Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mwezi haundami mara mbili ni mara mojaMwezi ni mmoja Muandamo tofauti
Nikurekebishe kidogo. Funga/Fungua kwa uonekanapo mwezi sio kuona mwezi. We ulipoanza kufunga uliuona?Imeamdikwa funga na fungua uonapo mwezi, sio fungua ukisikia muandamo wa mwezi. Full stop
Eid yetu Allha Akbar
TakibiruuOMAN, wao majirani kabisa wa Saudi Arabia wao Eid yao iko Jumamosi, India, Indonesia, Iraq, Iran nako huko ni Jmosi.
Nchi nyingi Eid ni Jmosi na sio Leo hii IJUMAA
Watu wanasema mambo ambayo hawayaelewi. Uislamu ni dini ya kanuni na kanuni zake ni kitabu Qur'an na Sunna yaani mwenendo wa mtume. Hakuna kufuata nchi hata kama ni saudia. Ikiwa wanachokifanya ni tofauti na kitabu na sunna basi tunafuata kanuni sio nchi.Ila mnamatatizo nyie watu, kabla ya kuwepo kwa simu na internet mlikuwa mnajuaje mambo ya mwezi kuonekana Kenya ili mjue kwamba ni Eid
Suni wao hula Eid el Fitr siku moja kabla, hali kadhalika huanza kufunga mfungo wa Ramadhani siku moja kabla ya hao wengine.Kwahiyo hizo nchi nyingine za Sunni nao hawali Iddy kesho?
Katika uislam suala la mwezi mwandamo lina hitilafu. Wanazuoni wanatofautiana rai katika kutafsiri mwezi muandamo. Wapo wanaosema ukionekana popote duniani kwa sababu ya utandawazi na mawasiliano basi imetihibiti wanauita mwezi wa kimataifa. Na wapo wanaosema sunna ni kuona wenyewe katika mamlaka ya eneo lenu.Umesoma Maelezo wanakula eid kulingana na muonekano wa mwezi
Na hiyo hitilafu inaanzia katika kutafsiri neno la kiarabu "suumu li ru'uuyatihi..." kuna wanaotafsiri kuwa ni " fungeni kwa kuonekana ..." na kuna wanaotafsiri kuwa ni "... fungeni kwa kuuona.."Umesoma Maelezo wanakula eid kulingana na muonekano wa mwezi
Na hiyo hitilafu inaanzia katika kutafsiri neno la kiarabu "suumu li ru'uuyatihi..." kuna wanaotafsiri kuwa ni " fungeni kwa kuonekana ..." na kuna wanaotafsiri kuwa ni "... fungeni kwa kuuona.."
Hapa wataalamu wabobevu a lugha wanafunua vitabu lukuki hoja na dalili.. kiasi kwamba msikilizaji kama sio alimu unaishia kuchanganyikiwa....
Mantiki rahisi kabisa ni kufuata mtume alifanyaje basi. Na ukifanya hivyo utaona ni sahihi kila nchi na mwandamo wake..
Na mwandamo ulizingatia uwepo vizjizi vya kutoweza kuuona mwezi basi hapo mnahesabu ikifika siku 30. Mmekamilisha. Allahu atuongoze katika njia sahihi.
Ccm na andazi,nachagua andaziNa wewe usiwe wa CCM
AahahaaaDini ni siasa za kale zilizovikwa joho la utakatifu wa Mungu asiyethibitishika.
Acha hizo..Kesho ijumaa kama Saud Arabia nchi ya mtume SAW hawatakula IDD basi JF wanipige ban ya masaa 24.
Hizi dini ni za magumashi amkeni.
Cc: Kiranga
Huku hakuna mwezi..haujaonekana.Sasa kama uku hawajaona ,kwa nini kulazimisha wale sawa na waliokwisha uona?si ni kusubiri tu
Allah akulipe kheri ndugu yangu.Mkuu Dr Matola PhD mambo ya waislamu ungewaachia tu wenyewe mkuu maana kila mtu anajua anachokifanya.
Kwa kukuhabarisha kuna misimamo ya aina mbili na yote ni sawa, kuna msimamo wa kufunga na kufungua kwa mwandamo wa mwezi wa kitaifa na hili halina ubaya.
Na pili kuna msimamo wa kufunga na kufungua kwa mwezi wa kimataifa yaani unaoandama popote na hili halina ubaya.
Bakwata wameamua kushikilia msimamo wa mwezi wa kitaifa na waumini wana uhuru wa kuwafuata au kuswali kesho, kuna ubaya gani? hapa kuna utapeli upi? sisi wengine tunaswali kesho na tuko huru kufanya hivyo.
Nashauri wakati mwingine ungeachana na haya mambo maana ni comments zako nyingi unazungumzia utapeli n.k shika kile unachokiona ni sawa na mambo ya waislamu waachie wenyewe.
Asante.
Walichokosa Bakwata ni eliimu mufti darasa la 7...Kesho ijumaa kama Saud Arabia nchi ya mtume SAW hawatakula IDD basi JF wanipige ban ya masaa 24.
Hizi dini ni za magumashi amkeni.
View attachment 2594651
Cc: Kiranga
Sasa ndio umeandika nini? Mambo mengine mngetuachia wenyewe Waislam.Kesho ijumaa kama Saud Arabia nchi ya mtume SAW hawatakula IDD basi JF wanipige ban ya masaa 24.
Hizi dini ni za magumashi amkeni.
View attachment 2594651
Cc: Kiranga