Viongozi hao wa Upinzani wametakiwa kuzichukua na Familia zao kwani watakuwa wanalipwa kila mwezi USD 5000 sawa na (Tshs. 11,595,000/=) na kupewa makazi, ndio maana tumeona tayari LISSU ameondoka na familia yake na wengine wanaofuata ni LAZARO NYARANDU, ZITTO KABWE, GODBLESS LEMA.
Watakaobaki nchini wametakiwa kuendelea kukijenga Chama ili watakaomaliza mafunzo wakirudi waanze mikakati ya kuivuruga Tanzania kwa kuanzisha Political Violence (Vurugu za Kisiasa) katika Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Na ndio maana hatumsikii JOHN MNYIKA, JOHN HECHE, HALIMA MDEE, ESTER BULAYA na wengine wakilalamikia kutishiwa maisha kwa kuwa wao wametakiwa kubaki nchini ili kuendelea kulinda uhai wa Chama na wataendelea kulipwa kama wenzao watakaokuwa wanaishi Ujerumani.
Watanzania tujiandae kwa jaribio la Pili maana jaribio la kwanza la kutaka kutuvuruga kwenye Uchaguzi huu wameshindwa kutokana na Umoja wetu, na sasa wanekwenda kuongeza ujuzi wa jinsi ya kutugawa ili waendeshe vurugu na kufanikiwa azma ya MABEBERU kutaka nchi isitawalike ili wao wavune mali kirahisi.
UMOJA NDIO SILAHA YETU!