Kama kweli Mungu yupo, basi hana nguvu

Kama kweli Mungu yupo, basi hana nguvu

hapo hapo ni mzinzi wa kutupwa, mlevi wa kutupwa halafu unataka Mungu abariki uzinzi.
sasa akikupa si utaishia kuhonga tu
 
Mungu yupo sema ujafanya sacrifice

Chinja jogoo rangi yyte pika kula supu,
Sheria chinja kwa mkono wako
Mungu anataka kafara(sacrifice) na hii ni siri ambayo viongozi wa dini weng hawakwambii ila wao wanafanya sana kafara
 
Yupo ila kumthibitisha siwezi na sijawahi kumuona ila naamini
 
Pole sana ndugu ila mungu yupo sema njia zake ndio ngumu inahitaji uvumilivu sana.
sababu lazima akuandae! huwa napenda kuziita Hekima za Mungu! Wengi wanakimbia njia zake maana lazima uache mabaya yote na umfuate..(uzinzi, wizi, kusengenya, ..e.tc).
Ndo maana wengi zinakuwa ngumu.
 
Umemkataa huyo Mungu kwa sababu unasema hajibu maombi. Lakini bado unaamini nguvu za kimizimu, uchawi, na uganga.

Je, ni kipi kinakufanya uamini miungu ya kimizimu au uganga, ilhali huwezi kuamini Mungu aliyedai kuumba vyote, ikiwa ni pamoja na hizo nguvu unazotaka kuziamini?
 
Habari zenu Wanajamiiforums.
Kwa mda niliotumia kumuomba Mungu na kutokupata majibu yoyote, nahitimisha kuwa nguvu za Mungu si nyingi kama tulivyoaminishwa.

Aisee nataka kuamia Mizimuni, Anayejua namna ya kutambikia Mizimu anielekeze, Mungu aliyeletwa na meli kwenye maisha yangu amefeli (Hana impact yoyote).

Am done.
Mimi mwenyewe nauhakika shetani ana nguvu,
 
Mtu akiamini mizimu ipo, Lakini haamini Mungu yupo. Huyo bado anakuwa kigeugeu. Mguu mmoja nje, mguu mwingine ndani.

Haiwezekani mtu uamini kuna nguvu za mizimu, Halafu usiamini uwepo wa Mungu.

Kwa sababu hata hiyo mizimu ni ya kufikirika tu, Haipo.

Mtu anakuwa kabadilisha "imani" ya kuamini tu.

Umetoka kuamini Mungu ambaye hayupo, Unakwenda kuamini mizimu ambayo haipo vilevile.
 
Ndio shida inaanzia hapo haijulikani Njia zake ni ngumu maana hazitabiriki unaweza kuwa loyal kwake na ukamuomba hata miaka 20 usione majipu.
Pengine hafanyi kazi kwa mtindo tunaohubiriwa.
 
Habari zenu Wanajamiiforums.
Kwa mda niliotumia kumuomba Mungu na kutokupata majibu yoyote, nahitimisha kuwa nguvu za Mungu si nyingi kama tulivyoaminishwa.

Aisee nataka kuamia Mizimuni, Anayejua namna ya kutambikia Mizimu anielekeze, Mungu aliyeletwa na meli kwenye maisha yangu amefeli (Hana impact yoyote).

Am done.
HE IS STILL GOD,hata asipojibu maombi , yeye Bado ni MUNGU...
 
Ndio shida ya kufanya jambo huku ukiwa na uhakika wa kwamba plan B yake ipo, huwezi kukifanya kwa ufanisi yaani kuingia miguu yote kwa maana unajua ukifeli huko huna pengine pa kukimbilia so uko na option moja tu.

Mambo ya kiroho yanahitaji maandalizi kwanza lakini pia inawezekana unachokiombea tayari kipo kwahiyo ni wewe tu kukifuata.
Unazidi kunichanganya na maneno mengi aisee
 
Mungu yupo na hapo ulipo una jeuri ya kusema kwa sababu ya Nguvu ya Mungu.
Hata hivyo huenda amesikia kilio chako siyo muda mrefu anakuja kumaliza shida zako.
 
Back
Top Bottom