Kama kweli unamchukia Hayati Magufuli fanya haya utuachie tunaompenda

Kama kweli unamchukia Hayati Magufuli fanya haya utuachie tunaompenda

Tanzania hamna private sector ila tuna wachuuzi na wahujumu Uchumi kama Itel muuza makasha ya simu na betri kupewa tenda ya kuagiza Sukari!!
Mkuu kama hakuna sekta binafsi, ndugu Kufulila anasimamia nini PPP?? Na TIC ni wa nini???

Na pili huyu unayesema ni mchuuzi ni mtumishi wa serikali??? Kama sio yupo Seka gani???

Kwa hiyo TRA inakusanya kodi kwa wahujumu uchumi halafu inawaacha tu??? Naomba utueleweshe vizuri hapa!!!
 
Unajiita "Zitto junior" so ni obvious utakuwa na mawazo,akili na chuki kali sana kwa magufuli kama alivyo kabwe tu.

Well, nakubaliana na wewe kwa asilimia kadhaa kwenye hiyo paragraph yako ya kwanza hasa hapo uliposema kwamba wakati jpm anaingia madarakani wabongo kwa kiasi fulani walikuwa na ufahamu au utambuzi kulinganisha na miaka ya nyuma yake...!!

Wapinzani kipindi cha Sita na makinda walijitahidi kuleta mshike mshike ambao ulichangia kwa kiasi kikubwa kuwaweka aware watanzania na ufisadi, ila kutokuchukuliwa hatua yoyote ile kwa mafisadi wenyewe kulifanya wabongo kuanza kupuuzia habari za kisiasa na matukio mbali mbali yanayoendelea nchini yanayohusu ufisadi.

Kuhusu kufundisha watu conspiracy theories hizo ni fikra zako binafsi ambazo ziwezi nikazinunua hilo nawaachia nyie wafusai wa zitto, mimi ninachojua ni kwamba alionesha nia ya dhati ya kulibadilisha taifa hili ikiwa pamoja na kulifanya kuwa hardworking nation na hiyo spirit tayari ilikuwa imeshaanza kumea.
Mkuu Magufuli alikuwa papa wa conspiracy theories, usikatae.

Unakumbuka hela za makinikia trilioni 400, kila mtanzania anapeleka ndinga aina ya Noah moja na mpunga wa ziada juu!!!

Ile ilikuwa nini mkuu kwa akili yako??? Unawaona watu kama mazoba ati??? Zitto jr yupo sahihi.

Peleka mahaba yako ya kidwanzi huko chato!!! Usitupigie kelele humu!!!
 
Kama ni teja nenda sober house, kama umelewa nenda kalale.
Mkuu kama walikuwa wanasiasa uchwara Magufuli alikuwa anawanunua kwa mpunga mrefu wa nini!!

Magufuli alikuwa mchafu kuliko nguruwe, Mkuu. Wewe endelea kumsafisha, sie twala bata Kizimkazi, Zanzibar!! 🤣🤣🤣🔊🎶🎵🎧
 
Kwani wanaoshindwa kujenga vitu kama hivyo hawakusanyi kodi toka kwenye vipato vyenu?
Mkuu nani kashindwa, kwani hiyo miradi anaijenga yeye sasa hivi??? Mbona unajitoa ufahamu kiajabu namna hii??!!
 
Jiwe ndiyo mtu wa hovyo kuliko wote waliowahi kupewa madaraka ya urais nchi hii:-
1. Alikuwa mporaji, mtekaji, muuaji na mpiga watu risasi.
2. Aliunda kundi la watu wasiojulikana lililokuwa linaua na kuteka watu.
3. Alikuwa muuaji wa uchumi wa nchi kwani alikuwa anapigana kufa kupona ili kuua sekta binafsi
4. Hivyo vidaraja unavyoviita flyover ni ushubwada tu ukilinganisha na mauaji ya watu
5. Alikuwa hapendi demokrasia. Alizima internet siku ya uchaguzi, aliwachukia wapinzani na upinzani na akawafukuza nchini wapinzani. Mshenzi sana yule.

Usinichoshe yanatosha kwa sasa
Wewe huna akili Tena mpumbavu. Leta ushaidi wa hata jambo Moja kati ya hayo uliyo Sema,,
 
Huyo mzee alikuwa jembe kweli kweli, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Alikuwa anafatilia miradi kwa umakini, na upigaji ulipungua kwa kiasi chake.
Mkuu unasema jembe, wakati wenzie waliotangulia walikuwa matrekta heavy duty, tena full four wheel!!!

Unatupigia makelele kuhusu jembe!!! Tena jembe la chuma chakavu, ndio utufanye tusilale, ebo! ama kweli dunia hii ina mambo acha nicheke, eti jembe!!! 🤣 🤣 🤣
 
Si bora JPm alijenga daraja ili kwa kutumia usimamizi mzuri wa Kodi zote...huyu wako mnaemshabikia kajimilikisha pesa zote anagawa na sasa kuna pesa inatoka inaitwa Goli la Mama...
Mkuu hakuna anayekubaliana na wazo kuwa Magufuli alijenga hiyo interchange kwa hela yake.

Kwa Mujibu wa rais samia Magufuli alificha hela kibao China, hapo kasimamia kodi yetu vizuri kivipi???

Mkuu unakumbuka kivuko cha kwenda Bagamoyo? Je, Magufuli alisimamia kodi yetu vizuri??? Unafiki sio mzuri.

Hakuna pia anayemsifia Samia kwa upuuzi wa namna hiyo, unakimbia hoja kwa kujificha kwenye maneno hayo!!!

Hapa nyeusi inaitwa nyeusi sio kijivu!!!
 
Mkuu acha kuruka mada, tulia hakuna mwenye vyeti Feki hapa.

Magufuli mwenyewe unayemhusudu alikuwa na cheti cha PhD Feki.

Tuliza mshono usirukeruke kama bisibisi Mkuu, jibu hoja hii.

Je, Magufuli kajenga interchange ya Ubungo kwa hela yake yaani mshahara wake au kwa mkopo wa world bank????
Tujikite kwenye utendaji.
 
Waliokua wameshindwa kujenga..Pesa hazikuwepo?. Kama zilikuwepo, kiliwashinda nn??

Kama hazikuwepo, Magufuli alitoa wapi??.
Kwani hao wengine walikaa madarakani bila ya kufanya chochote? Unataka kusema yote yaliyopo yalifanywa na JPM? Huyo JPM kuna mambo kibao katukosea sana.
Kama kiongozi anakera wananchi acheni asemwe, akitenda vizuri hilo ni sawa kwani ndio wajibu wake.
 
Nililia muda wote tangu alipotangazwa amefariki mpaka kuzikwa kwake, na hata leo ninaporudia kuangalia matukio ya msiba wake, wale wajeda na kina mama, wazee kwa vijana walivyokuwa wakishindwa kujizuia, huwa inanitoa machozi

Nilimkubali sana yule mzee, na hakika yangu, haijatokea kiongozi niliyewahi kumkubali na sijui kama atatokea tena kama yule mzee

Ila Mungu ni mwema, asikie kilio cha wote wanaonyanyasika na mabwanyeye ya CCM
Wewe inaonekana unapenda kulia
 
Umeandika upumbuvu tupu kama wewe ulivyo?

Ni lini umkubali mtu aliyekutoa ofisini kwa vyeti feki?
JPM alikuwa na mapungufu mengi tena yasiyokuwa na ulazima wowote ule. Na ni lazima pia akumbukwe kwa yale ya kipuuzi aliyofanya.
 
Kama
Niliona ni mtu wa maana ulivyochaguliwa kureview tafuti za AL, kumbe kuna maeneo unahitaji kupigwa brush ya maana. Serikali kujenga barabara, kuleta maji au kutoa huduma za afya ni jukumu lake la msingi. Serikali inatoza kodi kwa raia wake hivyo inapaswa kutumia fedha hizo kutoa huduma bora kwa wananchi.
Ile ilikuwa chai mkuu, hakuna kitu hapo, ni mjuaji mmoja wa Lumumba hapo. Mjanja mjanja na mtafuta fursa tu, sema ana vi exposure vya hapa na pale.
 

Usipite na gari lako Kijazi interchange.

Kwa wanao toka Mbezi kuelekea kariakoo na Posta pitia njia ya Goba au maji chumvi.

Fanya hivyo boss utakua na amani.

Tuache kudharau viongozi wetu tusitukane tuwaheshimu wote.

Kama unaona unakereka na uongozi wa kiongozi yeyote jenga hoja njoo na data kuliko kutukana viongozi njoo na data.

Humpendi lakini bado unajilazimisha kupita kwenye daraja alilosimamia. Huoni kama unajiumiza.
View attachment 3019558
Ujinga huu. Magufuli alikuwa rais ili ajifungie ikulu na kula raha? Alilazimishwa? Unajua kuna wengine ambao wangefanya makubwa zaidi ya haya lakini akawapora kura zao ili yeye awe rais?
 
Leo mtasema yote mnatuletea unafiki hapa. Sijawai kupewa pesa na mtu wala rushwa.
Linapokuja swala la kuusema ukweli lazima tuseme.
Kama humpendi kwanini unapita kwenye daraja alilosimamia huoni kama unaumiza moyo wako.
Kuna wakati unaonekana una akili na upeo mzuri. Kuna wakati unajitoa ufahamu unakuwa chawa. Kuna wakati unaonekana kama tapeli mtafuta fursa.
 
Mkuu nani kashindwa, kwani hiyo miradi anaijenga yeye sasa hivi??? Mbona unajitoa ufahamu kiajabu namna hii??!!
Unafikiri miradi mingine ingefanyika wakati huu endapo isinge anzishwa na JPM?
Kwa akili yako yenye ufahamu mkubwa umeshindwa kuona mradi wa umeme wa JNHP ingekuwa raisi wengine na kelele zile wangesita kuanzisha. Huyu aliyemalizia ni sababu hawezi kuachia Kati ipotee fedha bure.
SGR nayo ni vilevile, miradi mingi tu the list goes on ...
 
Leo ni leo mtasema yote mimi nipo tayari mnitukane ila msisahau kuweka like jamani.
 
Back
Top Bottom