Kama huna pesa hakuna mtu atakuheshimu. Hata wazazi wako watakudharau

Kama huna pesa hakuna mtu atakuheshimu. Hata wazazi wako watakudharau

Na hii heshima inaongelewa ni kitu gani? Huwa hawakusalimii?

Au unataka kuambiwa matatizo ya watu na kuombwa ushauri?

Na kwanini mtu atake kunyenyekewa?

Seems like it's asking for unnecessary attention.

As much as you'd want to blame them, it's YOU!
 
Kuna huu ukweli ambao ni vema kila mtu anatakiwa kuufahamu. Kwa asilimia kubwa heshima ya mtu huletwa na pesa alizonazo.

Kama huna pesa hata wazazi wako, kaka na dada watakudharau. watu baki ndiyo kabisa watakudharau. Na si kwamba hawakupendi. Watakupenda sana ila hawatakuheshimu.

Kifupi watakudharau. Ukionyeshwa dharau sababu huna pesa usikasirike, hao ndugu wanakupenda sana ni vile tu hawakuheshimu na umasikini wako.

Hapohapo, ukiona unaheshimiwa-heshimiwa sana na kunyenyekewa jua kuwa inaheshimiwa na kunyenyekewa pesa yako.

Usidhani labda watu wanakupenda sana. Binadamu hana aibu kabisa linapokuja suala la kuabudu pesa.

Tafuta pesa au kubaliana na hali.
Ushenzi tu
 
Hapo ndo utakutana na

Hapo ndo utakutana na vibinti vinafiki Mara ooh Ndubwi nimekumisi aggggggggrrr 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Me nkawa nasoma comment nacheka sana.
Wengine hata zawadi watakununulia kwenye birthday yako😆😆😆sijui kama ntaoa mimi maana dah walininyanyapaa sanaa
 
Katika familia ukiwa huna pesa jifunze kujitolea kufanya mambo mengine ambayo hayahitaji pesa.
Kama kuna shughuli piga kazi kuliko wengine, kama kuna mgonjwa wa kuhudumia na una nafasi nenda kahudumie kwa moyo wote. Ni mengi yapo ya kufanya na hakuna anakaye kudharau.
Pesa ni muhimu lakini sio kila kitu.
 
Naongelea ufanye kitu kwaajili yako mwenyewe sio kwaajili ya Kupata heshima Kutoka Kwa Watu wengine.
Mfano, unatafuta Pesa ATI ili uheshimiwe, badala ya kutafuta Pesa kwaajili ya mambo yako na familia yako.
Matokeo yake usipopata hizo Pesa unaishi Maisha ya msongo WA mawazo.
Na sio kwamba umefanya Makusudi Bali kazi ulikuwa unafanya.

Au unaenda Kanisani au msikitini ili Mungu na watu wakuheshimu, come on! Huo ni UTUMWA. Fanya kitu kwaajili yako mwenyewe kama kinakufurahisha na kama kinafaida kwako.

Au unakuta Binti analazimisha Aolewe ili apate heshima. Huo ni UTUMWA na upumbavu. Yaani ili uridhishe Watu.
Heshima sio kumridhisha MTU au kundi la Watu.

Heshima ni kufuata na kufanya Haki, ukweli na upendo. Hiyo ndio heshima.
Na Kati ya hayo sijataja Pesa, Gari, nyumba, n.k

Mtu Aishi Kwa maadili Mema, ajipende na kupenda Watu wanaomzunguka, Aishi Kwa Haki, awe Mkweli. Aishi Kwa uhalisia. Hapo atapata heshima ya kweli na inakuja Natural.

Wazazi wanaodharau Watoto wao kisa Hawana Pesa ni majinga, mazuzu, yasiyo na Maadili. Hiyo pia itaenda Kwa Watoto wanaodharau wazazi wao Kwa sababu ya vitu vya kijinga Jinga.

Na wapumbavu na mazuzu ndio huheshimu Watu Kwa sababu ya Pesa, utajiri, na Elimu. Wakati wenye Hekima na Werevu huheshimu Watu Kwa kuangalia maadili Mema wayafanyayo, utu, haki, upendo n.k.

Sisi Watibeli hata huku kwetu tumeshaweka Watu katika makundi mawili tuu, Wenye maadili na wasio na Maadili.
Ukiwa na Maadili Mema Kwa kweli hata kama ni mdogo wangu au mtoto wangu nitakuheshimu na kukupenda, na kukunyenyekea ikibidi.
Lakini ukiwa na Maadili mabaya hata ungekuwa Mama au Baba yangu au Rais au Waziri au tajiri namba moja Duniani, nitakudharau na kukuona kama Mavimavi tuu.
Hukumu hiyo ikitumika kwangu pia ni Haki.

Mimi MTU akinidharau Kwa sababu ya ukosefu WA maadili Kwa kweli ninajisikia vibaya Sana.
Labda nimefanya uasherati alafu MTU akanifumania Kwa kweli hata kama hatasema kitu nitakuwa Duni kwake Kwa muda mrefu.

Sisemi Kuwa Mimi ni mtakatifu kwamba sina Makosa au sina dhambi, nazungumzia heshima na kudharauliwa.

Pole Mchumba Kwa comment ndefu😊😊
We jamaa huwaga unavituko unaandika mambo ambayo hayana uhalisia
Hakuna binadamu asiyependa recognition kutoka kwa watu wengine
Mfano hapa jamiiforum kuna tuzo wanapewa kupitia member bora au story of change hio yote watu wanafanya ili wapate recognition kutoka kwa watu wengine

Makazin kuna tuzo za mfanyakazi bora hakuna mtu ambaye hafurahii kuwa sio mfanyakazi bora ukiangalia hapo utaona watu tunafanya kazi kwa bidii moja ya sababu ni kuwa recognition

Kwenye michezo kuna prize tofauti tofauti watu wanapewa na angalia ile furaha watu wanakua nayo wanapopewa hizo tuzo hiyo yote ni kutaka kufurahisha watu

Kwenye maisha na (nature) asili kilicho bora kinasifiwa siku zote na ndo raha ya maisha kila mtu anafurah anapofanya jambo linapogusa watu wengine, ukifanya jambo kwa ajili yako huwezi lifurahia

Unaposema ufanye jambo kwa ajili yako mwenye unakuaje motivated
kwa hiyo mkuu mda mwingi unajicontradict sana nyuzi zako nyingi zinapingana zenyewe yaan hujulikan unasimamia kipi

Ukiwa huna hela sio kwamba unadharauliwa kuna mambo ambayo yanahitaji fedha hata ukiambiwa utoe utahisu unadharauliwa ndo maana watu wanakupotezea sasa ukipotezewa usifikiri unadharauliwa ni kwamba huna msaada
 
Katika familia ukiwa huna pesa jifunze kujitolea kufanya mambo mengine ambayo hayahitaji pesa.
Kama kuna shughuli piga kazi kuliko wengine, kama kuna mgonjwa wa kuhudumia na una nafasi nenda kahudumie kwa moyo wote. Ni mengi yapo ya kufanya na hakuna anakaye kudharau.
Pesa ni muhimu lakini sio kila kitu.
Hilo haliwezekan dada katika hii dunia
 
Sijui Kwa nini Watu wanapenda kuheshimiwa.[emoji23][emoji23]
Yaani kuendeshwa na Maoni na Mtazamo wa wengine

Kuheshimiwa sio tafsiri yake hiyo.

Ukitaja kujua heshima ina maana gani,subiri siku mtu akutamkie maneno ya fedheha mbele za watu,sababu tu umevaa nguo chakavu au umekosa nauli kamili ndio utaelewa.

Kuna chakula cha mwili(ugali,mananasi,wali,kitimoto nk)halafu kuna chakula cha roho(heshima,upendo,kujaliwa)ukivikosa hivyo lazima usiwe sawa.
 
Nakuunga mkono

Miye unipende usinipende as long as am comfortable with my self I don't care

Huwezi ridhisha Kila mtu

Hauwezi kuwa comfortable for youself,ila una uwezo wa kupuuza yanayokunyima furaha.sababu umekata tamaa kabisa ya kuyapata na uwezekano haupo kabisa.

Ukiwa sehemu pia watu wakapuuza kabisa hali uliyo nayo,hilo pia litakukosesha amani.
 
Hilo haliwezekan dada katika hii dunia
Inawezekana nimeshashuhudia.
Dharau ni tabia mbaya tu za familia. Ikiwa ni familia mliyoishi kwa upendo tangu utotoni hamuwezi kudharauliana.

Nina mama yangu mdogo hana kazi, kiufupi hana kazi lakini ni mtu wa kujitolea sana hasa kwa wagonjwa na anafanya kwa moyo.
Wewe na pesa zako unaweza ukakosa nafasi ya kumuhudumia mgonjwa ndugu yako ya karibu lkn ndugu yako mwingine hana pesa lkn anao muda wa kukaa na mgonjwa. Unaanzaje kumdharau ndugu wa hivyo?

Tatizo la wasio kuwa na hela wanajishtukia sana, kitu kidogo atasema anadharauliwa kwasababu hana pesa.
 
Nakuunga mkono

Miye unipende usinipende as long as am comfortable with my self I don't care

Huwezi ridhisha Kila mtu
You're the same to me .. yaani ukizingatia yanayokuhusu tu hakuna kitu kitakuwazisha.. suala la kufikiria kuridhisha watu ndio mwanzo wa kujipa fikra zitakazokuumiza... Huwa sinaga time na mambo hayo.. ukinipenda it's okay na ukinichukia the same cause nothing else will be added after you love or you hate me..
 
Usipokua na lengo la kutafuta ela siutakua unapuyanga huku dunia jamaa kaongea ujinga
Lengo la kutafuta pesa ni kupata basic needs, as I said, i.e food, shelter, clothing, education, healthcare.

Baada ya kupata na kuwa na uhakika wa kupata basic needs then what?
 
Back
Top Bottom