Kama huna fikra za kikandamizaji, hauwezi kuishadadia Urusi

Kama huna fikra za kikandamizaji, hauwezi kuishadadia Urusi

Kama huamini kwamba Kiongozi anatakiwa kuabudiwa, hauwezi kuishadadia Urusi. Kama wewe unaamini kila mtu ana haki ya kuelezea hisia zake bila ya kutishwa na dola, huwezi kuishabikia Urusi.

Kama unataka Kiongozi akiwa madarakani asitumie madaraka hayo kujitajirisha, wewe na Urusi hamfanani. Kama unapenda demokrasia duniani, kaa mbali na Urusi. Kama unachukia viongozi Katili, jitenge na Urusi.

Kama siyo tabia yako kupenda wanasiasa wanaopenda rushwa na wanaozuia kukamatwa, iache Urusi ikae mbali na wewe.
Naomba nikuulize swali mkuu
 
Allen Kilewella je wewe ungekuwa ndio USA ungekubali mrusi ajenge base ya nuclear Cuba? Au Mexico? Tuanzie hapo kwanza!
 
Kama huamini kwamba Kiongozi anatakiwa kuabudiwa, hauwezi kuishadadia Urusi. Kama wewe unaamini kila mtu ana haki ya kuelezea hisia zake bila ya kutishwa na dola, huwezi kuishabikia Urusi.

Kama unataka Kiongozi akiwa madarakani asitumie madaraka hayo kujitajirisha, wewe na Urusi hamfanani. Kama unapenda demokrasia duniani, kaa mbali na Urusi. Kama unachukia viongozi Katili, jitenge na Urusi.

Kama siyo tabia yako kupenda wanasiasa wanaopenda rushwa na wanaozuia kukamatwa, iache Urusi ikae mbali na wewe.
Kama hutaki upinde kaa karibu na urusi.
 
Mfano mmoja mkataba wa gesi, na nasikia wameweka kambi kigamboni baada ya kugundua pande hizo kuna madini adimu sana duniani
Gesi wala siyo US ni kusingizia watu uongo tu. Kwa hiyo wametoka huko na kugundua kuna na Serikali haina taarifa? Waafrika tukuona wazungu waamejenga sehumu huwa tunaamini eneo hilo lina madini.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Marekani hana tofauti na mchawi, unamzaa mtoto, unamlea na kumsomesha mwisho wa siku anamla nyama. Usibabaishwe na vimisaada kwani marekani hapeleki msaada sehemu ambayo hakuna returns
marekan kaitaja wap hapo ? ndio maana nlisema ww ndo mjinga
 
Mwamposa:"Demokrasia ni sawa sawa na devil gasia
demokrasia ni nzur ila waafrika wengi mnataka demokrasia ikupe wewee sauti kuliko mwingine mwishowe mnaishia kuuana badala ya kukomesha ubinafsi wenu mnasingizia demokrasia
 
Watu tumelishwa matango pori kua marekani pekee ndio anademokrasia wengine wote hawana.Kunaambo mengi ya ajabu sana huko marekani ambayo nikinyume na haki za binadamu na demokrasia kwa ujumla.
umekaririshwa huna macho kuona kinachoendelea ? vitu vingine mnajitakia tu kuitwa majina ya ajabu
 
Mkuu nakupinga, hayo maswala ya haki haki ndo yanasabisha kuenea kwa ushoga na pia wanawake wanapewa kichwa kujiona wako sawa na wanaume,
ila wanaowatumia mashoga huku afrika si nyinyi wenyew au wanatumiwa na wazungu?
 
unataka tuishadadie marekani hii iliyovamia Iraq na kuuwa maelfu ya watu,, iliyovamia Libya na kuua maelfu ya watu Afghanistan, Vietnam etc. Punguza mahaba ndugu,,, kila uchao kufungulia nyuzi za kuiponda urusi utadhani unalipwa vile!!!
kuna kati yenu alisimama na hayo mataifa kuyasaidia kama wafanyavyo EUROPE dhidi ya Ukraine , nyiny ni wanafiki na unafik ndo unawaua
 
Labda nikukimbushe mwaka 2003 kama ulikuwa hujazaliwa, Marekani iliishutumu Iraq kuwa ina silaha za kikemikali, ikabidi watumwe wachunguzi wa kimataifa kwenda Iraq kukagua, na Iraq haikupinga.

Wakakagua hawakukuta hizo silaha wala residuals, wakatoa ripoti kuwa hakuna silaha hatarishi,

Marekani bila sababu yoyote akaivamia iraq, wakaua maelfu

Kuna wakari wanajeshi wa marekani waliua watoto kama wanacheza video games,

ICC ikataka kuwashitaki wakaijia juu kuwa wataiwekea vikwazo.

Urusi kaivamia ukraine kwa sababu ilikuwa ina mu host marekani na ni hatari kiusalama kwa urusi, NI KIPI KINA JUSTIFY UUAJI WA MAREKANI? AU KWA SABABU ALIUA WAARABU?

jitahidi ufuatilie maswala kiundani usipelekwe na mkumbo wa Western media
Iraq hii hii iliyoivamia Iran na Kuwait ? ndo unaitetea hapa ? na mliisaidiaj Iraq , nakumbuka nchi za middle east zilipiga kura kuunga mkono uvamiznww Iraq , sijui Urusi kule Ukraine alitumia sabab gan kuivamia
 
Iko hv wengi wanaomshabikia mrusi sio kwamba wanapenda anayoyafanya kwasasa,hata wao wanajua sio kitu poa,ila wanashabikia kwasababu tu mrusi kafanya kile ambacho marekani hatak watu wengine duniani wakifanye wakati mmarekani akitaka kufanya anafanya na hakuna wa kumzuia
sasa angefanya kwa mabeberu sio taifa changa
 
Back
Top Bottom