Kama Mtanzania wa kawaida, naomba kujua umuhimu wa hizi safari

Kama Mtanzania wa kawaida, naomba kujua umuhimu wa hizi safari

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Makamu wa Rais yuko Marekani kuhudhuria mkutano, Rais yuko Uingereza kwenye msiba.

Kuna mawaziri wako nje ya nchi kwa ziara mbalimbali. Mambo haya ni tofauti na awamu iliyopita.

Natamani kufahamu umuhimu wa hizi safari hasa hii ya makamu wa rais. Ikiwa baadhi ya marais wako msibani kuhudhuria mazishi ya Malkia Elizabeth II, akiwemo Rais wa nchi hii:

Je, kwa nini Rais asingeunganisha safari au kutoa hotuba kwa njia ya video comference kama alivyofanya Museveni kwa mkutano uliopita ili kupunguza gharama?

Hii mikutano na ziara zina tija?
Kama zina tija kwa nini tuendelee kukatwa tozo?

Tozo ni wizi!
Screenshot_20220919-173008.jpg
 
Viongozi nao ni wanadamu na wengine ni Globe trotters wanapenda kusafiri
 
Kwahiyo hata kwenye mikutano ya umoja wa mataifa "tusiende" ?

Hii nchi ina wananchi wanyanyasaji sijawahi kuona. 🚮 🚮
 
Mama amezidi jamaniiii ata kama . wewe kila siku yupo kwenye show..
 
Tozo zipo na kwa sasa karibia kila tasisi itataka kodi ya mapato, kila mkuu wa hiyo taasisi ataweza kutumia hizo tozo kadri awezavyo, kikosi cha zimamoto kiko mtaani kinadai kodi ya mapato kwa kila mfanyabiashara.
 
Mwisho wa siku wamewachoka wanawapandisha school bus😂
 
Back
Top Bottom