Kama Serikali inashindwa kuendeleza miradi midogo kabisa ya Mabasi ya mwendokasi. Je, hiyo treni na ndege wataweza kweli?

Kaka unajaribu kubadili fikra kuwa uhalisia. Mfumo wa serikali kufanya biashara ulifeli Dunia nzima miaka ya '80
Na nchi za ulaya zote walianza kuamini na kusapoti sekta binafsi kabla ya Karne ya 10.
Kampuni kubwa duniani NI za watu binafsi. Zio za ndege Wala za vinywaji.
Tanzania tunawatu wehu kweli. Simba inaajili kocha na wachezaji kutoka kila Kona wenye vipaji ndio wa kapata mafanikio.
Nmb manajment yote wazungu wenye vipawa vya usimamizi wa fedha na taaluma ndio maana imesimama.
Sisi wasomi wetu NI wasaka fursa sio talented. Mtu anakipawa Cha kuwa dokta anasoma uinjinia Sasa akija kwenye utendaji Hana Cha kuongezsa zaidi ya aliyoyasoma pindi akiwa chuo.
 
Kifupi wanaofanikiwa kwenye biashashara NI watu wenye vipawa vya UBUNIFU na kufanya biashara na sio wasomi. Wao ndio hubuni mbinu mpya za kutafuta masoko, kuvutia wateja na kusimAmia mitaji na kuchungulia fursa. Serikali haiwezi kuajili watu hao. Huajili kwa kuangalia vyeti na vyama vyao vya siasa.
Bodi za wakurugenzi kwa Kampuni kubwa huwa NI watu wenye hisa kubwa kwenye kampuni husika. Ikitokea limefilisika NI wao huwa wa kwanza kuumia.
Ila bodi ya wakurugenzi kwa mashirika ya Uma NI wateule wa Raisi au waziri. Wengi NI wanasiasa wastafu. Hawajui lolote kuhusu biashara na uenda uko kupokea posho tu sio kushauri.

Sio biashara tu vitu vya serikali vyote Hadi shule, hospital huduma NI mbovu kwa kukosa UBUNIFU.
 
Kosa Liliazna alipofanyiwa zengwe max maliopo, alionekana anafaidi sana marehemu dikteta alikua hapendi sekta binafsi

Max maliopo aliuwezea sana mfumo wa kie-lectronic wa mwendokasi
 

Jibu la hoja yako lipo kwenye hiyo aya ya mwisho.

Kwa kifupi kabisa, pitia historia ya uchumi ya Tanzania tangu kupata uhuru kisha toa pendekezo la uhakika jinsi Tanzania itakavyoweza kuwapata hao “viongozi wenye commitment na dhamira ya kweli ...” na kuwapa madaraka stahiki ya uongozi wa mashirika ya serikali.

Ukitoa jibu thabiti kuhusu changamoto hilo basi hakika hoja yako ya serikali kufanya biashara kwa ufanisi/ushindani haitakuwa na ubishi.

Nyerere alishindwa na alieleza kuwa tatizo kubwa lililoua mashirika ya umma ni “kutotilia umuhimu mkubwa kwenye suala la management”. Ukweli ni kwamba isingewezekana kwa jinsi serikali ilivyokuwa ikiendeshwa huku malengo ya kisiasa yakiwa na kipaumbele namba moja ilhali yakikinzana na ya kibiashara/kiuchumi mara kwa mara.
 

China wanafanya ubadhirifu kwenye mashirika ya umma wanachukuliwa hatua Kali, huku wapo na wanadunda mtaani

Ni Ujinga kila saa kutolea mfano wa china, Tanzania mtu anaiba na afanywi chochote kwa sababu tu ni kada wa chama na alikua mteule wa rais
 

Hiyo 526.6 ni kipato siyo malipo. Ndiyo maana imejumlishwa na haikutolewa kwenye mahesabu yao. But that is beside the point. Swali la muhimu ni je unaelewa kwamba hela za serikali ni hela za walipa kodi?
 
... Net Group Solutions waliopewa Tanesco na Mkapa waliifikisha wapi?
Net group walipewa NMB na ndio wameifanya Nmn kujisimamia, kujiendesha kwa faida, kulipa Kodi na kufadhili sekta za afya na ELIMU kwa kuwapa zaidi ya bilion moja kila mwaka kununulia vitanda au dawati
 
China wanafanya ubadhirifu kwenye mashirika ya umma wanachukuliwa hatua Kali, huku wapo na wanadunda mtaani

Ni Ujinga kila saa kutolea mfano wa china, Tanzania mtu anaiba na afanywi chochote kwa sababu tu ni kada wa chama na alikua mteule wa rais
Watu sio waelewa kabisa kuhusu uchumi. China ilikuwa masikini wa kutupwa mpaka miaka ya 1980'. Wakati huo Hong Kong iliyokuwa chini ya mwingereza ikikua kwa Kazi ya ajabu. Mwaka 1980 China ilifanya mabadiliko makubwa ya Sera za kiuchumi sawa na Urusi. Kuruhusu sekta binafsi na uwekezaji wa magharibi kulipelekea China kuwa taifa kubwa ulimwenguni. Watu binafsi wamekuwa matajili wakubwa. NI nchi yenye mabilionea wengi Sasa kuliko nchi yoyote duniani. Huko ndio kimalik kwa sekta binafsi
 
Mfano mzuri mwendokesa mwaka 2016 na 2017 Max malipo a private sector alikua anatoa huduma za kuuza tiketi kielectronic, mwanzon mwa 2018 serekali ikasitisha mkataba wake anapewa ttcl since then haya madudu ndo yakaanza
 
Hiyo 526.6 ni kipato siyo malipo. Ndiyo maana imejumlishwa na haikutolewa kwenye mahesabu yao. But that is beside the point. Swali la muhimu ni je unaelewa kwamba hela za serikali ni hela za walipa kodi?
Ndugu Grant funding ni jambo la kawaida nchi za wenzetu. Mfano kwa Tanzania ukipekuwa utakuta asilimia kubwa ya FDI za wawekezaji wa kati kutoka UK sources za investment funds ni government grants.

Serikali yao inaweza kuwa na sera za kusaidia sector fulani ya supply chain au area of concern za kibiashara Tanzania. Grants za namna hiyo zipo mpaka kesho provided unaishi huko na una permanent residency (hizo ni kwa raia wao tu) na kila mwaka mara mbili wanatoa update kama umejiunga na U.K aid. 👇


Ndio maana unaona wawekezaji wakubwa Tanzania ni UK citizens, lakini ni grants ambazo unalipa kama umekopa bank tofauti riba ni ndogo sana, tatizo watanzania wanaoshi huko na wenye makaratasi hawana business ideas or can’t write convincing business proposals or are just not bothered kwa wale wachache wanaojua.

Hizo grants za TfL na zenyewe zina minajili hiyo hiyo kama ulivyosoma asilimia kubwa ya grants zao ni kupitia cross-rail grant funding 👇


Hiyo fund ni kuchochea uwekezaji wa reli biashara za serikali na private wote wapo entitled to apply but kuna malipo sio bure. Nonetheless not a subsidy by any means.

Ni sawa na kutaka kusaidia wakulima kupitia bank ya kilimo watu wanunue matreka ili kukuza kilimo kwa mikopo nafuu. Kutoa mbolea za ruzuku, mikopo ya vikundi kwa vijana, walemavu na akina mama kupitia mapato ya halmashauri.

Hiyo ndio mifano kwa standard zetu, but not subsidy. More like a fiscal policy tool through a third part.
 
Mchangiaji hujamtendea haki mtoa mada. Unanamtaka ataje sababu za kwanini serikali inashindwa kuendesha biashara badala ya kujikita kwenye maoni yake yanayotokana na uzoefu anaouona juu ya serikali kuendesha biashara.

Ukweli ni kwamba kutokujua chanzo cha tatizo haimaanishi kutokuwepo kwa tatizo. Ukweli ni kwamba kubainisha sababu za serikali kushindwa kuendesha biashara si kazi rahisi hivyo bali kunahitaji utafiti wa kina na ni wajibu wa serikali yenyewe na si mtoa mada.

Mtoa mada yeye ni shuhuda tu wa matatizo yanayojitokeza katika biashara zinazoendeshwa na serikali. Mara nyingi matizo hujidhihirisha yenyewe na kwahiyo kila mwenye macho na akili anaweza kuyaona kama mtoa mada anavyoyaona kwenye biashara za serikali

Nilidhani ingekuwa vizuri kukubaliana na mtazamo wa mtoa mada kwamba serikali haiwezi kuendesha biashara badala kumtaka ataje sababu jambo ambalo ni nje ya uwezo wake.
 

Mbona hujibu swali nililokuuliza? Je unaelewa kwamba hela za serikali ni hela za walipa kodi?
 
Mbona hujibu swali nililokuuliza? Je unaelewa kwamba hela za serikali ni hela za walipa kodi?



Nilishakuwekea jibu hapo ☝️hizo grants ni mkopo kutoka serikalini wanalipa sio bure. Umeona mkopo wa £1.3 billion kwa jiji GLA (greater London authority) inayoendesha TfL; na TFL yenyewe imepokea £750 directly na umeambiwa kabisa ni loan from DfT (Department for Transport; wizara ya uchukuzi).

Kama umesoma biashara utakuwa unaelewa sources of investment finance; government grants ikiwa moja wapo na wanufaika includes private organization.

Anyway mada inasema serikali aiwezi endesha biashara na mabeberu hawafanyi ivyo; jambo ambalo si la ukweli.
 
China wanafanya ubadhirifu kwenye mashirika ya umma wanachukuliwa hatua Kali, huku wapo na wanadunda mtaani

Ni Ujinga kila saa kutolea mfano wa china, Tanzania mtu anaiba na afanywi chochote kwa sababu tu ni kada wa chama na alikua mteule wa rais
Hayo mashirika ya china hayaendeshwi kwa malengo ya kisiasa bali kwa mlengo wa biashara
 
Mkuu Yoda, tumetoka huko nyuma vizuri sana; lakini nikiri mchango wako huu hapa hukuupa uzito stahiki.

Sikuona la kujibu kwenye mchango huu hapa.

Nadhani 'fatique' uchovu wa mjadala umechukua nafasi yake.

'Anyway', bado naheshimu uungwana wa michango yako.
 
Unajua mkuu 'Opportunity', binafsi sina tatizo kabisa na serikali kuwaachia wanaoweza waendeshe mashirika hayo kwa ufanisi, sina tatizo kabisa juu ya hilo, mradi nchi/wananchi wanafaidika na huduma nzuri na nchi inapata haki yake toka kwenye mashirika hayo.

Sasa basi, ukikaa chini na kufikiri, serikali inayoshindwa hata kuendesha kishirika kama UDA tu, itakuwa na uwezo gani wa kuhakikisha nchi inafaidika toka kwa hawa tunaowaachia waendeshe? Viongozi ambao kila ukiangalia wana njaa ya kutisha sana kujinufaisha wao zaidi kuliko manufaa yanayopatikana ili wananchi na wao wafaidike.

Tatizo ndilo hilo, na sijui kama wewe una suluhisho juu ya hali hiyo.
 
Hayo mashirika ya china hayaendeshwi kwa malengo ya kisiasa bali kwa mlengo wa biashara
Basi sawa, kwa nini isiwe hivyo hata hapa kwetu?

Nadhani tunachanganya mambo kidogo hapa wakati tunaposema "malengo ya kisiasa". siasa gani hiyo?
Mimi naiita kwa "malengo ya kifisadi" siyo siasa hasa!
 
Hao(sekta binafsi) hatuwaachii waendeshe tu kama wanavyoendesha TICTS bandarini. Serikali ikiamua kuindoa ATCL na mwendokasi mikononi mwake hayo mashirika yanakuwa kampuni binafsi kabisa za mtu mmoja au wanahisa wenye hisa nyingi waliokidhi vigezo vya kuuziwa.

Serikali inabaki kukusanya kodi au ushuru tu kama inavyokusanya kwenye mabasi ya watu binafsi mikoani, daladala na inavyokusanya fastjet na precision airways na kusimamia sheria.
Nchi kufaidika ni kukusanya kodi yake inavyotakiwa baada ya kuyauza hayo makampuni katika mchakato wa wazi na unaozingatia vigezo na kanuni, kama hata hiyo kazi yake ya msingi haiwezi basi iombe isaidiwe.
 

Serikali haitakiwi kufanya biashara. Inajiongezea mzigo usio na sababu. Ingawa,lazima waamue kufanya biashara na taasisi au makampuni binafsi yenye kuaminika.
Yale mambo ya kubinafsha ATC kwa SA Airline au kuwapa reli ya kati wale wahindi ambao hawakuwa na lolote la kuongeza ni uhujumu uchumi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…