Kama Kocha Fahdu analipwa mamilioni kwa mpira huu basi viongozi wa Simba mjitafakari sana

Kama Kocha Fahdu analipwa mamilioni kwa mpira huu basi viongozi wa Simba mjitafakari sana

Wale wengine wanacheza vizuri kweli ila wanakandwa kweli. Yaani ni kama mwanamke mwenye sura nzuriii ila sasa...
😅
 

Attachments

  • 51c0f6564d254737988b9246d80894db.jpg
    51c0f6564d254737988b9246d80894db.jpg
    71 KB · Views: 3
Tatizo kubwa la simba wachezaji ni wabinafsi hawachezi ki team hivyo simba haieleweki inacheza formation gani.
Formation wanayocheza ni Ile ya kuishusha timu daraja,,kocha wa ivyo kimbinu ni mweupe kama nyeti za kuku!
 
Mutale na Kibu baba yao mmoja wale. Wanafanya kazi kuubwa ila sasa inapofika wakati wa kufunga au kutoa pasi za mwisho hapo ndio utajua hakuna mwenye akili kati yao. Wanachojua wao ni kudrible mpira tu na mbio kama "ngiri mkia juu zaga nje" badala ya kuachia mpira haraka. Ndio maana Mutale kila siku majeraha kwake ni nyumbani bora mwenzie Kibu kakomaa haumii hovyo hovyo. Ushauri wa bure kwa viongozi wa Simba huyo Mutale muuzeni au mtoeni kwa mkopo kwa sababu Fadlu anampenda pamoja na ubovu wake. Haiwezekani kwenye benchi una Awesu ambaye aliihitajika sana kuituliza timu pale mbele halafu unamwingiza Mutale ambaye anapenda anao anao na mbio zisizo na msingi na hata akipewa pasi za mwisho mbele ya goli hawezi kufunga.
 
Formation wanayocheza ni Ile ya kuishusha timu daraja,,kocha wa ivyo kimbinu ni mweupe kama nyeti za kuku!
Formation ya kutambaa ya Jana ndio ilikuwa the best😄😄 Kweli kufungwa kubaya UTO mnaweweseka 😂😂
 
Mmekaa kukosoa kila kitu kujiona mnajuaaa mpira..
Kuna watu wa ajabu sana nchi hii,wanadhani ushindi ni kitu rahisi,hata hao wageni wamekuja kwa nia ya kushinda,nao walijipanga na wala si ajabu kushinda ugenini,kama Utopolo walifungwa goli mbili bila hapa hapa nyumbani,kwa Nini Simba isipewe heshima yake Kwa kuwashinda wageni goli moja bila?
Ushindi ni ushindi TU Kuna siku utashinda kwa magoli mengi na Kuna siku utashinda kwa goli moja.
Mbona Al Ahily Tripoli tuliwapiga goli Tatu kwa moja?
Watu wakumbuke siku hazifanani.
 
Sijaona uwezo wa kocha kabisa na kunifanya niamini kweli Simba inae kocha, tulicheza na Pamba tukashambuliwa hivi hivi Kama sio uhodari wa kipa Camara Leo Bravos alikuwa anatudhalilisha.

Kwanza Fahdu hajui kupanga kikosi kabisa zaidi ya kubahatisha, pili timu inacheza kwa kiwango cha chini mno, Tatu kuna wachezaji anawachukia bila sababu za msingi mfano ni Awesu Awesu, hata akiamua kumpanga basi anampanga kuturidhisha sisi na ndio maana kipindi cha 2 lazima amtoe hata Kama mpira anautaka.

Viungo Ngoma na Okajepha wanapooza sana pale Kati, Mavambo kiwango kimepungua sana, yaan huwezi amini kama ile ni Simba.

Huyu Ahoua ndio usiseme, kazi yake ni kupiga penati tu, hana lolote alilolifanya Leo, Mukwala ndio hamna kitu kabisa

Huwezi kuniambia kuwa unautaka ubingwa kwa kiwango kibovu namna ile
Kocha hamna pale Mzee wa aggressive defense Leo ameanza na squad mbovu, game ya Leo was the soft game KIBU hakutakiwa kuanza NGOMA ana shida hata kugeuka ni shida.

Leo kama angeanza na squad hii ATEBA, MAVAMBO, AHOUA, CHASAMBI, BALUA, OKEJEPHA, FONDOH, AMZA, KAPOMBE, TSHABALALA na CAMARA angalau tungepata magoli ya kutosha.

Mchezaji kama MKWALA anatakiwa pale mnapotaka ku- disturb opponent, it's defensive oriented & not scoring lakini Kocha hakuona hili. Kibu anatoka Mwenye Rasta anaingia Kibu mwenye Kipara very awkward & fishy.
Tusipokuwa makini mpira wetu utarudi nyuma hawa watoto wa kariakoo wameleta makocha vimeo hata game ya Jana ni Upangaji plus Sub mbovu alizofanya Kocha ikapelekea Yanga kuchenyetwa viwili vya Moto.

Binafsi kuna kazi ya kufanya ili Timu ikae sawa though solution ni kufanya maingizo mapya hasa WINGERS na mbadala wa Kapombe.
 
Back
Top Bottom