Kama kweli Yesu aliteseka msalabani kwaajili yetu ili tusamehewe dhambi zetu, sisi tunatubu ili iweje?

Kama kweli Yesu aliteseka msalabani kwaajili yetu ili tusamehewe dhambi zetu, sisi tunatubu ili iweje?

Nawasalimu Salam ya wakati huu.

Kiukweli kabisa Mimi hili suala mpaka kesho sijawahi kulielewa,

Kama tunaambiwa kwamba dhambi zetu yesu alizimaliza msalabani sasa kwanini watu wanalia na kusaga meno kila siku wasamehewe dhambi zao?

Je, kuna makundi ya dhambi zilizosamehewa na ambazo bado ama?

Na kwanini kwenye kutubu lazima waanze kusema nisamehe Mimi mwenye dhambi?

Mwenye kunielewesha karibu sana.
Tabia ya Mungu au niseme utaratibu wa Mungu ni kwamba ukitenda dhambi lazima ufe, damu imwagike kabisa. zamani hizo wanadamu wakitenda dhambi ilitakiwa wamwage damu walau ya mnyama, kwa niaba ya dhambi ile waliyoitenda. meaning, ukitenda leo utamwaga damu na ile damu inahudu dhambi hiyo tu, haihusu dhambi utakazofanya keshokutwa au mwakani, hizo zitahitaji umwagaji damu wake. waisrael wamekuwa wakimwaga damu za kondoo, mbuzi, ng'ombe, na njiwa kwa namna hiyo kwa ajili ya upatanishi, ama la wao ndio wangekufa. mnyama unayetoa sadaka hiyo ya dhambi alitakiwa awe msafi, asiye na madoadoa wala uchafu wowote.

katika Agano Jipya, Mungu akaleta utaratibu mpya, ipatikane Damu ya mtu ambaye hana hatia kabisa yaani hajawahi kutenda dhambi, mtakatifu na msafi, ili afe kama sadaka ya kuchukua dhambi badala ya ng'ombe na mbuzi kuchinjwa kama sadaka. hakuna mwanadamu yeyote wa kawaida ambaye angeiweza hiyo kazi kwasababu wanadamu woote wana asili ya udhaifu wa dhambi, hata wale wanadamu waliopaa mbinguni kama kina Eliya, walishatendaga dhambi. hivyo, Mungu yeye mwenyewe akafanyika mwili (akaingia kwenye mwili wa mwanadamu ili auvae mwili huo kwa kuzaliwa kama mwanadamu), aishi kama mwanadamu, asitende dhambi yeyote, na asiwe na mbegu (sperm) ya mwanadamu ili Damu isiwe ya kibinadamu bali Damu ya Kimungu, aishi maisha ya kibinadamu, ashinde dhambi zote, halafu auawe kama kafara la dhambi za wanadamu wote. huyo ndiye Yesu Kristo aliyezaliwa pale Bethlehem.

kwa kifo chake, ukitenda dhambi, badala ya kuchinja ng'ombe, unatubu kwa kumwamini yeye, unasamehewa bila gharama yeyote nyingine, imani tu. wapo wachungaji manabii wa uongo wamejitokeza siku hizi wanasema kwasababu Yesu alikufa, hatutakiwi kutubu tena na watenda dhambi hawataenda motoni kwasababu Yesu aliichukua dhambi yetu yote. NO, ukitubu leo Yesu anakusamehe dhambi uliyotubu, ukitenda dhambi kesho baada ya kutubu, hiyo mpya haitasamehewa hadi utubu na kuacha, ama la utaenda nayo motono.

kwahiyo, kile kitendo chetu cha kutubu kwa specific dhambi, ni sawa na kwenda zizini na kuchagua mnyama wa kuchinja badala ya dhambi uliyoitenda. Yesu alichinjwa badala yako hivyo ukitubu kwa Jina lake, unasamehewa specific dhambi uliyotubu. hausamehewi zile utakazotenda kesho na keshokutwa, ndio maana kutubu kutakuwepo kila siku, unapaswa kujitakasa kila siku ukijua mwanadamu ana madhaifu kila iitwapo leo.

na sio dhambi tu, Yesu Kristo aliyachukua hata magonjwa yetu, aibu yetu na huzuni zetu. Isaya 52 na 53 inaeleza kwamba, jinsi alivyoishi awali, alikuwa mtu anayedhaniwa ni dhaifu, aliyedharauliwa hadi watu walitema mate wakimwona, alikuwa mtu wa huzuni nyingi mno na masikitiko, Yesu hakuishi maisha ya furaha. kwa kifupi, ili wale watakaomwamini waishi maisha ya furaha, yeye alibeba huzuni/aliishi maisha ya huzuni muda wote na masikitiko, aliposulibiwa aliumizwa mwili kwa mijeledi na kipigo ili kwa kupigwa kwake sisi tupone miili yetu isipate maumivu, hata tukipata anao uwezo kuyaondoa kwasababu aliyashinda na alilipa garama hiyo, alimwaga damu ili kwa Damu yake iwe kafara la dhambi za dunia nzima, meaning, yeyote ulimwenguni akija kwake kumwamini na kutubu, dhambi yake inalipika/inasameheka kwasababu alilipa deni la dhambi yeyote itakayofanywa na wanadamu wowote wale waliokuwepo na walioendelea kuzaliwa, deni lililipwa.

usijichanganye tunaposema Yesu alilipa deni, hii haimaanishi deni lilishalipwa hivyo tufanye tu dhambi hatutaadhibiwa kwasababu alilipa, NO, inamaanisha, ukifanya dhambi, badala ya kugarimia ng'ombe au kondoo, yeye alishamwaga Damu yake badala ya mang'ombe na makondoo, atakusafidha dhambi yako (ile tu unayotubu sio zile za kesho na keshokutwa hizo zitahitaji kutubu kupya).

na hakuna njia nyingine ya kusamehewa dhambi, wanadamu wote wasiopitia njia hii wataenda motoni moja kwa moja, meaning, waislam,wabudha na kadhalika wote imani yao haitawaokoa, ni watu wa motoni.
 
Nafsi yake ndiyo Mungu ndani ya mwili wa mwanadamu...kilicho sulibiwa ni mwili...(mwana wa adamu) na kilicho kufa na kufufuka siku ya 3 ni mwili siyo nafsi yake ...kumbuka msalabani anamwabia yule mtu kuwa leo hii utakuwa pamoja nami pema peponi...maana nafsi yake ndiyo mungu na mungu awezi kufa hata sekunde moja..hivyo nafsi ya mungu ilitwaa mwili wa mwanadamu husio na nafsi ya mwanadamu ili kujitoa sadaka kwa nafsi yake mwenyewe.
Kwa maneno mengine ni kwamba alikua anafanya maigizo?
 
Umaana na umuhimu wa kuungama na kutubu dhambi zetu umetokana na ukweli huo haswa kwamba Kristu alikufa msalabani.

Bila tukio la Kalvari, hata mwanadamu angelia machozi na kujigaragaza majivuni akiyaomboleza maovu yake, bado angeonekana mwenye hatia ileile mbele ya Mungu.

Hii ndiyo kusema kwamba Yesu alikufa ili kutununulia muda na uwezekano mwingine wa kutubu na kufanyika upya watoto watiifu wa Mungu.

Na haya yote hayatokei kwa juhudi zetu tu, bali nguvu za Mungu hushirikiana na nafsi yenye utashi ili kumwongoza hatua kwa hatua kutoka kwenye umateka na mitego ya Ibilisi hadi kwenye jukwaa la uhuru na uzima wa milele.

Msalabani Kalvari ndipo mahali makhususi ambapo mwanadamu anaweza kutambua lengo kamili la uumbaji na thamani yake kwa kuzingatia umbali ambao Mungu yuko radhi kwenda ili kumrejesha Kwake.
Mbona unanichanganya KRISTU au KRISTO yupi ni yupi?
 
Kutubu dhambi tunapokosea Kwa sisi Wakatoriki Huwa ni inaonesha kuwa umemkubali na kumpokea Yesu Kristo ili awe bwana na mwokozi wa maisha yetu.
Kwa hyo ili Yesu aweze kuzibeba zambi zako lazima umkubali kwanza kuwa bwana na mwokozi wako,hapo ndo atabeba dhambi zako
VP kuhusu Kwa wasabato na wengine ?
 
Hahahahah, ilinitokea Mimi Kuna magroup Facebook nilifuatilia yanahusu mambo ya kukosoa Mambo ya Mungu nikaamua niondoke nilianza kuhisi kupotea hivi na nikaona kama naanza kuhama reli. Nikablock makundi yote.

Mfano alihoji kwa ukubwa wa Safina aliyotengeneza Nuhu na vitu vilivyoingia ndani ni haiwezekani pamoja na stock ya chakula Chao. Maana Dunia ina Species milioni 6 na, Sasa piga Wawili Wawili na chakula Chao, zingatia Hali ya hewa na habitats zao, je waliishije na walitoshaje humo?

Pia akadai kwamba Kijiografia uMvua haiwei kunyesha ikagharikisha sehemu zote za Ardhi ya Dunia.

Ila ninavyoona Mimi hivi vitu ni Imani na ni unquestionable wewe amini Kisichowezekana kwa Binadamu kwa Mungu Kinawezekana.
Tatizo kila viashiria vipo vya Mungu hayupo vipo na vya Mungu yupo vipo
 
Tabia ya Mungu au niseme utaratibu wa Mungu ni kwamba ukitenda dhambi lazima ufe, damu imwagike kabisa. zamani hizo wanadamu wakitenda dhambi ilitakiwa wamwage damu walau ya mnyama, kwa niaba ya dhambi ile waliyoitenda. meaning, ukitenda leo utamwaga damu na ile damu inahudu dhambi hiyo tu, haihusu dhambi utakazofanya keshokutwa au mwakani, hizo zitahitaji umwagaji damu wake. waisrael wamekuwa wakimwaga damu za kondoo, mbuzi, ng'ombe, na njiwa kwa namna hiyo kwa ajili ya upatanishi, ama la wao ndio wangekufa. mnyama unayetoa sadaka hiyo ya dhambi alitakiwa awe msafi, asiye na madoadoa wala uchafu wowote.

katika Agano Jipya, Mungu akaleta utaratibu mpya, ipatikane Damu ya mtu ambaye hana hatia kabisa yaani hajawahi kutenda dhambi, mtakatifu na msafi, ili afe kama sadaka ya kuchukua dhambi badala ya ng'ombe na mbuzi kuchinjwa kama sadaka. hakuna mwanadamu yeyote wa kawaida ambaye angeiweza hiyo kazi kwasababu wanadamu woote wana asili ya udhaifu wa dhambi, hata wale wanadamu waliopaa mbinguni kama kina Eliya, walishatendaga dhambi. hivyo, Mungu yeye mwenyewe akafanyika mwili (akaingia kwenye mwili wa mwanadamu ili auvae mwili huo kwa kuzaliwa kama mwanadamu), aishi kama mwanadamu, asitende dhambi yeyote, na asiwe na mbegu (sperm) ya mwanadamu ili Damu isiwe ya kibinadamu bali Damu ya Kimungu, aishi maisha ya kibinadamu, ashinde dhambi zote, halafu auawe kama kafara la dhambi za wanadamu wote. huyo ndiye Yesu Kristo aliyezaliwa pale Bethlehem.

kwa kifo chake, ukitenda dhambi, badala ya kuchinja ng'ombe, unatubu kwa kumwamini yeye, unasamehewa bila gharama yeyote nyingine, imani tu. wapo wachungaji manabii wa uongo wamejitokeza siku hizi wanasema kwasababu Yesu alikufa, hatutakiwi kutubu tena na watenda dhambi hawataenda motoni kwasababu Yesu aliichukua dhambi yetu yote. NO, ukitubu leo Yesu anakusamehe dhambi uliyotubu, ukitenda dhambi kesho baada ya kutubu, hiyo mpya haitasamehewa hadi utubu na kuacha, ama la utaenda nayo motono.

kwahiyo, kile kitendo chetu cha kutubu kwa specific dhambi, ni sawa na kwenda zizini na kuchagua mnyama wa kuchinja badala ya dhambi uliyoitenda. Yesu alichinjwa badala yako hivyo ukitubu kwa Jina lake, unasamehewa specific dhambi uliyotubu. hausamehewi zile utakazotenda kesho na keshokutwa, ndio maana kutubu kutakuwepo kila siku, unapaswa kujitakasa kila siku ukijua mwanadamu ana madhaifu kila iitwapo leo.

na sio dhambi tu, Yesu Kristo aliyachukua hata magonjwa yetu, aibu yetu na huzuni zetu. Isaya 52 na 53 inaeleza kwamba, jinsi alivyoishi awali, alikuwa mtu anayedhaniwa ni dhaifu, aliyedharauliwa hadi watu walitema mate wakimwona, alikuwa mtu wa huzuni nyingi mno na masikitiko, Yesu hakuishi maisha ya furaha. kwa kifupi, ili wale watakaomwamini waishi maisha ya furaha, yeye alibeba huzuni/aliishi maisha ya huzuni muda wote na masikitiko, aliposulibiwa aliumizwa mwili kwa mijeledi na kipigo ili kwa kupigwa kwake sisi tupone miili yetu isipate maumivu, hata tukipata anao uwezo kuyaondoa kwasababu aliyashinda na alilipa garama hiyo, alimwaga damu ili kwa Damu yake iwe kafara la dhambi za dunia nzima, meaning, yeyote ulimwenguni akija kwake kumwamini na kutubu, dhambi yake inalipika/inasameheka kwasababu alilipa deni la dhambi yeyote itakayofanywa na wanadamu wowote wale waliokuwepo na walioendelea kuzaliwa, deni lililipwa.

usijichanganye tunaposema Yesu alilipa deni, hii haimaanishi deni lilishalipwa hivyo tufanye tu dhambi hatutaadhibiwa kwasababu alilipa, NO, inamaanisha, ukifanya dhambi, badala ya kugarimia ng'ombe au kondoo, yeye alishamwaga Damu yake badala ya mang'ombe na makondoo, atakusafidha dhambi yako (ile tu unayotubu sio zile za kesho na keshokutwa hizo zitahitaji kutubu kupya).

na hakuna njia nyingine ya kusamehewa dhambi, wanadamu wote wasiopitia njia hii wataenda motoni moja kwa moja, meaning, waislam,wabudha na kadhalika wote imani yao haitawaokoa, ni watu wa motoni.
Kuna mambo hayaingii akilini;

1. Kwamba Mungu alieumba dunia yote na vyote vilivyomo, ili akusamehe dhambi alihitaji damu ya ng'ombe, mbuzi nk la sivyo unakufa! Hii ina tofauti gani na ibada za mizimu walizokua wanafanya babu zetu???

2. Kwa maelezo yako, hakuna mwanadamu yeyote wa kawaida ambaye angeiweza hiyo kazi kwasababu wanadamu woote wana asili ya udhaifu wa dhambi. Kama wanadamu wote tumerithi dhambi kwa KUZALIWA na mwanadamu, iweje YESU nae azaliwe na mwanadamu yuleyule alierithi dhambi? Hii haimfanyi nayeye kurithi hiyo dhambi?

3. Hili suala la kwamba MUNGU alilazimika kujifanya mwanadamu, akateswa, akafa, akafufuka, ili MUNGU huyo huyo aweze kutusamehe dhambi tulizotenda KWAKE, ni kizungumkuti!

4. Umesema YESU alichukua sio tu dhambi zetu, bali na magonjwa yetu. Sasa kama ni hivyo mbona bado tuna magonjwa na tunatakiwa kutubu dhambi. Ina maana YESU alikufa kwa ajili gani..? Yaani maisha ya mwanadamu wa kabla ya YESU na baada ya YESU yamebadilika vipi kutokana na ujio wake, kama kila kitu kipo vile vile??
 
Ukiweza kujijibu hili swala utakua umeelewa pakubwa sana..

Dhambi ziliumbwa na nani?
 
Mimi ninavyoona haya mambo ya Mungu sisi wanadamu tunayajua kwa umbali sana sana yaani ni kama kipunje Cha ulezi ndo tunajua. Ila Kuna Mambo makubwa sana Kuhusu Mungu hatuyajui bado. Sasa hapa Kikubwa Wacha tuamini kwenye kakiwango hako hako kama kapunje ka ulezi. Mengine tutayajua Yesu akija au tukienda kukutana nae tutamuuliza maswali naamini atatujibu na atatuonesha Shetani na pia tutapata Fursa ya kumuuliza Shetani maswali chini ya usimamizi wa Yesu mwenyewe.
 
Huo ni mchongo tu ndio maana Wayahudi wenye akili mpaka leo hawaamini. Ila waliochonga nafikiri walitumia ulimwengu wa roho.
 
Mimi ninavyoona haya mambo ya Mungu sisi wanadamu tunayajua kwa umbali sana sana yaani ni kama kipunje Cha ulezi ndo tunajua. Ila Kuna Mambo makubwa sana Kuhusu Mungu hatuyajui bado. Sasa hapa Kikubwa Wacha tuamini kwenye kakiwango hako hako kama kapunje ka ulezi. Mengine tutayajua Yesu akija au tukienda kukutana nae tutamuuliza maswali naamini atatujibu na atatuonesha Shetani na pia tutapata Fursa ya kumuuliza Shetani maswali chini ya usimamizi wa Yesu mwenyewe.
Inawezekana pia hatuyajui kabisa, hata hicho tunachodhani tunajua huenda hatujui na hatujui kama hatujui.
 
Aliweka upatanisho, nafasi ya kupata msamaha. Vinginevyo ilikuwa "One mistake, one goal"
 
Mi naona hao Wanafunzi wa Yesu na Mitume wengine kama Muhammad, hawakututendea haki, walipaswa kuuliza maswali magumu kabisa yanayohusu Mungu na uumbaji. Walipaswa kuuliza maswali mengi kabisa mpaka kusiwepo na Mashaka yoyote. Anagalau Musa aliwahi kuuliza kinachoaminika kuwa Mungu kwamba kwani wewe ni Nani? Akasema "Mimi Niko ambaye Niko" "I am who I am"
 
Nawasalimu Salam ya wakati huu.

Kiukweli kabisa Mimi hili suala mpaka kesho sijawahi kulielewa,

Kama tunaambiwa kwamba dhambi zetu yesu alizimaliza msalabani sasa kwanini watu wanalia na kusaga meno kila siku wasamehewe dhambi zao?

Je, kuna makundi ya dhambi zilizosamehewa na ambazo bado ama?

Na kwanini kwenye kutubu lazima waanze kusema nisamehe Mimi mwenye dhambi?

Mwenye kunielewesha karibu sana.

Kama Baba yako ananunua maji ya kunywa kwa gharama zake na kuweka kwenye fridge, kwa nini ni lazima uchote na unywe? Ina maana akishanunua tu kiu yako inaisha!
 
Mi naona hao Wanafunzi wa Yesu na Mitume wengine kama Muhammad, hawakututendea haki, walipaswa kuuliza maswali magumu kabisa yanayohusu Mungu na uumbaji. Walipaswa kuuliza maswali mengi kabisa mpaka kusiwepo na Mashaka yoyote. Anagalau Musa aliwahi kuuliza kinachoaminika kuwa Mungu kwamba kwani wewe ni Nani? Akasema "Mimi Niko ambaye Niko" "I am who I am"

Mbona mtume Muhammad aliuliza maswali Magumu na Mungu akajibu

Alitaka kujua kama kweli Yesu alisurubiwa na alikufa Mungu akajibu

Quran 4:157
- Na kwa kusema kwao: Sisi tumemuuwa Masihi Isa, mwana wa Maryamu, Mtume wa Mwenyezi Mungu - nao hawakumuuwa wala hawakumsalibu, bali walifananishiwa tu. Na hakika walio khitalifiana katika haya wamo katika shaka nayo. Wao hawana ujuzi nayo wowote, ila ni kufuata dhana tu. Wala hawakumuuwa kwa yakini.
 
Kanuni ilikuwa kwamba MSHAHARA WA DHAMBI NI MAUTI.

Ndio maana wakati wa torati ya Musa, kulikua na sadaka za kuchinja ili kusamehewa dhambi.

Tendo la Kifo cha Yesu ilikua ni kuondoa ile kanuni ya Kifo kwa wanadamu wanapotenda dhambi.

Hivyo kwasasa ukitenda dhambi, badala ya kufa, kile kifo cha Yesu kinafidia hapo, na badala ya kutoa sadaka za kuchinja, Damu ya Yesu isiyo expire, damu ya thamani, inatosha kabisa kutumika kukutasa.

Kuhusu Yesu Kuwa Mungu hili ni jambo hata mimi kama mkristo nalifanyia utafiti kwa kujifunza. Japo maelezo mengi yanakuacha na maswali.

Wengine husema kwakua Mungu ni Roho ili aje ulimwenguni na kufanya hilo zoezi (kusulubiwa,kufa msalabani na kufufuka) ilibidi apitie mchakato wa kuwa na mwili wa damu na nyama (kuzaliwa)...

ukisema Mungu wako hawezi kufanya hivyo, bhasi tayari huyo sio Mungu. Kwani sifa ya Mungu ni KUWEZA YOTE.

Na ukikubali Yesu ni Mungu, Je kwanini alikua akimuomba Baba wa Mbinguni? Ukisema utatu mtakatifu, Biblia haijawahi andika neno utatu mtakatifu Mwanzo mpaka ufunuo hilo neno halipo.

Je Mimi naamini nini?
Naamini Yesu ni Mwana wa Mungu ( haina maana Mungu alizaa, bali ni cheo tu kuonyesha ukaribu wa Mungu na Yesu).

Naamini Yesu alikuja duniani kwa kazi ya kuleta msamaha wa dhambi kwa njia nyepesi zaidi na yenye upendo, na si hasira kama gharika au moto wakati wa sodoma.

Ndio maana mpaka leo, Hakuna Jina Lenye Mamlaka Ya Kiroho kama jina la Yesu. Kwa lugha yoyote inayotumika ilimradi unamaanisha YESU KRISTO, kuna nguvu, mapepo, majini, wachawi, mizimu vyote vinasalimu.

Sihitaji mafuta wala chumvi kushughulikia kazi za giza, nikijua kulitumia Jina la Yesu tu. Am Untouchable.

Ukimuona Muislamu Yoyote anamdhihaki Yesu bhasi jua huyo ni muislamu asie isoma Quran vema, kwani Yesu ambae wao wanamuita nabii Issa Ameandikwa kwa heshima kubwa katika Quran.

Hilo tu linatosha kujua YESU hakua wa kawaida kawaida.


Yesu alieandikwa kwenye Biblia matukio yake ni ya kweli na hakika, kwani timeline yake, imethibitika kupitia nyakati za watawala waliokuwepo wakati huo, ushahidi wa kaburi kuonyesha alikuwepo kweli, na historia za kawaida za wakati huo.

Ushahidi unaomthibitisha Yesu na maisha yake ni mkubwa sana, kuliko unaopindisha.

Asante.
 
Hizo ni story tu za kuibia wajinga!
 
Back
Top Bottom