Kama mlikuwa hamjui: CCM imeliongoza hili Taifa kwa uongo tangu ikiwa TANU hadi sasa.

Kama mlikuwa hamjui: CCM imeliongoza hili Taifa kwa uongo tangu ikiwa TANU hadi sasa.

Mkuuuu umechelewa mpaka tumeshibishwa matango pori ya kutosha? Sas mkuu vijana wa kileo tuanzie wapi? Maana Hoja zako ni rafiki kwa mustakabali wa vizazi vijavyo! Nimeshiba Sana kwa sauti yako ya maandishi
 
Tulia soma uelewe ndo utoe maoni yako. Mada inasema kuhusu CCM kuongoza hili Taifa kwa kutumia uongo. Na hili limeanzia tangu kipindi cha TANU.
Nini kinachokufanya unione kuwa sielewi ninacho kisoama hadi unihimize?
Mada ni mbovu kwa kujumuisha kijumlajumla kama ulivyo fanya.

Inawezekana hujui maana ya "kusema uongo"; lakini unajisikia kuwa mtaalam wa kutufundisha hayo unayo dhani wewe tuyaone yote kuwa ni uongo!
 
Nini kinachokufanya unione kuwa sielewi ninacho kisoama hadi unihimize?
Mada ni mbovu kwa kujumuisha kijumlajumla kama ulivyo fanya.

Inawezekana hujui maana ya "kusema uongo"; lakini unajisikia kuwa mtaalam wa kutufundisha hayo unayo dhani wewe tuyaone yote kuwa ni uongo!
Sasa kama mada ni mbovu kwa nini umepoteza muda wako kuja kusoma na ku comment kwenye mada mbovu? Au ndo sindano imegusa mfupa?
 
Tena kuna wakati wakatoa taarifa kuwa watu wanaiba miundombinu kumbe ukweli ni kwamba kulikuwa na shida ya umeme kwenye njia zao kulikotokana na kutoweka umeme wa kutosha kwenye njia na ku u balance vizuri kwenye njia zao.
Noma sana!
 
Tulia soma uelewe ndo utoe maoni yako. Mada inasema kuhusu CCM kuongoza hili Taifa kwa kutumia uongo. Na hili limeanzia tangu kipindi cha TANU.
Mada ni mbovu, usitake kulazimisha kitu kibovu kiwe bora.
Nani ataamini kuwa CCM ya viongozi laghai kama hawa waliopo sasa ni ile ile ya wakati ilipo anzishwa; au hata TANU iliyo ongoza juhudi za kupata uhuru!
Unapo andika kwa mihemkohemko bila ya kuweka tafakuri kwenye hoja unazo andika, wasomaji wataona kuwa huna umakini wowote.
Na udhaifu huu unajionyesha wazi katika maandishi yako toka enzi zile ulipokuwa umekomalia mfumo wa ubepari.
Inaonyesha akili yako ni "one track", inaposhikilia jambo; basi haina muda wa 'moderation' kwenye jambo hilo.
 
Au ndo sindano imegusa mfupa?
Unaelewa maana ya "sindano kugusa mfupa", lakini?

Sindano ikigusa mfupa kuna athari zipi unazozijuwa wewe?
Ni mwendelezo wa yaleyale niliyo kueleza toka mwanzo, enzi zile ukiimba nyimbo za "ubepari" humu JF.
Unayo tabia ya ku'exagerate' kwa kila jambo unalo lisemea. Sasa unajigaragaza kabisa juu ya "uongo" wakati wa TANU!
 
Mada ni mbovu, usitake kulazimisha kitu kibovu kiwe bora.
Nani ataamini kuwa CCM ya viongozi laghai kama hawa waliopo sasa ni ile ile ya wakati ilipo anzishwa; au hata TANU iliyo ongoza juhudi za kupata uhuru!
Unapo andika kwa mihemkohemko bila ya kuweka tafakuri kwenye hoja unazo andika, wasomaji wataona kuwa huna umakini wowote.
Na udhaifu huu unajionyesha wazi katika maandishi yako toka enzi zile ulipokuwa umekomalia mfumo wa ubepari.
Inaonyesha akili yako ni "one track", inaposhikilia jambo; basi haina muda wa 'moderation' kwenye jambo hilo.
Hoja upingwa kwa hoja. Ni vizuri kuonesha lipi lililosemwa hapo ni uongo?

CCM ilizaliwa mwaka 1977, na before kikikuwepo TANU. Sasa ni vizuri ukasema huo uongo hapo ulikuwa unaenezwa na kina nani ambao hawakuwa TANU!

Punguza obsession kijana!
 
Punguza obsession kijana!
Naona hujifunzi kitu. Ninakueleza lakini huwezi kuelewa. Kila unacho andika humu unatunga tu kichwani mwako, kama ulivyo tunga huo mstari hapo juu. Huo u-"kijana" umeutoa wapi?
Hiyo 'obsession' ni ya jambo gani? Ninapo sema wewe unayo 'obsession' ya ku-'exagerate' kwenye kila jambo unalolijengea hoja, bado huoni ukweli huo?
 
Naona hujifunzi kitu. Ninakueleza lakini huwezi kuelewa. Kila unacho andika humu unatunga tu kichwani mwako, kama ulivyo tunga huo mstari hapo juu. Huo u-"kijana" umeutoa wapi?
Hiyo 'obsession' ni ya jambo gani? Ninapo sema wewe unayo 'obsession' ya ku-'exagerate' kwenye kila jambo unalolijengea hoja, bado huoni ukweli huo?
Jifunze kujibu hoja kwa hoja. Unachokifanya hapa ni kupiga mdomo tu bila facts.

Great thinker anapinga hoja kwa kutoa hoja. Wengine wanafanya kama unavyofanya wewe! Maneno matupu!
 
Hoja
Jifunze kujibu hoja kwa hoja. Unachokifanya hapa ni kupiga mdomo tu bila facts.

Great thinker anapinga hoja kwa kutoa hoja. Wengine wanafanya kama unavyofanya wewe! Maneno matupu!
Hoja zipi?
Hivi kwa nini hutaki kuelewa?
Hivi unajichukulia hapa wewe kuwa "Great Thinker" kwa kuleta mada za aina hii humu?
 
Endelea kupiga mdomo ndugu.
'Factually', "sipigi mdomo", natumia vidole!
Naona kupindisha mambo ni tabia yako ya kudumu; kama hivyo unavyo dai humu kuwa CCM ya Samia, yenye ulaghai mwingi ni CCM ileile ya Mwalimu Nyerere na TANU ya enzi zile!
 
'Factually', "sipigi mdomo", natumia vidole!
Naona kupindisha mambo ni tabia yako ya kudumu; kama hivyo unavyo dai humu kuwa CCM ya Samia, yenye ulaghai mwingi ni CCM ileile ya Mwalimu Nyerere na TANU ya enzi zile!
Toa hoja zako ninapindisha kivipi? Toa hoja zako mambo niliyosema humu ni ya uongo au yamepindishwa kwa namna gani?
 
Toa hoja zako ninapindisha kivipi? Toa hoja zako mambo niliyosema humu ni ya uongo au yamepindishwa kwa namna gani?
Unapotoa maelezo kijumla jumla kama ulivyo fanya kwenye mada yako hii; ukaifananisha CCM ya ulaghai iliyopo sasa na CCM ya miaka ya 80, au TANU; halafu unajihisi umetoa hoja zinazotakiwa kujibiwa? Seriously, unaona hoja hapo ya kujibiwa?
 
Kofia na t-shirt zinatuponza!Ndio maana mdau mmoja humu alianzisha mada Moja,ili sm iondoke,watu waliozaliwa miaka ya 1960_1977,Wanatakiwa waondoke ili kizazi kipya kitawale,ila alituonea sio wote wenye mawazo ya kiesm!
Mwashambwa tatlaan sozani kama ni WA miaka ya sabini huko Hawa ni uchawa TU unawasumbua
 
Unapotoa maelezo kijumla jumla kama ulivyo fanya kwenye mada yako hii; ukaifananisha CCM ya ulaghai iliyopo sasa na CCM ya miaka ya 80, au TANU; halafu unajihisi umetoa hoja zinazotakiwa kujibiwa? Seriously, unaona hoja hapo ya kujibiwa?
Kwa hiyo hizi ndo hoja zako?

Kakojoe tu ukalale! Huu uzi umekuzidi sana uwezo!
 
Ni vile tu Watanzania wengi ni wajinga na sio wasomaji sana wa vitabu na wafuatiliaji wa masuala ya nchi yao.

Mlioshtuka leo kuhusu habari ya Tanzania kununua umeme nje kwa ajili ya matumizi ya mikoa ya Kaskazini wakati Serikali imekuwa ikijisifu kuzalisha umeme kuzidi matumizi yetu nawashangaa sana.

Kwa wale msiofahamu hakuna Chama cha siasa Afrika hii na nadhani duniani kinachoishi kwa uongo kama CCM. Na uongo wa CCM haujaanza leo, ulianza tangu ikiwa TANU na uliasisiwa na aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Tanganyika na Tanzania , Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Vitabu vya dini vinasema Shetani ni Baba wa Uongo ila kwa hapa Tanzania, baba wa uongo ni CCM.

Yafuatayo ni maeneo ambayo TANU na CCM waliwadanganya/Wamewadanganya Watanzania na wao wakaamini.

1. Suala la Oscar Kambona kutangazwa kuwa mhaini na ameolewa Uingereza. Jambo hili lilitangazwa na Serikali ya Nyerere mwaka 1967 baada ya Kambona kuamua kujiuzuru nafasi zote za Uongozi ndani ya Serikali na Chama baada ya kupingana na Nyerere kuhusu sera za Ujamaa. Watanzania kama mazuzu tuliamini huu uongo wa Nyerere na hadi tukatungishwa nyimbo mashuleni kuwa kambona Kaolewa Uingereza. Huu ulikuwa uongo wa Nyerere ili kuwarubuni Watanzania na kuwa label vibaya wanaompinga.

2. Suala la Nyerere kung'atuka kutangazwa ni kwa sababu eti ni Kiongozi mzuri na hataki kung'ang'ania madaraka. Mwaka 1985 CCM walitangaza na kueneza uongo unaoaminika hadi leo kuwa Nyerere aling'atuka kwa sababu hakuwa na tamaa ya madaraka wakati kiukweli kilichomkimbiza Nyerere ikulu ni mfululizo wa majaribio ya mapinduzi dhidi yake hasa ya mwaka 1981/1982 na lile la kutekwa kwa ndege ya ATCL kutokana na kushinikiza aondoke madarakani kwa sababu ya hali mbaya ya kimaisha/ kiuchumi iliyotokana na kufeli kwa sera zake za ujamaa.

3. Suala la kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 kuwa ni busara za Nyerere wakati ukweli ni kwamba baada ya kuanguka kwa Shirikisho la Kikokumunisti (USSR) nchi zote zilizokuwa zinaitegemea Urusi ziliamua kuchukua sera zinazofanana na za kimagharibi ili kuendelea kupata misaada kutoka Mataifa ya Magharibi.

4. Suala la Nyerere kuwa alikuwa kiongozi bora na hakuwa dikteta wakati kiuhalisia hakuna Kiongozi aliyekuwa dikteta nchi hii kama Mwalimu Nyerere. Kipindi cha Uongozi wake ndipo Watanzania wengi waliotofautiana nae kimawazo kama kina Bibi Titi Mohamed na Oscar Kambona walifunguliwa kesi za Uhaini na wengine wengi kuwekwa vizuizini chini ya Sheria ya kuweka watu kizuizini. Waliopona wachache walikimbia nje ya nchi na kurudi baada ya Nyerere kuondoka madarakani.

5. Suala la vita vya Uganda kuwa ilitokana na Iddi Amini kutaka kuuchukua mkoa wa Kagera wakati ukweli ni kwamba ugomvi wa Iddi Amini na Nyerere ulitokana na Nyerere kumpa hifadhi Obote aliyepinduliwa na Iddi Amini. Amini aliamini vikundi vinavyompinga ambavyo vingi vilikuwa vinashambulia Uganda kutokea Mkoa wa Kagera nchini Tanzania vinakuwa supported na Nyerere hivyo kuanza kuleta chokochoko mpakani na kuivamia Tanzania.

6. Suala la Corona kutokuwepo Tanzania kipindi cha awamu ya 5 (mwaka 2020/21) wakati kipindi hicho maelfu kama sio mamia ya watanzania walikuwa wanakufa kwenye hospitali zetu kwa ugonjwa wa Corona.

Kutokana na mifano hii michache, napenda kuwaambia Watanzania, CCM hawajawahi kuongoza hii nchi kwa ukweli. Kama wanashangaa leo kuambiwa tutanunua umeme Ethiopia wakati waliambiwa tunazalisha umeme unaozidi matumizi yetu basi watakuwa hawaijui CCM vizuri.

Ukweli uliopo kwenye suala la umeme ni kwamba matumizi yetu yanazidi kuongezeka kila kukicha hivyo hata huo Umeme wa Bwawa la Nyerere hautoshi. Pia pamoja na kuanza kazi kwa Bwawa la Nyerere, mabwawa mengine yanazidi kupunguza uzalishaji kila siku kutokana na kujaa matope na mabadiliko ya tabia nchi yaliyopunguza uwezo wa mabwawa hayo kuzalisha umeme kwa kiwango kinachopaswa. Ila ukweli huu kamwe Watanzania hamtaambiwa mtaletewa uongo wa kila na post za watu mbalimbali kutengeneza hoja uchwara kuutetea huo Uongo (Spinning)

Ikitokea CCM ikaanguka kwenye taifa letu jambo la kwanza watakalotakiwa kulifanya Viongozi wapya wa Tanzania ni kufanya maombi ya toba kwa Taifa kutokana na nchi hii kuendeshwa kwa uongo kwa miongo mingi sana.

Lord denning.
Mpaka vitukuu vyako hilo halitatokea, kwa mbadala upi.
 
Back
Top Bottom